This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Monday, April 22, 2013

RAIS TENGA ATOA MIPIRA YA DOLA 30,000


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametoa mipira zaidi ya 1,200 yenye thamani ya dola 30,000 za Marekani kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na vituo 21 vilivyo hai vya kuendeleza vijana (academies).
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) lilimpa Rais Tenga fedha hizo ikiwa ni shukrani kwake kwa kushughulikia mgogoro wa uongozi wa mpira wa miguu nchini Kenya uliodumu kwa miaka miwili; ambapo nchi hiyo kutokana na mgogoro huo ilikuwa na vyama viwili (KFF na FKL).
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mipira hiyo kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam leo (Aprili 22 mwaka huu), Rais Tenga amesema amefanya hivyo kwa vile anaamini kuwa mipira ndiyo kitu muhimu katika kuinua mchezo huo mahali popote.
“Dhamira yangi si kushukuru kwa hafla hii, bali kutoa sababu kwa nini nimefanya hivi. Ninaamini kwa kuanzia mipira ndiyo muhimu, pili kwa kufanya hivi itaonekana kweli mipira imegawiwa,” amesema Rais Tenga.
Amesema amesema mpira wa miguu kwa Tanzania unahitaji sana watu wa kujitolea, na yeye amefanya hivyo kwa kujitolea kutokana na ukweli shughuli anazotumwa na FIFA ni za kujitolea.
Rais Tenga ambaye pia alitumwa na FIFA kutatua matatizo ya uongozi wa mpira wa miguu katika nchi za Uganda, Zambia na Sudan Kusini amesema anaamini anapata fursa hizo kutokana na kuwa kiongozi wa TFF, na kwa kuwakumbuka waliomchagua ndiyo maana hakusita kupeleka fedha hizo kwenye mipira.
Amesema moja ya ndoto zake wakati anaingia kuongoza TFF mwaka 2004 ameshindwa kutimiza ni kusaidia mipira, kwani uwezo wa kununua mipira kwa wanaocheza katika ngazi ya chini hasa watoto haupo.
“Hizi kelele zote za maendeleo ya mpira wa miguu ni kwa sababu shuleni hakuna vifaa. Nia yangu ilikuwa shule zote zipate mipira, lakini hiyo ni moja ya ndoto nilizoshindwa kutekeleza. Vipaji haziwezi kupatikana kama watoto hawachezi.
“Tunashukuru sana kwa Serikali kurejesha mpira shuleni. Hata nitakapoondoka madarakani nikipata nafasi nitaendelea kuomba mipira kwa ajili ya shule,” amesema Rais Tenga.
Vyama vya mikoa ambavyo jumla ni 32 (Tanzania Bara na Zanzibar) kila kimoja kimekabidhiwa mipira 25 (kumi saizi namba tano, 15 saizi namba nne kwa ajili ya vijana). Kwa academies ambazo ni 21 kila moja imepewa mipira 25 (minane saizi namba tano, na 15 saizi namba nne).
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Almasi Kasongo, Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) Nassib Mabrouk na Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Riziki Majala.

MESSI AENDELEA KUONGOZA MSIMAMO WA WAFUMANIA NYAVU BARANI ULAYA,


Hakuna mabadiliko kwenye msimamo wa wafumania nyavu wanaowania kiatu cha dhahabu huku Lionel Messi akiendelea kuuguza jeraha lake,mpinzani wake wa karibu Cristiano Ronaldo akimaliza bila kufunga huku timu yake  Real Madrid ikipata ushindi wa mabao  3-1 dhidi ya Real Betis.
Kwingineko barani ulaya juma hili,nchini Ujerumani mshambuliaji wa  Bayer 04 Leverkusen Stefan Kiessling alifunga hat-trick dhidi ya Hoffenheim, mabao yalimpatia nafasi ya kuingia kwenye orodha ya 10 bora  kwa mara ya kwanza msimu huu.
Pia kulikuwa na mabao kutoka kwa Jackson Martinez wa porto , Radamel Falcao, Edinson Cavani,Robert Lewandowski na Luis Suarez.
HII NDIO ORODHA KAMILI PAMOJA NA POINTI
1. Lionel Messi (FC Barcelona) 42 x 2 = 84
2. Cristiano Ronaldo (Real Madrid) 31 x 2 = 62
3. Radamel Falcao (Atlético Madrid) 25 x 2 = 50
Jackson Martinez (FC Porto) 25 x 2 = 50
5. Edinson Cavani (Napoli) 23 x 2 = 46
Robert Lewandowski (Borussia Dortmund) 23 x 2 = 46
Luis Suarez (Liverpool) 23 x 2 = 46
8. Wilfried Bony (Vitesse) 30 x 1.5 = 45
9. Stefan Kiessling (Bayer Leverkusen) 21 x 2 = 42
Robin van Persie (Manchester United) 21 x 2 = 42
11. Philipp Hosiner (Austria Vienna) 27 x 1.5 = 40.5
Zlatan Ibrahimovic (Paris Saint-Germain) 27 x 1.5 = 40.5
13. Jonathan Soriano (Red Bull Salzburg) 25 x 1.5 = 37.5
14. Gareth Bale (Tottenham Hotspur) 18 x 2 = 36
Alfred Finnbogason (Heerenveen) 24 x 1.5 = 36
Michael Higdon (Motherwell) 24 x 1.5 = 36
Antonio Di Natale (Udinese) 18 x 2 = 36
Alvaro Negredo (Sevilla) 18 x 2 = 36
Graziano Pellè (Feyenoord) 24 x 1.5 = 36
20. Arturas Rimkevicius (FK Siauliai) 35 x 1 = 35
21. Miguel Pérez Cuesta ‘Michu’ (Swansea City) 17 x 2 = 34
Roberto Soldado (Valencia) 17 x 2 = 34
23. Eliran Atar (Maccabi Tel Aviv) 22 x 1.5 = 33
Carlos Bacca (Club Brugge) 22 x 1.5 = 33
Henrikh Mkhitaryan (Shakhtar Donetsk) 22 x 1.5 = 33
26. Rubén Castro (Real Betis Sevilla) 16 x 2 = 32
Rodrigo Lima (Benfica) 16 x 2 = 32
Stephan El Shaarawy (Milan) 16 x 2 = 32
29. Jozy Altidore (AZ) 21 x 1.5 = 30.5
30. Demba Ba (Newcastle United/Chelsea) 15 x 2 = 30
Christian Benteke (Aston Villa) 15 x 2 = 30
Oscar Cardozo (Benfica) 15 x 2 = 30
German Gustavo Denis (Atalanta) 15 x 2 = 30
Rafik Djebbour (Olympiakos) 20 x 1.5 = 30
Leigh Griffiths (Hibernian) 20 x 1.5 = 30
Mario Mandzukic (Bayern Munich) 15 x 2 = 30
Billy McKay (Inverness Caledonian Thistle) 20 x 1.5 = 30
38. Liam Boyce (Cliftonville) 29 x 1 = 29
39. Burak Yilmaz (Galatasaray) 19 x 1.5 = 28.5
Kalu Uche (Kasimpasa SK) 19 x 1.5 = 28.5
41. Rickie Lambert (Southampton) 14 x 2 = 28
Erik Lamela (Roma) 14 x 2 = 28
Francisco Medina Luna ‘Piti’ (Rayo Vallecano) 14 x 2 = 28
44. Andreas Cornelius (FC Copenhagen) 18 x 1.5 = 27
Gary Hooper (Celtic) 18 x 1.5 = 27
Niall McGinn (Aberdeen) 18 x 1.5 = 27
Raul Rusescu (Steaua Bucharest) 18 x 1.5 = 27
48. Aritz Aduriz (Athletic Bilbao) 13 x 2 = 26
Dimitar Berbatov (Fulham) 13 x 2 = 26
‘Éder’zito António Macedo Lopes (Sporting Braga) 13 x 2 = 26
Gonzalo Higuaín (Real Madrid) 13 x 2 = 26
Vedad Ibisevic (Stuttgart) 13 x 2 = 26
Romelu Lukaku (West Bromwich Albion) 13 x 2 = 26
Alexander Meier (Eintracht Frankfurt) 13 x 2 = 26
Albert Meyong (Vitoria Setúbal) 13 x 2 = 26
Giampaolo Pazzini (Milan) 13 x 2 = 26
Adám Szalai (Mainz) 13 x 2 = 26
Carlos Vela (Real Sociedad) 13 x 2 = 26

Taswira:Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Akabidhiwa Tuzo Ya Heshima Mkoani iringa

 Askofu  wa  kituo  cha maombezi  na uponaji cha  Overcomers Power Center (OPC) Dkt  Boaz Sollo (kushoto) akimakabidhi tuzo ya  heshima mfano  wa ramani ya  Tanzania  waziri mkuu  wa zamani Edward  Lowassa  jana katika hafla ya  kuchangia ujenzi  wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio Overcomers Fm ,katika harambee  hiyo Lowassa aliahidi kuachangia milioni 15  na kufanikisha kupata  Tsh zaidi ya milioni 75 zikiwemo  fedha taslimu na ahadi .
  waziri mkuu  wa zamani Edward  Lowassa akionyesha tuzo ya  heshima mfano  wa ramani ya  Tanzania aliyotunukiwa, kushoto kwake ni Askofu  wa  kituo  cha maombezi  na uponaji cha  Overcomers Power Center (OPC) Dkt  Boaz Sollo Mheshimiwa Lowassa Alikabidhiwa Tuzo Hiyo katika hafla ya  kuchangia ujenzi  wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio…
 Askofu  wa  kituo  cha maombezi  na uponaji cha  Overcomers Power Center (OPC) Dkt  Boaz Sollo (kushoto) akimakabidhi tuzo ya  heshima mfano  wa ramani ya  Tanzania  waziri mkuu  wa zamani Edward  Lowassa  jana katika hafla ya  kuchangia ujenzi  wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio Overcomers Fm ,katika harambee  hiyo Lowassa aliahidi kuachangia milioni 15  na kufanikisha kupata  Tsh zaidi ya milioni 75 zikiwemo  fedha taslimu na ahadi .
  waziri mkuu  wa zamani Edward  Lowassa akionyesha tuzo ya  heshima mfano  wa ramani ya  Tanzania aliyotunukiwa, kushoto kwake ni Askofu  wa  kituo  cha maombezi  na uponaji cha  Overcomers Power Center (OPC) Dkt  Boaz Sollo Mheshimiwa Lowassa Alikabidhiwa Tuzo Hiyo katika hafla ya  kuchangia ujenzi  wa kanisa na kuendeleza kituo cha radio Overcomers Fm ,katika harambee  hiyo Lowassa aliahidi kuachangia milioni 15  nakufanikisha kupata  Tsh zaidi ya milioni 75 zikiwemo  fedha taslimu na ahadi .Picha na Habari na Mdau Francis Godwin
--
WAZIRI  mkuu  mstaafu  Edward  Lowassa amesema kuwa mbali ya  kuwa  yeye  si tajiri ila bado ataendelea  kufanya kazi  yake kwa  ukaribu  zaidi na jamii  ikiwa ni pamoja na kushirikiana na  marafiki  zake  kusaidia na kuwataka  wale  wote  wenye kusema dhidi yake  kuendelea  kusema ila hatarudi  nyuma katika kutoa misaada kama njia ya  kutafuta baraka za Mungu.
Lowassa ambae  pia alikabidhiwa   tuzo ya  heshima kwa ajili ya  kuendeleza  kulipigania  Taifa  la Tanzania ,huku  mwenyewe akichangia kiasi cha Tsh milioni 15  na mbunge  wa jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe akichangia  milioni 9  kati  ya  fedha  zote  zaidi ya Tsh milioni 75 zilizochangwa kwa ajili ya   kuendeleza ujenzi  wa kanisa la OPC mkoani Iringa kama njia ya  kuhamasisha amani katika Taifa ametaka  watanzania  kuwapuuza  wale  wote wanaoeneza siasa  za uchochezi .
“Nataka  kuwaomba  leo wachukieni  wachochezi na pia niwaelezeni  kuwa mimi  si tajiri ila nina utajiri  wa  watu na ushawishi na ninafanya  mambo haya ili kumbukumbu yangu  iweze  kuandikwa  Mbinguni  na nimekuwa  nikialika watu  wengi  na nimekuwa nikifika   wacha  wenye  kusema waseme  watasema ila usiku  watalala wenyewe ….sitaacha  kusaidia kwa kuogopa kusemwa”
Akizungumza katika hafla  hiyo  iliyoandaliwa na kituo  cha maombezi na uponyaji mkoani Iringa Overcomers Power  Center (OPC) na kufanyika katika  ukumbi  wa St Dominic mjini Iringa leo  Lowassa  alisema kuwa yeye  si tajiri kama ambavyo  watu  wanavyofikiri ila amekuwa akipewa  nguvu na rafiki  zake ambao  wamekuwa  wakimuunga mkono pindi anapoalikwa katika hafla  mbali mbali.
“Nataka  kwanza  kuwashukuru  ndugu zangu  wa mkoa  wa Iringa na napenda  kumshukuru  zaidi Askofu Dkt  Boaz Sollo kwa kunialika  mkoani Iringa …..ila napenda  kuwaeleza  kuwa  si kwamba nachangia michango mbali mbali katika jamii kama mimi ni tajiri  ila mimi ni mtumishi nisiye na faida na nayaweza yote  katika  yeye anitiaye nguvu Pia  nawashukuru  sana  wabunge  wenzangu ambao  wamepata  kushiriki name  leo katika  ziara  hiyo  akiwemo  mbunge machachari  bungeni Deo  Filikunjombe , Kagi Lugola  na dada yangu  Ritta Kabati  bila kumsahau mbunge Mendradi Kigola kwa kuungana nami leo naamini nao  wamepanda  mbegu  bora”.
Lowassa  alisema kuwa anatambua  bado ana mialiko migi  sana na lazima anaifanyia kazi mialiko yote kama ambavyo jamii imepata  kumwalika na kuwa hata  hatua ya  mkoa  wa Iringa kumpa  tuzo hainamanishi  kuwa ni mwisho wa  yeye  kualikwa.
Hata  hivyo  Lowassa  alisema  kuwa  kwa upande  wake anapongeza  jitihada za askofu Dkt  Sollo kwa  kuwa na mipango na mitazamo ya  kulisaidia  Taifa  kwa kuanzisha  ujenzi  wa kanisa kwa ajili ya  kudumisha amani na  kwenda mbali  zaidi kwa  kuanzisha  kituo cha  radio  Overcomers  Fm   chambo ambacho  kitatumika  kudumisha amani ya mkoa wa Iringa na Taifa  pia
Kuhusu amani ya Taifa  la Tanzania  LOwassa alisema  kuwa alikuwa ni miongoni mwa watu  walioalikwa Kenya  katika sherehe ya  kuapishwa Rais mpya wa Kenya  Uhuru Kenyatta ila  sehemu kubwa ya  wote  waliotoa  salam zao  walitumia muda mwingi kupongeza  vyombo vya habari kwa kulinda amani na hivyo  kuvitaka  vyombo  vya habari za Tanzania na wanahabari  kuendelea  kuandika habari bila kuhatarisha amani ya Taifa
“Tusiruhusi amani ya nchi  yetu  iyumbishwe na mtu  awaye  yeyote  na kila mtanzania anapaswa  kulinda amani  hii  kwa nguvu  zote ….Nawaombeni  wanahabari  tunzeni amani  yetu…wapuuzeni  wale  wote  wanaoch0chea machafuko katika Taifa  hili ….tuachane na  udini  wala ukabila katika  taifa  letu  ila  “
Katika  hatua  nyingine  Lowassa  aliwapongeza  wabunge wa CCM ambao  wameendelea  kupigania wanyonge  bungeni akiwemo  Deo Filikunjombe mbunge wa Ludewa na mbunge wa jimbo la Mwibara Kagi Lugola  kuwa ni miongoni mwa wabunge ambao  amekuwa akiwapenda kutokana na kusema kweli  bungeni.
Kwa upande  wake mbunge  Filikunjombe alisema kuwa mbali ya kutoa ahadi ya  kuchangia  kiasi cha Tsh milioni 9 ila bado atamwalika  Lowassa  jimboni kwake  Ludewa na kuwa kanisa  hilo la OPC halijakosea  kumpa tuzo ambayo ni ramani  ya  Tanzania kutokana na Lowassa kuwa ni mtu  wa  watu mpendwa na  watu na kuwa tuzo  hiyo  ina maana kubwa na hawajakupa ramani ya jimboni kwako Monduli  
Filikunjombe  alimtaka  Lowassa  kuendelea  kuchapa kazi na  kuwa hajakosea  kuwaalika  wao kwani bungeni  kuna  wabunge  zaidi ya  300 ina amewachagua wao  pekee ni jambo la kumshukuru  na  kumfananisha L0wassa  na mti  unaopigwa mawe  kuwa ni mti wenye matunda
“Nakuomba  Lowassa simama Imara  sisi  wana Iringa  tupo nyuma yako na niseme  tuna kazi kubwa ya kuifanya katika Taifa  hili kubwa ni  kumwomba Mungu na makanisa na dini  zote  kuungana katika maombi  zaidi kwani  vita  ni kubwa mbele “
Kwa  upande  askofu  Dkt  Sollo  mbali ya  kumpongeza Lowassa bado  alisema kuwa  wao kama kanisa wataendelea  kumwombea  afya njema na kuona kuwa mambo yake yanafanikiwa na ndio maana ya kumpa  tuzo  hiyo  ya heshima.
Sollo alisema kuwa mchango  wa TSh milioni 15  ulioahidiwa na Lowassa na ule  wa milioni 9  ulioahidiwa na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo  Filikunjombe ni mchango ambao  wao wanaupongeza na kuwapongeza  wabunge  wengine akiwemo Ritta Kabati aliyeahidi Tsh milioni 2 ,Benki ya  wananchi Mufindi milioni 2 , mwenyekiti  wa CCM mkoa  wa Iringa Jesca Msambatavangu milioni 2  mfanyabiashara Salim Abri milioni  1 na wengine  wengi ambao  wamepelekea  kupata  zaidi ya Tsh milioni zaidi ya 75  pesa taslim na ahadi .

BUNGE FILAMU PRODUCTION IKO MBIONI KUZINDUA FILAMU YA " WAZIRI BOYA"


BAADA ya Bendi ya Bunge Modern Taarabu kufanya uzinduzi wao wa albamu yao ya nyimbo tano iliyokuwa na jina la 'FU*K YOU'! jijini Dodoma, taasisi nyingine ya sanaa Bungeni ya Bunge Filamu Production nayo iko mbioni kuzindua filamu yao mpya ya 'Waziri boya'.
Filamu hiyo iliyosheheni wasanii na watunzi mbalimbali na mahiri katika ya uigizaji inaongozwa na msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Fleva) Joseph Mbilinyi maarufu kwa majina ya Mr II ama Sugu.
Yafuatayo ni majina ya washiriki katika filamu hiyo ....vikundi vyao vya sanaa katika mabano na utunzi wa kazi zao mbele 
-(SUGU:- Mbunge Mbeya mjini Chadema). "Mambo mengine nchi hii hayaendi kutokana na serikali pumbavu, hatuwez kuwa na wazir wa elim boya.
-(LIVINGSTONE LUSINDE:- Mbunge Mtera CCM). "Kuna wabunge ambao wana mimba zisizotarajiwa bungeni.
- (JUMA NKAMIA:- Mbunge Kondoa kskz CCM). "Siongei na Mbwa bali naongea na mwenye Mbwa.
-(PETER MSIGWA:-Mbunge Iringa Mjini Chadema). "Serikali ina tatizo kwa kuwa kuna akili ndogo inatawala vichwa vikubwa.
- (ANNA ABDALA:- Viti maalum CCM). "Sikufurahishwa na kauli ya Lusinde kwamba tunamimba zisizotarajiwa.
-(LETICIA NYERERE:- Viti maalum Chadema). "Kwa kuwa wanaume wengi wanabaka, kifunguliwe kituo wafundishwe kutongoza.  
-(ALLY KESI:- Mbunge Nkasi CCM). "Serikali iruhusu raia walime bangi wapate fedha za kigeni.
-(DIDAS MASABURI, Meya wa Jiji la Dar es Salaam CCM) "Baadhi ya wabunge wanafikiri kwa makalio.
sources habari mpya

BI KIDUDE UMEKWENDA, UMEACHA MAJANGA YA WASANII WA KIKE BONGO!

Stori:Sifael Paul

Kishindo cha kuondoka kwako kwenye uso wa dunia tunayoishi kinaweza kuwa kikubwa ama kidogo au hakuna kabisa kutokana na mazingira au heshima uliyojijengea katika jamii.


Fatma Binti Baraka maarufu kwa jina la Bi Kidude aliaga dunia wiki iliyopita akiwa na zaidi ya miaka 100. Bado jina lake linatamkwa kwenye vinywa vya wengi na linaweza kuendelea kutamkwa kwa miaka mingi zaidi.
Bi Kidude, mwanamke shujaa mzaliwa wa Visiwani…Stori:Sifael Paul
Kishindo cha kuondoka kwako kwenye uso wa dunia tunayoishi kinaweza kuwa kikubwa ama kidogo au hakuna kabisa kutokana na mazingira au heshima uliyojijengea katika jamii.


Bi Kidude, mwanamke shujaa mzaliwa wa Visiwani Zanzibar alileta mapinduzi katika muziki asilia wa mwambao. Aliitangaza Zanzibar, Tanzania na Bara la Afrika sehemu mbalimbali duniani alipokwenda kwa ziara za kimuziki. Inaaminika alifanya kazi hiyo ya muziki, mafunzo ya unyago na biashara ya hina na wanja kwa zaidi ya miaka 90.
Katika kipindi chote, Bi Kidude hakushuka kimuziki hadi pale mdomo ulipoanza kuwa mzito kutokana na uzee miaka 10 kabla ya kifo chake Aprili 17, mwaka huu baada ya kuugua maradhi ya kisukari na kongosho kwa muda mrefu.
Pia inaaminika kuwa ndiye msanii mkongwe zaidi aliyekuwa akipanda jukwaani na umri mkubwa ukilinganisha na wengine unaowajua.
Shukurani kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kukuza na kuutangaza muziki wa mwambao miaka hiyo kabla akina Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Snura Mushi, Aisha Ramadhan ‘Isha Mashauzi’, Khadija Kopa na wengine wengi hamjazaliwa na hata baada ya kuzaliwa.
Mkumbuke kuwa matunda ya muziki mnaofanya, Bi Kidude ndiye aliyekwangua barabara.
Ngoja leo nizungumze na mastaa wa muziki wa kike Bongo. Najua mpo wachache lakini kati yenu hakuna anayeweza kupiga kifua kuwa amesaidia kukuza muziki wa kizazi kipya kama alivyofanya legendary Bi Kidude katika muziki asilia wa mwambao.
Wengi wenu mmeishia njiani mapema. Hii ni kwa sababu msingi mliouweka haukuwa imara na hata kama mlikuwa na malengo, basi mlishindwa kuyapigania.
Historia ya Bi Kidude inatutoa huko kwenye kukata tamaa mapema, ama kwa kukutana na vigingi vingi tukashindwa kuvivuka au kwa kupenda zaidi starehe na kusahahu kazi.
Wapo akina Ray C, Sister P, Rah P, Zay B na hata akina Maunda Zorro, Besta, K-lyn na wengine wengi. Labda Mwasiti na Lady Jaydee ambaye ameamka usingizini na kuanza harakati za kuupigania muziki huo.
Mnaonaje mipango mliyojiwekea akina Linah, Recho, Dyna, Vanessa na wengine? Je, mtafikia kiwango cha Bi Kidude ambaye asilimia 90 na ushee ya maisha yake aliitumia katika muziki?
Nawajua baadhi yenu ambao mmeingia kwenye muziki na sanaa nyingine kwa malengo tofauti. Hebu ona wakongwe wa kike kwenye Bongo Fleva wako wapi?
Wale tuliowasikia kitambo wakicheza kihasara majukwaani walionekana na wanaume wakaolewa na kuachana na muziki. Unajua kwa nini? Hamkuwa na lengo la kuukuza na kuuendeleza muziki huo. Mlikuwa mnataka wanaume na mkapata kama wanavyofanya wenzenu kwenye tasnia ya filamu.
Kwa taarifa yenu jamii imewashtukia, haitaki kuwasikia kwa kuona kuwa ninyi ni wazugaji au wazinguaji. Badilikeni. Jipangeni kama kweli mnataka kuweka heshima kama ya Bi Kidude.
Ulevi wa aina zote kuanzia pombe hadi unga, ufuska au umalaya, tamaa mbaya, dharau, majungu, fitina, kujigawa makundi na mengine yanayofanana na hayo yatawaangusha tu, mtabaki kulalamikia kubaniwa na kuombwa rushwa ya ngono jambo ambalo si kweli. Heshima ni jinsi unavyojiweka. Kwa heri Bi Kidude lakini wasanii wa kike Bongo wasipobadilika na kujitambua ni majanga tupu. For the of game!

GODBLESS LEMA AIBUKA KIDEDEA...RUFAA YA KESI YAKE IMETUPILIWA MBALI

Rufaa ya kesi ya Mbunge wa Arusha mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema imetupiliwa mbali na mahakama kumtangaza mbunge huyo kuwa ni halali.

Rufaa hiyo ilisikilizwa na majaji watatu wa Mahakama Rufaa Tanzania ambao ni Engili Kileo, Salum Massati na Benard Luanda kwa pamoja wametupilia madai ya rufaa hiyo.
Mahakama hiyo  imewaamuru tena wakata rufaa walipe gharama zote za kesi.

KIMENUKA!

Kwa tukio hili, vijana wa mjini wanasema; kimenuka! Hivi karibuni wanawake watano ambao majina yao hayakuweza kufahamika mara moja walinaswa usiku mnene wakifanya mapenzi na wanaume wawili kwenye chumba kimoja kilichopo Mwananyamala jijini Dar.
Watu hao walinaswa katika…

UPELELEZI WA KESI YA VITENDO VYA KIGAIDI VYA LWAKATARE WAKAMILIKA


Jeshi la Polisi nchini limekamilisha upepelezi kuhusu kesi inayomkabili Wilfred Lwakatare na mwenzake Ludovick Joseph kuhusu tuhuma za vitendo vya ugaidi vinvyzomkabili. Jalada la kesi hiyo linaandaliwa kupelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, DDP kwa hatua zaidi.

Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Isaya Mghulu akizungumza na wanahabari leo hii, amesema upelelezi huo umezingatia matukio mbalimbali ya uhalifu yaliyofanyika hapa nchini.

Kuhusu kumwagiwa tindikali kada wa CCM bwana Musa Tesha, katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Iguga mwezi Septemba wa mwaka 2011, tayari watuhumiwa wawili wamekwisha kufikishwa mahakamani na upelelezi upo katika hatua za mwisho. Endapo watabainika watuhumiwa wengine, nao watafikishwa mahakamani kwa muda muafaka.