This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, March 28, 2013

MENEJA WA KAMPUNI YA NDEGE YA FASTJET ATIWA MBARONI




MENEJA wa Wafanyakazi wa Ndani ya Ndege wa Kampuni ya Fastjet Emma Donovan, alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam kujibu shtaka linalomkabili la kutoa lugha ya matusi.
Emma (40) alipandishwa kizimbani jana na kusomewa shtaka hilo na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, mbele ya Hakimu Joyce Minde.

Katuga alidai Machi 19 mwaka huu Emma alimtolea lugha ya matusi Samson Itinde jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Emma alikana shtaka hilo ambapo Katuga alidai upelelezi umekamilika na kuomba kupangiwa tarehe kwa usikilizwaji wa awali.
Hakimu Joyce alisema kuwa dhamana ya mshtakiwa iko wazi lakini kwa kuzingatia vigezo vya dhamana vitakavyotolewa kwa kuwa mshtakiwa ni raia wa kigeni.
Alitaja masharti ya dhamana kuwa mshtakiwa anatakiwa kuwasilisha hati yake ya kusafiria au kutoa fedha taslim sh milioni tano na pia awe na wadhamini wawili ambao ni Watanzania.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 9 ili kupangwa tarehe ya kuanza kwa usikilizwaji wa awali.

MBUNGE WA CHAMBANI (CUF) AFARIKI DUNIA

Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF), Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis enzi za uhai wake.
Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF), Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis afariki dunia. Mbunge huyo alianguka jana ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao…
Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF), Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis enzi za uhai wake.
Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF), Jimbo la Chambani, Salim Hemed Khamis afariki dunia. Mbunge huyo alianguka jana ghafla akiwa katika kikao cha kamati ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ndogo za bunge jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ikiendelea na kikao chake.

MACHANGUDOA WAJIUZA MBELE YA NYUMBA YA WAZIRI MKUU....


Issa Mnally na Richard Bukos-GPL
KWELI ni aibu kwa taifa kama la Tanzania, lenye ulinzi uliotimia lakini ni ajabu sana kuwaona wanawake wanaoishi mjini kwa kutegemea biashara haramu ya kuuza miili ‘machangudoa’ wamefikia kuifanya jirani kabisa na makazi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mizengo Pinda.

Wiki iliyopita, waandishi  wetu  waliwanasa machangudoa hao wakiwa wanazurura kwenye Barabara ya Kenyatta inayopita mbele ya makazi ya waziri mkuu takriban mita 80 kutoka barabarani kwa lengo la kujiuza.


Ili kulijua hilo kwa undani, waandshi wetu walijifanya wateja kabla ya kuwapiga picha ili kuweza kuzungumza nao mawili matatu kuhusu kuwepo eneo hilo lenye heshima zake.
Mmoja wa ‘wauza sukari’ hao aliyejitambulisha kwa jina la Hawa, mkazi wa Kinondoni, alikiri yeye na wenzake kufanya biashara hiyo kwenye eneo hilo.


“Ni kweli mimi na wenzangu tunapiga kambi eneo hili, huwa ikifika usiku tunaanzia kule Coco halafu tunakuja hadi huku, lakini mbona maswali mengi, unataka tufanye biashara kama vipi sepa,” alisema changu huyo akianza kupandisha jazba.


Kikubwa walichokiongea machangu hao walisema barabara hiyo yote hupitwa na viongozi wakubwa na wafanyabishara ambao baadhi yao ni wateja wao wakubwa. Wakasema hawamwamini sana mteja anayekwenda na Bajaj au Bodaboda kwa vile wanasumbua kutafuta eneo la kufanyia ngono.


“Wateja wetu wengi ni wale tunaomalizana ndani ya gari, hawa wa Bajaj na Bodaboda wengi wanataka kwenye majani, ni rahisi kukamatwa na polisi wa doria,”
alisema changudoa mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Suzy lakini hakuwa tayari kutaja yaliko makazi yake.

Inakuwaje wauza miili hao watanue eneo ambalo kimazingira linapitiwa na viongozi mbalimbali wazito kama vile mabalozi wa nje waliopo Tanzania, mawaziri, akiwemo waziri mkuu mwenyewe ambaye ni jirani kabisa na makazi yake?

Yapo madai kwamba, askari wanaovalia mavazi ya kiraia ambao wanapaswa kuhakikisha usalama wa eneo lote la Coco Beach wanakaushia matendo hayo kwa kile kinachodaiwa wanapozwa na kitu kidogo.


“Askari wapo, lakini sema baadhi yao wanatufahamu, kwa hiyo ikitokea na sisi mambo yetu yamekaa vizuri tunachekiana,” alisema Suzy.

RIPOTI YA MAKONGO HIGH SCHOOL KUHUSU KUFELI KWA DOGO JANJA NA UTORO WA KUPINDUKIA


Baada ya taarifa kuenea kuhusu uwepo wa msanii Dogo Janja nchini Afrika Kusini kwa show alizopata zilizofanyika ndani ya wiki tatu, Uongozi wa shule anayosoma ya Makongo Sekondari, umetoa taarifa kuhusu mwenendo wake pamoja na matokeo aliyopata ya kidato cha pili.
 
Michael Alfred Mbaula ambae ni Afisa taaluma amesema “mahudhurio ya Dogo Janja darasani yalikua mazuri na alikua anashirikiana vizuri na wenzake kipindi kilichopita ila mara yake ya mwisho kuingia darasani ni novemba 2012, na kwa sasa atalazimika kurudia kidato cha pili kwa sababu amefeli kwa wastani mdogo ambao usingemruhusu kuendelea na kidato cha tatu”

 
Kuhusu kauli ya Dogo Janja kwamba juzi alipokwenda Afrika Kusini alikua ameomba ruhusa ya wiki mbili shuleni, Mbaula amesema “sio kweli kwamba aliomba ruhusa na wala ofisi haina taarifa japo shule haina tatizo akitoa taarifa hata katikati ya masomo iwapo anatakiwa kufanya shughuli za mziki kwa sababu Makongo ni shule ya vipaji, kuomba ruhusa ya wiki moja au mbili ambazo alikua akiziomba mwaka uliopita ndani ya mwezi mmoja ni sahihi ila kukaa miezi mitatu bila kuja shule ndio tatizo”

 
Mbaula amesema “Dogo Janja amefeli kidato cha pili kwa kupata wastani wa 27 ambapo alifanya vibaya sana kwenye hesabu kwa kupata sifuri, Civics alipata 27, historia 33, Jiografia 22, Kiswahili 46, Kiiingereza 42, Phisics 20, Chemistry 30, Biology 27, Commerce 8, Bookkeeping 11 hivyo ni lazima arudie darasa kitu ambacho anaweza kukifanya hapahapa Makongo”

UNAPOPATA FEDHA, ‘USIZITUMBUE’ KANA KWAMBA KESHO HAIPO!

Leo nataka kuzungumzia tabia ya baadhi ya watu kutumia fedha wanazozipata kwa fujo kana kwamba wameambiwa kuwa kesho wanakufa. Hakuna asiyefahamu umuhimu wa pesa, na kutokana na hilo, wengi wamekuwa wakipambana usiku na mchana kuhakikisha wanazipata.
Cha ajabu sasa, wapo ambao wanatumia nguvu na akili zao kuzitafuta fedha hizo lakini mwishowe wanazimwaga kwa matumizi yasiyo na mbele wala nyuma.

Utakubaliana na mimi kwamba wapo watu ambao leo hii wanashinda wakibeba zege, kuzibua mitaro, kubeba mizigo na kazi nyingine nzito lakini jioni wanapopata ujira hukimbilia baa na kuzitumbua kwa staili ya lete kama tulivyo.

Ninachokizungumza kipo huko mtaani, watu…
Leo nataka kuzungumzia tabia ya baadhi ya watu kutumia fedha wanazozipata kwa fujo kana kwamba wameambiwa kuwa kesho wanakufa. Hakuna asiyefahamu umuhimu wa pesa, na kutokana na hilo, wengi wamekuwa wakipambana usiku na mchana kuhakikisha wanazipata.
Cha ajabu sasa, wapo ambao wanatumia nguvu na akili zao kuzitafuta fedha hizo lakini mwishowe wanazimwaga kwa matumizi yasiyo na mbele wala nyuma.
Utakubaliana na mimi kwamba wapo watu ambao leo hii wanashinda wakibeba zege, kuzibua mitaro, kubeba mizigo na kazi nyingine nzito lakini jioni wanapopata ujira hukimbilia baa na kuzitumbua kwa staili ya lete kama tulivyo.
Ninachokizungumza kipo huko mtaani, watu wanatumia pesa kama vile wana uhakika wa kuendelea kuzipata kila siku. Ndiyo maana nadiriki kusema kwamba kutumia pesa ovyo ni sawa kabisa na kujiandalia ufukara wa baadaye.
Wapo watu wengi tu ambao kwa sasa ni mafukara wa kutupwa lakini utakapojaribu kuangalia historia yao huko nyuma utagundua walikuwa na pesa nyingi ila walikuwa wakizutumia kana kwamba wanamkomoa mtu lakini leo wanaishi maisha ya kuungaunga, hawana mwelekeo.
 Sikatai kwamba matumizi ya mtu yanatokana na kipato chake na ndiyo maana mtu anayepokea mshahara wa shilingi milioni moja kwa mwezi hawezi kuwa na matumizi sawa na mtu anayepokea laki moja lakini je, kuwa na kipato kikubwa ndiyo kukufanye utumie fedha zako ovyo eti kwa sababu tu una uhakika wa kupata nyingine mwezi ujao?
Jamani tukumbuke kwamba, maisha ni kupanda na kushuka. Leo hii unafanya kazi katika kampuni ama shirika fulani lakini uwezekano wa kuwepo katika shirika hilo kwa kipindi chote cha maisha yako ni mdogo. Unaweza kuachishwa kazi wakati wowote.
Sasa kama ulikuwa unatumia ovyo pesa uliyokuwa unaipata, unatarajia nini kama siyo kuingia kwenye ufukara ambao kwa kiasi fulani ungeweza kupunguza ukali wake kama ungekuwa makini katika matumizi ya pesa zako?
Utumiaji ovyo wa pesa ni kuzitumia bila mpangalio tena wakati mwingine katika mambo ambayo si ya msingi lakini tutambue kwamba, ufujaji wa pesa hauko katika anasa tu kama vile ulevi, kuhonga na mambo mengine kama hayo, bali pia katika mambo ambayo hata yakikosekana hayawezi kuleta athari.
Tafiti mbalimbali zimeonesha kwamba, wengi ambao hutumia pesa ovyo ni athari za malezi waliyoyapata kutoka kwa wazazi wao tangu utotoni. Mzazi ndiye anayeweza kumfundisha mtoto wake kutokuwa na nidhamu katika pesa.