This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Tuesday, May 14, 2013
KOCHA KIM KUZUNGUMZIA MECHI YA MOROCCO
Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu kwenye jiji la Marrakech nchini Morocco. Taifa Stars ilishinda mechi yake iliyopita jijini Dar es Salaa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco.
Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania…
Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Taarifa zinazohusiana
Taarifa zinazohusiana
Anasema aliandika taarifa hiyo kuwahakikishia watoto wake kwamba hakuwa kwenye hatari ya kupata saratani tena.
Kulingana na Jolie madaktari walisema kuwa uwezekano wake kupata Saratani ya matiti ni asilimia 87 huku akiwa na asilimia 50 uwezo wake wa kuugua Sarati ya mfuko wa uzazi.
''Niliamua kuchukua hatua mwenyewe ili kuzuia uwezekano wowote wa kuugua Saratani hiyo,'' alisema Jolie.
Alisema kuwa shughuli hii ilianza mwezi Februari na kukamilika mwishoni mwa mwezi April.
Uwezekano wapunguzwa.
Katika taarifa iliyoandikwa na Bi Jolie na yenye kichwa, 'Uamuzi wangu wa kimatibabu', Bi Jolie alieleza kuwa mamake alipambana na Saratani kwa miaka kumi na kufariki akiwa na umri wa miaka 56.Alisema kuwa alielewa fika kuwa siku moja atawahi kuugua Saratani na ndio maana akachukua uamuzi wa kufanyiwa upasuaji huo mgumu wa wiki tisa ambao ulihitaji kukatwa matiti.
Uwezekano wake wa kuugua saratani sasa umeshuka kutoka 87% hadi 5%.
Alimsifu mumewe Brad Pitt, kwa kumuunga mkono na kumfariji kwa kila aliyopitia, na kusema kuwa ametulizwa na kuwa wanawe hawakupata lolote katika matokeo ya uchunguzi wa madaktari tangu kufanyiwa upasuaji.
"ninahisi kuwa na nguvu kwa uamuzi niliofanya, na kwa kuwa ninasalia kuwa mwanamke hata baada ya kuondoa viungo hivyo,'' alisema Bi Jolie.
"kwa mwanamke yeyote anayesoma maneno haya, natumai ataweza kujua kuwa wanaweza kufanya uamuzi.''
Muigizaji huyo, ambaye ameshinda tuzo nyingi kwa uigizaji wake, pia ni mtunzi wa filamu na mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa anayehusika na harakati za kibinadamu.
Wakati alipokuwa anafanyiwa upasuaji, Bi Jolie alizuru Jamuhuri ya Kidremokrasia ya Congo pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague.
Jolie pia alihudhuria mkutano wa mawaziri wa mambo ya nchi za kigeni wa G8, kuhamasisha dunia kuhusu dhulma za kingono katika maeneo ya vita.
CHANZO. BBC SWAHILI
GODBLESS LEMA ASAKWA NA POLISI WA U.K KWA KOSA LA KUMBAKA FLORA BAHATI LYMO
MWIZI KWA KUTUMIA BODABODA AUAWA!
KIJANA mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja anayedaiwa ni mzoefu wa wizi kwa kutumia usafiri wa pikipiki ‘bodaboda’, ameuawa baada ya kumliza mwanamke aliyetambulika kwa jina la Jusmini.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita maeneo ya Mwenge jijini Dar, saa tatu usiku ambapo inadaiwa mwanamke huyo alikuwa akikatiza mitaa hiyo huku akiwa ameweka mkoba wake kwapani.
Ikadaiwa mwanamke huyo akiwa eneo hilo huku akiamini yuko salama, ilitokea bodaboda kwa nyuma ikiwa imebeba abiria na ghafla alishangaa anakwapuliwa mkoba wake.
“Unajua yule mama alikuwa akitembea kwa kujiamini lakini inavyoonekana wale jamaa ambao ndiyo zao kuwaibia watu walikuwa wamemlia ‘timing’ tangu aliposhuka kwenye daladala.
“Tuliposikia makelele ya mwizi, tulimfuata mama huyo na tulipomuuliza akatuambia ameibiwa mkoba wake huku akituonesha vijana hao ambao muda huo walikuwa wakikimbia,” kilieleza chanzo hicho kilichoshuhudia tukio zima.
Ikaelezwa kuwa, kufuatia maelezo ya mwanamke huyo, baadhi ya watu wenye hasira kali wengine wakiwa kwenye pikipiki waliamua kuwakimbiza wezi hao ambapo mmoja alishuka na kukimbia kivyake huku mwenye bodaboda akizuiwa kwenye geti kuu ya kutokea magari.
“Alipozuiwa akaona imeshakua soo, akashuka na kuitelekeza pikipiki yake kisha akataka kudandia gari nyingine lakini watu wakafanikiwa kumkamata kwenye mataa ya Mwenge ambapo magari yalisimama, jamaa alishushiwa kichapo hadi akauawa,” kiliendelea kupasha chanzo hicho.
Baada ya kijana huyo kuuawa, polisi walifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wake. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela (pichani)alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema taarifa za kifo cha kijana huyo hazijafika mezani kwake lakini akasema anaendelea kufuatilia.
KASHIFA YA NGONO YALITAFUNA BUNGE LETU....WABUNGE WADAIWA KUBEBANA NA KUPEANA MIMBA
![](http://4.bp.blogspot.com/-UDD-WPifrck/UZIUeGTbAkI/AAAAAAAAf9E/LicL_YUfuiw/s1600/11.jpg)
SKENDO nzito inalitafuna Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikitawala madai kwamba kuna wabunge wawili wanawake, wamejazwa mimba na waheshimiwa wenzao wanaume.
Awali, ulitawala uvumi kuwa mmoja wa wabunge wa upinzani (viti maalum), akitokea Kanda ya Kaskazini, amepewa ujauzito na mheshimiwa mwingine ambaye ni kiongozi anayeshika nafasi za juu kwenye moja ya vyama vikuu vya upinzani nchini (wote majina yao tunayahifadhi kwa sasa).
Kashfa hiyo ya mtunga sheria huyo kupewa mimba na mheshimiwa mwenzake ambaye ni mume wa mtu, ilipata mbeleko na kuifanya ivume zaidi, baada ya Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde, kulipuka bungeni: “Humuhumu ndani kuna wabunge wanawake wenye mimba zisizotarajiwa.”
Lusinde, alitamka hayo Aprili, mwaka huu, wakati akichangia hotuba ya bajeti, Ofisi ya Waziri Mkuu, kipindi ambacho bunge lilikuwa limechafuka kutokana na wabunge kurushiana ‘mipasho’ wao kwa wao.
Kauli ya Lusinde, pamoja na kupokelewa tofauti na wabunge wengi wanawake, wakidai mheshimiwa mwenzao amewadhalilisha, upande mwingine, katika ‘vikao vya kwenye korido’, matukio ya vicheko na kugonga mikono yalitawala na kunena kwa msisitizo “message delivered”, yaani ujumbe umefika.
Katika kufanyia kazi kila kinachozungumzwa, mwandishi wetu alizungumza na baadhi ya wabunge ambapo Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, alisema: Unajua madai ya mimba yanawahusu wanawake, kwa hiyo waulizwe wenyewe.
“Kama umenitafuta mimi kwa kigezo kwamba ni mbunge kijana, basi waulize wabunge vijana wanawake,” alisema Mnyika.
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, alikiri kufahamu kuwepo kwa tuhuma kwamba wapo wabunge wamepeana mimba lakini hawezi kuwa na uhakika kwa sababu uhusiano wa kimapenzi ni jambo la faragha.
“Hayo madai yapo, yanazungumzwa. Wapo wanaotajwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi, hayo ni mambo ya faragha. Sijui pengine walioanzisha haya madai wana vipimo vyao,” alisema Kafulila.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Morogoro, Sara Msafiri, alisema kuwa haiwezekani wabunge kupata mimba zisizotarajiwa kwa sababu ni watu wazima.
“Wabunge tunapata mafunzo ya uzazi, kwa hiyo kama ni mimba basi mtu anakuwa amepanga kuipata. Hakuna kitu kama hicho. Hata hilo la kutoa mimba halipo kabisa, sijawahi kusikia mtu amefanya hivyo bungeni,” alisema Sara.
Mbunge mwingine wa Viti Maalum (Chadema), Chiku Abwao, alisema: “Hakuna mbunge anayepata mimba isiyotarajiwa, kwanza nilimshangaa mbunge kutamka mambo kama hayo, alistahili kuwaambia watoto, lengo lake lilikuwa kudhalilisha wanawake.”
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Munde Tambwe, alisema: “Ile kauli ya Lusinde kwamba kuna wabunge wanapata mimba zisizotarajiwa, nadhani kuna mtu alikuwa anamlenga, kwa hiyo mimi siwezi kulizungumzia.”
PICHA 5 ZA WANAFUNZI WA MANZESE WALIOVAMIWA NA MASHETANI LEO ASUBUHI
Wanafunzi wa shule ya Sekondari Manzese iliyopo Manzese Uzuri, jijini Dar es Salaam wamevamiwa na mashetani na kuanguka hovyo darasani huku wakipiga kelele na kuongea maneno yasiyoeleweka na kusababisha hofu kutanda maeneo hayo.
Tukio hilo limetokea kuanzia saa nne asubuhi ambapo alianza mwanafunzi mmoja kupiga kelele na kuanguka wakati wakiendelea na masomo ambapo alitolewa nje ya darasa lakini cha kushangaza waliendelea kuanguka wengine wengi huku wakipiga kelele na kupigana kama vichaa.