Na Mwandishi WetuMITANDAO
 mingi ya kijamii na kurasa binafsi za mawasiliano zinazopatikana ndani 
ya simu za viganjani kama Instagram, WhatsApp na BBM (Blackberry 
Messenger) zinazomilikiwa na baadhi ya wasichana wanaosoma Chuo Kikuu 
cha Dodoma (Udom) zimejaa mambo ya ngono na kashfa kwa baadhi ya wabunge
 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Unyemeleaji taarifa
 uliofanywa na Ijumaa kwa muda mrefu kwenye huduma hizo za mawasiliano 
ya kisasa  umebaini wanafunzi wa kike wamewabatiza jina la ‘mabuzi yao’ 
baadhi ya wabunge.
Bila kupepesa mitandao hiyo imekuwa pia 
ikitumiwa na wasichana hao kuuza miili yao huku ufahari kama si ujanja 
ukiwa ni mtu kujipatia bwana mwenye cheo cha ubunge ambaye anaaminika 
waleti yake haikaukiwi fedha kutokana na posho za vikao na utumishi wa…
                                 
Na Mwandishi WetuMITANDAO
 mingi ya kijamii na kurasa binafsi za mawasiliano zinazopatikana ndani 
ya simu za viganjani kama Instagram, WhatsApp na BBM (Blackberry 
Messenger) zinazomilikiwa na baadhi ya wasichana wanaosoma Chuo Kikuu 
cha Dodoma (Udom) zimejaa mambo ya ngono na kashfa kwa baadhi ya wabunge
 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Unyemeleaji taarifa 
uliofanywa na Ijumaa kwa muda mrefu kwenye huduma hizo za mawasiliano ya
 kisasa  umebaini wanafunzi wa kike wamewabatiza jina la ‘mabuzi yao’ 
baadhi ya wabunge.
Bila kupepesa mitandao hiyo imekuwa pia ikitumiwa 
na wasichana hao kuuza miili yao huku ufahari kama si ujanja ukiwa ni 
mtu kujipatia bwana mwenye cheo cha ubunge ambaye anaaminika waleti yake
 haikaukiwi fedha kutokana na posho za vikao na utumishi wa umma.
SIKILIZA TUKUPASHE
“Shoga naona unawapanga tu waheshimiwa,” 
mchangiaji mmoja kupitia kundi la BBM alichangia kwenye moja ya picha 
aliyoweka rafiki yake akiwa amepozi na mbunge mmoja kutoka mikoa ya 
Magharibi  (jina kapuni) ambapo bila haya majibu ya mwenye ukarasa huo 
yalikuwa: “Maisha bila mabuzi hayaendi bi dada.”
Upekuzi wa 
kiintelijensia wa Ijumaa ulichungulia dokezo za wachangia mada na 
kubaini kuwa waheshimiwa wanaoingia mjengoni kama wawakilishi wa 
wananchi wanachukuliwa kama mabuzi kwa tafsiri ya kuchunwa fedha huku 
kipindi cha vikao vya bunge vikichukuliwa kama nyakati za migodi kutema 
dhahabu.
MAMBO YA KUFEDHEHESHA
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wasichana 
hao wa chuo wamekuwa wakihifadhi picha za utupu za wabunge wenye 
uhusiano nao kwenye simu zao za mikononi walizowapiga walipokuwa 
wakifanya nao ngono ambapo wakati mwingine huzitundika
mitandaoni kwa kubipu na kuziondoa haraka lengo likiwa ni kuwaonesha ushahidi huo marafiki zao.
Miongoni
 wa wabunge waliokumbwa na aibu hiyo ambao Ijumaa liliziona picha zake 
za aibu ni pamoja na mbunge anayetoka kanda ya Kusini, mwingine kanda ya
 ziwa na mmoja kutoka jijini Dar es Salaam huku waziri mwenye heshima 
kubwa naye akiingia mkenge kwa kupiga picha na msichana wakiwa kitandani
 vifua wazi.
WANAFUNZI WA KIUME WANASEMAJE?
Ijumaa lilipowauliza baadhi ya 
wanafunzi wavulana wanaosoma chuoni hapo juu ya kuwepo kwa tabia za  
baadhi ya wabunge kutembea na wanafunzi wa kike walikiri na kuongeza 
kuwa ukata ndiyo unaosababisha baadhi ya wanachuo wajitongozeshe kwa 
waheshimiwa.
“Wanachofuata ni fedha siyo mapenzi, wapo wasichana hapa
 kipindi cha bunge hawaonekani kabisa chuoni, wanakuwa na waheshimiwa 
wakistarehe, kuna wengine wanasomeshwa, wanahudumiwa,” alisema 
mwanafunzi mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Bonny.
IJUMAA LINASEMAJE?
Dawati la Ijumaa linawatahadharisha waheshimiwa
 wabunge wenye tabia za ukware kuachana na mambo ya kihuni, badala yake 
wajiheshimu vinginevyo watajikuta matatizoni na kuambulia aibu kubwa 
mbele ya jamii kwa kuanikwa kwenye magazeti siku si nyingi pia picha zao
 za aibu zitafikishwa kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda.