This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, May 18, 2013

MICHUANO YA SAFARI LAGER HIGHER LEANING NATIONAL POOL CHAMPIONSHIP KUANZA RASMI KESHO JIJINI MWANZA

Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari ambapo pia alitumia fursa hiyo kukabidhi jezi kwa washiriki, kulia ni captein wa timu ya SAUT Jimmy Nikitas,  inayotetea taji la ubingwa wa pool kwa vyuo nchini.


Mashindano ya Safari Lager Higher Leaning Pool kwa mkoa wa Mwanza yanataraji kuanza kutimua vumbi kuanzia kesho katika ukumbi wa Villa Park jijini Humo.

Kwa mujibu wa Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum amesema kuwa Mashindano ya Higher Leaning Pool kwa mkoa wa mwanza yatashirikisha vyuo vinne ambavyo ni CBE Mwanza, Chuo cha Bugando, SAUT na TIA ambapo vyuo hivyo vitashindana kupata mwakilishi  mmoja atakaye shiriki mashindano ya Pool Taifa kwa mikoa mingine hapa nchini kama Mbeya, Dar es salaam, Morogoro, Dodoma, Kilimanjaro na Arusha  
Kushoto aliyesimama ni Afisa habari wa michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool Machel akitoa ufafanuzi juu ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa kwa vyuo shiriki kupitia michuano hiyo.

Zawadi kwa washindi Timu za Pool 
Mshindi wa kwanza mkoa ni shilingi laki 5
Mshindi wa pili shilingi laki 3
Mshindi wa tatu shilingi laki 2
Na mshindi wa nne shilingi laki 1

Washindi Single wanaume 
Mshindi wa kwanza shilingi laki 1.5
Mshindi wa pili shilingi laki 1

Washindi Single wanaume
Mshindi wa kwanza shilingi laki 1
Mshindi wa pili shilingi elfu 50. 



Timu captein wa timu bingwa Chuo cha SAUT Jimmy Nikitas (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuelezea jinsi timu yake ilivyojiandaa kwa michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool 2013.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha SAUT Jimmy Nikitas kwaajili ya michuano hiyo inayotaraji kuanza rasmi kesho Villa Park Resort Mwanza.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha Bugando Bernad Okamo, kwaajili ya michuano hiyo inayotaraji kuanza kutimua vumbi rasmi kesho katika Viunga vya burudani vya Villa Park Resort Mwanza.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha CBE Mwanza George Izengo, kwaajili ya michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool inayotaraji kuanza rasmi kesho Villa Park Resort Mwanza.


Meneja wa Matukio wa bia ya Safari mkoa wa Mwanza Bernad Nahum (kushoto) akimkabidhi jezi timu captein wa Chuo cha TIA Beatrice Benignus, kwaajili ya michuano ya Safari Lager Higher Leaning Pool inayotaraji kuanza rasmi kesho viunga vya burudani Villa Park Resort Mwanza.

MKUU WA GENGE LA MATAPELI WANAOJIFANYA MAAFISA WA TAKUKURU ANASWA JIJINI MWANZA, ALIKUWA AKITUMIA HIRIZI KUFANIKISHA WIZI

Mtuhumiwa Simon Jumbe anayetajwa kujifanya afisa wa Takukuru.
 TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Mwanza imefanikiwa kumnasa mtu mmoja ambaye anasadikika kuwa mkuu wa genge la watu wanaojifanya Maafisa wa Ofisi ya TAKUKURU Mkoani hapa.


Akitoa taarifa kwa waandishi wa Habari ofisini kwake Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza Ayubu Akida alisema kwamba kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo aliyefahamika kwa jina la Simon Jumbe (32) lakini amekuwa akitumia majina mengie kwa kujiita Mapunda na SP ni kutokana na mtego uliowekwa na maafisa wake.
Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Mwanza Ayoub Akida, akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo.
“Tuliweka mtego huo kutokana na kuwepo taarifa za siri kutoka kwa raia wema ambapo walitueleza kwamba kuna wimbi la baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiwadanganya watu kuwa wao ni maafisa na watumishi wa TAKUKURU baada ya kuweka mtego Mei 13 mwaka huu tumefanikiwa kumnasa huyu maeneo ya Kata ya Mkuyuni Wilayani Nyamagana” alisema Akida.

 Kamanda Akida alieleza kwamba tangu mwezi April na Mei tumekuwa katika hekaheka za kuwatafuta watu hao baada ya taarifa za kuwepo watu hao wanaojitambulisha kuwa watumishi na wamekuwa akiwadanganya watu na kufanya kazi ambazo si za ofisi ya Takukuru ikiwa ni zile za Taasisi zingine za serikali.

Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Mwanza Ayoub Akida
“Katika kipindi hicho tuliweza kupokea taarifa za matukio kumi ya kutoka kwa watu waliotapeliwa katika Wilaya za Misungwi na Jiji la Mwanza ambapo baada ya kumnasa mtuhumiwa huyu na kumhoji alidai kuwa yeye peke kwa kutumia utapeli huo ameweza kujipatia kiasi cha shilingi milioni 4,637,000/= kutoka kwa watu kumi na mbili”alisema Kamanda.

Naye mmoja wa watu walioathirika na kutapeliwa aliyejitambulisha kwa jina la James Belindo mkazi wa Nyakato Buzuruga Wilayani Ilemela alisema kwamba  alimfahamu mtuhumiwa kwasababu alikuwa jirani yake naye mtuhumiwa alitumia mwanya huo wa ujirani akimweleza kuwa kuna magari 12 yameletwa ofisini kwao yaani TAKUKURU hivyo kuna nafasi za kazi ambazo anaweza kumuunganishia.

James Belindo mmoja kati ya waliotapeliwa
Bofya play msikilize kwa kina hapa chini.
“Alidai kama nina ujuzi wa kuendesha gari yaani udereva basi nimwambie,  nilimweleza sina lakini kuna jamaa yangu, naye akasema hamna tabu nimpeleke atakuwepo ofisi ya Takukuru Mkoa, akaomba vyeti na leseni kisha akamweleza kuwa inatakiwa kufunguliwa majarada matano na kuomba kiasi cha 475,000/- lakini hakupata kazi hiyo”alieleza kwa masikitiko.

Kamanda Akida amewatahadharisha wananchi kuwa makini na kundi la matapeli hao wanaojifanya watumishi wa Takukuru ambao wamekuwa wakiidhalilisha na kuipaka matope ofisi yake na kuharibu taswira iliyopo kwa jamii na kuwataka kufika ofisi za Takukuru na kutotoa fedha bila utaratibu wa taasisi hiyo.

Aidha alisema kwamba kutokana na kuwepo kundi hilo ofisi yake imewataka wananchi kuendelea kutoa taarifa za siri zitakazofanikisha kunaswa kwa watu hao ambao wamekuwa wakiwadanganya kuwatafutia kazi,kuwatisha ili wawapatie fedha kunyume na huduma zinazotolewa na ofisi za Takukuru Wilayani na Mkoa.
 

Hirizi iliyotumiwa na mtuhumiwa Simon Jumbe

Baada ya kuhojiana naye kwamaana alikuwa anaficha ila baada ya 'kumsalimia sana' mtuhumiwa alisema kuwa hirizi hii huwa anailamba asubuhi, akishailamba asubuhi yule mtu aliyepanga kwenda kuonananaye, akishaonana naye hawezi kupingana naye kwa kila atakachomwamuru afanye.


Mtuhumiwa Simon Jumbe akiri tuhuma dhidi yake
huyu ndiye anayetajwa kujifanya afisa wa 

Takukuru
Bofya play hapa chini kumsikiliza.
Akitaka kupatiwa fedha atapewa, hata vingine vya kufikirika kwa kutumia akili kuwa haviwezekani mtapeliwa atakubali kama vile kutoa fedha akafunguliwe akaunti nakadhalika.

Iliwachukuwa muda maafisa hao kuipata hirizi hiyo iliyokuwa ikitumiwa na mtuhumiwa huyo, kwani alikuwa ameifunga ndani kwenye kaptula ya jeans, juu akiwa amevaa mashati matatu, yaani T-shirt mbili za mikono mirefu moja ikiwa nyeupe na shati moja juu yake. 

Hivyo aliweza kubadilika badilika kutokana na mazingira, kwamba anaweza kufanya tukio la utapeli mahali fulani ndani ya dakika chache anahamia upande wa pili wa 
barabara akavua shati la juu na kuwa na T-shirt rangi nyingine akijiunga na watazamaji wa tukio. 

Hii ni kwa mujibu wa mmoja kati ya maafisa wa Uchunguzi TAKUKURU waliofanikisha kumnasa tapeli huyo.

Katika hatua nyingine  Jumbe amekiri kwa kauli yake kwenye mahojiano kushiriki kingono na wanafunzi 24 wa Chuo cha SAUT,   na wengine 16 wa Chuo cha Ualimu Butimba kwa gia hiyo hiyo ya kuwalaghai kuwa atawapatia nafasi ya ajira Takukuru. 

YANGA YAIGONGA SIMBA 2-0, YATWAA KOMBE LA VPL


Wachezaji wa Yanga SC wakishangilia na kombe lao baada ya mechi dhidi ya Simba SC.
Timu ya Yanga leo imewaadhibu watani wao wa jadi, Simba SC baada ya kuwalaza kwa bao 2-0  katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao ya Yanga yamefungwa na Didier Kavumbagu na Hamis Kiiza. Baada a mchezo huo, Yanga SC ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom mwaka huu, walikabidhiwa kombe lao.

MLINZI WA BAR ACHINJWA KIKATILI NA MAJAMBAZI USIKU WA KUAMKIA LEO




Mlinzi wa baa ya Darajani Stop Over iliyo kando kando ya barabara kuu ya Morogoro Dar es salaam jirani na daraja la Mzambarauni  Bw Mika Athumani amechinjwa na majambazi usiku wa kuamkia leo.


Habari zilizopatikana eneo la tukio zilidai kwamba majambazi hayo yalivamia baa hiyo iliyojitenga usiku wa manane na kumvamia mlinzi huyo na kumchinka kama kuku na baadae kuvunja baa hiyo na kuimba vitu mbali mbali.

Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari, la polisi kufuatia mwili huo kutenganiswa vibande viwili..



Sehemu aliyochinjiwa mlinzi huyo aliyefahamika kwa jina Mika Athumani.
Akihojiwa na mwandishi wetu,  mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi alidai kwamba majambazi hao walimvamia mlinzi wake na kumchinja na baadae walivunja Counter ya baa hiyo pamoja na duka ililipojirani na baa hiyo na kuiba vitu mbali mbali.
 

Alipoulizwa kwamba kuna taarifa zinadai kwamba mlinzi huyo alikutwa akiwa amelala Bw Mushi alisema"  inawezekana lakini hakuna mtu mwenye uhakika na jambo hilo kwani sote hatukuwepo,wakti tukio hilo linatokea"
Mwananachi akishuhudia damu ya mlinzi huyo kwa hudhuni
Baskeli ya Mlizni huyo ikiwa imetapakaa damu ambapo inadaiwa mlinzi huyo alikuwa amelala kwenye eneo hilo
Redio ambayo majambazi hayo waliiangusha nje ya baa hiyo
Majaira ya saa 12 asubuhi ya leo wananchi walishuhudia maduka mawili ya baa hiyo yakiwa wazi huku mwili wa mlizni huyo umekutwa upande wa baa ukiwa umechinjwa na kutenganishwa kichwa na mwili
Umati wa watu ukishuhudia tukio hilo muda mfupi uliopita
Gali la polisi likiondoka eneo la tukio na mwili wa marehemu
Wananchi nao waliondoka eneo hilo la tukio
Mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi akihojiwa na waandishi wa habari eneo la tukio

Majirani wa eneo hilo wakihojiwa na waandishi wa habari
Baadhi ya watu waliokuwepo eneo hilo la tukio walidai kwamba mlinzi huyo alikuwa amelala hivyo majambazi hayo yalimvamia na kumpora siraha zake na kishi kumchinja shingoni..
Mwandishi wetu alishuhudia mtoto wa marehemu pamoja na mjukuu wa marehemu wakiangua vilio eneo la tuko baada ya kuuona mwili wa mazazi wao aliyeuwawa kikatili baadae wote wawili walipanda gari la polisi na kuondoka nao.

PROFESA JAY; NA SAKATA LA JIDE VS RUGE



Stori:Chande Abdallah

WIKI hii kwenye Funguka na Risasi tunaye mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Joseph Haule, ‘Profesa Jay’ ambaye anafunguka juu ya bifu kati ya Judith Wambura ‘Jide’ na Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti wa Clouds Media, Ruge Mutahaba.

Profesa Jay naye ametajwa katika sakata hilo kutokana na kushirikishwa katika wimbo wa Joto Hasira ambao wengi wameutafsiri kuwa na vijembe kwa Ruge.
Funguka: Mambo vipi Profesa, nimekutafuta ili nipate msimamo wako kwenye bifu kati ya msanii mwenzako (Jide) na Ruge.

Profesa Jay: Kwanza nianze kusema kuwa mimi sina upande wowote ambao ninaweza kuusimamia, sipo kwa Ruge wala kwa Jide.

Funguka: Kumekuwa na…