This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, May 28, 2013

"SINA SHAKA NA UMAARUFU WANGU"....LOWASSA


MBUNGE wa Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, amesema hana shaka na umaarufu wake Monduli wala Tanzania kwa ujumla.
 
Kauli hiyo aliitoa jana wakati akifungua kampeni za udiwani wa Kata ya Makuyuni huku akikishangaa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kupeleka mgombea wake katika Kata hiyo.


“Eti hawa wanathubutu kujinadi na kujigamba kushinda udiwani Monduli ya Lowassa wakisema watapata kura kwa asilimia 90 jamani haya ni kweli?,” alihoji Lowassa na kuongeza:

“Ndugu zangu sina shaka na umaarufu wangu Monduli wala Tanzania.”

Katika mkutano huo, aliwaambia wananchi kwamba anahitaji kuona wakikiadhibu CHADEMA kwa kukipa pigo ambalo hawajawahi kulipata mahali popote nchini.

“Ndugu zangu atakayewapa kura hawa CHADEMA wana wa Makuyuni atakuwa amenichoma kisu mimi, naomba msiwape kura hata moja, naomba muwafundishe adabu,” alisema Lowassa.

Akikishambulia chama hicho kwa kutumia helikopta katika Kata hiyo, alisema siku zote vita vya kiafrika vinapiganwa kwa kutumia askari wa miguu na si helikopita.

Alisema CCM inatumia askari wa miguu kuhakikisha inashinda vita vyake, hivyo haitatishika na helikopita hiyo.

Alikirushia kombora chama hicho kwa kukitaka kisimame hadharani na kujipapanua kama hakihusiki na vurugu zinazoendelea nchini.

Alisema kama kweli hakihusiki na vurugu zilizopo nchini basi viongozi hao wanapaswa kujihoji ndani ya nafsi zao kama kweli hawahusiki.

“Nawaomba hawa CHADEMA wajihoji ndani ya nafsi zao kama kweli hawahusiki na vurugu hizi, je wanaifanyia nchi yetu mema au mabaya,” alihoji Lowassa.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI MBALIMBALI ADDIS ABABA, ETHIOPIA


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani Mh…
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Marekani Mh Liberata Mulamula walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha kwa mazungumzo Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS Michel Sidibe walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS Michel Sidibe na ujumbe wake walipokutana pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS Michel Sidibe pamoja na Mratibu wa Masuala ya Ukimwi wa Marekani Balozi Eric Goosby walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamaica Bi. Portia Simpson Miller walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Waziri Mkuu wa Jamaica Bi. Portia Simpson Miller walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulishaWaziri Mkuu wa Jamaica Bi. Portia Simpson Miller kwa Mhe Gideon Moi, Seneta wa Kaunti ya Baringo nchini kenya na ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha KANU cha nchi hiyo walipokutana pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Misri Mohamed Morsi walipokutana wakati wa mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika Mkutano wa kawaida wa 21 wa Umoja wa Afrika katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa taaisi ya kimataifa inayoshughulikia mapambano dhidi ya Ukimwei, Kifua Kikuu na Malaria ya The Global Fund Dkt Mark Dybil na afisa wa taasisi hiyo Bi Shu-shu Tekle-Haimanot walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifanya mazungumzo na Katibu Mtendaji wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR) professor Ntumba Luaba na ujumbe wake walipokutana na kufanya mazungumzo pembeni ya mkutano na sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya Umoja wa Afrika (AU) katika makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa, Ethiopia.
(PICHA ZOTE NA IKULU)

AIRTEL YAZINDUA MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS 2013‏

Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano Mallya, akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa progamu ya Airtel Rising Stars 2013 uliofanyika katika Ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo, wengine ni Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo (katikati) na Makamu wa Raisi wa TFF Ramadhani Nasibu. Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo akikazia jambo wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye halfa ya uzinduzi wa programu ya Airtel 2013 uliofanyika katika Ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo kushoto ni…
Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano Mallya, akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa progamu ya Airtel Rising Stars 2013 uliofanyika katika Ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo, wengine ni Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo (katikati) na Makamu wa Raisi wa TFF Ramadhani Nasibu. Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo akikazia jambo wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye halfa ya uzinduzi wa programu ya Airtel 2013 uliofanyika katika Ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo kushoto ni Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano Mallya, Makamu wa Raisi wa TFF Ramadhani Nasibu na Kaimu katibu mkuu wa TFF Sunday Kayuni.
Baadhi ya wachezaji wa Airtel Rising stars wa mwaka 2012 wakisalimiana na Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo, Makamu wa Raisi wa TFF Ramadhani Nasibu na Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano Mallya wakati wa uzinduzi wa progamu ya Airtel Rising Stars 2013 uliofanyika katika Ofisi za TFF jijini Dar es Salaam leo.
Wakizindua programu ya Airtel Rising Stars 2013 Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo, Makamu wa Raisi wa TFF Ramadhani Nasibu na Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano Mallya, Kaimu katibu mkuu wa TFF Sunday Kayuni na mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu Dar es Saalam Almasi Kasongo wakati wa uzinduzi wa Airtel Rising Stars 2013.
Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano Mallya, Mkurugenzi wa Michezo Leonard Thadeo, Makamu wa Raisi wa TFF Ramadhani Nasibu, Kaimu katibu mkuu wa TFF Sunday Kayuni wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wachezaji wa Airtel Rising stars wa mwaka 2012.
---
AIRTEL YAZINDUA MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS 2013‏
Dar es Salaam, Jumanne 28 Mei 2013… Airtel Tanzania leo imezindua michuano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars. Airtel imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kudhamini mashindano hayo ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) pamoja na serikali kukuza vipaji vya soka nchini Tanzania.

Huu ni mwaka wa tatu mfululizo tangu kampuni ya airtel ianze kudhamini mashindano ya Airtel Rising Stars ambayo huanzia ngazi ya mkoa hadi Taifa. Fainali za Airtel Rising Stars Taifa hufatiwa na kliniki ya soka ya kimataifa kwa wachezaji nyota chini ya ukufunzi wa makocha mahili wa vijana kutoka klabu ya Manchester United.

“Nafurahi kwamba tumepiga hatua na leo tunazindua msimu wa tatu wa Airtel Rising Stars ambao bila shaka utakuwa wa ushindani na wa kusisimua”, alisema Beatrice Singano, Mkuu wa Idara ya mawasiliano ya Airtel Tanzania. Uzindinduzi huo ulifanyika katika ofisi za TFF.

Singano alisema: “Airtel imevutiwa na mwitikio wa vijana wengi waliojitokeza kujiandisha na kushiriki katika mashindano ya Airtel Rising Stars katika miaka iliyopita. Ni matumaini yetu kwamba vijana wengi zaidi watajitokeza kushiriki mwaka huu”.

Singano alisema mpango huu kabambe unawalenga wasichana na wavulana nchi nzima ili kuwapa fursa ya kuonyesha vipaji vyao kwa mawakala wa soka, makocha na mamlaka nyingine zinazohusika na programu za kuendeleza vipaji vya soka. Mwaka huu Airtel Rising Stars itajumuisha jumla ya timu 24 za wasichana na wavulana kutoka mikoa ya Mwanza, Mbeya, Morogoro, Ilala, Kinondoni Temeke, Kigoma, Tanga na Ruvuma ambao baadhi yao watateuliwa kuunda timu za mikoa yao katika fainali za Taifa. Vile vile mashindano ya Taifa yatatumika kuteua timu itakayoiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa (inter-country tournament)
Akizunguma katika hafla hiyo, mgeni rasmi Mkurugezi wa Michezo nchini Bw. Leonard Thadeo alisema serikali inatambua juhudi zinazofanywa na Airtel kuwekeza kwenye programu ya soka ya vijana ambao ndiyo nguzo mhimu kwa maendeleo ya mchezo wa soka nchini. Kauli yake iliungwa mkono na Makamu wa Pili wa Rais wa TFF Bw Basibu Ramadhani ambaye alisema program za soka za vijana ndio njia pekee ya kuinua kiwango cha soka nchini.

“Tumeshudia vipaji vingi katika mashindano yaliyopita na bila shaka michuano ya mwaka huu yataendelea kutoa vipaji vingine vingi. Natowa wito kwa timu kubwa hapa nchini kutumia fursa hii kupata wachezaji chipukizi kwa ajili kuimarisha timu zao. Nawatakia washiriki wote mashindano mema na wazingatie nidhamu na taratibu ya mchezo wa soka.” alisema Thadeo.

Programu hii ya Afrika inaungwa mkono na klabu kubwa ya Manchester United kwa lengo la kubaini vipaji vya soka na kuviendeleza ili kuweza kuonekana kwa mawakala, makocha na kupata nafasi ya kutambulika kitaifa na kimataifa.

Ushirikiano wa Airtel na Manchester United katika kuendeleza soka ya vijana ni utekelizaji wa makubaliano yaliyotiwa saini kati ya pande hizo mbili mwezi Disemba 2010 ambayo yanaiwezesha Airtel kutumia hazina ya ufundi wa soka kutoka klabu hiyo kubwa duniani kuendeleza vijana chipukizi barani Afrika.

Vijana wanaoshiriki Airtel Rising Stars mwaka huu hapa nchini wanatajiwa kuanza kujiandikisha mwezi ujao na jumla ya timu 24 kutoka mikoa 9 zitashiriki.

Airtel ni kampuni ya simu za mikononi inayofanya biashara barani Afrika katika nchi za Burkina Faso, Chad, Congo Brazzaville, Democratic Republic of Congo, Gabon, Ghana, Kenya, Madagascar, Malawi, Niger, Nigeria, Rwanda, Seychelles, Sierra Leone, Tanzania, Uganda, na Zambia.

WANAFUNZI WAPIGA KURA ZA SIRI ILI KUWAFICHUA WALIMU WANAOFANYA MAPENZI NA WANAFUNZI



KATIKA hali isiyo ya kawaida, wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyasubi, iliyopo Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, wamepiga kura za siri ili kuwafichua walimu wenye tabia ya kufanya mapenzi na wanafunzi wao shuleni hapo.

Uamuzi wa kupigwa kura hizo ulifikiwa hivi karibuni kwenye Kikao cha Baraza la Shule la Watoto ambacho kiliitishwa kwa lengo la kujadili vurugu zilizokuwa zikijitokeza shuleni hapo na kusababisha baadhi ya walimu kupigwa.

Kikao hicho kiliitishwa na Mratibu wa Mradi wa Haki Yangu Sauti Yangu, mkoani humo, Bw. Gerald Ng’ong’a na
Kkubaini kuwa, sababu moja wapo iliyochangia vurugu hizo ni baadhi ya walimu kufanya mapenzi na wanafunzi wao.


Inadaiwa hali hiyo pia imechangia wanafunzi wengi waliomaliza kidato cha nne shuleni hapo kupata matokeo mabaya, kuporomoka kwa kiwango cha elimu kutokana na walimu kutotimiza wajibu wao kikamilifu.

Baadhi ya wanafunzi waliozungumza katika kikao hicho, walisema chanzo cha vurugu ni wanafunzi wa kiume kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi wa kike hivyo wanachukizwa na kitendo cha baadhi ya walimu kutembea na wapenzi wao.

Walisema kutokana na hali hiyo, wanafunzi wa kiume waendapo mitaani hujiunga na vikundi vya wahuni ambao huchukua hatua za kuwateka na kuwapiga walimu wao ili kulipa visasi.

Hata hivyo, wanafunzi hao walipotakiwa kuwataja walimu wenye tabia hiyo waliomba ufanyike mchakato wa upigaji kura za siri ambapo kazi hiyo ilisimamiwa na walimu pamoja na wazazi walezi ambao walishiriki kikao hicho.

Kura hizo ziliwataja majina ya baadhi ya walimu wenye tabia hiyo na majina ya wanafunzi wanaoshiriki kufanya nao mapenzi lakini hazikutangazwa kwa kuwa ni siri na zitawasilishwa kwa uongozi wa shule ili wahusika waitwe na kuonywa.

Katika hatua nyingine, baadhi ya wanafunzi shuleni hapo walilalamikia kitendo cha walimu wao kuwapa adhabu kubwa zisizolingana na makosa wanayoyafanya wakitolea mfano wa adhabu ya kugaragazwa chini kwa kosa la kutokutoa ada ambalo walisema si kosa lao bali ni la wazazi.

Kutokana na hali hiyo, Bw. Ng’ong’a, aliwashauri wazazi, walezi kuhakikisha wanafanya vikao vya mara kwa mara ili waweze kurejesha hali ya amani na utulivu shuleni hapo.

"Nimesikitishwa kusikia miaka minne hamjaitisha kikao chochote cha Bodi ya Shule wala cha wazazi, hali hii inachangia mambo mengi kutopatiwa ufumbuzi wa haraka pale yanapojitokeza.

"Ni muhimu kuwa na vikao vya mara kwa mara pamoja na Baraza la Shule la Watoto ili kutoa fursa ya kusikiliza kero mbalimbali walizonazo," alisema Bw. Ng’ong’a.

Imeandikwa na Suleiman Abeid, Kahama
via MAJIR

CHANZO CHA KIFO CHA MSANII ALBERT MANGWEA

 

Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.

Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear  na   M to the P  ambaye walikuwa room moja walitakiwa kurudi Tanzania leo  wakitokea  Afrika kusini..

Walipowapitia,  waliwakuta wamezima kwenye room wote wawili baada ya kuji overdose madawa ya kulevya...
 
Mpaka sasa M to the P yupo hoi  katika  hospitali ya St. Hellen  huku  msanii Ngwair  akiwa  tayari  amekwishaaga  dunia.....

Tunaendelea  kufuatilia  undani wa  tukio  hili

R.I.P NGWAIR
 
 
 
 

Habari  zilizotufikia  ni  kwamba  msanii  Albert Mangwair  amefariki  dunia akiwa  Afrika  kusini

Chanzo  cha  kifo  hicho  bado  hakijafahamika  lakini  taarifa  za  awali  zinadai  kuwa  msanii  huyo  hakuamka  tangu  alipolala .

Mtandao huu unaendelea  kuifuatilia  habari  hii  

R.I.P   Ngwair