This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Wednesday, July 17, 2013
Airtel na UNESCO kuzindua radio jamii Karagwe Bukoba
WANAJESHI 7 WALIOUAWA DARFUR FULL STORY
TANZANIA imeingia kwenye majonzi mazito baada ya wanajeshi wake 7 kuuawa na waasi wa Jimbo la Darfur nchini Sudan inayoongozwa na Rais Omary Bashir walipokuwa katika kazi ya ulinzi wa amani nchini humo.
TANZANIA imeingia kwenye majonzi mazito baada ya wanajeshi wake 7 kuuawa na waasi wa Jimbo la Darfur nchini Sudan inayoongozwa na Rais Omary Bashir walipokuwa katika kazi ya ulinzi wa amani nchini humo.
Habari za uhakika kutoka kwa chanzo cha kuaminika, wanajeshi wa Tanzania walikuwa wakiusindikiza msafara wa amani wa Umoja wa Mataifa (UN) uliokuwa ukitokea eneo la Khor Abeche kwenda Nyara Darfur na kushambuliwa na waasi hao.
Inadaiwa kuwa wanajeshi wa Tanzania walihamaki na kujaribu kutoa msaada wa kumuokoa mwenzao ndipo lilipotokea shambulio hilo ambalo pia limesababisha wanajeshi wengine 14 kupatwa na majeraha.
Wanajeshi hao wa Tanzania wameuawa wakiwa wanapigania amani na kutii kifungu cha 6 cha sheria cha majeshi ya kulinda amani duniani ambacho kinapiga marufuku wanajeshi kujibishana kwa silaha na waasi.
Wanachotakiwa kufanya ni kukimbia au kujilinda kwa kujihami bila ya kuleta madhara kwa upande wa pili vinginevyo wasingekufa kama wasingeitii sheria hiyo.
TANZANIA YALIA NA KIFUNGU NA.6
Akizungumza na waandishi wa habari nchini mwishoni mwa wiki iliyopita, Msemaji wa Jeshi la Tanzania, Kapambala Mgawe alisema Tanzania inatarajia kufanya mazungumzo na Umoja wa Mataifa (UN) ili kuomba kifungu hicho namba 6 kinachowakataza wanajeshi wanaolinda amani kujibu mapigo kiondolewe.
Pamoja na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete kuwalilia wanajeshi hao, vilio vimetawala kila kona ya nchi.
HEBU ONA
Kutokana na asili ya majina ya wanajeshi hao, kila pembe ya nchi inaweza kuguswa kwa njia moja ama nyingine na vifo hivyo;
Sajenti Shaibu Othuman na Koplo Mohammed Juma, hawa wanawakilisha vilio upande wa Pwani ya Tanzania kuanzia Zanzibar hadi Kusini mwa Tanzania kwenye Mikoa ya Lindi na Mtwara.
Wengine ni Koplo Oswald Chaula na Pte. (Private) Rodney Ndunguru, hawa wanawakilisha Nyanda za Juu Kusini katika Mikoa ya Iringa, Mbeya na Ruvuma.
Wakati marehemu Pte. Peter Werema anawakilisha Kanda ya Ziwa hususan katika Mkoa wa Mara ambao sambamba na mikoa mingine ya jirani nao wameguswa na msiba huo.
Kilio hicho kimesambaa hadi katika mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania ikiwemo Arusha na Kilimanjaro kutokana na kifo cha Pte. Fortunatus Msofe .
Aidha, mwanajeshi mwingine Koplo Mohammed Chikilizo naye amesababisha vilio katika mikoa ya Pwani.
FRANK ATISHIWA KUUAWA
MSANII wa Filamu za Kibongo, Mohammed Mwikongi ‘Frank’ amedai kutishiwa kuuawa baada ya kupokea ujumbe mfupi wa meneno ‘sms’ kutoka kwa mtu anayekulikana kwa majina ya Jonathan Lyradu.
“Mara ya kwanza nilijua amekosea namba, nikamuuliza anamuhitaji nani, lakini akanitumia meseji nyingine na kunitaja jina langu huku akiendelea kunitisha na…
Na Mwaija Salum
MSANII wa Filamu za Kibongo, Mohammed Mwikongi ‘Frank’ amedai kutishiwa kuuawa baada ya kupokea ujumbe mfupi wa meneno ‘sms’ kutoka kwa mtu anayekulikana kwa majina ya Jonathan Lyradu.
Frank amesema alianza kupokea meseji hizo tangu mwezi uliopita ambapo Lyradu amekuwa akimtishia kusitisha pumzi yake hapa duniani.
“Mara ya kwanza nilijua amekosea namba, nikamuuliza anamuhitaji nani, lakini akanitumia meseji nyingine na kunitaja jina langu huku akiendelea kunitisha na kunimwagia mvua ya matusi kwa kweli nilimshangaa kwani simjui mtu huyo,” alisema Frank.
Msanii huyo alisema ametoa taarifa katika Kituo Kidogo cha Polisi Tabata na kufungua jalada TBK/RB/2750/13 TAARIFA.
Katika utafiti wa awali uliofanywa na polisi wakati wa kumsaka mtu huyo anayemtishia maisha Frank anaonekana katika mitandao kuwa ni mkazi wa maeneo ya Magomeni, Sinza na Bamaga, Mwenge jijini Dar.
DIAMOND AFUTURU NA KIMADA!
HIVI karibuni mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenaswa akifuturu na hawara yake, Penniel Mungilwa ‘Penny’, kitendo ambacho kimewashangaza wengi na baadhi kufikia hatua ya kumponda kuwa anakwenda kinyume na Uislam.
Tukio hilo lilijiri nyumbani kwa Diamond maeneo ya Sinza- Mori jijini Dar ambapo mbali na mastaa hao, pia walikuwepo waumini wengine wa dini hiyo walioalikwa katika chakula hicho kitakatifu.…
Na Musa Mateja
HIVI karibuni mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ amenaswa akifuturu na hawara yake, Penniel Mungilwa ‘Penny’, kitendo ambacho kimewashangaza wengi na baadhi kufikia hatua ya kumponda kuwa anakwenda kinyume na Uislam.
Wakizungumza na gazeti hili mara baada ya kumuona Penny ambaye ni demu wa Diamond akiwa eneo hilo, baadhi ya waumini walisema walishangazwa na uwepo wake kwani sheria ya dini ya Kiislam hairuhusu kuwa karibu na kimada hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
“Huyu kijana kafanya jambo zuri la kuwafuturisha wenzake ila amekosea kumualika yule mwanamke wake, yule kwake ni kimada na kwa sheria za dini yetu huruhusiwi kabisa kumkaribia, sasa ona wanafuturu pamoja na wanashikanashikana, ile siyo sawa,” alisema muumini mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.
“Kihalali kwanza anatakiwa amsilimishe kisha amlipie mahari ndipo amuoe lakini kinyume na hapo atakuwa anaishi na hawara na kuwa naye karibu ni kujichumia dhambi anazoweza kuziepuka.”
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya mashehe wenye heshima kubwa Tanzania nao walionesha kukerwa na kitendo alichokifanya Diamond na kusema kinakiuka maadili ya dini yao.
Walisema, mwanamke ambaye hajaolewa anayeishi au kuwa karibu na mwanaume na wakati mwingine kuzini, huyo ni kimada na hana nafasi kwenye Uislam.
Huyu ni Katibu Mkuu wa Taasisi ya Mashehe na Wanazuoni Tanzania anasema: “Lengo la swaumu ni kumfanya mtu kuwa Mchamungu na Mchamungu ni yule anayefanya yale aliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu na kuacha aliyokatazwa.
“Katika Uislam kuwa na hawara inakatazwa, si kwa kipindi hiki tu cha Mwezi Mtukufu bali hata baada. Kwa hiyo kufuturu na hawara ni kinyume na Uislam na unapata dhambi.”
Ni Mnajimu maarufu nchini. Yeye anasema kuwa, hawara hakubaliki kidini hivyo hatakiwi kupika futari wala kuwa naye karibu kwa namna yoyote, kufanya hivyo ni kwenda kinyume na taratibu za funga na maadili ya Uislam.
Shekh Alhad Musa Salum
Huyu ni Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Kuhusiana na hili la Diamond la kufuturu na Penny anasema kuwa, uhawara hauruhusiwi katika Uislam na wanaoendekeza hilo waache mara moja ili waweze kupata radhi za Mwenyezi Mungu.
Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Shaaban Simba hivi karibuni aliwasihi Waislam kutimiza nguzo hiyo muhimu ya Uislam na kuwataka wahakikishe wanafuata sheria na taratibu zilizowekwa ili waweze kufikia lengo la kufunga.