This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Wednesday, April 24, 2013

GODBLESS LEMA ANASAKWA NA POLISI KWA NGUVU ZOTE....WANADAI KUWA YEYE NDO MWANZILISHI WA VURUGU ZA ARUSHA LEO


Kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Arusha kililazimika kutumia Mabomu ya Machozi kuwatuliza wanafunzi waliokuwa wakishinikiza kuandamana baada ya mwanafunzi mwenzao kuuawa kwa kuchomwa kisu na watu wasiojulikana majira ya saa nne usiku wa kuamkia leo.  

 Tukio hilo liliamsha hisia za wanafunzi hao na kuwafanya wakusanyike kuelekea kwa mkuu wa mkoa wa Arusha kwa madai kwamba matatizo yao huwa hayafikishwi ipasavyo, hivyo wanataka kuyawasilisha wenyewe.   

Juhudi za uongozi wa chuo kuwatuliza wanafunzi hao zilishindikana, na ilipofika majira ya saa nne asubuhi, Mbunge wa jimbo la Arusha alifika katika eneo hilo kuwasikiliza wanafunzi hao. 

"Tunatoa dakika thelathini mkuu wa mkoa awe ameshafika hapa, kama hajafika ndani ya muda huo, tunaandamana wote, mimi mbele nyie nyuma mpaka ofisini kwake" alisema 

Mheshimiwa Lema.Baada ya mkuu wa mkoa kufika eneo la tukio aligoma kuzungumza na wanafunzi hao, akidai kwamba hawezi kuongea mpaka Mh.Lema aondoke, ndipo atapanda kuzungumza na pia alilalamika kwamba hamna kipaza sauti kwa hiyo hawez kupaza sauti yake kuzungumza na watu wasio na nidhamu. 
 
Maneno hayo yalipandisha hasira ya wanafunzi hao lakini walitulizwa, na kipaza sauti kikaandaliwa katika ukumbi wa chuo maaruf kama "main cafetaria" ili mkuu huyo azungumze.
Wanafunzi walikusanyika eneo hilo kumsikiliza lakini alivyoanza kuongea, wanafunzi walisikika wakimzomea kwa madai kwamba ameonesha dharau.  
Wanafunzi walianza kuzomea na kumrushia chupa zaa maji na mawe  mkuu wa mkoa na hapo ndipo ilibidi mabomu ya machozi yatumike kuwatuliza wanafunzi wa chuo hicho. 
Kwa muda wa masaa mawili imekuwa ikisikika milio ya mabomu chuoni hapo mpaka hali ilipo tulia kabisa. 
Kwa sasa hali ni shwari chuoni hapo ila polisi wametapakaa huku na kule wakisema wanamtafuta Mbunge wa jimbo la Arusha kwa madai kuwa ndiye anaye chochea mgomo huo wa wanafunzi. 

Mbunge huyo alikimbia kuelekea kusikojulikana na kutelekeza gari yake chuoni hapo, ambayo polisi walilazimika kuivuta kwa "breakdown" car kuelekea kituo cha polisi. kama inavyoonekana katika picha.
Gari ya Mh.Godbless Lema ikiochukuliwa na polisi kutoka eneo la tukio
Polisi wakichukua gari ya mbunge wa jimbo la Arusha

PICHA: HUU NDO UNYAMA WALIOTENDEWA WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

Picha  ya  marehemu  Henry Koga  baada  ya  kuchomwa  kisu  na  kufariki  hapo hapo  jana  usiku  katika  chuo  cha  uhasibu  Arusha.....

Mwanafunzi  huyo  Alikuwa Masomoni Mida Ya Usiku Na Alipomaliza Aliondoka Na Kuelekea Maeneo Ya Esami. Kabla Hajafika Eneo La Malazi (Hostel) alipigiwa Simu na Mwenzake amsubiri Ili Waende Wote Hostel. 
   Marehemu  Henry  katika enzi za uhai wake....

Wakati anamsubiri Rafiki Yake Kwenda Hostel, Kuna Bajaj Ilifika Eneo Hilo Na Watu Hao Wasiojulikana Wakataka Pesa Kutoka Kwa Mwanafunzi Huyo...Wakati  wakiendelea  kuzozana, rafiki  yake  naye  alifika.....
 
Majibu Ya Wanafunzi Hao Hayakuwafurahisha Watu Hao Na Ndio Walipochomoa Kisu Na Kumchoma Mmoja wa Vijana Hao Tumboni Na Shingoni na Kupoteza Maisha Hapo Hapo....

Mauaji  hayo  yamesababisha  vurugu  kubwa  chuoni  hapo  zilizopelekea  kupigwa  mawe  mkuu wa  mkoa

UMEZISOMA HIZI?

VURUGU KUBWA CHUO CHA UHASIBU:....MKUU WA MKOA APIGWA MAWE, GODBLESS LEMA AFICHWA..!!


Vurugu  kubwa  zimeibuka  chuo  cha  uhasibu cha Arusha   baada ya mwanachuo kuchomwa kisu na mwanaakijiji na kufariki dunia....

Baada  ya  tukio  hilo, wanafunzi  walitoa  taarifa  kwa  mkuu wa chuo lakini  hakuwapa msaada wowote.


Walipokosa  msaada,wanafunzi  hao walianza  kuandamana  na taarifa zikafikishwa kwa mbunge  Godbless  lema ....


Mbunge  huyo  bila   hiyana akawasili na kufanikiwa kuwatuliza wanachuo hao maana nyumbani kwa Godbless  lema si mbali na chuo hicho ...

Baada  ya  taarifa  kumfikia Mkuu wa mkoa, ilimbidi  aliwasili na kuanza kuzungumza na wanachuo lakini baada ya kugundua uwepo wa Lema alianza kuongea  kwa  lugha  mbovu  na  ndipo wanachuo walipo kasirika na kuanza kumpiga mawe.


Hali  ilipochafuka,FFU  waliingia kazi  ya  kutuliza  ghasia...Hali ni mbaya sana lakini cha kushangaza askari mmoja aliwatonya wanachuo wamfiche Lema


Godbless  Lema  anasakwa mpaka sasana  hajulikani alipo baada ya wanachuo kumficha kusiko julikana.