This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, May 11, 2013

MWANAMKE AUAWA KWA KUPIGWA RISASI KIFUANI NA MAJAMBAZI JIJINI DAR



Majambazi yamempora mama mmoja kiasi cha shilingi milioni kumi na kutokomea kusikojulikana....
Tukio hilo limetokea leo saa 5:16 jioni  na inavyosemekana  ni  kuwa mwanamke  huyo  alikuwa akitoka benki ya CRDB tawi la Uhuru ambapo majambazi yakiwa na pikipiki yalikuwa yakimfuatilia..
Alipotoka ,majambazi  hayo  yalimfuata na kuligonga gari lake makusudi   na ndipo dada huyo aliposimama ili angaalie nani kagonga gari yake ambapo jambazi mmoja alishuka na kumpiga risasi ya kifuani na kutokomea na kiasi hicho cha pesa. ..

Clouds Media Group yazindua msimu wake mpya kwa kishindo



Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh Zitto Kabwe ambae pia ni mdau kubwa wa Muziki hapa chnini,pia alikuwa ni mmoja wa wazungumzaji kwenye semini hiyo iliyohusu na  harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi za wasanii,iliyofanyika mapema leo kwenye ukumbi wa hoteli ya African Dreams,nje kidogo ya mji wa Dodoma.…


Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh Zitto Kabwe ambae pia ni mdau kubwa wa Muziki hapa chnini,pia alikuwa ni mmoja wa wazungumzaji kwenye semini hiyo iliyohusu na  harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi za wasanii,iliyofanyika mapema leo kwenye ukumbi wa hoteli ya African Dreams,nje kidogo ya mji wa Dodoma.kutakuwepo na kampeni ya matembezi ya hisani ya harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi za wasanii yatakayofanyika kesho,wabunifu na wavumbuzi mbalimbali, mseto wa shuguli mbalimbali zitahusishwa.  Aidha pia mchana huu kutakuwepo na burudani hadhara ya sanaa za kisasa na za kitamaduni,mpira, chakula na bidhaa mbalimbali za kitanzania katika uwanja wa jamhuri .
 Mmoja wa wasemaji kwenye semina hiyo aliyejitambulisha kwa jina la   Patrick Ngowi  kutoka kampuni ya Helvetic Solar Contractors, akizungumzia fursa mbalimbali kuhusiana na mambo ya ujasiliamali na pia alielezea ni namna gani amefanikiwa mpaka kufikia kumilimiki lampuni yake binafsi kupitia fursa alizokuwa akikumna na nazo na kuzifanyia kazi vilivyo. 
 Mmoja wa washiriki wa semina hiyo akiuliza swali kwa Mh Zitto Kabwa kuhusiana na mambo mbalimbali ya ujasiliamali na namna ya kuzitumia fursa hizo katika kujikwamua kimaisha.
 Mh Zitto kabwe akimsikiliza mmoja wa washiriki wa semina hiyo alipokuwa akiulizwa kuhusiana na suala la fursa zinazopatikana kwa vijana na namna ya kuzitumia katika ujumla wa kujikwamua na ugumu maisha,ambapo watanzania wengi wamekuwa wakizilalamikia.



Mtangazaji wa clouds FM kupitia kipindi cha Power Breakfast-Gerald Hando akiikaribisha Meza kuu pamoja na wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye uzinduzi wa msimu mpya wa Clouds Media Group unaokwenda sambamba na ujumbe wao thabiti kabisa  ulioitwa MADE IN TANZANIA,ikiwa na hamasa kubwa ya kuleta msingi wa fursa kwa watanzania, msukumo ikiwa ni kuwashawishi watanzania kuanza kuzifanyia kazi
fursa hizi kwa umoja na maendeleo ambapo TWENZETU, inakuwa neno rasmi la
mawasiliano.Kama vile haitoshi kutakuwepo na kampeni ya matembezi ya hisani ya harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia
wa kazi za wasanii yatakayofanyika kesho,wabunifu na wavumbuzi mbalimbali, mseto wa shuguli mbalimbali
zitahusishwa  ikiwemo semina ya fursa kwa
watanzania,burudani hadhara ya sanaa za kisasa na za kitamaduni,mpira, chakula
na bidhaa mbalimbali za kitanzania zitapatikana uwanja wa jamhuri mapema leo mchana.

Mmoja wa wasemaji kwenye semina hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Zenno  Ngowi kutoka kampuni ya Tanzania Home Expo akizungumzia fursa mbalimbali kuhusiana na mambo ya ardhi,ujenzi,na mengineyo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria kwenye semina hiyo leo mjini Dodoma.





Mmoja wa wasanii mahiri wa Mashairi,Mrisho Mpoto akifafanua jambo kuhusiana na mambo mbalimbali katika suala zima la wasanii kujipa nafasi ya Fursa mbalimbali zinazojitokeza mbele yao na namna ya kuzifanyia kazi na kuziboresha zaidi.
Mhe Zitto Kabwe akiwasili kwenye semina hiyo mapema leo,ambaye pia alikuwa ni mmoja wa wasemaji wa semina hiyo.
Pichani ni washiriki wa semina hiyo kutoka sehemu mbalimbali mjini Dodoma leo.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia jambo kwenye semena iliyokuwa ikiendelea mapem leo kwenye hoteli ya African Dreamz,nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Mtangazaji wa Clouds FM,Loveness Love a.k.a Diva akijitambulisha kwenye semina hiyo
Mtangazaji wa Clouds FM,Shaffih Dauda akijitambulisha kwenye semina hiyo.
wadau wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye semina hiyo iliyoibua changamoto nyingi.
Kutoka Clouds FM,Millard Ayo,Dina Marios pamoja na Zamarad wakifuatilia jambo
Mtangazaji wa Clouds FM,Arnold Kayanda Diva akijitambulisha mbele ya washiriki waliofika kwenye semina hiyo.
Baadhi ya wasanii wakiwa ndani ya semina hiyo katika harakati rasmi za vita dhidi ya uharamia wa kazi zao,ambapo matembezi ya hisani yamepangwa kufanyika kesho na Waziri Mkuu Mh.Pinda anatarajiwa kuyapokea matembezi hayo.
Msanii Afande Sele na Msanii mwenzake wakiwa ndani ya semina hiyo wakifuatilia yaliyokuwa yakizungumzwa.
Mtangazaji wa Kipindi cha jahazi,Mussa Hussein akijitambulisha.
Mtangazaji wa Clouds FM,B Dozen akijitambulisha
Mbwiga Mbwiguke nae kama kawa akijitambulisha kwa washiriki wa semina hiyo.
Zamarad Mketena akijitambulisha pia.

HUKUMU YA SHEHE PONDA MAAJABU!

5 Comments
Richard Bukos na Makongoro Oging'

MAAJABU yamejitokeza kwenye hukumu iliyomkabili Katibu wa Jumuiya za Kiislamu Tanzania, Shehe Ponda Issa Ponda na wenzake 49, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam juzi Alhamisi baada ya katibu huyo kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje na wengine kuachiwa huru.
...Akiwa Mahakamani akingoja hukumu yahe
SIRI YA KUPEWA KIFUNGO CHA NJE

Wakati wa utetezi wake mahakamani hapo baada ya kuingizwa hatiani na hakimu, Shehe Ponda kupitia wakili wake, Said…

...Akiwa Mahakamani akingoja hukumu yahe
SIRI YA KUPEWA KIFUNGO CHA NJE
Wakati wa utetezi wake mahakamani hapo baada ya kuingizwa hatiani na hakimu, Shehe Ponda kupitia wakili wake, Said Njama aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa sababu amekaa gerezani kwa muda mrefu (tangu Oktoba, 2012).
Pili, Ponda alisema ni kesi yake ya kwanza kupatikana na hatia hivyo yeye si mtu tishio katika jamii.
WANAUME WALIA, WANAWAKE WACHEKA!!
Imezoeleka katika jamii nyingi wanawake ni viumbe dhaifu, wasioweza kuvumilia machungu na hivyo ni wepesi kumwaga machozi, lakini siku ya hukumu, wanaume walioachiwa huru ndiyo waliomwaga machozi bila kujizuia (angalia picha Uk.1).
Baadhi ya wanaume hao waliamua kupiga magoti na kuinua mikono juu huku wakilia kwa furaha ya kuwa huru.
Sasa, wakati hali ikiwa hivyo kwa wanaume hao, wanawake wao walishangilia ‘ushindi’ kwa vicheko vya furaha na kuonesha alama ya ushindi kwa kunyoosha ngumi juu, jambo lililowaacha vinywa wazi watu wengine na kuhoji iweje wanawake wacheke, wanaume walie?
Katika tukio hilo, wanawake ndiyo waliokuwa na kazi ngumu ya kuwabembeleza wanaume hao wasitishe kutoa machozi, jambo ambalo si kawaida kutokea.

WAGOMA KUONDOKA KIZIMBANI BAADA YA KUACHIWA HURU
Mara nyingi washitakiwa wanapoambiwa wako huru hutoka mkuku kizimbani wakati mwingine bila hata kugeuka, hali inayotafsiriwa kwamba huona kizimbani ni mahali penye nuksi, lakini washitakiwa hao walishangaza watu baada ya kuambiwa wako huru waondoke kizimbani lakini wao waliendelea kujiachia bila hofu wakisikiliza kesi ya Ponda ambaye alipatikana na hatia katika shitaka la pili ambalo ni kuingia kinguvu eneo lililokuwa likigombewa (Marcas).

HAKIMU ASOMA HUKUMU NA MSALABA SHINGONI
Maajabu ya tatu mahakamani hapo ni kitendo cha hakimu aliyekuwa akisoma hukumu hiyo, Agustina Mmbando kuvaa mkufu wenye msalaba ambao ulikuwa ukining’inia shingoni bila kujali kwamba ni rahisi watu kujua imani yake hasa kutokana na aina ya kesi.

SERIKALI ILIVYOJIPANGA
Baada ya kutangazwa kwa hukumu ya Ponda, vurugu na mayowe ya kushangilia vilitawala ndani na nje ya mahakama hiyo lakini askari zaidi ya 100 waliojikoki silaha za kutosha, yakiwemo mabomu, risasi za moto na maji ya kuwasha walikaa tayari kuwakabili.
Askari hao walikuwa katika magari aina ya Land Rover ‘Difenda’ zisizopungua 9, pikipiki 20 na farasi 2 walilizunguka kundi kubwa la watu lililoonekana kutaka kuchafua hali ya hewa na kulituliza.
Akiwa na kipaza sauti, afisa mmoja wa jeshi la polisi alilitaka kundi hilo kutawanyika kwa amani mahakamani hapo vinginevo jeshi hilo lingetumia nguvu ya ziada.

PONDA ASAINI FOMU, HAKIMU AMPA CHEO
Ponda alitakiwa kujaza fomu maalum zenye maelekezo ya hukumu yake huku hakimu akimtaka kwenda kuwa mlinzi wa amani na mtatuzi wa migogoro katika jumuiya yake.

MGOGORO WA ARDHI UPO PALEPALE
Licha ya hukumu hiyo, Hakimu Mmbando alisema kuhusu kesi ya mgogoro wa ardhi iliyokuwa ikimkabili Shehe Ponda, mahakama yake haina uwezo wa kusikiliza, hivyo akawashauri walalamikaji kama wanataka kuiendeleza waende Mahakama ya Ardhi.
Kesi iliyomtia hatiani ni shitaka la pili la kuvamia eneo la Marcas, Chang’ombe, jijini Dar kinyume na taratibu.

WAFUASI WATAKA KULISUKUMA GARI LA PONDA
Nje ya mahakama hiyo, wafuasi wa Ponda waliokuwa wakimsubiri walimshangilia baada ya kumwona na kutaka kulisukuma gari lake dogo aina ya Isuzu kama shujaa wa ‘milenia’ lakini dereva wake aliongeza kasi na kutokomea eneo hilo.

MAANDAMANO KUELEKEA MSIKITI WA MANYEMA
Pamoja na Ponda kutimua zake, wafuasi wake waliokosa nafasi ya kuongea nje baada ya kesi kumalizika, waliandamana wakisema wanakwenda Msikiti wa Manyema, Kariakoo, Dar kwa lengo la kuzungumza mawili matatu.

LULU AITWA DUBAI

 

HABARI zilizonaswa na mwandishi  wetu  zinaeleza kuwa nyota wa sinema Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameitwa katika Jiji la Dubai, Falme za Kiarabu kwa ajili ya kula  bata ikiwa ni pole yake kwa kusota Gereza la Segerea kwa karibu mwaka mmoja.

Chanzo kimoja  kilipenyeza habari kuwa mapedeshee hao wamemualika staa huyo huku ikinyetishwa kwamba, vigogo wa sanaa hiyo Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ndiyo watakaomsindikiza.
 

“Mapedeshee wamemtumia mamilioni ya fedha Lulu, wanataka kufanya naye pati ya pamoja kwa vile ni miongoni mwa mastaa wa Bongo wanaokubalika nchini humo na pia kumpa pole kwa kukaa gerezani muda mrefu.
 

“Mbali na sherehe hiyo, watakapokuwa nchini humo wanatarajia kuendeleza filamu ambayo wameanza kuirekodi hapa Bongo,” kilisema chanzo hicho.
 

Hata hivyo, chanzo kiliweka wazi kwamba kwa sasa, Lulu si rahisi kusafiri nje ya Bongo kwa vile kesi aliyonayo ina mipaka ya sehemu za kwenda.
Alipotafutwa Dk. Cheni juu ya ishu hiyo, alisema waliomuita Lulu si mapedeshee bali ni Wabongo waishio kule, lakini masharti ya kesi yake hawezi kusafiri nje ya Tanzania.
Dk. Cheni akaulizwa kuhusu yeye na Steve Nyerere kuwepo kwenye safari hiyo ambapo alisema hana ufafanuzi zaidi, akakata simu.

JESHI LA TANZANIA LATAMBA TENA.....LINASEMA KAZI YAKE NI MOJA TU AMBAYO NI KUWAFUMUA WAASI WA M23 HUKO KONGO


JESHI la Wananchi Tanzania (JWTZ), limesema limeanza kuwapeleka askari wake nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo (DRC) kulinda amani na kuhakikisha wananyang’anywa silaha zote waasi wa kundi la M23 ili nchi hiyo itawalike.

Kutokana na hatua hiyo, JWTZ limesema halitishwi na vitisho vya M23 kutokana na kujiandaa vizuri kila idara, ikiwa ni lengo la kutaka kuona wananchi wa DRC wanaishi kwa amani, tofauti na sasa ambako kumekuwa na vitendo vya kinyama dhidi ya wanawake na watoto wadogo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, wakati wa kutoa tamko la jeshi hilo, Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe, alisema kamwe hawatishwi na kundi la M23.

Alisema wanashangazwa na kitendo M23 kutoa vitisho, wakati askari wanaokwenda huko wanatoka nchi za Afrika Kusini, Malawi na Tanzania.

“Kwa nini iwe Tanzania pekee, sisi hatuwezi kutishwa na kikundi cha wanamgambo 1,000, tunasema tunakwenda kutimiza jukumu la Umoja wa Mataifa (UN) kuhakikisha DRC inatawalika na silaha zote wananyang’anywa,

“Tanzania tuna historia kubwa ya kuleta ukombozi na amani ndani ya nchi za Afrika, zikiwamo Commoro, Afrika Kusini, Liberia, Sudan na Lebanon, ndiyo maana vikosi vyote vitatu vinaongozwa na Mtanzania, Brigedia Jenerali James Mwakibolwa.

“Tulipokwenda Commoro, tulihisi kama damu itamwagika lakini hali ilikuwa tofauti kabisa na isitoshe ni askari mmoja tu aliteleza na kuanguka majini, sasa hawa M23 wao wamepata wapi mafunzo.

“Itakumbukwa Idd Amin Dada, alikuwa anajigamba na kusema anataka kuja kunywa chai Dar es Salaam, lakini aliishia kuchungulia visiwa vya Ukerewe… majigambo ya M23 ni ishara ya kuanza kuwa na wasiwasi,” alisema Kanali Mgawe.

Alisema kikosi kilichoanza kwenda DRC,kinajulikana kama Tanzania Bataria One –DRC (TANZBATT-1 DRC) na kuongeza kwamba kila baada ya miezi sita kutafanyika mabadiliko kadri itakavyohitajika.

Alisema kutokana na vitisho hivyo, bado Tanzania ni salama na itakuwa kuwa salama na kuwataka Watanzania kuondoa hofu juu ya matukio yanayotokea hivi sasa.

Alisema vifaa vya askari, wanaokwenda Kongo vimekamilika na tayari UN imevifanyia ukaguzi na kuridhia vinakidhi mahitaji katika kuimarisha ulinzi na usalama.

Kuhusu mzozo wa Tanzania na Malawi, alisema nchi hizo bado zina uhusiano mzuri wa kidiplomasia.

Mapema wiki hii, Rais Jakaya Kikwete aliwakabidhi askari wa JWTZ bendera mkoani Pwani, ikiwa ni ishara ya kuanza safari ya kuelekea DRC.

VIDEO YA CHID BENZ ALIPOCHEZEA KICHAPO PALE MAISHA CLUB


 Jumapili hii kwenye ukumbi wa New Maisha Club, kulitokea ugomvi kati ya rapper Chidi Benz na Kalapina aliyekuwa na show yake pamoja na Kikosi cha Mizinga. 


Tukio lilitokea baada ya Chidi Benz kupanda ghafla kwenye stage na kumnyang’anya kipaza MC wa show hiyo wakati Nikki Mbishi alipokuwa kwenye stage. 

Baada ya kupanda juu, Chidi aliyekuwa amelewa alianza kuwaongelesha na kuwaimbia mashabiki waliokuwa wakimshangilia. 


“Naomba niongee kitu kimoja ambacho ninyi watu woote ambao mpo humu ndani mtasikiliza, au vipi, nimeingia na beibe beibe, nimeingia VIP halafu nimemuona Nikki Mbishi anachana hapa stage, Nikki njoo njoo Nikki njoo, sijui show ya nani kwasababu yako wewe nimekuona nilikuwa paleeee, nimepita nimekuja hapa nimekuona mdogo wangu, sasa nini sasa, piga keleleeee,” alisikika akisema Chidi huku watu wakimshangilia na baadaye microphone kuzimwa. 
 
Baadaye Kalapina alipanda kwenye stage na kuchukua microphone, “Oii ambaye hahusiki na show ashuke,” alisema Kalapina na kumfuata Chidi kisha kumpiga na kumwangusha chini. “Ninyi mnamwachia mtoto m*** apande kwenye stage,” alisema Kalapina wakati huo Chidi Benz aliyekuwa anataka kurudi tena kwenye stage kupigana akiwa ameshikiliwa na watu wa ulinzi.

VIDEO : CHID BENZ ACHEZEA KICHAPO KWA MARA NYINGINE  TOKA  KWA  KALAPINA 

ASKARI ALIYEMUUA MTOTO MDOGO WA RISASI AKAMATWA......CHADEMA WAANDAMANA, POLISI YAJIBU MAPIGO

ASKARI Polisi wa Kituo cha Tarime mkoani Mara mwenye namba D. 4662 Koplo Mathew, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za uzembe uliosababisha kifo kwa risasi cha mwanafunzi wa darasa la kwanza wa shule ya Msingi Rebu, Deus Jacob (9).
Kifo hicho kilitokea wakati polisi wakiwa kwenye harakati za kukamata mtuhumiwa, Marwa Bisara, mkazi wa kitongoji cha Songambele kata ya Sabasaba mjini hapa, aliyekuwa akituhumiwa kwa shambulio na kudhuru mwili.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tarime/Rorya, Justus Kamugisha, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 10 jioni katika kitongoji cha Songambele, baada ya Koplo Mathew na askari wenzake wakiwa na mlalamikaji, wakifuatilia mtuhumiwa na kumkuta na wenzake katika pagala wakivuta bangi.
 
Wakati polisi wakijiandaa kumkamata, mtuhumiwa Bisara alimvamia Koplo Mathew akitaka kumnyang'anya bunduki na katika purukushani hiyo, risasi zilifyatuka na moja kumpata Deus kichwani na kumuua papo hapo baada ya kichwa kufumuka.
Kamanda Kamugisha alisema chanzo cha mauaji ni mtuhumiwa Bisara kukaidi amri ya kukamatwa. Lakini mwenzake Julius Maseke (38) mkazi wa mtaa wa Ronsoti alikamatwa akiwa na misokoto 47 na kilo 3.25 za bangi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote.
 
Polisi ilitoa mwito kwa raia wema kutoa taarifa kwa vyombo husika watakapomwona Bisara na inaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele alionya wanasiasa waache kulitumia tukio hilo kisiasa kwa kuwa marehemu Deus hakuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. 
Alionya hivyo kwa alichokisema ni baadhi ya wafuasi wa Chadema kuchocheana kufanya vurugu wakihamasishana kuchukua mwili wa marehemu huyo na kufanya maandamano kwenda Bomani ziliko ofisi za Mkuu wa Wilaya na Kituo cha Polisi.
 Hata hivyo, maandamano hayo yalizimwa na Polisi kwa kutumia mabomu ya kutoa machozi na mwili huo uko katika mochari ya hospitali ya wilaya na unatarajiwa kuzikwa leo.

NI USIKU WA HIP HOP NA MIC KING DAR LIVE MEI 25, 2013


wakazi wa dodoma waupokea kwa kishindo msimu mpya wa clouds Fm