This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, October 9, 2014

BAADA YA KIPA DE GEA KUTISHIA KUONDOKA OLD TRAFFORD, PETER CECH NAE ATINGISHA KIBERITI DARAJANI ATISHIA KUONDOKA KAMA HATAKUWA MLINDA LANGO NAMBA MOJA

Cech akitolewa nje baada ya kuumia bega la kushoto wakati Chelsea ikabiliana na Atletico Madrid dimbani Vicente Calderon msimu uliopita katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya mchezo ambao ulikwisha kwa timu kutoka suluhu.
Mlinda lango nyota na mwenye heshima kubwa Stanford Bridge, Petre Cech amefunguka kwenye vyomba vya habari leo hii na kusema kama ataendelea mlinda lango chaguo la pili (namba 2) katika klabu ya Chelsea, ni baro akaondoka na kutafuta klabu nyingine itakayompa nafasi ya kwanza.
Cech alipata jera kubwa katika bega lake la kushoto msimu uliopita wakati Chelsea ikipepetana na Atletical Madrid mwezi July katika mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya hali iliyomfanya yeye kumalizia msimu wa 2013/2014 akiwa nje ya dimba tangu pale alipo pata majeraha na nafasi yake kuchukuliwa na Mark Schwarzer kabla ya Thibault Courtois kurejea Chelsea akitokea Atletical Madrid alipokuwa akicheza kwa mkopo. 
 
Petre Cech ni mmoja wa wachezaji nguli katika klabu ya The Blues, kwani mpaka sasa amedumu klabu hapo kwa takaribani miaka 10, huku akifanikiwa kuichezea klabu hiyo michezo 500. Lakini, tangu msimu wa 2014/2015 uanze Cech hakuendelea kuwa golikipa chaguo namba moja katika klabu ya Chelsea kwani mlinda lango anayechipukia kwa kasi,Thibault Courtois 22, ameoneka kufanya vizuri sana kitendo kilichomfanya Jose Mourinho kumuamini zaidi.

Huyu pia ni goli kipa bora wa ligi kuu nchiniUingereza msimu uliopita wa 2013/2014
Cech amekariri akilalama kuwa, haoni sababu yeye kusugua benji akiwa kama chaguo namba mbili kwa Mourinho kwani kuna michezo mikubwa na migumu ipo mbele yake kama vile, michuano ya mabingwa wa Ulaya ya 2016 pamoja na majukumu makubwa aliyonayo katika timu ya taifa, hivyo kucheza kama chaguo namba mbili kwa Chelsea anaona ni hatari sana kwani anaamini itadhoofisha uwezo wake.
Petre Cech alichechea Chelsea kwa mara ya kwanza tangu msimu huu uanze wakati Chelsea ikicheza dhidi ya Arsenal Juma pili iliyopita Dimbani Stanford Bridge, baada ya Courtois kuumia. Mchezo huo ulimalizika kwa Chelsea kuibuka na ushindi wa magoli 2-0, kichapo ambacho kiliendelea kumpa Arsena rekodi mbaya ya kuchezea kichapo mara kwamara wanapokutana na Chelsea kwa muda mrefu.

REDD'S MISS TANZANIA 2014 KUFANYIKA MLIMANI CITY JUMAMOSI HII


Mkurugenzi wa Kampuni ya Rino International Agency ambao ni waratibu wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo,juu ya onyesho la Redd's Miss Tanzania 2014 linalotarajiwa kufanyika Oktoba 11,2014 katika Ukumbi wa Mlimani City,Jijini Dar.Katikati ni Meneja wa Kinywaji cha Redd's ambao ni Wadhamini Wakuu wa Mashindano hayo,Victoria Kimaro na kushoto ni Meneja Maria Stopes Tanzania,Anna Shanalingigwa.Picha zote na Othman Michuzi.

Meneja wa Kinywaji cha Redd's ambao ni Wadhamini Wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Victoria Kimaro (kushoto) akizungumzia zawadi watakayotoa kwa Washindi watakaopatikana kwenye Shindano hilo la Redd's Miss Tanzania 2014,ambapo mwaka huu mshindi wa kwanza katika kinyang'anyiro hicho atajinyakulia kitita cha sh. Mil. 18 taslim huku washindi wengine wakiendelea kuondoka na zawadi mbali mbali.Katikati ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Rino International Agency ambao ni waratibu wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga na kulia ni Meneja wa Hoteli ya JB Belmont,Gillian Macheche pamoja na Afisa Habari wa Miss Tanzania,Hidan Ricco.

Sehemu ya Wanahabari pamoja na Warembo watakaoshiriki kwenye kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania 2014 wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Kampuni ya Rino International Agency ambao ni waratibu wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga alipokuwa akizungumza.




Sehemu ya Warembo watakaoshiriki kwenye kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania 2014

Warembo watakaoshiriki kwenye kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania 2014 wakipata "SELFIE" mwanana kabisa.

WEMA ASHINDWA KULIPA MAPIGO YA DANGOTI


 Mwana mitindo maarufu na msaani wa bongo movie wema sepetu ameshindwa kujibu mapigo ya bwana wake diamond kwa kushindwa kumpa zawadi katika siku yake ya kuzaliwa kwake

Thursday, July 24, 2014

Mlipuko waua 40, Nigeria

Watu wapata 40, wameuawa katika milipuko mikubwa miwili iliyotokea katika mji wa Kaduna, kaskazini mwa Nigeria. Katika mlipuko wa kwanza wa kujitoa mhanga watu 25 waliuawa, huku wengine 15 wakiuawa katika eneo lililokuwa na msongamano wa watu katika mji wa Kawo.
Shambulio hilo pia lilimlenga kiongozi wa upinzani na kiongozi wa zamani wa kijeshi Jenerali Muhammadu Buhari.
Shambulio la kwanza lilimlenga kiongozi mashuhuri wa kiislam aliyeambatana na wafuasi wake alipokuwa akitoka katika eneo la katikati ya Kaduna alikomaliza kufanya muhadhara kwa ajili ya mwezi mtukufu wa ramadhani. Maelfu ya watu walihudhuria tukio hilo la mwaka.
Kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo, watu 25 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa. Shambulizi la pili lilimlenga kiongozi wa juu wa upinzani ambaye pia ni rais wa zamani Jenerali Muhammadu Buhari ambako nako wamekufa watu 19. Wote wawili, kiongozi wa kiislam na kiongozi wa upinzani wamenusurika bila kujeruhiwa.
Mwanahabari wa BBC amesema aliona viungo vya binadamu vikiwa vimetapakaa katika eneo kubwa la mlipuko. Kamishina wa polisi wa jimbo la Kaduna Alhaji Umar Usman Shehu amesema mlipuko ulisababishwa na anayehisiwa kujitoa muhanga.
Hakuna kundi lolote lililojitokeza kuhusika na mlipuko huo. Kundi la Boko Haram ambalo bado linawashikilia wanafunzi wasichana 200 kwa takribani siku 100 sasa, limeshafanya matukio ya kulipua mabomu kwa kujitoa muhanga katika miji mingi kaskazini mwa naijeria ukiwamo mji mkuu Abuja.
CHANZO BBC,(A.I).