
This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Thursday, May 2, 2013
Tuesday, April 30, 2013
PADRI WA KANISA KATOLIKI HUKO MOSHI AFUMANIWA LIVE NA MKE WA MTU AKIWA UCHI WA MNYAMA
Pamoja na kunaswa huko, vyanzo havijaeleza humo chumbani wawili hao walikuwa wakifanya nini!
Habari zinadai siku ya tukio, mwanamke huyo aliingia nyumbani kwa padri huyo ambapo baadhi ya ndugu wa mumewe walikuwa wakimfuatilia baada ya madai yaliyokuwepo kwamba ana ukaribu wenye maswali mengi na mtumishi huyo wa Mungu.
“Unajua siku nyingi ilivuma kwamba Mama P na Father Ngowi wana ukaribu wenye maswali mengi, mume wake alifuatilia na kubaini ni kweli lakini akashindwa kuutenganisha ukaribu wao,” kilidai chanzo.
Chanzo: Sasa siku hiyo baada ya ndugu wa mume kumfuatilia mpaka anaingia kwa Father Ngowi, wakaona ni bora watafute mpigapicha ili kupata picha za tukio ambazo zitakuwa ushahidi siku za mbele.
“Walipompata wakazama ndani, sekeseke likaanzia hapo. Walimkuta mwanamke huyo na mtumishi wa Mungu wapo kitandani.”
Habari zinadai kwamba kufuatia tukio hilo, tayari Kanisa Katoliki limemweka kitimoto padri huyo ambaye alikuwa akihudumu katika Parokia ya Korongoni, Moshi Vijijini kabla ya kuhamishwa na kupelekwa Parokia ya Makomu, Marangu ambako inadaiwa ameshushwa cheo.
Inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo, Father Ngowi alikana kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake lakini alipobanwa sana na mabosi wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Moshi, alikiri na kudai ibilisi alimpitia na kuomba kanisa limsamehe na kutompa adhabu kali ambayo itamuathiri kisaikolojia.
Hili ni tukio kubwa na la aina yake kuwahi kulikumba Kanisa Katoliki nchini kwa padri wake kudaiwa kukutwa na mke wa mtu chumbani kwake!
Kuna madai kwamba mwaka jana (2012), Father Ngowi, mbele ya waumini wake alisoma barua yenye kukana shutuma zote zilizoelekezwa kwake kwamba amekuwa na ukaribu wenye maswali mengi na wake za watu.
Taarifa zilidai kuwa padri huyo aliweka wazi akisema si kweli kwamba amekuwa na ukaribu unaotajwa, akawataka waumini wake wapuuze tuhuma hizo alizosema zina mwelekeo wa kuchafua sifa yake na taswira ya Kanisa Katoliki kwa jumla.
Hayo ni madai ya vyanzo vyetu ambavyo viliambatanisha na picha mbalimbali za tukio hilo lenye kushtua waumini sambamba na namba za simu za padri huyo kwa ajili ya mawasiliano ili kujiridhisha.
BAJETI KIPORO WIZARA YA MAJI YATINGA TENA BUNGENI LEO
Bajeti hiyo ilitarajiwa kupitishwa tangu Alhamisi wiki iliyopita, lakini kutokana na ufinyu wa fedha zilizotengwa, takribani wabunge wote waliochangia mjadala wake, wakiwemo wa CCM, waligoma kuiunga mkono.
Pamoja na mjadala wa Bajeti ya Maji kuendelea leo, pia Wizara ya Maliasili na Utalii, inatarajiwa kuwasilisha bajeti yake ya mwaka 2013/2014, itakayojadiliwa kwa siku mbili, ambapo wabunge wengi wanatarajia kuzungumzia suala la mgogoro wa ardhi Loliondo.
MVUA YASABABISHA MAFURIKO JIJINI DAR LEO
"LAZIMA TUZIKAGUE KUCHA ZA LEMA..... TUPO TAYARI KUFA....."HAYA NI BAADHI YA MABANGO YA WAANDAMANAJI HUKO ARUSHA
Mbele ya hakimu Joyce Msofe na mawakili Kimomogoro na Humphrey Mtui wanaomtetea, Lema amesomewa shitaka la kosa la uchochezi linalomkabili kwamba aliwachochea wanafunzi wa chuo cha uhasibu Arusha kumzomea Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kuwaambia wanafunzi kuwa Mkuu huyo wa Mkoa, “hajui chuo cha uhasibu kilipo, amekuja akiwa amechelewa na anaingia hapa kama anaingia kwenye send off.”
Mtuhumiwa alifanikiwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni kuwepo kwa mtu mmoja mwenye kitambulisho kinachokubalika kisheria na kuweka rehani kiasi cha shilingi milioni moja.
Baada ya kutoka mahakamani hapo, Lema alielekea kwenye maeneo ya Ofisi za chama, CHADEMA. kwa maandamano makubwa
MZEE WA KANISA ALIVYOZIKWA HAI
NI zaidi ya ukatili! Katika hali isiyowahi kufikiriwa na binadamu aliyeumbwa na Mungu, baadhi ya vijana wa Kijiji cha Mkwajuni Wilaya ya Chunya, Mbeya wamemzika akiwa hai aliyekuwa msaidizi wa padri, Katekista Flavian Mwamosi Mwachirui (68) wakimtuhumu kusababisha kifo cha Peter Robert (28) mkazi wa kijijini hapo.
Tukio hilo lililoshtua wengi katika eneo hilo lilitokea saa nane mchana wa Ijumaa…
Na Mwandishi Wetu, Chunya
NI zaidi ya ukatili! Katika hali isiyowahi kufikiriwa na binadamu aliyeumbwa na Mungu, baadhi ya vijana wa Kijiji cha Mkwajuni Wilaya ya Chunya, Mbeya wamemzika akiwa hai aliyekuwa msaidizi wa padri, Katekista Flavian Mwamosi Mwachirui (68) wakimtuhumu kusababisha kifo cha Peter Robert (28) mkazi wa kijijini hapo.
Tukio hilo lililoshtua wengi katika eneo hilo lilitokea saa nane mchana wa Ijumaa iliyopita kwenye Makaburi ya Maweni kufuatia kijana Peter kufariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni ndugu wa mzee huyo (jina tunalo) aliweka wazi kwamba, dhambi ya ukatili huo wa kutisha ilianza pale marehemu Peter alipokumbwa na mauti akiwa anatibiwa kwa mganga wa kienyeji ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Simulizi hii ya kweli inaendelea kuwa, wakati ndugu na jamaa wakilia na kuomboleza na ratiba ya maziko ikitangazwa, ndipo baadhi ya ndugu hao wa marehemu waliibuka na kudai eti kifo cha Peter si cha Mungu, kwa sababu kilikuwa na mkono wa binadamu!
Ndugu hao walipoona watu hawawaelewi waliposema marehemu kafa kwa kurogwa, wakaenda mbele zaidi, wakamtaja mzee Flavian Mwamosi Mwachirui ambaye ni katekista mstaafu aliyekuwa akihudumu katika Kigango cha Mkwajuni hadi 2007.
SIKU YA MAZISHI YAFIKA
Madai ya baadhi ya ndugu hao yalinaswa na vijana kadhaa wa kijiji hicho ambao waliapa kwa miungu wao kwamba lazima marehemu wamzike na ‘muuaji’ wake, yaani mzee Mwachirui. Inauma sana!
“Siku ya kumzika Peter, kuna vijana walisikika wakisema marehemu watamzika na mzee Mwachirui tena wakaongeza kuwa watamzika mzee huyo akiwa hai ili aone maumivu ya kifo utadhani walimuona akimuua huyo Peter,” kilisema chanzo huku kikibubujika machozi.
Chanzo kikaongeza: “Watu wa huku wanaishi kwa kutumia akili za waganga wa kienyeji. Mganga akisema unakosa mazao shamba kwa sababu mama yako anakuroga, basi mama huyo atauawa! Mbeya si sehemu salama tena.”
Kaburi la kumzikia marehemu Peter lilimalizika kuchimbwa, vijana waliokuwa wakiliandaa waliagiza wazee wa kimila wafike kwa lengo la kuangalia utaratibu wa mazishi na kukagua ukubwa wa kaburi lenyewe kama lipo sawa.
Wito huo uliwagusa wazee wanne wa kijiji hicho, (masikini ya Mungu) akiwemo Mzee Mwachirui ambaye vijana hao walimsisitiza yeye asogee jirani kabisa na kaburi.
Bila kujua alibakiza sukunde chache za kuishi duniani, mzee huyo alisogea na kuchungulia kaburi ili atoe utafiti wake kwa vijana hao wenye moyo wa kikatili kuliko wanyama wa porini, akiwemo simba anayekula wenzake.
Ilikuwa kufumba na kufumbua, kijana mmoja aliyeshika sururu alimpiga nayo kichwani mzee huyo hali iliyomfanya ayumbe.
Kama vile haitoshi, wapo vijana waliomsindikiza kwa kumpiga na marungu hadi akaangukia kaburini.
MAISHA NDANI YA KABURI
Chanzo kikasema: Masikini mzee wa watu, alijaribu kujiokoa kwa kutaka kutoka kaburini lakini wale vijana wakamwamuru akae, alipokataa alizidi kupigwa.
“Ilifika mahali aliishiwa nguvu huku akijiona. Mbaya zaidi vijana waliokuwa wakimfanyia unyama huo anawajua kwa majina na alijaribu kuwaita mmoja mmoja ili wamwachie lakini wapi!”
Kinachoumiza zaidi, mzee huyo aliingia kaburini na nguo zake, suruali iliyofungwa mkanda mweusi, nguo ya ndani, shati jeupe la mikono mirefu lenye mistari ndani akiwa ametinga ‘singlendi’. Miguuni alikuwa pekuwa.
APOTEZA FAHAMU, WAMWEKEA JENEZA JUU YAKE, WATIA UDONGO
‘Wauaji’ hao walipojiridhisha kwamba mzee huyo hakuwa na uwezo wa kutoka kaburini, walichukua fito wakamfunika nazo kisha wakafukia udongo mchache, juu yake wakaliweka jeneza la marehemu Peter, wakafukia udongo kwa majembe na masepetu mpaka kaburi kukamilika. Ni zaidi ya ukatili uliowahi kufanywa mwaka 2013!
KAMA VILE HAITOSHI
Baada ya kukamilika kwa zoezi la mazishi kundi la vijana lilipiga mbio hadi nyumbani kwa marehemu mzee Mwachirui na kuiteketeza nyumba yake huku wakiapa kuwa, hakuna kutoa siri ya tukio hilo. Walisema walichokifanya ni ‘siri ya jeshi’.
WANAKIJIJI WAKERWA, WAKIMBILIA SERIKALINI
Baada ya tukio hilo, baadhi ya wananchi walikimbia hadi kwa Mwenyekiti wa Kijiji, Credo Kayanza na kumpa ripoti ya unyama huo.
Naye mwenyekiti alipoona ni unyama uliopita kiwango cha ubinadamu alishika njia hadi kwa diwani wa kata hiyo, Chesco Ngairo ambapo wote kwa pamoja walikimbia hadi Kituo cha Polisi Mkwajuni na kusema yote huku wakiomba maafande wenye uwezo wa kivita kufika kijijini hapo kushughulikia hali hiyo.
KABURI LAFUKULIWA
Polisi walifika kijijini hapo kwa spidi ya ndege ya kijeshi na kukuta tukio likiwa bichi, wakawaamuru baadhi ya vijana kulifukua kaburi hilo zoezi ambalo lilifanyika baada ya vijana hao kulipwa fedha!
Baada ya kufukua kaburi,
jeneza la marehemu Peter ndilo lililoanza kutolewa na kuwekwa pembeni, zikafuata fito kisha mwili wa marehmu mzee Mwachirui ambao uliwekwa pembeni pia.
Polisi wakaamuru mwili wa Peter uzikwe, wao wakaondoka na mwili wa mzee Mwachirui hadi Hospitali ya Misheni ya Mkwajuni kwa ajili ya uchunguzi na kujiridhisha juu ya kifo chake.
Madaktari waliokuwa zamu walithibitisha kuwa, mzee huyo alishaaga dunia, hivyo ndugu wakakabidhiwa mwili huo kwa ajili ya
kwenda kuuzika sehemu nyingine lakini katika makaburi alikozikwa Peter.
HUYU HAPA KAMANDA WA POLISI MBEYA
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, pia ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kuamini mambo ya ushirikina na uchawi kwa madai kuwa hakuna faida zaidi ya kuchochea migogoro.
MADAI YA NYUMA
Kwa miaka mingi, marehemu mzee Mwachirui na wenzake wawili ambao majina yao hayakutajwa walikuwa wakituhumiwa kwa vitendo vya kishirikina licha ya kwamba hakuna aliyewahi kuona matukio yao laivu au kuwa na ushahidi mkononi.
HAMMER Q AMTOA MANUNDU MKEWE BAADA YA UTAMBULISHO WA TX MOSHI
Hiki ni kipigo ambacho Salha alikipata baada ya kumtambulisha rafiki yake wa kiume ambae ni Tx Moshi kwa mumewe Hammer Q.
Baada ya utambulisho huo....sinema ya ngumi na mateke ilianza....


















