This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Saturday, September 28, 2013
MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE AZURU NEBRASKA NCHINI MAREKANI
MBUNGE MSIGWA AMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA MKAKATI WAKE WA KUPAMBANA NA UJANGILI , ASEMA YUPO TAYARI KUWATAJA WANAOTUMIA AMBULENCE KUSAFIRISHA PEMBE ZA NDOVU IRINGA
| Mwenyekiti wa MANET Bw Zuberi Mwachura kulia akieleza mkakati wa kupambana na vitendo vya ujangili katika hifadhi ya taifa ya Ruaha leo |
| Mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akifafanua jambo |
MBUNGE wa jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (chadema), Mchungaji Peter Msigwa amempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa mkakati wake wa kunusuru vitendo vya ujangili katika hifadhi za Taifa.
Kuhusu watu maarufu mkoani Iringa wanaojihusisha na biashar a ya pembe za ndovu na hata kutumia magari ya umma kama Ambulence kusafirisha pembe hizo za ndovu alisema kuwa ana idadi yao ndevu zaidi na kuwa katika kikao cha bunge kijacho ataweka hadharani majina yao.
Kiongozi wa wanaharakati wa mtandao wa kupambana na vitendo vya ujangili katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha Fundi Mihayo alisema kuwa mbinu mbali mbali zinatumika katika kusafirisha pembe za ndovu ikiwa ni pamoja na usafiri wa boda boda kutumika sasa kuendeshea vitendo vya ujangili .
Alisema usafiri huo umekuwa ukitumika kuvushia pembe za ndovu katika maeneo ya vizuizi na hivyo kutaka ulinzi na upekuzi mkubwa unahitajika katika kukomesha vitendo hivyo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa MANET Zuberi Mwachura alisema kuwa lengo la mtandao huo ni kuendelea kupambana na vitendo vya ujangili katika maeneo ya hifadhi nchini .
Kwani alisema kuwa usalama wa wanyama pori na mazingira yao ni walazima kwa maendeleo yetu hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kujua na kufahamu eneo ambalo wanatoka au wanaishi watu wanao fanya au kushiriki au kujihusisha na vitendo vya ujangili ni jukumu letu kuhamasisha jamii ya wananchi wote wajione wana wajibu wa kushiliki katika vita dhidi ya ujangili.
“..lazima tukubali kwamba ujangili upo, Pamoja na changamoto zake, lakini hatuwezi kukaa kimya tukiacha majangili waendelee kuteketeza tembo wetu. …. Mwanzo wa mafanikio katika jambo lolote ni dhamila na nidhamu, ya kupanga na kutekeleza. ….. Kwa kukubaliana katika nia hii ya kupambana na ujangili ni vizuri tuwe na tamko la dhamira yetu ya kujinasua katika Lindi Kubwa la ujangili wa Tembo”
Ulimboka, Costa na Pawasa wachambua uchezaji Simba
RECHO ATUPIA NUSU UTUPU
Picha hiyo ambayo Recho amevaa shati tupu (inayoonesha ndani) bila kuvaa kitu kingine chochote, aliitupia kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo mashabiki na marafiki zake walichangia huku wakimlaumu kuwa hakufanya vizuri kuiweka picha hiyo ya aibu mtandaoni.
Paparazi wetu alimuuliza Recho kulikoni? Akajibu…
Stori: Gladness Mallya
MSANII wa filamu za kibongo, Rachel Haule ‘Recho’ hivi karibuni aligeuka kituko baada ya kutupia picha ya nusu utupu katika mtandao wa kijamii.
Picha hiyo ambayo Recho amevaa shati tupu (inayoonesha ndani) bila kuvaa kitu kingine chochote, aliitupia kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo mashabiki na marafiki zake walichangia huku wakimlaumu kuwa hakufanya vizuri kuiweka picha hiyo ya aibu mtandaoni.
Paparazi wetu alimuuliza Recho kulikoni? Akajibu hivi:
“Nawapenda sana marafiki zangu lakini mimi sijaona tatizo la hii picha kwa sababu ni ya kawaida sana sioni ubaya wake.”
MAADHIMISHO YA MIAKA 18 YA KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU YAFANYIKA DAR
Kwaya iitwayo Mwalusanya inayoundwa na wafanyakazi wa kituo hicho, ikitumbuiza wakati wa maadhimisho hayo.…
Maadhimisho ya miaka 18 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) yalifanyika juzi Septemba 26, jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na waasisi wa kituo hicho, wanachama, wanafunzi wa baadhi ya shule za Sekondari na msingi, viongozi wa dini na serikali na wadau wengine.
Wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika Makao Makuu ya LHRC, Kijitonyama, mmoja wa waasisi wake, Dr. Ringo Tenga alielezea historia ya kituo hicho kilichoanzishwa 1995 ambapo lengo lake ni kupambana na matukio ya uvunjivu wa haki za binadamu.
Mkurugenzi wa kituo hicho, Dr. Hellen Kijo-Bisimba akizungumza wakati wa maadhimisho hayo alisema licha ya kukumbana na changamoto nyingi, kituo chao kimepata mafanikio mengi.
Aliyetaja baadhi ya mafanikio hayo kuwa ni kuweza kuwatetea watu ambao kwa namna moja au nyingine hawakutendewa haki.
Mmoja wa watu aliyekuwa wa kwanza kutetewa na kituo hicho alikuwa marehemu Adam Mwaibabile aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Nipashe na Radio One mkoani Ruvuma.
Alisema baada ya mwandishi huyo kufungwa kwa uonevu, walikwenda Ruvuma ambapo walimpigania na kufanikiwa kumtoa katika kifungo alichohukumiwa na matukio mengine.
Kuhusu changamoto wanazokutananazo alisema ni kunyimwa vibali vya kufanya kazi na baadhi ya watendaji wa serikali wanapokwenda mikoani, kuitwa wanasiasa wa Chadema, chama cha kidini nk.
Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio yaliyojiri wakati wa maadhimisho hayo.
SEMINA YA KAMATA FURSA TWENDZETU KWA VIJANA INAVYOENDELEA JIJINI MWANZA




Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), Bi. Magreth Chacha alipokuwa akiwasili kwenye semina ya kamata fursa Twendzetu, ndani ya ukumbi Gold Crest, jijini Mwanza asubuhi hii.

Naibu Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Mh. Januari Makamba akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mh Stephen Masele (mwenye miwani) akisalimiana na Mkurugenzi wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB),Bi.Magreth Chacha walipokuwa wakiwasili kwenye semina ya kamata fursa Twendzetu, ndani ya ukumbi Gold Crest, jijini Mwanza asubuhi hii,pichani kati ni Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji Clouds Media Group, Bw. Ruge Mutahaba.

Baadhi ya Wakazi wa mji wa Mwanza na vitongoji vyake wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwenye semina ya kamata fursa Twendzetu, ndani ya ukumbi Gold Crest, jijini Mwanza asubuhi hii.

Tuesday, September 24, 2013
TIMU YA NETIBOLI YA UTUMISHI YAICHARAZA UJENZI MABAO 48-5
Timu ya Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma ikisalimiana na timu ya Wizara ya Ujenzi kabla ya mechi leo.
Timu ya Netiboli ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma imeendelea kufanya vizuri katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) kwa kuifunga timu ya netiboli ya Wizara ya Ujenzi mabao 48-5 katika mchezo uliofanyika kwenye viwanja vya Chuo Kikuu Dodoma leo mchana.
Katika mechi hiyo,timu ya Utumishi ilionekana kuumiliki mchezo kwa kiasi kikubwa kitendo kilichopelekea wachezaji wa timu ya Wizara ya Ujenzi kutokujiamini na hatimaye kupoteza mabao yao kwa wingi katika dakika ishirini za mwanzo ambapo Utumishi ilifunga mabao 12 kupitia mchezaji wake Fatma Ahmed (GS) na mengine 11 kupitia mchezaji wake Anna Msulwa (GA).
Timu ya Wizara ya Ujenzi ilitumia mbinu mbalimbali kurudisha mabao lakini ilifanikiwa kufunga bao 1 kupitia mchezaji wake Kaundime Kizaba (GA).
Kipindi cha pili cha mchezo huo Utumishi iliendelea kwa kasi ileile na kufanikiwa kuifunga timu ya Wizara ya Ujenzi mabao 25 huku Ujenzi ikifunga mabao 4.
Akiongea mara baada ya mchezo huo Kocha wa timu ya Wizara ya Ujenzi Bw.Abilai Ally alisema kuwa timu yake imejitahidi sana katika kiwango chake kwa kuwa ni timu changa.
“Mchezo ni mzuri lakini timu yetu bado ni changa kimashindano na ni mara ya kwanza kushiriki mashindano haya” alisema Bw.Ally.
Aidha,alifafanua kuwa timu hiyo ina upungufu wa wachezaji kitendo kilichopelekea kuelemewa na mchezo na kufungwa mabao mengi.
Naye mchezaji wa timu ya Utumishi Bi.Amina Ahmed (GD) alisema kuwa mchezo umeonekana mzuri kwa upande wa timu ya Utumishi kwa sababu kila mchezaji ametumia nafasi yake vizuri kwa kucheza inavyotakiwa.
Timu ya Utumishi yenye lengo la kunyakua ubingwa katika mechi zijazo imeendelea kujinoa zaidi ili kufikia lengo huku ikihakikisha haipotezi mchezo wowote katika michezo ya SHIMIWI inayoendelea mjini Dodoma.



















