This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.
Friday, March 29, 2013
MSANII MAARUFU AMFUMANIA,ANYWA SUMU
MCHEKESHAJI wa Kundi la Mizegwe, Rashid Coster ‘Maringo Saba,’ anadaiwa kumfumania mkewe anayefahamika kwa jina la mama Zai kisha kuamua kunywa sumu ikisemekana kuwa alitaka kujiua kwa hasira.
Chanzo makini kilichoomba hifadhi ya jina kimenyetisha kuwa, Maringo Saba aliandaa mtego wa fumanizi baada ya kuhisi mkewe anamsaliti kwa rafiki yake anayefahamika kwa jina moja la Sam.
Chanzo hicho kilizidi kushuka na mistari kwamba, baada ya staa huyo kuandaa mtego, ulizaa matunda Jumatano ya Machi 20, mwaka huu ambapo alimfumania mkewe akijivinjari na jamaa.
Sosi huyo alizidi kubainisha kuwa, mke wa Maringo Saba alipoona mumewe amemjazia umati kwa fumanizi hilo, alitimua mbio kwa vile ilidaiwa Maringo Saba alitishia kumfanyia kitu mbaya.
“Ilikuwa vurumai,…
MCHEKESHAJI wa Kundi la Mizegwe, Rashid Coster ‘Maringo Saba,’ anadaiwa kumfumania mkewe anayefahamika kwa jina la mama Zai kisha kuamua kunywa sumu ikisemekana kuwa alitaka kujiua kwa hasira.
Chanzo makini kilichoomba hifadhi ya jina kimenyetisha kuwa, Maringo Saba aliandaa mtego wa fumanizi baada ya kuhisi mkewe anamsaliti kwa rafiki yake anayefahamika kwa jina moja la Sam.
Chanzo hicho kilizidi kushuka na mistari kwamba, baada ya staa huyo kuandaa mtego, ulizaa matunda Jumatano ya Machi 20, mwaka huu ambapo alimfumania mkewe akijivinjari na jamaa.
Sosi huyo alizidi kubainisha kuwa, mke wa Maringo Saba alipoona mumewe amemjazia umati kwa fumanizi hilo, alitimua mbio kwa vile ilidaiwa Maringo Saba alitishia kumfanyia kitu mbaya.
“Ilikuwa vurumai, watu waliokusanyika kufanya fumanizi walimtembezea kichapo Sam kabla hajafanikiwa kuchoropoka kwenye himaya ya chumba hicho na kujisalimisha katika Kituo cha Polisi Mwananyamala CCM,” kilisema chanzo.
Chanzo kingine kilicho karibu na mchekeshaji huyo (jina lipo) kilidai kuwa, baada ya tukio hilo, Maringo Saba alikutwa chumbani kwake amezidiwa ndipo ndugu zake walipomkimbiza kwenye Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa za madaktari, imedaiwa kuwa staa huyo alikutwa na kiasi kikubwa cha sumu mwilini ambayo haikujulikana mara moja ni ya aina gani.
Mara baada ya taarifa hizo kutua kwenye dawati la Amani, waandishi wetu walifika Hospitali ya Mwananyamala na kumkuta mchekeshaji huyo akiwa amewekewa dripu za dawa huku ndugu zake wakisema jamaa alichanganya pombe na dawa na siyo sumu kama ilivyodaiwa.
“Ndugu yetu hakunywa sumu, alichanganya dozi ya malaria na pombe ndiyo maana alizidiwa ghafla,” alisema mmoja wa ndugu hao aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Khalfan.
Hata hivyo, maelezo ya Rashid yalipingana na ya baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo ambao kwa sharti la kutoandikwa majina yao gazetini walikiri msanii huyo kukutwa na sumu mwilini.
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwinjuma, Allen Mwakitalima alikiri kuwepo kwa fumanizi, lakini kuhusu kunywa sumu alisema alisikia kwa watu mtaani ingawa kwake hajafikishiwa taarifa rasmi.
“Habari za fumanizi kwa Maringo Saba lilifika kwangu kiofisi, hata polisi walishakuja kuniulizia, ila kuhusu kunywa sumu nilisikia kwa watu mtaani, lakini sijapata taarifa rasmi kutoka kwa mjumbe wake, kwa hiyo likinifikia nitalishughulikia kiofisi,” alisema mwenyekiti huyo.
Thursday, March 28, 2013
MENEJA WA KAMPUNI YA NDEGE YA FASTJET ATIWA MBARONI
Katuga alidai Machi 19 mwaka huu Emma alimtolea lugha ya matusi Samson Itinde jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Emma alikana shtaka hilo ambapo Katuga alidai upelelezi umekamilika na kuomba kupangiwa tarehe kwa usikilizwaji wa awali.
MBUNGE WA CHAMBANI (CUF) AFARIKI DUNIA
Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF), Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis afariki dunia. Mbunge huyo alianguka jana ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao chake.
MACHANGUDOA WAJIUZA MBELE YA NYUMBA YA WAZIRI MKUU....
Wiki iliyopita, waandishi wetu waliwanasa machangudoa hao wakiwa wanazurura kwenye Barabara ya Kenyatta inayopita mbele ya makazi ya waziri mkuu takriban mita 80 kutoka barabarani kwa lengo la kujiuza.
Ili kulijua hilo kwa undani, waandshi wetu walijifanya wateja kabla ya kuwapiga picha ili kuweza kuzungumza nao mawili matatu kuhusu kuwepo eneo hilo lenye heshima zake.
Mmoja wa ‘wauza sukari’ hao aliyejitambulisha kwa jina la Hawa, mkazi wa Kinondoni, alikiri yeye na wenzake kufanya biashara hiyo kwenye eneo hilo.
“Ni kweli mimi na wenzangu tunapiga kambi eneo hili, huwa ikifika usiku tunaanzia kule Coco halafu tunakuja hadi huku, lakini mbona maswali mengi, unataka tufanye biashara kama vipi sepa,” alisema changu huyo akianza kupandisha jazba.
Kikubwa walichokiongea machangu hao walisema barabara hiyo yote hupitwa na viongozi wakubwa na wafanyabishara ambao baadhi yao ni wateja wao wakubwa. Wakasema hawamwamini sana mteja anayekwenda na Bajaj au Bodaboda kwa vile wanasumbua kutafuta eneo la kufanyia ngono.
“Wateja wetu wengi ni wale tunaomalizana ndani ya gari, hawa wa Bajaj na Bodaboda wengi wanataka kwenye majani, ni rahisi kukamatwa na polisi wa doria,” alisema changudoa mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Suzy lakini hakuwa tayari kutaja yaliko makazi yake.
Inakuwaje wauza miili hao watanue eneo ambalo kimazingira linapitiwa na viongozi mbalimbali wazito kama vile mabalozi wa nje waliopo Tanzania, mawaziri, akiwemo waziri mkuu mwenyewe ambaye ni jirani kabisa na makazi yake?
Yapo madai kwamba, askari wanaovalia mavazi ya kiraia ambao wanapaswa kuhakikisha usalama wa eneo lote la Coco Beach wanakaushia matendo hayo kwa kile kinachodaiwa wanapozwa na kitu kidogo.
“Askari wapo, lakini sema baadhi yao wanatufahamu, kwa hiyo ikitokea na sisi mambo yetu yamekaa vizuri tunachekiana,” alisema Suzy.
RIPOTI YA MAKONGO HIGH SCHOOL KUHUSU KUFELI KWA DOGO JANJA NA UTORO WA KUPINDUKIA
Baada ya taarifa kuenea kuhusu uwepo wa msanii Dogo Janja nchini Afrika Kusini kwa show alizopata zilizofanyika ndani ya wiki tatu, Uongozi wa shule anayosoma ya Makongo Sekondari, umetoa taarifa kuhusu mwenendo wake pamoja na matokeo aliyopata ya kidato cha pili.
Michael Alfred Mbaula ambae ni Afisa taaluma amesema “mahudhurio ya Dogo Janja darasani yalikua mazuri na alikua anashirikiana vizuri na wenzake kipindi kilichopita ila mara yake ya mwisho kuingia darasani ni novemba 2012, na kwa sasa atalazimika kurudia kidato cha pili kwa sababu amefeli kwa wastani mdogo ambao usingemruhusu kuendelea na kidato cha tatu”
Kuhusu kauli ya Dogo Janja kwamba juzi alipokwenda Afrika Kusini alikua ameomba ruhusa ya wiki mbili shuleni, Mbaula amesema “sio kweli kwamba aliomba ruhusa na wala ofisi haina taarifa japo shule haina tatizo akitoa taarifa hata katikati ya masomo iwapo anatakiwa kufanya shughuli za mziki kwa sababu Makongo ni shule ya vipaji, kuomba ruhusa ya wiki moja au mbili ambazo alikua akiziomba mwaka uliopita ndani ya mwezi mmoja ni sahihi ila kukaa miezi mitatu bila kuja shule ndio tatizo”
Mbaula amesema “Dogo Janja amefeli kidato cha pili kwa kupata wastani wa 27 ambapo alifanya vibaya sana kwenye hesabu kwa kupata sifuri, Civics alipata 27, historia 33, Jiografia 22, Kiswahili 46, Kiiingereza 42, Phisics 20, Chemistry 30, Biology 27, Commerce 8, Bookkeeping 11 hivyo ni lazima arudie darasa kitu ambacho anaweza kukifanya hapahapa Makongo”
UNAPOPATA FEDHA, ‘USIZITUMBUE’ KANA KWAMBA KESHO HAIPO!
Utakubaliana na mimi kwamba wapo watu ambao leo hii wanashinda wakibeba zege, kuzibua mitaro, kubeba mizigo na kazi nyingine nzito lakini jioni wanapopata ujira hukimbilia baa na kuzitumbua kwa staili ya lete kama tulivyo.
Ninachokizungumza kipo huko mtaani, watu…
Utakubaliana na mimi kwamba wapo watu ambao leo hii wanashinda wakibeba zege, kuzibua mitaro, kubeba mizigo na kazi nyingine nzito lakini jioni wanapopata ujira hukimbilia baa na kuzitumbua kwa staili ya lete kama tulivyo.
Ninachokizungumza kipo huko mtaani, watu wanatumia pesa kama vile wana uhakika wa kuendelea kuzipata kila siku. Ndiyo maana nadiriki kusema kwamba kutumia pesa ovyo ni sawa kabisa na kujiandalia ufukara wa baadaye.
Wapo watu wengi tu ambao kwa sasa ni mafukara wa kutupwa lakini utakapojaribu kuangalia historia yao huko nyuma utagundua walikuwa na pesa nyingi ila walikuwa wakizutumia kana kwamba wanamkomoa mtu lakini leo wanaishi maisha ya kuungaunga, hawana mwelekeo.
Sikatai kwamba matumizi ya mtu yanatokana na kipato chake na ndiyo maana mtu anayepokea mshahara wa shilingi milioni moja kwa mwezi hawezi kuwa na matumizi sawa na mtu anayepokea laki moja lakini je, kuwa na kipato kikubwa ndiyo kukufanye utumie fedha zako ovyo eti kwa sababu tu una uhakika wa kupata nyingine mwezi ujao?
Jamani tukumbuke kwamba, maisha ni kupanda na kushuka. Leo hii unafanya kazi katika kampuni ama shirika fulani lakini uwezekano wa kuwepo katika shirika hilo kwa kipindi chote cha maisha yako ni mdogo. Unaweza kuachishwa kazi wakati wowote.
Sasa kama ulikuwa unatumia ovyo pesa uliyokuwa unaipata, unatarajia nini kama siyo kuingia kwenye ufukara ambao kwa kiasi fulani ungeweza kupunguza ukali wake kama ungekuwa makini katika matumizi ya pesa zako?
Utumiaji ovyo wa pesa ni kuzitumia bila mpangalio tena wakati mwingine katika mambo ambayo si ya msingi lakini tutambue kwamba, ufujaji wa pesa hauko katika anasa tu kama vile ulevi, kuhonga na mambo mengine kama hayo, bali pia katika mambo ambayo hata yakikosekana hayawezi kuleta athari.
Tafiti mbalimbali zimeonesha kwamba, wengi ambao hutumia pesa ovyo ni athari za malezi waliyoyapata kutoka kwa wazazi wao tangu utotoni. Mzazi ndiye anayeweza kumfundisha mtoto wake kutokuwa na nidhamu katika pesa.














