This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, March 26, 2013

MWANAFUNZI UDSM AJINYONGA HADI KUFA


Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka wa pili Kitivo cha Sheria, Joseph Bernadina (25), amejinyonga kwa kutumia kamba na kukutwa ameifunga juu ya mti, katika eneo la Yombo chuoni hapo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Utawala, Profesa Yunus Mgaya, alithibitisha  kutokea kwa tukio hilo na kwamba alipata taarifa hizo jana asubuhi.

Aliongeza kuwa Jumamosi iliyopita alipokea simu kutoka kituo cha polisi cha chuo hicho akielezwa kuwa kuna mwanafunzi alitishia kujiua, lakini aliwahishwa hospitali na kupatiwa ushauri kutoka kitengo maalum cha washauri wa chuoni hapo na kuruhusiwa Jumapili.

“Nilikuja tena kushituka leo asubuhi napokea simu kutoka kwa mshauri wa wanafunzi kuwa kuna wanausalama wamemkuta mwanafunzi akiwa amejinyonga juu ya mti huku akiwa na karatasi kwenye mfuko wa sharti ikimtambulisha pamoja na ujumbe uliosema, kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote kwani amejiua kwa ridhaa yake --asisumbuliwe mtu yeyote kwani nimefanya hivi kwa maamuzi yangu mwenyewe pia nizikwe kwetu--” alisema.

Profesa Mgaya alisema taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na Uongozi wa chuo kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu na kwamba Chuo kitagharamia kuusafirisha mwili kama alivyoomba katika ujumbe aliouacha wa kupelekwa wilayani Ludewa Mkoa wa Iringa.

Naye rafiki wa marehemu, Daniel Mwamlima, alisema marehemu hakuwahi kuzungumza chochote kilichoashiria kuwa ana matatizo wala mgogoro na mtu yeyote.  Alisema walimuacha hospitalini Jumamosi na kesho yake kumchukua, lakini  baadaye aliwatoroka.

“Sasa leo (jana) asubuhi tulipata taarifa za mwanafunzi kujinyonga mbaya zaidi tukakuta ni yeye,” alisema Mwamlima.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho (DARUSO), Yasini Athumani, alisema wamezipokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alithibitisha kutokea kwa tukio na alisema uchunguzi wa awali umebaini kwamba marehemu aliwahi kuwa na historia ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kupata matibabu ya ugonjwa wa msongo wa mawazo.

WATEJA WANAOTUMIA HUDUMA YA M-PESA SASA KUTUMIA ATM ZA DTB KUTOLEA FEDHA

Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester Bahati (kushoto) akiwaelezea waandishi wa habari jinsi ya kutoa fedha  kwenye mashine za kutolea fedha za DTB kupitia huduma ya Vodacom M PESA ambapo sasa wateja wanaotumia huduma hiyo wanaweza kutoa pesa kupitia mashine hizo popote walipo nchini.  Huduma hiyo imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim.…
Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester Bahati (kushoto) akiwaelezea waandishi wa habari jinsi ya kutoa fedha  kwenye mashine za kutolea fedha za DTB kupitia huduma ya Vodacom M PESA ambapo sasa wateja wanaotumia huduma hiyo wanaweza kutoa pesa kupitia mashine hizo popote walipo nchini.  Huduma hiyo imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim.
Meneja  Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim, akitoa fedha kwa mara ya kwanza baada ya kuzinduliwa kwa huduma ya kutoa fedha kupitia mashine za kutoa fedha za DTB kupitia huduma ya M PESA. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester Bahati.
Salum Mwalim na Sylvester Bahati wakifurahi baada ya kutoa fedha kwa mara ya kwanza kupitia mashine za kutoa fedha za DTB kwa huduma ya M PESA.
Dar es Salaam, 26th Machi, 2013 ...Ukuaji wa teknolojia ya huduma maarufu ya kutuma, kupokea fedha pamoja na kufanya malipo ya huduma mbalimbali kwa njia ya simu za mkononi ya kampuni ya Vodacom ya M-pesa inazidi kupanuka na hivyo kuongeza kiwango cha matumizi ya huduma hiyo kuzidi kuboresha maisha na kuyafanya kuwa rahisi zaidi.

Katika kufikia mafanikio hayo Benki ya Diamond Trust (DTB) leo imetangaza ubia wa kibiashara na kampuni ya Vodacom Tanzania ubia ambao unawawezesha wateja wa M-pesa kuwa na uwezo wa kutoa fedha kutoka katika akuanti za M-pesa kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM) za benki ya Diamond Trust.

Wakitangaza na kuzindua huduma hiyo jijini Dar es salaam Mkuu wa Kitengo za Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester Bahati,  amesema hayo ni mafanikio mengine ya kibishara kwa benki hiyo ya DTB katika kupanua wigo wa huduma na namna benki hiyo inavyoweza kuunganisha teknolojia ili kuleta urahisi kwa watanzania.

“DTB inayo Furaha kubwa kuwa sehemu ya mapinduzi ya kiteknolojia hapa nchini. Hii ni huduma ya kwanza na ya aina yake ambayo hakuna shaka kwamba inaashiria uwezo wa DTB katika kuleta ufumbuzi wa namna bora ya kutumia teknolojia kurahisisha maisha.”Amesema Bahati

“Tukishirikiana na Vodacom tunawawezesha wateja wa M-pesa walio karibu na benki zetu na hususan mtandao wa ATM kuwa na uhakika wa kutoa fedha kutoka akaunti zao za M-pesa saa ishirini na nne katika siku zote saba za wiki.”

Bahati amesema jambo hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibenki sanjari na kuboresha hali ya maisha na uchumi kwa watanzania wote mijini na vijijini.

Hata hivyo hii ni frusa ya kipekee kwa wateja wa benki ya DTB ambao wamejiandikisha kwa ajili ya huduma ya M-Pesa hawana haja tena ya kutembelea matawi ya benki hiyo ili kuweza kuweka amana zao au kuhamisha fedha kwa biashara, marafiki na familia zao. Pia uzinduzi wa huduma hiyo utawezesha kujenga urahisi wa kuruhusu wasiotumia huduma ya benki kupata huduma za kifedha karibu nao.

Azma ya DTB ni kuzidi kuongeza kasi na maboresho ya utoaji wa huduma kwa wateja wake na washirika wake wengine kwa kuhakikisha inaendelea kupanua wigo wa huduma zake ikiwemo kuongeza ATMs, matawi na huduma nyinginezo kwa lengo la kusogeza karibu huduma za kibenki nchi nzima.

Kwa upande wake Afisa Mkuu wa M- Biashara wa Vodacom Jacques Voogt, amesema, "Hii ni hatua nyingine ambayo tunaifikia leo. Kampuni ya Vodacom inaendelea kupanua mtandao wake wa huduma ya M-Pesa.”
Voogtz ameongeza kuwa ubia huo ni mwendelezo wa azma ya kampuni ya Vodacom kutumia fursa za teknolojia ya M-pesa kuzidi kuleta amsiha ya watu mikononi mwao kutumia simu za kiganjani.

“Wateja wa Vodacom M-pesa wanayo sababu nyingine ya kujivunia kuwa sehemu ya mtandao mpana wa huduma hii salama, rahisi na yenye kuaminika zaidi nchini wakiunganishwa na makampuni na hata tasisi zaidi ya 200 kufanya malipo ya huduma na manunuzi kwa urahisi na wepesi zaidi kupitia simu za viganjani.”Aliongeza Voogtz

Kuhusu DTB…..
Kuhusu Vodacom Tanzania:

Kampuni ya Vodacom Tanzania Limited ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na jamii katika shughuli za maendeleo kupitia taasisi yake ya Vodacom Foundation. Vodacom Foundation ina nguzo kuu tatu: Afya, Elimu na Ustawi wa Jamii. Hadi sasa taasisi hiyo imechangia zaidi ya miradi 120 ya kijamii nchini. Aidha, imeshinda tuzo mbalimbali za kitaifa na za kimataifa katika nyanja ya Uwajibikaji wa Mashirika kwa Jamii. Hizi ni pamoja na East African CSR Awards na Diversion and Inclusion Award ambayo hutolewa na kampuni mama ya Vodafone.
Vodacom Tanzania Limited ni kampuni ya simu za mikononi inayoongoza Tanzania inayotumia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano. Vodacom Tanzania ni kampuni tanzu ya Vodacom Group (Pty) Limited, South Afritca, ambayo pia ni kampuni tanzu ya Vodafone Group UK. Vodacom Group (Pty) Limited inamiliki hisa ailimia 65 Vodacom Tanzania na asilimia 35 zilizobaki zinammilikiwa na Mirambo Ltd.

WABUNGE ZITTO KABWE NA AZAN WAMALIZA MAFUNZO YAO YA JKT KAMBI YA MGAMBO 835KJ LEO


Mbunge wa Kigoma CHADEMA, Zitto Kabwe pamoja na Wabunge wenzake kadhaa vijana leo wakemaliza rasmi mafunzo yao ya awali ya JKT katika kambi ya Mgambo 835KJ kilichopo Mkoani Tanga.



Pichani juu ni Zitto Kabwe akijiandaa kwenda katika gwaride la mwisho na picha chini akiwa shambani pamoja na Mbunge mwenzake  Iddi Azan, Abdallah haji, Raya Ibrahim na Antony Mbassa kambi ya Mgambo 835KJ.

Aidha Zitto Kabwe amesema anafuraha iliyo pitiliza kumaliza mafunzo hayo na ameweka historia ya kubwa katika maisha yake hii leo. Anapasha zaidi katika wakati wa Zoezi la kulenga shabaha alifanikiwa kulenga risasi 3 akiwa amelala, 3 akiwa amepiga magoti na 1 akiwa amesimama.

ALIYEMGONGA TRAFIKI ENEO LA BAMAGA AFIKISHWA MAHAKAMANI




Akiteta jambo na Issa Mnally  ndani ya mahakama kabla ya hakimu kuwasili. 


  Waandishi wa habari wakimpiga picha (Simbo) wakati akiingia mahakamani...


Akiondoka eneo la mahakama mara baada ya kesi kuahirishwa akiwa na wakili wake.
 Jackson  Simbo anayedaiwa kumgonga kwa gari marehemu trafiki Elikiza Nko wiki iliyopita maeneo ya Bamaga-Mwenge  jijini Dar ss Salaam amepandishwa kizimbani leo katika mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. 

Mshitakiwa huyo ameachiwa kwa dhamana hadi kesi hiyo itakapo tajwa tena Aprili 15 mwaka huu