This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Friday, February 28, 2014

Benki ya Dunia yaisimamishia Uganda msaada

S_77135.png
Benki ya dunia imesitisha mkopo wa dola milioni 90 kwa Uganda wa kuimarisha sekta ya afya kufuatia kupitishwa kwa sheria inayoharamisha ushoga na kutoa adhabu kali kwa watakaopatikana na hatia
Hatua hiyo ya benki ya dunia haikutarajiwa na wengi kwani taasisi hiyo mara nyingi hujiepusha kuingilia masuala ya ndani ya kisiasa ya nchi wanachama au kuhusiana na masuala kama haki za mashoga, kuepuka kuzishurutisha nchi wanachame wake 188.
Hata hivyo msemaji wa benki hiyo David Theis amesema katika barua pepe kuwa wamesitisha mradi huo wa kuboresha sekta ya afya ya Uganda hadi watakapoufanyia tathmini na kuhakikisha malengo yake ya maendeleo hayataathiriwa na sheria hiyo mpya ya kuharamisha ushoga.
Rais wa benki hiyo Jim Yong Kim amewatumia wafanyakazi wake barua akisema benki ya dunia inapinga ubaguzi na itawalinda wafanyakazi wake wote na kuongeza kupitishwa kwa sheria hiyo ya Uganda sio nchi ya kwanza kufanya hivyo kwani ushoga umeharamishwa katika nchi 83 na zaidi ya nyingine 100 zinawabagua wanawake.
Mkopo ulikuwa uimarishe sekta ya afya
Licha ya kusimamishwa kwa mkopo huo wa dola milioni 90,benki ya dunia bado ina miradi mingine nchini Uganda ya kiasi cha dola bilioni 1.56. Mkopo huo ulitarajiwa kuidhinishwa hapo jana na ulipaswa kuangazia miradi ya kuboresha afya ya uzazi,afya ya watoto wachanga na uzazi wa mpango
Kutiwa saini kwa sheria hiyo ya kuharamisha ushoga Uganda na Rais Yoweri Museveni mapema wiki hii kumeibua shutuma kali kutoka kwa nchi za magharibi na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Norway,Denmark na Uholanzi zimetangaza kuwa zitasitisha misaada kwa serikali ya Uganda kutokana na sheria hiyo na nchi nyingine wafadhili ikiwemo Marekani pia zimetishia kusitisha misaada na kutafakari upya uhusiano kati yao na Uganda.
Ghadhabu hiyo ya nchi za magharibi kuhusu kuharamishwa kwa ushoga ambayo adhabu yake ni kifungo cha maisha gerezani kwa watakaokutikana na hatia imeporomosha thamani ya shilingi ya Uganda na kusababisha Benki nchini humo kuingilia kati kwa siku mbili mfululizo
Kutiwa saini kwa sheria hiyo ya kuharamisha ushoga Uganda na Rais Yoweri Museveni mapema wiki hii kumeibua shutuma kali kutoka kwa nchi za magharibi na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Norway,Denmark na Uholanzi zimetangaza kuwa zitasitisha misaada kwa serikali ya Uganda kutokana na sheria hiyo na nchi nyingine wafadhili ikiwemo Marekani pia zimetishia kusitisha misaada na kutafakari upya uhusiano kati yao na Uganda.
Ghadhabu hiyo ya nchi za magharibi kuhusu kuharamishwa kwa ushoga ambayo adhabu yake ni kifungo cha maisha gerezani kwa watakaokutikana na hatia imeporomosha thamani ya shilingi ya Uganda na kusababisha Benki nchini humo kuingilia kati kwa siku mbili mfululizo
Serikali ya Uganda haina wasiwasi
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Uganda Ofwono Opondo amesema Uganda inaweza kujiendeleza bila ya misaada kutoka nchi za magharibi na kuongeza Uganda haina wasiwasi na hatua hizo kwani ni wakati kwa Afrika kupinga ukoloni, utumwa na ubabe kutoka magharibi.
Mwanaharakati ambaye amekuwa katika mstari wa mbele kuwatetea mashoga nchini Uganda Frank Mugisha alikutana na maafisa wa ngazi ya juu wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani mjini Washington hapo jana kuomba usaidizi utakaowalinda mashoga.
Ofisi ya kutetea haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa umelaani kuchapishwa kwa majina ya watu wanaodaiwa kuwa mashoga nchini Uganda katika gazeti moja la udaku nchini humo na kuonya hatua hiyo inakiuka haki ya kuwa na faragha na kuonyesha wazi kuwa maisha ya mashoga yamo hatarini.
Kiongozi wa upinzani Uganda Kizza Besigye ameishutumu serikali kwa kutumia suala hilo kuwahadaa raia wa nchi hiyo ili wasiangalie masuala muhimu kama ufisadi au kuwepo kwa jeshi la Uganda Sudan Kusini.(E.L)

BANZA: NILIANZA SIGARA, BANGI, UNGA ILA SASA…

MWIMBAJI mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ amefunguka mazito juu ya matumizi mabaya ya bangi na madawa ya kulevya ikiwa ni pamoja na jinsi alivyokuwa akiyatumia.
Akizungumza kupitia Kipindi cha Mtu Kati cha Global TV Online mwanzoni mwa wiki hii, Banza alikiri kutumia madawa ya kulevya na kusema; “Nilianza kuvuta sigara ya kawaida, nikaja bangi na baadaye madawa ya kulevya aina ya Heroin ambapo alikuwa akiyatumia kwa…
MWIMBAJI mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ amefunguka mazito juu ya matumizi mabaya ya bangi na madawa ya kulevya ikiwa ni pamoja na jinsi alivyokuwa akiyatumia.
Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ kabla ya kufanya mahojiano na Global TV Online.
Akizungumza kupitia Kipindi cha Mtu Kati cha Global TV Online mwanzoni mwa wiki hii, Banza alikiri kutumia madawa ya kulevya na kusema; “Nilianza kuvuta sigara ya kawaida, nikaja bangi na baadaye madawa ya kulevya aina ya Heroin ambapo alikuwa akiyatumia kwa kuchanganya na sigara au bangi.
“Ujana ulisababisha nikajiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya ila sasa nimeacha kabisa na nawashauri vijana wenzangu kuwa mbali na kilevi hicho kwani kama huna kipato cha kutosha unaweza kugeuka kibaka maana mwili ukizoea ni vigumu kuacha.”

Real Madrid yaisulubu Schalke 04

ronaldo_8e1ea.jpg
Na Fadhy Mtanga
REAL Madrid imejihakikishia kucheza robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya kuitandika Schalke 04 ya Ujerumani mabao 6-1. Mchezaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo, mchezaji aliyevunja rekodi ya usajili ulimwenguni Gareth Bale pamoja na mchezaji mahiri Karim Benzema walihakikisha kila mmoja wao anatupia nyavuni magoli mawili ili kuifanya Real Madrid, vinara wa ligi kuu nchini Hispania, kuisulubu vilivyo Schalke 04 tena kwenda dimba lake la nyumbani, Veltins-Arena. Bao la kufutia machozi la Wajerumani hao lilifungwa na Klaas Jan Huntelaar katika dakika ya 90.
Alikuwa Karim Benzema katika dakika ya 13 tu alipopokea mpira kutoka kwa Cristiano Ronaldo na kuutumbukiza wavuni kama ishara ya ufunguzi rasmi wa karamu ya magoli ya miamba hao wa soka nchini Hispania. Kisha, panapo dakika ya 21, mchezaji aghali zaidi aliyesajiliwa kutoka Tottenham Hotspur ya Uingereza, Gareth Bale akautia mpira kimiani baada ya kupokea pasi kutoka kwa Karim Benzema.

Mwamuzi Howard Webb, anayetajwa kuwa mwamuzi bora zaidi duniani kwa sasa alipopuliza kipenga kuashiria mapumziko, Real Madrid wakarejea vyumba vya mapumziko wakiwa tayari na magoli mawili nunge.

Timu hizo ziliporejea dimbani kwa ngwe ya mwisho, ilimchukua Cristiano Ronaldo dakika saba tu kuibadili pasi kutoka kwa Gareth Bale kuwa goli la tatu. Dakika tano baadaye, dakika ya 57, Karim Benzem akafungua awali ya pili ya ufungaji kwa wasukuma ndinga hao machachari alipofunga bao la nne dhidi ya Schalke 04. Kama ilivyo kanuni ya hesabu za pythagoras, Karim alifunga goli hilo kwa kupata usaidizi kutoka kwa yule yule aliyempa pasi awali, Cristiano Ronaldo.

Dakika ya 69 ya mchezo, ikawa zamu tena ya Gareth Bale kuutia mpira wavuni baada ya kupokea pasi nzuri ya Sergio Ramos. Ubao wa matokeo ukasoma Schalke 04 0 Real Madrid 5. Matokeo hayo yalidumu kwa dakika 20 tu kwani panapo dakika ya 89 ya mchezo krosi ya Karim Benzema ikamfikia Cristiano Ronaldo. Naye hakufanya ajizi, akaitia wavuni na kuwafanya mashabiki wa Real Madrid kote ulimwenungi kushangilia kwa tambo na kujidai kwa kila namna.

Dakika iliyofuata, Klaas Jan Huntelaar aliyekuwa tayari amelimwa kadi ya njano panapo dakika ya 72, akafunga bao la kuwafutia machozi wenyeji wa mchezo huo.

Kwa matokeo hayo, Schalke 04 inahitaji miujiza ili isonge mbele. Timu hizo zinatarajia kukwaana tena katika mchezo wa pili utakaokimbizwa dimbani Santiago Bernabeu jijini Madrid, Hispania majuma matatu yajayo.

Kwingine barani Ulaya, Galatasaray iliikaribisha Chelsea, vinara wa ligi kuu ya Uingereza. Dakika ya 9 tu ya mchezo huo uliopigwa katika dimba la Turk Telekom, Fernando Torres akaifungia Chelsea goli la kuongoza. Chelsea ikawa timu ya kwanza kutoka Uingereza kufunga goli katika hatua hiyo ya 16 ya michuano ya UEFA. Timu zingine kutoka Uingereza, Machester City, Arsenal na Manchester United ziliambulia kichapo cha magoli 2-0 kutoka kwa Barcelona, Bayern Munich na Olympiakos.

Chelsea iliendelea kuongoza ikiwa ugenini hadi dakika ya 65 pale Aurelien Chedjou alipofunga akisaidiwa na Wesley Sneijer. Matokeo hayo yanaipa ahueni ya goli la ugenini Chelsea. Timu hizo zinatarajia kutimuliana vumbi tena wiki tatu zijazo pale mitaa ya Fulham, London katika dimba la Stamford Bridge.

STEVE NYERERE AMWAGIA SIFA LULU

Stori: Mayasa Mariwata

RAIS wa Bongo Movie Unit, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amemmwagia sifa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuwa ni binti mdogo lakini sasa anajitambua tofauti na wasanii wengine wakubwa.
Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Akipiga stori na Ijumaa Steve alisema kuwa, mbali na umakini katika kazi zake za kisanii, sasa hivi yuko makini sana na maisha yake kiasi kwamba ni nadra sana kumkuta na skendo za kijingajinga.…

RAIS wa Bongo Movie Unit, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amemmwagia sifa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuwa ni binti mdogo lakini sasa anajitambua tofauti na wasanii wengine wakubwa.
Akipiga stori na Ijumaa Steve alisema kuwa, mbali na umakini katika kazi zake za kisanii, sasa hivi yuko makini sana na maisha yake kiasi kwamba ni nadra sana kumkuta na skendo za kijingajinga.
Steve Nyerere.
“Achilia mbali hao mastaa wote unaowajua wewe, mimi nikiwa kama kiongozi wa Bongo Movie siwezi kusema uongo, namkubali sana Lulu kwani ni binti mdogo na anajitambua na sasa siyo mtu wa kuendekeza mambo ya starehe kama wengine, pia huwezi kumuona viwanja kirahisi, katulia anafanya kazi,” alisema rais huyo.

RED HANDED! NJEMBA AUVAA MTEGO AKIWA NA MKE WA RAFIKI YAKE GESTI

 
MAANDIKO yanasema ‘usitamani mali ya mtu mwigine’! Ni kweli kabisa, onyo hilo lilichukua fursa yake kufuatia njemba mmoja aliyejulikana kwa jina la Anton John Mwaweje kunaswa laivu gesti na mke wa rafiki yake aliyefahamika kwa jina moja la Chalz.

Mke wa mtu sumu: Anton John Mwaweje baada ya kunaswa akiwa na mke wa rafiki yake gesti.
Tukio hilo lilijiri mwanzoni mwa wiki hii kwenye gesti moja maarufu (jina tunalo) iliyopo Buguruni- Malapa jijini Dar es Salaam.
Katika sakata hilo ilidaiwa kuwa, Mwaweje alikuwa akiifahamu vyema familia ya Chalz sambamba na mke wake (jina lipo) lakini hilo hakulijali na kumtokia mke wa Chalz ambaye kwa utamaduni wa Kiafrika ni shemejiye.
Mshangao: Anton John akishangaa baada ya kuba
Habari zikazidi kudai kwamba, ilifika mahali katika kumtaka shemejiye huyo ambaye alikuwa akimkatalia katakata, Mwaweje alitumia gia nyingine ikiwemo ya kumuahidi mambo manono kama angekubali kuivunja amri ya 6 ya Muumba na yeye.
Chanzo cha habari kiliendelea kudai kuwa,  ‘Mungu si Athuman wa Lucas’ siku isiyo na jina jamaa alimtumia ujumbe (SMS) mke wa mwenzake kwa kutumia maneno ya kumtoa nyoka pangoni kumbe muda huo bwana simu alikuwa nayo mwenye mke.
Misosi na mitungi: Baadhi ya misosi na vinywaji vilivyokutwa chumbani humo.
Chalz alimwita mkewe na kumuuliza ni nani aliyemtumia ujumbe huo? Ndipo mke akaanika ukweli akisema:
“Mume wangu, wala usikonde. Aliyetuma ujumbe huo si mwingine, ni Anton…”
Mume:  “(akihamaki) Anton huyuhuyu?”
Mke: “Huyuhuyu mume wangu. Amekuwa akinitaka kimapenzi kwa muda mrefu sana, namkatalia lakini hasikii.”
Za mwizi 40: Bwana Anton John akiwa na pingu mkononi baada ya kunaswa na kamanda wa OFM pamoja na wanausalama.
Pia, mwanamke huyo alimwonesha mumewe meseji kibao ambazo jamaa huyo amekuwa akimtumia na zile ambazo yeye amekuwa akimkatalia.
“Sasa sikia, mkubalie,” mwanaume huyo alimwambia mke wake huku midomo ikimcheza kwa hasira.
Chini ya usimamizi wa mumewe, mwanamke huyo aliwasiliana na Anton na kumwambia alikuwa na nafasi wanaweza kukutana kwa ajili ya kumsaliti Chalz.
Baada ya kupanga mipango ya kukutana, mume huyo alipiga simu Global Publishers kwenye kitengo cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) na kuomba msaada wa fumanizi ambapo alibahatika kukuta kuna kamera mpya zimewasi tayari kwa kazi kama hizo.
Baada ya kupata maelezo ya Chalz, OFM ilishirikiana na Jeshi la Polisi Buguruni –Kwamnyamani jijini Dar na kuandaa mtego ambapo Jumatatu iliyopita, saa nane na ushee mchana, Anton ambaye naye inasemekana ana mke aliuingia mtego na kunasa kwenye chumba namba 5 akiwa na mke mwema huyo.
Ndani ya chumba hicho, Anton alikutwa na boksa  tayari kwa mlo wa wizi ambao alibakia kuendelea kusikia njaa. Mezani, kulikuwa na chipsi kuku na pombe ambazo zingewapa stimu kabla ya mchezo.
Kitendo cha Chalz kumnasa jamaa huyo na mkewe kitandani kilimpandisha munkari ambapo nusura afanye ndivyo sivyo lakini alitulizwa na polisi waliokuwa eneo hilo kwa ajili kulinda usalama.
Kilichofuata baada ya hapo, mgoni huyo akiwa na pingu mkononi alipelekwa kwenye kituo hicho cha polisi ambapo awali, Chalz alitoa ripoti ya malalamiko baada ya kugundua  jamaa huyo anataka kumtumbukiza mkewe kwenye mstari wa usaliti.
Mpaka OFM wanaondoka kituoni hapo, taratibu za kisheria kuhusiana na kesi hiyo zilikuwa zikiendelea huku mgoni huyo akiwa chini ya ulinzi mkali.


WASANII WAZINDUA KAMPEINI KUHAKIKISHA MAPENDEKEZO YAO KIKATIBA YANASIKILIZWA

Wasanii mbalimbali wakifuatilia kuhusiana na katiba iliyokataliwa kusikilizwa.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la sanaa (BASATA), Godfrey Lebejo Mngereza akihutubia wasanii.…
Wasanii mbalimbali wakifuatilia kuhusiana na katiba iliyokataliwa kusikilizwa.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la sanaa (BASATA), Godfrey Lebejo Mngereza akihutubia wasanii.
Wana Hip hop kutoka kushoto, Danny Msimamo, Quick Racka, Profesa Jay, Nikki wa Pili na Kala Pina.
Batuli (kulia) na Monalisa wakiwa katika pozi leo Uwanja wa Vijana, Kinondoni.
Wasanii mbalimbali walikuwepo.
WASANII mbalimbali katika nyanja za sanaa leo wameungana katika ukumbi wa Vijana, Kinondoni  katika kuzindua rasmi kampeni ya kuhakikisha mapendekezo yao kikatiba yanasikilizwa na kupitishwa.
Akizindua kampeni hizo, Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Godfrey Lebejo Mngereza alisema:
“Tupo pamoja na wasanii wote, tutahakikisha wasanii wetu wanasikilizwa na kutekelezewa. Haiwezekani msanii kukosa haki zake za msingi kwa muda mrefu.” Alisema.
Awali, Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) wakishirikiana na Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TAMUNET) waliandaa na kupeleka mapendekezo mawili yaliofikishwa kwenye Tume ya Katiba. Pamoja na kupokelewa hapakuwepo na jambo lolote lililotokana na mawazo hayo ambalo lilichukuliwa na kuingizwa kwenye Rasimu ya Katiba.
Mapendekezo mawili waliokuwa wameyatoa awali ni pamoja na kutaka wasanii kutambuliwa katika Katiba kama moja ya makundi maalum, kama vile walivyotajwa wavuvi, wakulima, wafugaji na kadhalika.
Pendekezo la pili lilikuwa ni kuweka kipengele cha kulinda na kuendeleza Haki za Miliki Bunifu katika Katiba mpya.

WANACHAMA WA SACCOS YA WALIMU KILOLO WATAKIWA KUREJESHA MADENI


Afisa  ushirika mkoa  wa Iringa John Kiteve  akifungua mkutano huo
 
Mwakilishi wa CRDB Iringa akifuatilia matukio  katika mtandao huu 

Mwakilishi wa benk ya CRDB Iringa Bw Bruno  akiwahamasisha  kujiunga na bima mbalimbali  


Afisa ushirika mkoa wa Iringa John Kiteve akifungua mkutano mkuu wa Saccos ya  Walimu Kilolo leo
Na  Francis Godwin Blog
WANACHAMA wa  chama cha   kuweka na kukopa  cha  Kilolo Teacher’s  Saccos wilayani  Kilolo  mkoani  Iringa  wametakiwa  kujenga  uaminifu  katika  kulipa madeni ya  mikopo  ambayo  wamekopeshwa badala ya  kugeuza ni  sadaka  kwao.
Wito  huo  umetolewa na afisa  ushirika  wa  mkoa wa Iringa  John  Kiteve  wakati  akifungua  mkutano mkuu  wa mwaka  leo  mjini  Kilolo.
Kiteve  alisema  kuwa  wapo  baadhi ya  wanachama  wasio  waaminifu ambao  wamekuwa  wakiomba mikopo na mara  baada ya  kupewa  mikopo  hiyo wamekuwa  wakishindwa  kurejesha  mikopo   hiyo  jambo  ambalo  linachangia  vyama  vingi  vya  ushiriki na mikopo  kuyumba hapa nchini.
“ wapo  baadhi  ya  wanachama  ambao  si  waaminifu  wamekuwa  wakichukua  mikopo  na wakati  wakihama  wamekuwa  wakihama na madeni  ya  saccos  bila kufika  ofisini  za  Saccos na kueleza  jinsi ambavyo atarejesha  mikopo  hiyo.
Hivyo  aliwataka  wanachama hao  kujenga utamaduni  wa  kurejesha  mikopo kwa  wakati  ikiwa ni  pamoja na  kutumia  mikopo  hiyo  kwa maendeleo  badala ya  kutumia  mikopo kwa anasa  ambazo  zitakwamisha  urejeshaji wa madeni ya mikopo  yao.
Pia  Kiteve  alisema  kuwa  Saccos  hiyo  ya walimu  wilaya ya  kilolo ni moja kati ya  Saccos  ambazo  zimekuwa  zikifanya  vema na kuwa  tofauti na  saccos  nyingine za  walimu  nchini  kutokana na utaratibu mzuri  wa Saccos  hiyo kuwaunganisha  walimu wa  shule za msingi na  sekondari.
Hata  hivyo  alisema ili kuondoa matabaka katika Saccos  hiyo ni  vema  wanachama  wote  kuwa  kitu kimoja  badala ya  kuwepo kwa matabaka  kati ya  walimu wa  shule za msingi na Sekondari jambo ambalo litaua nguvu ya  Saccos  hiyo.
  katibu  wa  chama  hicho  Fabian  Chavala alisema  kuwa  chama   hicho  kilianzishwa  mwaka 2007 na  kupata  usajili wake  IR 465 kikiwa na  wanachama  60 wakiwemo  wanaume 36 na  wanawake 24 ila  kwa  sasa  kina  wanachama 516  kati yao ni  walimu wa   shule za msingi ni 416 na  wengine  waliobaki ni  kutoka  shule za sekondari.
Hata  hivyo  alisema  kumekuwepo  na mafanikio makubwa katika  chama hicho  kwa chama  kuongeza wanachama kwa kasi na kuwa na jengo lake pamoja na  kuwa na mahusiano mazuri na taasisi za kifedha  hasa benk ya CRDB
Mwenyekiti  huyo  alisema kuwa wanachama  wa chama  hicho  wameendelea  kunufaika na mikopo  na kuwa hadi sasa  wanachama 35  wamekopeshwa  mikopo ya ununuzi wa vyombo  vya usafiri yakiwemo  magari  manne na pikipiki 31,wanachama 343 wamepewa  mikopo ya ujenzi wa nyumba za kisasa ,wanachama 156 wamekopeshwa mikopo ya masomo ya  watoto  wao na wanachama 28  wamepewa  mikopo ya biashara na  kilimo .(P.T)