Thursday, October 9, 2014

BAADA YA KIPA DE GEA KUTISHIA KUONDOKA OLD TRAFFORD, PETER CECH NAE ATINGISHA KIBERITI DARAJANI ATISHIA KUONDOKA KAMA HATAKUWA MLINDA LANGO NAMBA MOJA

Cech akitolewa nje baada ya kuumia bega la kushoto wakati Chelsea ikabiliana na Atletico Madrid dimbani Vicente Calderon msimu uliopita katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya mchezo ambao ulikwisha kwa timu kutoka suluhu.
Mlinda lango nyota na mwenye heshima kubwa Stanford Bridge, Petre Cech amefunguka kwenye vyomba vya habari leo hii na kusema kama ataendelea mlinda lango chaguo la pili (namba 2) katika klabu ya Chelsea, ni baro akaondoka na kutafuta klabu nyingine itakayompa nafasi ya kwanza.
Cech alipata jera kubwa katika bega lake la kushoto msimu uliopita wakati Chelsea ikipepetana na Atletical Madrid mwezi July katika mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya hali iliyomfanya yeye kumalizia msimu wa 2013/2014 akiwa nje ya dimba tangu pale alipo pata majeraha na nafasi yake kuchukuliwa na Mark Schwarzer kabla ya Thibault Courtois kurejea Chelsea akitokea Atletical Madrid alipokuwa akicheza kwa mkopo. 
 
Petre Cech ni mmoja wa wachezaji nguli katika klabu ya The Blues, kwani mpaka sasa amedumu klabu hapo kwa takaribani miaka 10, huku akifanikiwa kuichezea klabu hiyo michezo 500. Lakini, tangu msimu wa 2014/2015 uanze Cech hakuendelea kuwa golikipa chaguo namba moja katika klabu ya Chelsea kwani mlinda lango anayechipukia kwa kasi,Thibault Courtois 22, ameoneka kufanya vizuri sana kitendo kilichomfanya Jose Mourinho kumuamini zaidi.

Huyu pia ni goli kipa bora wa ligi kuu nchiniUingereza msimu uliopita wa 2013/2014
Cech amekariri akilalama kuwa, haoni sababu yeye kusugua benji akiwa kama chaguo namba mbili kwa Mourinho kwani kuna michezo mikubwa na migumu ipo mbele yake kama vile, michuano ya mabingwa wa Ulaya ya 2016 pamoja na majukumu makubwa aliyonayo katika timu ya taifa, hivyo kucheza kama chaguo namba mbili kwa Chelsea anaona ni hatari sana kwani anaamini itadhoofisha uwezo wake.
Petre Cech alichechea Chelsea kwa mara ya kwanza tangu msimu huu uanze wakati Chelsea ikicheza dhidi ya Arsenal Juma pili iliyopita Dimbani Stanford Bridge, baada ya Courtois kuumia. Mchezo huo ulimalizika kwa Chelsea kuibuka na ushindi wa magoli 2-0, kichapo ambacho kiliendelea kumpa Arsena rekodi mbaya ya kuchezea kichapo mara kwamara wanapokutana na Chelsea kwa muda mrefu.

0 comments: