This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Sunday, July 14, 2013

MKUU WA MKOA MOROGORO AFUNIKA KWA KUCHEZA KWAITO UKUMBINI

Stori:Dustan Shekidele,Morogoro

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera juzikati alionyesha wananchi wake umahiri mkubwa wa kuucheza muziki mtindo wa Kwaito huku akiwafunika vibaya vigogo wa Benki ya NMB Mkoa wa Morogoro waliokuwa wakicheza naye.
Hapa Akikonga kwaito na wazee wenzake
Bendera alionyesha umahiri huo ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Morogoro kwenye sherehe kabambe ya kumuaga aliyekuwa Meneja wa Benki ya  NMB Tawi la Wami aliyefahamika kwa jina moja tu la Bushiri aliyehamishiwa Wilaya…
Stori:Dustan Shekidele,Morogoro
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera juzikati alionyesha wananchi wake umahiri mkubwa wa kuucheza muziki mtindo wa Kwaito huku akiwafunika vibaya vigogo wa Benki ya NMB Mkoa wa Morogoro waliokuwa wakicheza naye.
Hapa Akikonga kwaito na wazee wenzake
Bendera alionyesha umahiri huo ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Morogoro kwenye sherehe kabambe ya kumuaga aliyekuwa Meneja wa Benki ya  NMB Tawi la Wami aliyefahamika kwa jina moja tu la Bushiri aliyehamishiwa Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro ambapo mkuu wa mkoa alisakata Kwaito kwa mbwembwe nyingi.
“Hakika Bendera ni mwanamichezo, kumbe siyo kwenye soka tu bali hata kwenye dansi yumo, umeona pale ni kama wanashindanishwa lakini kama ni ushindi basi angepewa yeye,” alisikika akisema mwalikwa mmoja aliyejitambulisha kwa jina na John Sheki.
Licha ya kuwa mwanasiasa na kuonesha umahiri wa kucheza dansi, Bendera aliwahi kuwa Kocha wa Timu ya Taifa, Taifa Stars mwaka 1983 hadi 1986 na akawa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mpira wa Miguu (FAT) mwaka1978 hadi 1979.
Sherehe hiyo iliyofana ilihudhuriwa na wafanyakazi wa matawi yote ya NMB Mkoa wa Morogoro na baadhi ya wateja wa benki hiyo ambao walikuwa wageni waalikwa na ilianza saa 2 usiku ikafika tamati saa 6 usiku huku gumzo likiwa ni usakataji wa Kwaito wa Bendera.

RAY C AFUTUKA

Stori: Mwandishi  Wetu
Mwanamuziki staa wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye amepotea katika anga la muziki kwa kipindi kirefu kutokana na matatizo ya matumizi ya madawa ya kulevya, amejitokeza akiwa amefutuka.
Hivi karibuni, Ray C ameibuka na kuanza kutundika picha na vipande vya video zake katika kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii, ikiwa ni sehemu ya kujiweka karibu na mashabiki wake.
Kufuatia ishu hiyo, kumeibuka mshtuko mkubwa kwa baadhi ya watu kutokana na picha hizo kumuonesha ‘bidada’ akiwa amenenepeana ghafla tofauti na alivyozoeleka.

UNENE UNATOKANA NA DOZI?
Baadhi ya mashabiki wake katika mtandao wa Instagram walidai kuwa inawezekana unene huo unatokana na dozi ya kuacha ‘unga’.
Hata hivyo, wengine walimshukuru Mungu kwa kuwa sasa afya ya mwanadada huyo inaonekana kurudi katika hali yake ya kawaida tofauti na miezi kadhaa aliporipotiwa na gazeti hili akiwa amezimika kutokana na matumizi ya unga.

AFUTUKA
Katika picha hizo, Ray C anaonekana kufutuka usoni, kifuani na mapajani ambapo awali kabla ya matatizo hakuwa hivyo.
Wengi walimshukuru Mungu kumuona tena Ray C akiwa mzima pamoja na ukimya wake katika muziki.
Ray C amekuwa akitundika picha hizo kwa ajili ya mashabiki na marafiki hasa kupitia Instagram akiambatanisha na maelezo huku nyingine zikizungumza zenyewe.

HATAKI KUTAJA ANAPOISHI
Maelezo ya picha hizo yamekuwa yakielezea maisha ya Ray C kwa sasa akiwa kwenye mjengo wa maana bila kutaja ni sehemu gani.
Kwa mujibu wa mashabiki wa Ray C, mwanadada huyo kwa sasa anakula bata tu huku akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye anamuita ‘Daddy’ kwa kuwa ndiye aliyemsaidia kimatibabu.

DAKTARI ANASEMAJE?
Daktari mmoja maarufu jijini Dar aliyehojiwa na gazeti hili, alibainisha kuwa kinachosemwa na mashabiki wa Ray C kwamba kinachomnenepesha ni dozi ya kuacha madawa ya kulevya, kinaweza kuwa kweli au kisiwe kweli.
Aliongeza kuwa kunenepa kunachangiwa na vitu vingi kama kupata maisha mazuri yasiyohusisha msongo wa mawazo au mihangaiko ya hapa na pale hivyo anachofanya ni kula, kulala na kustarehe tu.

SHEIKH MKUU WA WILAYA YA ARUMERU AMWAGIWA TINDIKALI NA KUUMIZWA VIBAYA



Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Said Juma Makamba amejeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa maji yanayohisiwa kuwa tindikali na watu wasiojulikana juzi usiku akiwa nyumbani kwake jijini Arusha.

Shekhe Makamba, ambaye amelazwa katika Wodi ya Majeruhi kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, amejeruhiwa vibaya maeneo ya usoni, kifuani na mgongoni huku akiendelea na matibabu.

Akizungumza kwa tabu, shekhe huyo alisema tukio hilo lilitokea saa 5 usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake kwa Mromboo Arusha, wakati akijiandaa kulala baada ya kutoka kuswali Swala ya Tarawei.

Shekhe Makamba ambaye pia ni Imamu wa Msikiti wa Sekei mjini Arusha, alisema baada ya swala hiyo alirejea nyumbani kwake akisindikizwa na vijana wawili ambao walikuwa wakiswali pamoja na kuingia ndani ya nyumba yake ili kulala.

Alisema hata hivyo, kabla ya kulala alikwenda kujisaidia katika choo cha nje na kwamba wakati akirudi ili aingie ndani akipitia nyuma ya nyumba ghafla alimuona mtu akiwa amesimama jirani na mlango.

Alieleza kuwa wakati akitaka kumwangalia zaidi alishtukia mtu
huyo akiinua mkono na kumwagia maji yaliyompatia maumivu makali usoni na kifuani.


‘’Wakati natoka msalani nikipitia uwani kwangu niliona kama mtu ameinama pembeni yangu wakati najaribu kumsogelea ili nijue ni nani nilihamaki mtu huyo akinimwagia maji yaliyonisababisha maumivu makali sana yenye asili ya moto na ngozi kuanza kubabuka,’’ alisema shekhe huyo.

Aliongeza kuwa baada ya tukio hilo alianza kupiga kelele kuomba msaada ambapo majirani walijitokeza na kumpa msaada wa kumpeleka hospitali, kwa vile wakati huo macho yake yalikuwa hayaoni na wakati wote alikuwa  akilia.

Pamoja na kujeruhiwa vibaya sehemu za usoni, kifuani na  mgongoni, pia ana majeraha  kwenye mikono na machoni na hali yake bado ni mbaya japo madaktari wanaendelea kumpatia matibabu.

Kaimu Katibu wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Abdallah Masoud akizungumzia tukio hilo alieleza kushitushwa nalo akisema limefanana na lile la Katibu wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Abdulaziz Jonjo ambaye mwaka jana alilipuliwa kwa bomu nyumbani kwake akiwa amelala.

Alisema kuwa matukio hayo yamekuwa yakijirudia huku wahusika wakishindwa kutiwa mbaroni na kudai kuwa matukio hayo yanahusiana na masuala ya kigaidi. Aliongeza kuwa pamoja na kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi, lakini wamekuwa hawapati matunda ya kukamatwa kwa watuhumiwa ingawa alisema wanajulikana.

Kwa upande wake,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi wameanza uchunguzi wa tukio hilo na kwamba taarifa zitatolewa pindi washukiwa watakapotiwa mbaroni kwani uchunguzi bado unaendelea na kwamba hakuna  mtu anayeshikiliwa hadi sasa.


Thursday, July 11, 2013

UGANDA CRANES YAWASILI KWA MPAMBANO WA JUMAMOSI

Mashabiki wa Uganda waliofika uwanjani kuipokea timu yao.

Wachezaji wa The Cranes walipowasili.
Kocha Sledojovik Micho na msaidizi wake, Sam Timbe, wakiwai na kikosi hicho.…
Mashabiki wa Uganda waliofika uwanjani kuipokea timu yao.
Wachezaji wa The Cranes walipowasili.
Kocha Sledojovik Micho na msaidizi wake, Sam Timbe, wakiwai na kikosi hicho.
Wakiingia kwenye basi waliloandaliwa.
Mwenyekiti wa Waganda wanaoishi Tanzania, Hellen Tusiime,  alikuwa mkuu wa mapokezi hayo.
Wakiwa tayari kwa safari kuingia jijini.
TIMU ya taifa ya Uganda (The Cranes)  mchana huu imewasili uwanja wa ndege Dar es Salaam kwa ajili ya kujiwinda kwa mchezo wao dhidi ya timu ya taifa  (Taifa Stars) unaotarajiwa kufanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumamosi hii.

PICHA : RICHARD BUKOS / GPL  

SHUGHULI MBALIMBALI ZA RAIS KIKWETE IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO JULY 11, 2013

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Balozi wa Sweden nchini Mhe Lennarth Hjelmaker aliyeonana naye kwa ajili ya kuwasilisha Ujumbe kutoka Serikali yake leo Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Balozi wa Sweden nchini Mhe Lennarth Hjelmaker aliyeonana naye kwa ajili ya kuwasilisha Ujumbe kutoka Serikali yake leo Ikulu, jijini Dar es Salaam.…
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Balozi wa Sweden nchini Mhe Lennarth Hjelmaker aliyeonana naye kwa ajili ya kuwasilisha Ujumbe kutoka Serikali yake leo Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Balozi wa Sweden nchini Mhe Lennarth Hjelmaker aliyeonana naye kwa ajili ya kuwasilisha Ujumbe kutoka Serikali yake leo Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana  na Balozi wa Sweden nchini Mhe Lennarth Hjelmaker aliyeonana naye kwa ajili ya kuwasilisha Ujumbe kutoka Serikali yake leo Ikulu, jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mhe Hamisi Amir Msumi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili la Viongozi wa Umma leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mhe Hilda A. Gondwe kuwa Mjumbewa Baraza la Maadili la Viongozi wa Umma leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimuapisha Mhe Celina Augustine M. Wambura kuwa Mjumbe wa Baraza la Maadili la Viongozi wa Umma leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali wakipiga picha ya pamoja na Mwenyekiti mpya wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Serikali Mhe Hamisi Amiri Msumi pamoja na wajumbe wapya Mhe Hilda A. Gondwe na Mhe Celine Augustine M. Wambura na viongozi wa Tume hiyo leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
(PICHA NA IKULU)

UGANDA CRANES YAWASILI KUIKABILI STARS


Kikosi cha Timu ya Taifa ya Uganda 'The Cranes'.
Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) imewasili Dar es Salaam leo tayari kwa mechi ya kwanza ya mchujo kusaka tiketi ya Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani (CHAN) kati yake na Tanzania (Taifa Stars) itakayochezwa Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

The Cranes inayofundishwa na Mserbia Sredojvic Micho imetua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 5.30 asubuhi kwa ndege ya Air Uganda, na imefikia hoteli ya Sapphire.

Timu hiyo leo (Julai 11 mwaka huu) itafanya mazoezi saa 9 alasiri kwenye Uwanja wa Karume, wakati kesho saa 9 alasiri itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, kabla ya kuipisha Taifa Stars itakayoanza…
Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) imewasili Dar es Salaam leo tayari kwa mechi ya kwanza ya mchujo kusaka tiketi ya Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani (CHAN) kati yake na Tanzania (Taifa Stars) itakayochezwa Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
The Cranes inayofundishwa na Mserbia Sredojvic Micho imetua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 5.30 asubuhi kwa ndege ya Air Uganda, na imefikia hoteli ya Sapphire.
Timu hiyo leo (Julai 11 mwaka huu) itafanya mazoezi saa 9 alasiri kwenye Uwanja wa Karume, wakati kesho saa 9 alasiri itafanya mazoezi Uwanja wa Taifa, kabla ya kuipisha Taifa Stars itakayoanza mazoezi saa 10 kamili jioni.
Taifa Stars inayofundishwa na Mdenmark Kim Poulsen, na kudhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, leo kwa mujibu wa program yake haitakuwa na mazoezi.
Wachezaji wanaounda The Cranes ni makipa Ismail Watenga, Kimera Ali na Muwonge Hamza. Mabeki ni Guma Dennis, Kasaaga Richard, Kawooya Fahad, Kisalita Ayub, Magombe Hakim, Malinga Richard, Mukisa Yusuf, Savio Kabugo na Wadada Nicholas.
Viungo ni Ali Feni, Birungi Michael, Frank Kalanda, Hassan Wasswa, Kyeyune Said, Majwega Brian, Mpande Joseph, Muganga Ronald, Ntege Ivan, Owen Kasule, wakati washambuliaji ni Edema Patrick, Herman Wasswa na Tonny Odur.

MAMA MZAZI WA PROFESA JAY AGONGWA NA GARI NA KUFARIKI DUNIA....


Picha kushoto ni Profesa J akiwa na mama yake mzazi Bi Rosemary Majanjara Haule enzi za uhai wake...
 
Mama  mzazi  wa  Msanii Profesa Jay  amefariki dunia  usiku  wa  kuamkia  leo  baada  ya  kugongwa  na  gari  maeneo  ya  mbezi  juu  jijini  Dar  alikokuwa  anaishi  na  mwanae.


Habari  zinadai  kwamba, marehemu Bi. Rosemary Manjara  Haule  aligongwa na gari akiwa  anavuka barabara kuelekea  dukani  mida ya saa mbili  na  kwamba  baada  ya  kugongwa  wasamaria  wema walimkimbiza  hospitali  ya  Tumbi  kwa  kutumia  bajaji ambako  mauti  ilimkuta  huko

Profesa  Jay  amethibitisha   hilo  na  kudai  kwamba  ilikuwa  ni  vigumu  sana  kuamini.Mama  yake  alimpigia  simu  na  kumwambia  kuwa  kagongwa  na  gari  na  kwamba  yuko  polisi.Ghafla  simu  yake  ikawa  haipatikani...


Profesa  anasema  kwamba  wakati  anapigiwa  simu  alikuwa  katika  mgahawa  wa  nyumbani  lounge,Namanga Dar  ambako  alikuwa  katika  kikao  na  Lady  jaydee  na  mumewe.

"MAMA ALINIAMBIA MWANANGU NIMEGONGWA NAGARI....NJONI KOPOLISINAANDIKISHA....   MWANANGU NAKUFA....  ALINIAMBIA MAMA NA MARA SIMU IKAKATIKA. KILA NILIPOJARIBU KUPIGA IKAWA HAIPATIKANI..." ALISEMA PROFESA J KWA UCHUNGU. 

Mungu  ailaze  roho  ya  marehemu  mahali  pema  peponi.