This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, March 29, 2014

AJALI MBAYA: MWANAFUNZI MAKONGO AFARIKI KATIKA AJALI YA BAJAJ NA LORI


Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Makongo, Priscus Mallya, baada ya kufariki katika ajali ya lori na Bajaj.
Mwili wa  Priscus Mallya ukiwa katikati ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi baada ya ajali.
Bajaji ambayo mwanafunzi alikuwa amepanda akielekea shuleni Makongo ikiwa eneo la ajali.
 
MWANAFUNZI wa kidato cha nne, Shule ya Sekondari Makongo, Priscus Mallya, amefariki dunia katika ajali iliyolihusisha lori na Bajaj katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi eneo la Bamaga, Dar.
Kwa mujibu wa watu waliokuwa eneo la tukio wakati ajali hiyo ikitokea, wamesema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ndani ya Bajaj pamoja na wenzake wawili wakielekea shuleni Makongo ambapo walikutana uso kwa uso na lori kisha kumrusha na kutokea upande wa pili

AIBU: DENTI WA KIKE MWANACHUO AVULIWA NGUO HOSTEL BAADA YA KUIBA SIMU AINA YA BLACKBERRY



tanamaa zinazidi kuwaponza dada zetu siku hizi, binti mmoja huko nigeria amejikuta matatani baada ya vidume kumsaula nguo zote baada ya kuiba simu ya mwenzake wanaelala nae chumba kimoja,

mkasa ulianza pale binti alipotafuta simu yake kwa mda wa masaa matatu bila mafanikio ndipo alipowaita wenzake nakuanza kupekua, atimaye wakapata wazo la kuipiga simu hyo ambayo iliita mfukoni mwa mwizi huyo. alipoambiwa apokee mwizi huyo aliruka mita mia mbili ndipo mzozo ulipozidi majirani wakaingia na kuamua kumvua nguo zote na kumuacha mtupu wa mnyama na ndipo simu ilikutwa kwenye nguo ya ndani ya binti huyo.....hii nifundisho kwa wale kina dada wapenda vya bure na tamaa za hapa na pale

MWALIMU ANASWA LIVE AKIJIUZA MBAGALA DAR...!JIONEE MWENYEWE HAPA


AIBU! Wakati Wakristo bado wapo kwenye Kwaresma, mama aliyejitambulisha kuwa ni mwalimu wa shule ya msingi, amenaswa laivu akijiuza maeneo ya Mbagala-Zakhem jijini Dar. 
Mwalimu akiwa ameduwaa baada ya kunaswa kwenye sakata hilo.
 Tukio hilo la kusikitisha lilijiri Machi 24, mwaka huu ambapo awali, wakazi wa eneo hilo waliwatonya mapaparazi wa Operesheni Fichua Maovu (OFM) kuwa kuna danguro kubwa maeneo ya Kizuiani ambalo limesheheni madadapoa wa kila aina wakiwemo mabinti wadogo. 

Chanzo hicho kilimwaga data kuwa, kuna mzee maarufu kwa jina la babu katika eneo hilo ambaye amekuwa akiwapa machangudoa hifadhi katika banda lake na kuwapa magodoro chakavu kwa malipo ya shilingi elfu moja kwa kila kichwa. 

KISIKIE CHANZO
“Jamani kwenye danguro hili kila aina ya uchafu upo. Wanatukwaza sisi Wakristo ambao tupo katika kipindi hiki cha Kwaresma,” kilitiririka chanzo hicho cha kuaminika maeneo hayo.
 

OFM KAZINI
Ili kujiridhisha na taarifa hizo, makamanda wawili wa OFM walitimba katika danguro hilo wakajifanya wateja ambapo walimchukua mmoja na kubaini kuwa ni mwalimu wa shule ya msingi.

 
Mwalimu na wenzake wakiwa chini ya ulinzi.
 TUJIUNGE NA CHANGU MWALIMU
“Kaka ongea fasta nipe changu, usinione hivi mimi ni mwalimu wa msingi, mshahara haukidhi halafu isitoshe serikali haijatulipa malimbikizo yetu, watulipe bwana pengine tunaweza kujikwamua,” alisema changu huyo ambaye alimtaka kamanda wa OFM alipie shilingi elfu kumi kama malipo ya huduma tendo moja.
 

POLISI WAITWA
Baada ya kujiridhisha kwa uwepo wa biashara hiyo, OFM waliwapigia simu polisi wa Kituo cha Kizuiani, wakafika na kufanikisha zoezi la kuwakamata machangu wapatao 16 pamoja na babu anayewapa hifadhi ili wauze miili.

 
...Wakiingizwa kwenye gari la polisi.
 VIBANDA KIBAO VYABAINIKA
Wakati zoezi la kuwakamata likiendelea maeneo hayo, vilibainika vibanda vingi  ambavyo machangu hao hufanyia uchafu wao pamoja na mfuko mkubwa ambao madadapoa hao huhifadhia nguo zao za heshima kabla hawajaingia ‘mzigoni’.
 
  WAACHA WATOTO NYUMBANI
Baadhi ya machangudoa hao waliotiwa mikononi mwa polisi, walikiri kuwa wamewaacha watoto wao nyumbani huku wengine wakidai ni wake za watu hivyo kuomba wasipigwe picha kukwepa aibu pindi zitakapochapishwa gazetini.

 
Watuhumiwa wakiwa kwenye gari la polisi chini ya ulinzi mkali.
 “Jamani msitupige picha sisi wengine tuna watoto na waume zetu, tunaomba msamaha jamani,” walisikika madadapoa hao.  
 WAFIKISHWA POLISI
Baada ya kamatakamata kukamilika, machangu hao pamoja na mzee huyo walipandishwa kwenye difenda la polisi na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Kizuiani kwa ajili ya uchunguzi zaidi kabla ya kufikishwa Mahakama ya Jiji kujibu mashitaka ya uzururaji.

HIVI NDIVYO VYAKULA 10 AMBAVYO MWANAUME ANATAKIWA KULA ILI KUONGEZA UWEZO WAKATI WA TENDO LA NDOA.


CHAZA NA PWEZA
Aina hizi za samaki zinazovuliwa baharini huwa na madini ya zink na chumvi ambayoyanatajwa kusaidia uzalisha wa vichocheo vinavyohamasisha msisimko wa mwili wakati wa tendo la ndoa.

POMEGRANATE

Ni aina fulani ya matunda mekundu yanayofananana na apple. Haya yatajwa kusaidia kuamsha mishipa ya fahamu na kuweka mawasiliano sahihi ya mwili na hivyo kumuongezea mtu uwezo kwa kufanya tendo la ndoa kwa hamasa kubwa.


Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. 


Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume na kuacha idadi ya wanawake wanaokabiliwa na tatizo hilo kwa mujibu wa uchunguzi kubaki na asilimia 13.




Pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili.




Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina kumi ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa. Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo:




PILIPILI
Pilipili zilizocheshwa zimetajwa kuwa na uwezo wa kusaidia msukumo wa usambazaji damu mwilini, ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo unaoweza kumfanya mtu akawa na hisia kali za kimapenzi. Kwa msingi huo, ni vema kwa wale wanaokabiliwa tatizo la uwezo wa kufanya mapenzi wakatumia pilipili si kwa wingi bali kwa kiwango stahili, ili waamshe hisia zao.



PARACHICHI
Aina nyingine ya chakula ambacho husaidia kuongeza uwezo wa mtu kufanya tendo la ndoa ni Parachichi. Tunda hili linauwezo mkubwa wa kuzalisha vitamini E ambayo husaidia katika uzalishaji wa homoni. Inatajwa kuwa watu wanaotumia tunda hili kwa wingi huwana msisimko mkali wa kimapenzi na kwa upande wa wanawake husaidia kuongeza majimaji yenye utelezi sehemu za siri na hivyo kuzuia uwezekano wa kuchubuka wakati wa kujamiiana.




NDIZI
Wakati unafikiria uwezo wa kufanya vema tendo la ndoa unatakiwa kuwaza juu ya uimara wa misuli ya mwili ambayo inatajwa kuwa ni sehemu kuu na yenye muhimu katika kujamiiana. Kwa msingi huo ulaji wa ndizi mbivu unatajwa kusaidia kujenga misuli mwilini na kumfanya mtu aweze kuwa hodari katika tendo la ndoa.



CHOKOLETI
Ulaji wa Chokoleti huongeza uchangamfu mwilini na, hivyo kumuwezesha mtu anayeshiriki tendo la ndoa kuwa na mguso sahihi kwenye fikra zake, jambo litakalomuwezesha kupokea hisia za mapenzi kwa urahisi zaidi ya mtu ambaye anakwenda kwenye uwanja wa sita kwa sita akiwa mchovu wa mawazo.





MVINYO MWEKUNDU
Mvivyo mwenyekundu unatajwa kuwa na uwezo wa kuuchangamsha mwili na kuongeza msukumo wa damu, kiasi cha kumuondolea mtu uchovu kabla na baada ya tendo la ndoa, hivyo ni muhimu kunywewa hasa na wale ambao wanasumbuliwa na tatizo la kushindwa kurudia tendo. 



MBEGU ZA MATUNDA
Mchangayiko wa mbegu mbalimbali za matunda, mfano tikiti, maboga husaidia kuondoa ACID mwilini na kumfanya mtu ajione ni mwenye afya njema.



VANILLA
Vanila husaidia kuamasha hamasa mwili.


Mwisho wa aina hizi za vyakula ni TIKITI MAJI ambalo linatajwa kuwa na virutubisho vingi vyenye uwezo wa kuusaidia mwili kuwa na nguvu za kutosha kufanya tendo la ndoa.

RAIS JAKAYA KIKWETE AMESEMA NITAVUNJA BUNGE LA KATIBA NA KUENDELEA NA KATIBA YA ZAMANI KAMA WAJUMBE AWATAACHA FUJO




RAIS Jakaya Kikwete amesema kama mchakato wa upatikanaji Katiba Mpya utakwama kwa namna yoyote, Katiba iliyopo sasa itafanyiwa marekebisho na kuendelea kutumika.
 
Alisema kama Kiongozi Mkuu wa Serikali ni wajibu wake kuwaeleza ukweli wananchi kama alivyowasilisha hotuba yake kwa wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba Mjini Dodoma, kuhusu hatari ya muundo wa Serikali tatu ambayo ndiyo iliyopendekezwa kwenye rasimu.
 
Rais Kikwete aliyasema hayo juzi wakati akijibu risala ya wazee wa Wilaya ya Muheza, mkoani Tanga, waliofanya mazungumzo naye nyumbani kwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Subira Mgalu, akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani humo.
 
Alisema Katiba ni jambo muhimu katika nchi na itatumika kwa miaka 50 ijayo hivyo ni wajibu wa wajumbe kupitisha Katiba bora ambayo utekelezwaji wake hautakwama baada ya kupitishwa.
 
Aliongeza kuwa, pamoja na kasoro zilizopo kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba, bado hakuwasemea wajumbe wa Bunge hilo katika hotuba yake aliyoitoa bungeni bali aliamua kuweka bayana kasoro husika ili wajumbe waamue wenyewe muundo wa Serikali mbili au tatu kwani uamuzi ni wao.
 
"Mimi niliamua kutoa maoni yangu baada ya kuona Rasimu ina kasoro kwenye muundo wa Serikali tatu, sikuchukua mamlaka ya wajumbe wa Bunge hili au kuwaongoza, bali nilieleza kile ninachoamini kinaweza kutupa Katiba bora.
 
"Katiba si kwa ajili ya matumizi ya leo tu, bali kwa vizazi na vizazi, tusije kutengeneza Katiba ambayo haitekelezeki, lakini wenye maamuzi ni wajumbe wenyewe, mimi siwezi kuwatolea uamuzi lakini kama Katiba Mpya itashindwa kupatikana, hii iliyopo itafanyiwa marekebisho na mambo yataenda," alisema.
 
Akisoma risala ya wazee hao, Katibu wao Bw. Hamis Mzee, alisema wao kama wazee wanaunga mkono hotuba aliyoitoa kwa wajumbe wa Bunge hilo kwani imelenga kuwahurumia Watanzania na mzigo wanaotaka kubebeshwa na watu wachache.
 
"Sisi tunaunga mkono hatuba yako, msimamo wetu ni Serikali mbili ambazo ndizo zenye uwezo wa kuwahudumia wananchi vizuri si Serikali tatu," alisema Bw. Mzee.
 
Awali Mwenyekiti wa wazee hao, Dorothy Kihampa alisema Rais Kikwete amekuwa akiwapenda wazee na wao wanamuombea kama alivyoanza salama, basi atamaliza salama uongozi wake.
Msimamo Baraza la vyama
 
Wakati huo huo, Baraza la Vyama vya Siasa, jana limetoa tamko kuhusu mwenendo wa Bunge Maalumu la Katiba na kusisitiza hauridhishi kama ilivyotarajiwa na watu wengi.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Dodoma jana, Mwenyekiti wa baraza hilo, Bw. Peter Mziray alisema hali hiyo inatokana na migongano mingi inayotokea ikiongozwa na makundi ya vyama vya siasa na wanasiasa kwa nyadhifa zao tofauti.
 
"Tumekuwa tukifuatilia na kuangalia kwa makini mchakato huu na kuona wanasiasa kama wadau wakubwa wanaweza kuukwamisha kutokana na malumbano yasiyo na tija na mienendo na matendo yasiyokubalika," alisema Bw. Mziray.
 
Aliongeza kuwa, wanasiasa wamekuwa wakilalamikiwa katika mchakato huo ambapo Kamati ya Uongozi ya bara hilo, imebaini uwepo wa makundi yasiyo rasmi ndani ya Bunge hilo.
 
"Mfano wa makundi haya ni UKAWA na Tanzania Kwanza, inaonesha Bunge hili linayatambua makundi haya ambayo kimsingi kutambulika kwake, kunachochea mgawanyiko, kujenga uhasama kati ya wajumbe hivyo kudhoofisha dhana ya kufanya kazi pamoja na kufikia maridhiano.
 
"Tunatoa wito kwa wajumbe wote wa Bunge hili, kuacha kujihusisha na makundi haya badala yake wachambue na kuunga mkono hoja kwa uzito wa hoja yenyewe na kuzingatia maslahi ya Taifa badala ya kuzingatia mtazamo au msimamo wa kundi fulani," alisema Bw. Mziray.
 
Aliwataka wananchi kutambua kuwa, Bunge hilo ndio nyenzo muhimu ya kupata Katiba Mpya wanayoitaka hivyo ni vyema wakashiriki kuwahimiza wawakilishi wao watekeleze majukumu yao vizuri kwa kuepuka kufanya vitendo vya aibu na kuacha kujali masilahi binafsi bali watangulize utaifa.
 
"Kamati hii inasikitishwa na ukosefu wa nidhamu ndani ya Bunge hili jambo ambalo halikubaliki hata kwa watoto wa shule ya msingi wawapo darasani," alisema.
 
Alitoa wito kwa wajumbe wa Bunge hilo kuzingatia kanuni ambazo zinakataza vitendo vyovyote vya utovu wa nidhamu pamoja na kuzomea bali kila mjumbe anaweza kutoa hoja na inaweza kupingwa au kukubaliwa bila kuzomea.
 
Bw. Mziray alisema, kutokana na mwenendo wa Bunge hilo ni vyema Kamati ya Uongozi wa baraza hilo, ikutane na viongozi wote wakuu wa vyama vya siasa ambao si wajumbe wa baraza ili kushauriana na kuokoa mchakato huo.
 
Mbowe atoa lawama
Katibu wa Kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), ambaye ni mjumbe wa Bunge hilo, Bw. Freeman Mbowe, ameitupia lawala sekretarieti ya Bunge Maalumu la Katiba akidai inaonekana kupokea maelekezo kutoka serikalini juu ya uendeshaji wa Bunge likiwemo suala la kubadilisha kanuni za Bunge hilo.
 
Bw. Mbowe aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ubadilishwaji wa kanuni na kuongeza kuwa, suala la kubadilisha kanuni bila ridhaa ya wajumbe ni kutengua azimio la Bunge hilo ambalo ndilo linalopitisha kanuni hizo.
 
Alisema kitendo hicho kinaashiria kutaka kulivuruga Bunge hilo ili mchakato wa kupata Katiba Mpya usifanikiwe kwani kanuni hizo zilitungwa kwa kipindi kirefu kupitia semina isipokuwa kanuni ya 37 na 38 inayoeleza aina ya upigaji kura.
 
"Aliyepewa jukumu la kubadilisha kanuni hizi ni nani, inaonekana Sekretarieti ya Bunge hili inapata maelekezo kutoka nje ya Bunge kwa maana ya serikalini, wanakaa na kuamua mambo ya Bunge hili na kutuletea, sisi UKAWA tunataka haki itendeke, hatimae kupata Katiba Mpya kwa maslahi ya wananchi," alisema.
 
Aliongeza kuwa, suala la mabadiliko ya kanuni ni jambo la msingi kwa kila mjumbe kwani wakati wa kuzipitisha kulikuwa na vikao vya mashauriano miongoni mwa pande mbili zilizokuwa zikivutana katika suala hilo hivyo kitendo cha kuzifungua kanuni hizo ni mkakati wa makusudi wenye kutaka kuleta chuki bungeni.
 
Kwa upande wake, Profesa Ibrahim Lipumba alizungumzia hotuba ya Rasi Jakaya Kikwete na kusema, imesikitisha kwani hakuona umuhimu wa masuala ya Muungano na haki za wanawake.
 
Alisema Rais Kikwete alipaswa kulizindua Bunge hilo kwa kuwataka wajumbe kutoa maoni yao juu ya Rasimu ya Pili ili baadaye maoni hayo yapelekwe kwa wananchi lakini Rais alivunja kanuni za Bunge kwa kuhutubia masilahi ya CCM.
 
Prof. Lipumba aliongeza kuwa, UKAWA hawapo tayari kuondoka katika Bunge hilo na kuwaacha wajumbe wa CCM waandike Katiba yao kwani watakuwa wamewaangusha wananchi wanaowawakilisha ili kupata Katiba bora.

VIBAKA WACHOMWA MOTO BAADA YA KUTUMIWA KUIBA COMPUTER..!!



Watu wawili ambao hawajafahamika majina yao wameuwawa kwa kuchomwa moto  na wananchi wanaozaniwa kuwa na hasira kali  katika kijiji cha Kagongwa wilayani Kahama  Mkoani Shinyanga baada ya kudaiwa kuiba  vitu mbalimbali ikiwemo Komputa.
Tukio hilo limetokea leo  majira ya saa tano asubuhi baada ya watuhumiwa hao kujaribu kuwakimbia viongozi wa Sungusungu waliokuwa wanawashikilia baada ya kuwakamata.
Kwa mujibu wa Mashuhuda wamesema vijana hao walikuwa ni tishio katika mji huo kutokana na kuiba marakwamara hivyo wananchi baada ya kuwakamata wameamua kuwachoma moto kwa madai kuwa iwe ni fundisho kwa  wengine.Wamesema Awali watuhumiwa walikamatwa na sungusungu ya kijiji cha Iponya wilayani humo Kabla ya kuamriwa wakaoneshe vitu hivyo ndipo wakapata mwanya wa kukimbia.Diwani wa kata ya Kagongwa Hamis Kashantole Ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa kata hiyo amekataa kuzungumzia tukio hilo kwa madai kwamba  hana muda wa kuongea.Jeshi la polisi wilayani Kahama limethibitisha kutoikea kwa tukio hilo na hadi sasa  uchungizi Unaendelea .

TRENI YA MIZIGO YAPATA AJALI ENEO LA GULWE WILAYA YA MPWAPWA


Wafanyakazi walioajiriwa na shirika la Reli Tanzania (TRL) wakitoa mchanga kwenye kichwa cha treni ya mizigo kilichopata ajali usiku wa kuamkia katika stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa. Katika ajali hiyo watu wawili wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa na kulazwa katika hospital ya Benjamin Mkapa Wilayani Mpwampwa.
Sehemu ya mabehewa ya mafuta na ngano ambayo hayakusombwa na maji katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika stesheni ya Gulwe, hiyo imetokea saa 9.15 usiku. Treni hiyo ya Mizigo ilikuwa ikitokea Dar es Salaam na kuelekea Mkoani Kigoma na ilikuwa na mabehewa yaliyobeba ngano, sukari na mafuta.
Njia ya Reli iliyoondolewa na maji katika stesheni ya Gulwe Wilaya ya Mpwampwa kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha maeneno mbambali nchini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka akitoka kwenye maji baada ya kuangalia kichwa cha treni kilichopata ajali na kusombwa na maji katika stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa, usiku wa kuamkia leo,

Sunday, March 2, 2014

Magazetini leo Jumapili March 02 2014



.

Matokeo ya mchezo wa Yanga vs Nacional Al Ahly

MAF3Klabu bingwa ya Tanzania bara Dar Young Africans leo imefanikiwa kushinda mchezo wa kwanza wa hatua ya raundi ya pili CAF Champions League dhidi ya mabingwa watetezi wa kombe hilo Nacional Al Ahly ya Egypt.
Mchezo huo uliopigwa katika dimba la uwanja wa taifa Dar es Salaam uliotawalia kwa kiasi kikubwa na Yanga ambao walipoteza nafasi nyingi katika kipindi cha kwanza na mpaka timu zinaenda mapumziko hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzie.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa upande wa Yanga walionekana kutafuta bao kwa nguvu, mpaka kufikia dakika ya 50 tayari walishapata kona tisa ambazo hazikuzaa matunda. Wakati muda ukizidi kuyoyoma na mashabiki wa Yanga wakiwa wameanza kukata tamaa ya kupata ushindi dhidi ya waarab, Nadir Haroub Cannavaro aliwainua maelfu ya mashabiki wa Yanga katika dakika ya 82 baada ya kuipatia timu yake bao la kuongoza.
Mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho ubao wa matokeo ulikuwa unasomeka 1 kwa moja na 0 kwa waarabu. Timu hizi zitarudiana jijini Cairo wiki mbili zijazo.