This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, March 5, 2013

WOMEN CELEBRATIONS 2013



















Vazi la kitenge ndio vazi lililotawala kwa asilimia 90% siku ya Women's Celebration, mavazi hayo yalioshonwa kwa mitindo aina mbali mbali yaliwapendeza sana wageni waliohudhuria shughuli hiyo pale Diomond Jubilee, V.I.P Hall, March 3,2013.

MITINDO YA NYWELE






Masuala ya Nywele nayo hayakuwa nyuma katika shughuli hiyo ya Women's Celebration ,Diamond Jubilee V.I.P hall, march 3,2013.

TFF IMEPENDEKEZA KIKAO NA Mukangara KIFANYIKE KESHOKUTWA (MACHI 7 MWAKA HUU ) AU MARCH 13 MWAKA HUU

TFF IMEPENDEKEZA KIKAO NA Mukangara KIFANYIKE KESHOKUTWA (MACHI 7 MWAKA HUU ) AU MARCH 13 MWAKA HUU


 


 

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewasilisha rasmi maombi ya kuonana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara ili kuzungumzia uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya 2012.

Maombi hayo yaliwasilishwa rasmi Wizarani jana (Machi 4 mwaka huu) ambapo TFF imependekeza kikao hicho kifanyike keshokutwa (Machi 7 mwaka huu) au Machi 13 mwaka huu.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Machi 2 mwaka huu kujadili tamko ya Waziri kutengua matumizi ya Katiba ya 2012 ndiyo iliyopendekeza kikao hicho kwa lengo la kusikiliza upande wa TFF katika suala hilo.

ZFA YAKUBALI MAKUNGU KUACHIA NGAZI YAMSHUKURU KWA KILA JAMBO KUPATA RAIS MWINGINE NDANI YA SIKU TISINI




 http://2.bp.blogspot.com/-UNDYNdEEiHE/UQLWWRa7WzI/AAAAAAAAMBM/jZ2c-2YRQYM/s640/amani+makungu.jpg
Kamati ya Utendaji ya Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), Kimeridhia  Maombi ya Aliyekuwa  Rais chama hicho , Aman Ibrahim Makungu kuachingazi nafasi hiyo.
Katika Barua iliyoandikwa na ZFA Machi 4, mwaka huu,  , iliyoisainiwa na Makamu wa Rais Kisiwani Unguja, ambaye pia ni Kaimu Rais wa ZFA kikatiba, Alhaj Haji Ameir, ikiwa na Kumbukumbu namba. ZFA/PRESIDENT/VOL.11/05.

Barua hiyo inasomeka  Kamati ya Utendaji ya ZFA Taifa, imekaa na kujadili kwa kina ombi la kujiuzulu kwa Makungu, na kutafakari kwa makini na hatimaye kufikia uamuzi wa kulikubali ombi hilo.

 ZFA Taifa imemshukuru Aman Makungu kwa msaada wake alioutoa huku wakimuomba aendelee kuwa na chama hicho wakati wowote atakapohitajika.
Nakala za barua hiyo zimetumwa kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Michezo la Zanzibar pamoja na Msaidizi Katibu ZFA Kisiwani Pemba.

Kwa mujibu wa Katiba ya ZFA, sasa ni wazi kuwa kunalazimika kufanyika uchaguzi mwingine ndani ya siku 90.
Itakumbukwa kuwa miezi miwili iliyopita, Rais wa ZFA, Aman Ibrahim Makungu aliandika barua ya kuomba kujiuzulu nafasi hiyo kwa kile kilichoelezwa katika barua hiyo kuwa ni 
kuchoshwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho wasiotaka mabadiliko huku wakionekana kuwagawa baadhi ya wajumbe wa ZFA kwa kisingizio cha U-Unguja na U-Upemba, 
ambapo Kamati ya Utendaji ya ZFA Taifa walilikataa ombi hilo kwa madai kuwa litachangia kurejesha nyuma soka la Zanzibar.

NDOTO ZA MACHESTER UTD KUTWAA TAJI LA ULAYA ZAISHIA KATIKA MJADARA MKUBWA ULAYA


FERGUSON ASUSIA WANAHABARI KISA KADI NYEKUNDU


Manchester United's Nani

Kocha wa Manchester United  Sir Alex Ferguson hakuwa tayari kuzungumza na vyomb vya habari ,baada ya timu kusukmwa nje ya ligi ya mabingwa barani ulaya Dhidi ya   Real Madrid katika uwanja wa   Old Trafford.
Ferguson alishindwa kumvumilia  mwamuzi kutoka uturuki Cuneyt Cakir baada ya kumpa kadi nyekund Nani baada ya kumfanyia rafu mbaya  Alvaro Arbeloa katika dakika ya  56 wakati United ilikuwa ikongoza kwa goli la kujifunga la  Sergio Ramos's. 
Sir Alex Ferguson
Kocha msaisizi wa United  Mike Phelan alimwakilisha Feg  katika mahojiano baada ya mechi kumalizka  : "Chumba cha kubadilishia sio salama kwetu Kocha mkuu amekasirsihwa na maamuzi ya mwamuzi wa leo ndio maana hayuko hapa .
na mimi ndiye nitakaye zungumza 
 
"Sidhani kama mkufunzi mkuu atakuwa sawa kuzungumza .
Naongea haya ili muone ni kwa jinsi gani tumesikitishwa hii ni klabu kubwa duniani  ."
Phelan : "Tumesikitishwa na kuumia sana tuna mashaka kwanini limetokea na kwa sababu gani limetokea .
 sio rahisi mkiwa kumi kiwanjani mkacheza na real Madrid .
" Waamuzi wapo kiwanjani ili kufanya Maamuzi lakini unatakiwa kufanya maamuzi ya maana . 
Najua vyombo vya habari na watazamanji duniani  kote wametazama hili na watakuwa na maoni tofauti lakini tumesikitishwa sana."

NDOTO ZA MACHESTER UTD KUTWAA TAJI LA ULAYA ZAISHIA KATIKA MJADARA MKUBWA ULAYA

Cristiano Ronaldo of Real Madrid reacts after scoring his team's second goal during the UEFA Champions League Round of 16 Second leg match between Manchester United and Real Madrid 
Ndoto za Manchester United's kutwaa ubingwa wa ulaya zimemalizka kwa mjadara mkubwa huku kocha Man u    Sir Alex Ferguson na wachezaji wakikiona kiwanja cha OT ni Kikubwa kuliko wakati mwingine.
United walionekana tayari wameanza kuingia hatua ya Robo fainali mara baada ya kipindi cha pili Kuanza huku  Real Madrid's ikijitia matatani mara baada ya Sergio Ramos's kujifunga mwenyewe na kuipa goli United  ambalo ilikuwa likichagizwa na sare ya goli moja kwa moja  katika mchezo wa kwanza uliofanyika  Bernabeu. 
Man Utd v Real Madrid
Lakini mchezo ulibadilika baada ya Mwamuzi kutoka Uturuki  Cuneyt Cakir's Kumlima kadi nyekundu Luis  Nani baada ya kumchezea vibaya Mchezaji  Real Madrid Alvaro Arbeloa katika dakika ya  56  - kadi ambayo iliwanyong'onyesha wachezaji wa United .
Vijana wa Jose Mourinho's , waliongeza bidii , na kutumia pengo la hilo ambapo mchezaji wa zamani na kiungo wa Tottenham  Luka Modric na kijana wa zamani wa Timu hiyo   Cristiano Ronaldo walitumia dakika sita kusawazisha na kufunga goli la ushindi na kusonga mbele katika hatua Robo fainali .
Man Utd v Real Madrid
Baada ya luis Nani Kupewa kadi nyekundu Ferguson's alinoneka kuto kuamini kinachotokea na kumshutumu  mwamuzi kuwa hakutenda haki  baada kutolewa mchezaji wake  .
Mourinho sasa atakuwa analisaka taji la tatu la ligi ya mabingwa barani ulaya akiwa na klabu tatu tofauti  wakati Manchester utd wanatakiwa kujikita katika makombe ya nyumbani ambapo jumapili watakuwa wakipambana na chelsea katika kombe Fa huku wakiwa wanaongoza alama 12 dhidi ya bingwa mtetezi Manchester city .
 
Huenda mwaka huu ukawa kama 1996, ambapo England haikuwa na timu yoyote kwenye hatua ya robo fainali, kwani Chelsea na Manchester City walishatolewa na Arsenal wapo ukingoni wanapoelekea Ujerumani wiki ijayo.

Baada ya mechi Rio Ferdinand alimwendea mwamuzi na kujidai kumpigia makofi kana kwamba anampongeza, bila shaka kuonesha kuudhiwa na uamuzi wake wa kumpa kadi nyekundu Nani, na pengine kuwanyima penati kadhaa walizodhani walistahili.




Kiwanda cha sukari cha Mahonda visiwani Zanzibar kuzalisha Tani 400 za Sukari safi ikiwa ni sawa na Tani 40 kwa siku.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd akiangalia waya wa umeme aina ya shaba ambao amezuia mauzo yake hadi uongozi wa kiwanda cha sukari utapokaa pamoja na Wizara ya fedha kufikia maamuzi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akiuagiza Uongozi wa Kiwanda cha sukari Mahonda kukaa pamoja na Wizara inayosimamia Fedha Zanzibar ili kufikia mwafaka wa matumizi ya waya wa umeme wa aina ya shaba ambao tayari ulikuwa umeshauzwa.  
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitembelea kiwanda cha sukari Mahonda akiwa pamoja na Uongozi wa Kiwanda hicho. Picha na Hassan Issa –Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar

Polisi wasaka wauaji wa kigogo UVCCM

eshi la Polisi mkoani Arusha linawasaka wanawake wawili kufuatia kifo cha kutatanisha cha mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa kupitia Mkoa wa Arusha, Benson Peter Mollel (26). Inadaiwa kuwa wanawake hao walikuwa na Mollel kabla ya kufariki dunia ghafla juzi katika chumba cha hoteli moja jijini hapa. Tukio hilo lilitokea mchana baada ya mwili wa merehemu kugunduliwa na wahudumu wa hotel hiyo walipotaka kukifanyia usafi chumba alichokuwa amelala marehemu huyo . Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alisema jana kuwa marehemu alifika hoteli hapo, Machi 2 mwaka huu jioni na kupanga katika chumba namba 208. Alisema Polisi baada ya kupata taarifa za tukio hilo, wanaendelea na msako kuwatafuta wanawake hao ambao walikuwa na marehemu kabla ya kukutwa na mauti ya ghafla. Alisema kuwa mmoja wa wanawake hao alikwenda na marehemu hotelini hapo saa 7.00 usiku na mwingine alikwenda hotelini hapo asubuhi saa 5.00 asubuhi. Sabas alisema polisi baada ya kufika hotelini hapo walimkuta marehemu na kuchukua mwili wake na kuhifadhi hospitali ya Mkoa Mount Meru.