Jengo hilo ambalo kwa sasa lipo katika hatua ya linta linajengwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Tenknolojia Profesa Makame Mbarawa akishirikiana na nguvu za wananchi.
Kutolewa kwa fedha hizo ambazo zitanunulia vifaa vya ujenzi vinavyohitajika kwa ajili ya kazi ya kuezeka pamoja na vifaa vingine vya kumalizia ujenzi ni matokeo ya juhudi za makusudi za mfuko huo za kusaidia miradi ya kijamii yenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa wananchi hapa nchini.
Akikabidhi mfano wa hundi kwa wakazi wa Mkanyageni katika hafla iliyoongozwa na Waziri Profesa Mbarawa, Mkuu wa Mfuko huo Yessaya Mwakifulefule amesema Vodacom Foundation imekuwa na dhamira ya dhati ya kusaidia maisha ya watanzania mijini na vijijini ili kuboresha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya na uwezeshaji wanawake kiuchumi.
“Tunajisikia furaha sana leo kuona Vodacom Foundation ipo hapa Michenzani kuendeleza azma yake ya kuunga mkono juhudi za maendeleo, tutachangia fedha ambazo zitatumika kununulia vifaa vya ujenzi kumalizia ujenzi wa kituo cha afya katika eno hilli.”Alisema Mwakifulefule.
Hata hivyo Mwakifulefule aliwapongeza wakazi wa Shehia ya Michenzani na jimbo zima la Mkanyageni hususan vijana kwa namna wanavyojitolea kushiriki katika miradi ya maendeleo jambo ambalo amesema huenda limechangia kwa kiasi kikubwa kumpa nguvu Waziri Prof;Mbarawa ambae ni mweneyeji wa eneo hilo kusaidia maendeleo.
“Nimezunguka sehemu mbalimbali hapa nchini hamasa na ari niliyoiona hapa ni ya kipekee jinsi ambavyo wananchi mnavyojitolea katika miradi ya maendeleo hili ni jambo zuri na linawapa moyo wahisani wa maendeleo.”Alisema Mwakifulefuke na kuongeza. “Na sisi katika fedha tutakazozitoa kumalizia ujenzi zinahusisha fedha za kulipia gharama za mafundi na vibarua mbao ni miongoni mwenu. Kwa namna hiyo tunaamini kuwa tutakuwa pia tunaimarisha hali ya uchumi wa vijana wa eneo hili.”
Kwa upande wake Waziri Profesa Mbarawa ameishukuru Vodacom Foundation kwa kukubali kusaidia kumalizia ujenzi wa kituo hicho,
“Nawashukuru Vodacom Foundation kwa kuja hapa na kusaidia maendeleo yetu ila nataka niwaambie wananchi kwamba haya yote hayaji tu hivihivi bali hutafutwa.” Alisema Profesa Mbarawa
Waziri huyo wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia aliwashukuru vijana na wakazi wa Mkanyageni kwa jinsi wanavyojitoa na kuwaeleza kuwa hiyo ni silaha muhimu ya maendeleo hivyo waupeke kudanganywa na badala yake waangalie namna gani ya kuleta maendeleo na kiwanga mkono wale wanaowaletea maendeleo badala ya kukubalia hila za kuwabeza.
Vodacom Foundation imekuwa ikichangia miradi mbalimbali ya maendeleo Zanzibar ambapo pia hivi karibuni imeahidi kutoa boti mbili za uvuvi kwa vikundi vya vijana Pemba na Unguja kusaidia juhudi za serikali ya Zanzibar za kutengeza ajira kwa vijana.
Mbali na mchango huo, Mwishoni mwa mwaka jana, Vodacom Foundation ilisaidia wanawake wajasiriamali zaidi ya 300 kwa kuwaptia mikopo nafuu isiyo na riba wala dhamana yenye thamani ya zaidi ya Sh. 27 Milioni katika kisiwa cha Unguja pamoja na kuahidi kuchangia Sh 15 Milioni kwenye mfuko wa maendeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar.