Wednesday, March 20, 2013

DIAMOND: NIMEMTUNDIKA MIMBA PENNY






Diamond akipozi na Penny.
Kwa mujibu wa Diamond, ni kweli yeye na Penny ambaye ni presenta wa Kituo cha Runinga ya DTV wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza kabla hata ya ndoa waliyopanga siku zijazo.
Diamond alifunguka kuwa tayari amempa mrembo huyo gari la kutembelea huku akimwagizia lingine jipya aina ya Hyundai ix35.
...Wawili hao wakiwa katika pozi la kimahaba.
“That’s true (ni kweli) nimemtia mimba Penny, unajua sipendi kusema mpenzi wangu, sasa hivi ni mama watoto wangu. Ni kweli pia nimempa gari kwa sababu ya mizunguko ya kwenda kliniki na nini, nikaona siyo vizuri kwenda kugombea daladala,” alisema Diamond.
Gari hilo jipya aina ya Hyundai ix35 gharama yake inakadiriwa kufikia Sh. milioni 50. 

0 comments: