Hivi leo, endapo utamkuta Wema akiwa ametulia kisha ukamtishia ukitumia sauti ya juu kuyataja majina ya Diamond na Penny, kuna uwezekano mkubwa mrembo huyo akavunja mguu kwa kukimbia ‘spidi’ kali.
Hivi leo, endapo utamkuta Wema akiwa ametulia kisha ukamtishia ukitumia sauti ya juu kuyataja majina ya Diamond na Penny, kuna uwezekano mkubwa mrembo huyo akavunja mguu kwa kukimbia ‘spidi’ kali.
![](http://2.bp.blogspot.com/-ygAorB3QV3I/Tp55ApJEHrI/AAAAAAAAA0g/2sMfaM_jiE0/s1600/14.jpg?width=650)
Simu ikapigwa; inadaiwa kuwa Wema aliamini Diamond hapindui kwake, kwa hiyo alipiga simu kwa kujiamini.
Kilichozungumzwa; baada ya simu kupokelewa, inadaiwa kwamba Wema aliomba Diamond afungue moyo ili penzi lao lirudi kama zamani.
Misifa kazini; Diamond aliposikia sauti ya Wema ikimbembeleza, ‘bichwa’ likamvimba, papo hapo, akaanza kumrekodi mrembo huyo.
Eti Diamond hataki ‘drama’; mwanamuziki huyo, anasikika akimjibu Wema kwamba hawezi kurudiana naye kwa sababu itaonekana wanafanya drama (maigizo).
Diamond anafunguka: “Hapa hakuna drama wala nini, wala sikufanyii drama. I am in love with Penny (nipo kwenye penzi na Penny) na wewe unajua. Sipendi na sipendezewi kwa sababu mwisho wa siku yatakuja kutokea matatizo, sitaki.”
Penny naye; mrembo huyo anayemmiliki Diamond kwa sasa, aliingilia mazungumzo kati ya M’bongo Fleva huyo na Wema, kisha anasikika akimpa vidonge vyake, mrembo huyo: “Wema unaweza kutuacha tulale?”
Wema akasalimia; mrembo huyo ambaye juzijuzi alikata shilingi milioni 13 kumtolea faini msanii Kajala Masanja na kumwokoa na jela, hakutetereka kusikia sauti ya Penny kwenye simu, badala yake akamsalimia: “Uko poa?”
Penny akaliendeleza: “Yeah, niko poa mamy wangu. Hivi kwa nini hutaki kitu kitakachokufanya uwe na amani? Sisi hatutaki matatizo na wewe.”
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgMHrcQF4yMja_24axMPHCj-q4T3c32maHuSP3vsjX10wk-jO-x9_fH2eGae8CszLzLp7kGee9RWB_vW1ZfvK9f7SnVNG9e3F-57IIzMRPN6G80l0yzH7oOYouECZ5PrFLYUQG68PL3T7A/s1600/wema.jpg?width=650)
Alipohojiwa na paparazi wetu kuhusiana na ishu hiyo, Wema alikataa katakata kwamba sauti inayosikika kwenye rekodi ya mazungumzo hayo siyo ya kwake, akaongeza kuwa alishaachana na Diamond siku nyingi zilizopita na kamwe hawezi kufanya kitu kama hicho.
“Hao kama wananichokonoa wapate ‘kick’ wafanye kimpango wao na siyo kutumia jina langu, mimi ni staa mkubwa Tanzania na kila mtu ananijua, waniache na maisha yangu kwa sababu sipendi kuongeaongea. Hata hili kama usingeniuliza, nisingesema chochote,” alisema mrembo huyo.
DIAMOND JE?
Diamond alipozungumza na ripota wetu, alisema kuwa sauti hiyo alimrekodi Wema kwa lengo la kumwonesha ni kiasi gani hivi sasa yupo kwenye uhusiano ‘siriaz’ na Penny.