KWA mara ya kwanza tangu atoke mahabusu ya Gereza la Segerea, Dar kwa dhamana, staa wa filamu na video za wasanii wa Bongo Fleva, Elizabeth Michael ‘Lulu’ au Lizy amefunguka juu ya uhusiano wake na aliyekuwa mwandani wake, marehemu Steven Kanumba na kusababisha gumzo kubwa mitandaoni.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiMVK7zodSlxX4jbmf9y_m2Wa01CItOsw81BzIcS9TFbwKV4wq8_aB5b3FmMh4O2texlVgYXUcZngKze0wIIGLcOhLo-l0ytcAn11xECicKAGoCMwlopOhEfggfAxg1lXGw2zEKi5vs5hV0/s1600/226456_132699626807000_100002008907798_220856_161342_n.jpg?width=640)
“Ulikuwa zaidi ya baba, kaka, mpenzi, mume, ndugu na rafiki…sitaacha kukulilia katika maisha yangu yote!! R.I.P daddy yangu Steven Kanumba.”
Ndani ya muda mfupi, kauli hiyo ya Lulu ilipata maoni mengi huku baadhi ya watu wakimpa pole kumtia moyo na wengine wakijibizana kwa hasira juu ya ishu hiyo.
Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia marehemu Kanumba ambayo inatarajiwa kuanza kuunguruma muda wowote.
0 comments:
Post a Comment