This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, March 7, 2013

waziri wa denmark aandaliwa dhima ya kitaifa

d (1)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri Mkuu wa Denmark Mhe. Hell Thorning-Shmidt  katika dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Ikulu jana usiku

d (2)
d (5) d (6)  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akigonganasha glasi ya kutakiana afya njema na  Waziri Mkuu wa Denmark Mhe. Hell Thorning-Shmidt  katika dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Ikulu jana usiku.
 C27B2231
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu wa Denmark Mhe. Hell Thorning-Shmidt wakiangalia ngoma za utamaduni za kundi la JKT  katika dhifa ya kitaifa aliyomwandalia Ikulu jana usiku

MAMA SALMA AZINDUA KISIMA CHA MAJI -MWANZA

IMG_3758  Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, Mama Salma Kikwete akikata utepe ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi kisima cha maji kilichochimbwa katika hospitali ya mkoa wa Mwanza, Sekou Toure,kwa msaada wa Kampuni ya Bia ya Serengeti. Kisima hicho kimegharimu shilingi milioni sabini. wa pili kulia  ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ndugu Paschal Mabiti na kushoto ni Mwenyekiti wa Kampuni ya bia ya Serengeti Jaji Mark Bomani na wamwisho kulia ni  Mkurugenzi wa Mawasiliano Kampuni ya bia ya Serengeti Nandi Mwiyombela. Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 7.3.2013.

IMG_3777
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akifungua koki ya maji wakati wa kuzindua rasmi kisima cha maji katika hospitali ya mkoa wa Mwanza, Sekou Toure .
IMG_3972Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikewte akiwahutubia mamia ya wafanyakazi na wananchi wa jiji la Mwanza baada ya kuzindua rasmi kisima cha maji katika hospitali ya Sekou Toure tarehe 7.3.2013.
IMG_3747

mamilioni wamuaga rais wa venezuela


 Mwili wa Chavez ukipitishwa katika barabara za mji mkuu Caracas
Mwili wa Chavez umelazwa katika kituo cha mafunzo ya kijeshi mjini Caracas na marais wa nchi jirani walifika kutoa heshima zao za mwisho akiwemo Rais wa Bolivia Evo Morales na mwenzake wa Argentina Cristina Fernandez de Kirchner.Mama yake na watoto wake walikusanyika mbele ya jeneza kutoa heshma zao .

Kifo chake kilitangazwa na serikali ya Venezuela Jumanne wiki hii
 
Mwaka uliofuata Chavez alichaguliwa na wananchi kuongoza kwa muhula wwingine wa miaka sita kuiongoza Venezuela .Watu wengi waliangua kilio huku wakichukua picha za kiongozi wao aliyefariki dunia .
 
Mwaka 2011 Chavez alisema kuwa anapokea matibabu ya Saratani nchini Cuba 
 
Chavez alionekana kama mpigania haki za watu maskini kwa kusisitiza sera zake za kisosholisti na kuzichanganya na demokrasia.
Mwili wa Chavez ulipitishwa katikati ya mji mkuu Caracas na kusindikizwa na maelfu ya watu waliomuunga mkono,Watu wengi waliangua kilio huku wakichukua picha za kiongozi wao aliyefariki dunia .
 
Chavez alikuwa na maadui wengi pamoja na wale waliomuona kama mwokozi wao kwa sababu ya sera zake za kisosholisti.Watu wengi waliangua kilio huku wakichukua picha za kiongozi wao aliyefariki dunia .
 
Hugo Chavez hakupendwa na kila mtu Venezuela wakati wa utawala wake.Wapinzani wa Hugo Chavez wakisherehekea katika moja ya kumbi za maburudiko baada ya kupokea habari za kifo chake mjini Florida, Marekani. Picha Kwa Hisani ya Reuters na AFP
……………………………………………………..

Mwili wa mareheu rais Hugo Chavez wa Venezuela, umelazwa katika kituo cha mafunzo ya jeshi katika mji mkuu Caracas Mapema leo mwili wa marehemu Chavez ulipitishwa kwenye umati mkubwa wa wafuasi wake katika mitaa ya mji mkuu Caracas. Watu wengi waliangua kilio huku wakichukua picha za kiongozi wao aliyefariki dunia.Mama yake na watoto wake walikusanyika mbele ya jeneza kutoa heshma zao .

Makamu wa rais Nicolas Maduro anaongoza shughuli hiyo. Mwili wa rais Chavez umepelekwa katika chuo cha kitaifa cha mafunzo ya kijeshi ambapo utazikwa kesho Ijumaa. Bwana Chavez alifariki akiwa umri wa miaka 58 baada ya kuugua Saratani kwa zaidi ya miaka miwili. Maelfu ya watu awali walikwenda barabarani mjini Caracas kutoa heshima zao za mwisho kwa Chavez wakifuatana na gari lililokuwa limebeba jeneza lake kuelekea katika chuo cha mafuzno ya jeshi.

Mazishi ya kitaifa ya Chavez yatafanyika Ijumaa. Mkuu wa ulinzi wa Rais alinukuliwa akisema kuwa alikuwa na bwana Chavez alipofariki. Generali Jose Ornella, alisema kuwa Chavez alifariki kutokana na mshtuko wa moyo na katika siku zake za mwisho kabla ya kifo cha ealisema angependa kuendelea kuishi. Jeneza lake lililokuwa limefunikwa bendera ya nchi hiyo uliwekwa katika ukumbi ambao ni kumbukumbu ya waliopigania uhuru wa watu wa Amerika ya Kusini

Maelfu ya watu walipanga foleni kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu Chavez, wakiwemo maafisa wa serikali na viongozi wa Amerika ya Kusini,kama Rais wa Bolivia Evo Morales na Rais wa Argentina Cristina Fernandez de Kirchner.

Source: BBC SWAHILI

YASEMAVYO MAGAZETI YETU

j 001 602f8

j 002 99345
j 003 5f85a
j 004 92b01
j 005 c0a65
j 006 d914b
j 007 c07f6
j 008 82d42
j 009 3e665
j 010 72521
j 011 dbe0f
j 012 4a030
j 013 a1d07
j 014 87915
j 015 4ad24

WANAWAKE WASHEREKE SIKU YAO KWA KUPEWA KIPAO MBELE

1 93513
Ofisa Mawasiliano Mwandamizi, Mradi wa CHAMPION, Muganyizi Mutta akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Iringa katika ukumbi wa royal hotel mafinga wiki hii.
Na Denis Mlowe, Iringa
WANAHABARI nchini wametakiwa kuandika habari zinazolenga kukuza usawa wa jinsia katika vyombo vyao vya kazi.
Ofisa Mawasiliano Mwandamizi, Mradi wa CHAMPION, Muganyizi Mutta alisema hayo wiki hii wakati wa mafunzo ya wanahabari mkoani Iringa yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Royal Park mjini Mafinga.Mutta alisema, uwiano wa habari zinazoripotiwa na vyombo vya habari nchini kuhusiana hauko sawa hivyo kushindwa kufikia malengo ya uwiano wa nusu-kwa-nusu ambao unahimizwa kwa sasa kote ulimwenguni.Alisema, vyombo vingi vya habari kuanzia magazeti, televisheni na radio kwa asilimia kubwa vimebeba habari za wanaume kuliko wanawake, jambo ambalo linapaswa kubadilika.


“Vyombo vingi vya habari vimeegemea katika habari ambazo hazina usawa kwa upande wa wanawake kuanzia kwenye habari zenyewe, picha zanazochapishwa na matangazo ambayo yameegemea upande wa jinsia ya kiume,” alisema.

Mutta alisema, tofauti ya uwiano huo inaanzia ngazi za chini katika jamii hadi kwenye sekta nyingine, hivyo kuwataka wanahabari kuondokana na mtazamo huo hasi ambao haulengi kuleta usawa na zaidi humbagua mwanamke.

Aidha, alitoa mfano wa vichwa vya habari vinavyotumika katika vyombo vingi vya habari, hususan magazeti, ambavyo vinamuonyesha mwanamke kama ndiye mwathirika mkubwa katika masuala yote ya ujinsia.

“Kati ya vitu vinavyokuwa na tofauti ni katika kuchagua vichwa vya habari, picha zinazochapishwa katika vyombo vya habari, sentensi zinazotumika na maneno vinaonyesha ni kiasi gani mwanamke anabaguliwa katika vyombo vya habari” alisema Mutta

Naye Paulina Kuye mwandishi wa habari wa radios Nuru Fm alisema kwamba wanawake wengi wanakosa kujiamini katika kufanya kazi za uandishi wa habari na kukata tamaa kutokana na kutokukubali kukosolewa.

“Sisi wanawake pia tunachangia sana kuwa wachache katika tasnia ya habari na kutojiamini kwetu nacho ni chanzo kikubwa sana kufanya fani hii kutawaliwa na wanaume” alisema Kuye.

Ipc yalaani alichofanyiwa kibanda

0ppppppp df988
Na  Francis  Godwin,Iringa

KLABU  ya  Waandishi  wa Habari Mkoa  wa Iringa (IPC) imeeleza kusikitishwa na wimbo la vitendo vya ukatili na ukiukwaji  wa haki  za binadamu vinavyoendelea   kujitokeza  kwa  wanahabari  hapa nchini na  kulitaka  jeshi la  polisi kuusaka mtandao huu  wa utekaji wa  wanahabari nchini.Akizungumza na wanahaari mjini hapa leo , Mwenyekiti  wa IPC. Frank Leonard  alisema muda umefika kwa wanahabari nchini kote bila kujali tofauti zao kufanya tathimini ya mahusiano na wadau wao ili tahadhari zianze kuchukuliwa.

Akizungumzia tukio la  kinyama ambalo amefanyiwa  Mwenyekiti  wa  Jukwaa la  Wahariri Nchini, Absolom Kibanda ambae  pia ni Mhariri  wa Kampuni ya New Habari, Leonard alisema nimuhimu kwa wanahabari kukataa kuendelea kushuhudia wenzao wakinyamazishwa kwa kufanyiwa vitendo vya ukatili ikiwa ni pamoja na kuuawa.

Alisema katika mazingira ya kushangaza, ukuaji wa tasnia ya habari unaolenga kuchochea maendeleo ya nchi, unakwenda sambamba na mfululizo  wa matukio yanayolenga kuipunguza kasi hiyo.
Alisema baadhi ya wanahabari wanaofuatilia na kuchapisha au kurusha matukio yanayohusu maslai ya umma wamekuwa wakifukuzwa, wakitukanwa, wakinyang'anywa au kuvunjiwa vifaa vyao vya kazi, wakipigwa na kuuawa jambo linaouwa semokrasia, haki na maendeleo ya nchi.
"Ni wazi usalama  wa wanahabari upo mashakani; ni muhumi tukaitathimini hali hiyo na kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na kupunguza mahusiano ya kudumu na  wadau  wasiopenda uwepo  wa vyombo  hivyo  vya habari," alisema.

Alisema  wakati matukio ya wanahabari kushambuliwa yakishamiri, kasi ya vyombo vya dola katika kuwasaka na kuwafikisha wahusika katika mikono ya sheria ni ndogo ikilinganishwa na matukio yanayohusu wadau wengine likiwemo jeshi la Polisi.
Leonard alisema wanahabari wanatakiwa kushikamana na kupaza sauti zao juu ili matukio ya aina hiyo yakomeshwe na yanapotokea wahusika wasakwe kwa nguvu zote na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema unyama uliofanywa kwa Kibanda, unakumbusha majonzi kwa watanzania ambao bado hawajasahau jinsi Mwandishi  wa  Channel Ten na Mwenyekiti  wa IPC, Marehemu  Daudi Mwangosi alivyouawa kinyama na Polisi wakati akitimiza wajibu wake Septemba 2, mwaka jana katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Pia  tukio la  kutekwa kwa mtangazaji  wa Redio Kwizera-Kibondo Issa Ngumba na  kukutwa akiwa ameuwawa kinyama pamoja na matukio mengine ya uvamizi  wa  wanahabari  likiwemo  la akina  Said Kubenea  na Ndimara  Tegambwage kumwagiwa  tindikali   wakiwa ofisini kwao.

"Tunajiona kama watoto tusio na msaada; kilio chetu hakifiki mbali; tuko katika wakati  mgumu tunapokuwa katika mazingira ya kutimiza wajibu wetu kwasababu hatujui nani ni adui wa habari na wanahabari," alisema.
Wakati hayo yakitokea kwa wanahabari, Leoanard alikwenda mbali zaidi na kuzungumza uwepo wa baadhi ya wanahabari wanaofurahi wakiona wanahabari wenzao wanaokutwa na matukio ya aina hiyo.
"Wapo, tena wengi tu na wengine wanajulikana; kwa lugha za mtaani wanaitwa risasi kidole, kazi yao ni kuvujisha taarifa ya kazi zinazofanywa na wanahabari wenzao kwa wadau wanaofahamiana nao; lengo lao ni kupata ujira lakini ujira unaouwa haki ya watanzania ya kupata habari zinazohusu maendeleo yao bila kujali kama ni mbaya au nzuri," alisema.
Katika kuchochea maendeleo ya taifa, Leonard alisema habari ni muhimu katika ujenzi wa Taifa; ukimfanyia unyama mwandishi wa habari unaongeza manung'uniko katika jamii na kuzorotesha maendeleo.
Alisema Jeshi la Polisi linapaswa kutumia nguvu zake zote kuwasaka wahusika wa tukio lililomkuta Kibanda na kuwafikisha katika vyombo vya dola ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye hila dhidi ya wanahabari na vyombo vya habari.