This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Tuesday, March 12, 2013
BASI UNAAMBIWA HUYU NDIO MTOTO WA MIAKA 8 ALIYEMUOA HUYU MWANAMKE WA MIAKA 61
Mtoto huyu aitwae Sanele amekaririwa akisema “nilimwambia mama yangu, nahitaji kweli kuoa na nimefurahi nimemuoa Helen lakini nikikua nitaoa mwanamke wa umri wangu”
Mama mzazi wa Sanale anasema “babu yake ndio alimchangulia Sanale amuoe Helen kwa sababu yeye(Babu) anampenda, na wamefanya hivyo ili kutimiza maagizo ya wazee wa koo ambao wameshafariki, yani ni kama matambiko”
Manyara Yashinda Tuzo ya Vipaji Miss Utalii 2013
Hata hivyo, mchuano ulikuwa mkali zaidi kati ya Miss Utalii, Lindi Manyara na Kagera ambao walionesha Umahili mkubwa wa kucheza ngoma za asili na kupelekea kuingia katika hatua ya Tatu Bora. Katika Hatua hiyo ya Tatu Bora washiriki hao walicheza wimbo mmoja ujulikanao kwa jina la katope kutoka kundi la ngoma za asili la kibiriti ambao ni mchanganyiko wa ngoma mbalimbali wa makabila ya ngoma za kusini.
Hali hiyo iliwafanya wapenzi wa fani ya urembo waliofurika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala kuto kuamini kwamba wanao cheza jukwaani ni Mabinti wa Kizazi kipya ambao kwa Hali ya kawaida ya sasa ni nadra sana kumuona sister Duu tena Mrembo kucheza ngoma za asili kwa ufasaha na umahili mkubwa. Wapenzi hao walijikuta wakiacha viti vyao na kuanza kushangilia kwa nguvu mwanzo hadi mwisho huku wakiwapongeza waandaaji wa shindano la Miss Utalii Tanzania kuwa ni Hazina kubwa ya utamaduni wa Mtanzania na Wengine wakithubutu kusema Miss Utalii ni mtambo wa kurekebisha tabia kwa kuweza kuwabadirisha fikra za mabinti hao wa kizazi kupya mashindano hayo kwa ya kuwa kucheza ngoma za asili ni ushamba hadi kuwafanya kuwa wacheza ngoma mahili tena hadhalani bila ya Aibu na kwa kujivunia utamaduni na Ngoma za Asili Tanzania.
Wapenzi hao waliohudhuria katika shindano hilo wakisika kwa nyakati tofauti kuitaka na kuishauli Serikali na mamlaka za utalii kudhamini shindano la Miss Utalii Tanzania kwa Faida ya Jamii na Taifa kwani shindano hili limedhihilisha uwezo mkubwa wa sio tuuu kuhifadhi utamaduni wa mtanzania bali pia kuhamasisha na kutangaza utalii wa tanzania kitaifa na kimataifa.
“Shindano hili ni zuri na ni lakipekee lakini tatizo inaonekana waandaaji hawajapata wadhamini wa uhakika, kwanini Serikali isiwasaidie hawa,” alisema Jafary Shaibu mpenzi ma mashindano ya urembo.
Akizungumza katika Shindano hilo ambalo Mwanamuziki wa Kimataifa Che Mundugwao alikonga nyoyo za watu kwa Muziki wake wenye asili ya kitanzania, Mgeni Rasmi, Maabad Suleiman Hoja Mustahiki Meya wa Manispaa ya Temeke aliwapongeza sana washiriki na washindi lakini alitoa shukurani za pekee kwa waandaaji wa mashindano haya kwa kuipa manispaa na wilaya ya Temeke Heshima kubwa ya kuwa wenyeji wa Tukio hili la kitaifa lenye hadhi ya kimataifa.
Kiongozi huyo alisema Manispaa ya Temeke na Wilaya inayouwezo wa kuwa wenyeji wa matukio makubwa ya kimataifa na kitaifa kama la Miss Utalii Tanzania 2012/13, hivyo kutoa fursa ya pekee kwa Temeke kujitangaza kiutalii, kitamaduni na kiuwekezaji ndani na nje ya Nchi. Pia aliahidi kuwa Manispaa ya Temeke kuendelea kuunga mkono kwa hali na mali ili kufanikisha fainali hizo ambazo zitafikia kilele katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Dar es Salaam.
Mshindi wa Tuzo hiyo ya Vipaji ambaye alishangiliwa na washiriki wote baada ya kutangazwa kama mshindi, alizawadiwa udhamini wa kusoma kozi ya Kiwango cha Diploma katika chuo chochote nchini.
Fainali za Taifa za Miss Utalii Tanzania mwaka huu Zimedhamiwa na: Mtwana Catering Services, Ikondolelo Lodge, Zizou Fashion, Coca Cola Kwanza, VAM General Suppries Limited,Global Publishers, TANAPA, Ngorongoro Crater, Lakeland Africa, Clouds Media Group, Star Tv, Vailey Spring,Dotinata Decoration,Tone Multimedia Group, Baraza la sanaa la Taifa (BASATA )
mh.kinana ashawishi wachina kuwekeza nchini
NA BASHIR NKOROMO, CHINA
KATIBU Mkuu wa Chama CHa Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amekiomba Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) kuhimiza wananchi wa China kuchangamkia fursa ya kuwezeka nchini Tanzania.
Alisema, Wachina kuwekeza na kushiriki shughuli nyingi za kiuchumi Tanzania ni miongoni mwa kiunganishi kikubwa kitakachoweza kudumisha urafiki na undugu wa siku nyingi kati ya nchi hizo mbili ambao hadi sasa ni wa kupigiwa mfano duniani.
"Hivi sasa Tanzania imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji, hivyo ninyi ndugu zetu wa China, ni vema mkaitumia fursa hii kuwekeza. Hii itazidi upanua zaidi wigo wa mahusiano ya kirafiki tulionayo kwa miaka mingi sasa", alisema Kinana.
Kinana alisema, baadhi ya maeneo ya uwekezaji yanayoweza kuleta tija katika uchumi wa Tanzania na China ni Kilimo, kwa sababu hivi sasa Tanzania imejizatiti sana katika sekta hiyo ili kuifanya kuwa nyenzo ya uhakika kuinua na kukuza uchumi.
Akizungumza na Kinana, Xianyao alisema, China inatambua fursa za kiuchumi zilizopo Tanzania, na ipo tayari kuzitumia fursa hizo, kwa kuwa mbali na kuleta faida kwa Tanzania lakini itasaidia pia kuinua uchumi wa China na watu wake.
Alisema, licha ya China kuwa na changamoto za kijamii ikiwemo ukosefu wa ajira kwa vijana wake, lakini imejitahidi kupambana na changamoto hizo chini ya uongozi imara wa CPC na sasa ni moja ya nchi zilizopiga hatua kiuchumi duniani.
Xianyao alisema, China imeweza kupiga hatua kutokana na kujikita katika uchumi wa soko, kilimo cha kitaalam na viwanda na sasa imeweza kufanya idadi kubwa ya wananchi wa China kusihi maisha ya nafuu mbali ya changamoto ambazo ni lazima kuwepo.
Katika ziara hiyo Kinana amefuatana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar), Vuai Ali Vuai, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Khadija Aboud, Katibu wa NEC, Siasa na Uhuaisno wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martine Shigela, Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi, Khamis Suleiman Dadi, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi na Mohammed Yusuf Mohamed.
Wengine ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu Titus Kamani, Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na maofisa wa Chama.
Kinana anafanya ziara ya siku kumi nchini China kutokana na mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China, na anafanya ziara hiyo ikiwa ni ya kwanza kuifanya nje ya nchi, tangu alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Oktoba mwaka jana mjini Dodoma.
CPC imemwalika Kinana ili kupata fursa ya kubadilishana uzoefu kisiasa na katika nyanja za uchumi ambapo kwa upande wa CCM itapata fursa kubwa ya kushuhudia jinsi gani China imeweza kupiga hatua katika uchumi wa nchi hiyo.
Airtel yamzawadia mkazi wa Rufiji millioni 15 kupitia promosheni ya Amka millionea
JK OPENS THE CONFERENCE ON THE STRATEGIC IMPORTANCE OF INTELLECTUAL PROPERTY (IP) POLICIES
salaam today March 12, 2013.
DKT. BILAL AKUTANA NA CITIBANK
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mkurugenzi wa Citibank’s Patrick Dewide na Mkurugenzi Mtendaji wa Citibank Tanzania Joseph Carasso (kushoto) wakati walipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam kwa mazungumzo.( Picha na OMR).