This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, February 6, 2014

PICHA YA MTOTO WA SHAKIRA KWA FANS WAKE .....


This is cute!!!! 

Shakira and her husband Gerald Pique welcomed a baby boy some weeks ago and they named him Milan Pique!

"SIDHANI KAMA USHIRIKINA UNAFAIDA KATIKA MUZIKI"...POMMY DIMPOZZ


Baada ya taarifa kuenea katika mitandao kuhusu Diamond anatumia mganga wa jadi katika kazi zake za muziki....
 
Leo kupitia Clouds Fm double XXL katika jiwe la wiki rafiki yake wa karibu 'Ommy Dimpoz' aliweza kusema kwa upande wake hadhani kama vitu vya ushirikina vinaleta faida katika upande wa muziki na wala hajawahi kujihusisha navyo maishani mwake.


Swali:Mara ya mwisho baada ya kukutana na Diamond Platinum hamjawahi kuzungumzia mambo ya ushirikina"Kusema kweli mara mwisho nakumbuka nilikutana naye na tukazungumzia kuhusu show yangu lakini mambo mengi hatujazungumza.Ommy Dimpoz alisema

HIVI NDIVYO MATUMAINI ALIVYOPOKELEWA JIJINI DAR



   Matumaini (katikati) akisaidiwa na wasanii wenzake muda mfupi baada ya kutua.

    Bi. Mwenda akiwa amembeba Matumaini mgongoni.

    Matumaini (kulia) akiwa na Bi. Mwenda (wa pili kushoto) na anayefuata (kushoto) ni msanii mwenzake Kiwewe wakisubiri gari la kumpeleka hospitali.

    Askari wakiwaelekeza wasanii kukaa upande mmoja ili apate hewa.

    Matumaini akiwa amebebwa mgongoni na msanii mwenzake, Mariam Athuman ‘Kalunde’ akimpeleka kwenye gari.

   Mama mkubwa wa Matumaini, Bi. Elizabeth (kushoto) na Matumaini (katikati) wakiwa ndani ya gari tayari kuelekea hospitali ya Amana.

    Rais wa Shirikisho la Filamu nchini (TAFF), Simon Mwakifwamba akizungumza na wasanii maeneo ya Amana wakati Matumaini akiwa kwa daktari.
-----------
MSANII wa vichekesho ambaye alikuwa nchini Msumbiji, Tumaini Mwakibibi ‘Matumaini’ jana alipokelewa na wasanii wenzake kibao baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar akiwa hoi kutokana na kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.

Matumaini alitua uwanjani hapo jana majira ya saa 9:30 alasiri ambapo kutokana na hali yake kuwa mbaya wasanii walimbeba mgongoni na kumfikisha kwenye gari ambapo walimpeleka moja kwa moja hospitali ya Amana alikolazwa mpaka sasa akiendelea kupatiwa matibabu.

Mshuhudie Shilole akiwa ndani ya vazi la Kanga moja kitandani….

STAA wa mduara Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’  ameamua  kuachia  picha  adimu  akiwa  kitandani  na  kanga  moja  tu  bila  chochote  kama  ishara  ya  kuwashukuru  mashabiki  wake  kwa  sapoti  kubwa  ambayo  wamekuwa  wakimpa  na  kumfanya  awe  juu  kimuziki…
Domo  langu  limefanikiwa  kuzinasa  nakala  adimu  za  picha  hizo  kama  zinavyoonekana  hapo  chini
sh sh1

Wafahamu vijana 10 wa kitanzania wenye mvuto zaidi hapa nchini

Siku hizi ni tofauti kabisa na zamani  ambapo tumezoea kuona watu wazima/wazee peke yao ndio watu wenye uwezo mkubwa na nguvu sana kwa hapa Tzee,siku zinavyozidi kuendelea mambo yanazidi kubadilika na siku hizi vijana ndio watu wanao-hustle juu chini kuweza kupata success hata zaidi ya wazee wao waliotangulia,kwa hapa Tzee tumeweza kupata baadhi ya vijana maarufu ambao ni most powerful na wenye influence kubwa kwa vijana wenzao.
Diamond Platnumz
1175277_290618997742804_1713839130_n
Jina lake halisi ni Naseeb Abdul,so far ni msanii anayelipwa zaidi kuliko msanii yeyote wa bongo fleva hapa Tzee,na kuongoza kulipwa zaidi katika show zake za nje na ndani ya nchi.ukimuongelea Diamond platnumz hivi sasa Africa lazima utakuta idadi flani hivi ya watu wanamfahamu msanii huyu na hiyo ni mbali na huko ulaya na kwingineko duniani,ameweza kufanya kazi zake za muziki na wasanii wakubwa duniani na kuweza ku-share stage moja na wasanii akiwemo rick ross,Ludacriss ,Psquare na wengine wengi,mbali na muziki pia ni ambassador wa cocacola zero,goodwill ambasador wa malaria na ni moja ya wasanii wanaosaidia na kujitolea katika shughuli mbalimbali za kusaidia jamii.
Flavian Matata
flaviana-matata-0
Kutoka mshindi wa kwanza wa miss universe Tanzania mwaka 2007 na kwenda kuiwakilisha tanzania mwaka huo huo,Flaviana aliweza kuingia kwenye top 15 , kuingia nusu fainali na baadae kushika nafasi ya Sita na ndiye aliyekuwa mtanzania wa kwanza kushiriki mashindano hayo ya miss universe huku akiwa amenyoa nywele zake tofauti na washiriki wenzake,it was a game changer kwa jina la Tanzania kujulikana kuwa kuna vipaji vingi vilivyofichika. Matata ameshiriki katika matangazo mengi sana akiwa kama model,mwaka 2011 aliweza kushinda tuzo ya model of the year award ya Arise magazine ya huko nchini Lagos Nigeria,ametokea katika magazine mbalimbali duniani yakiwemo Dazed & Confused, Glass Magazine, L’Officiel and i-D Magazine. mbali na advertisement amefanya modeling ya mavazi ya brand za wanamitindo maarufu duniani kama  Mustafa Hassanali, Vivienne Westwood, Tory Burch, Suno, na  Louise Gray,pia kushirikishwa katika picha za kutangaza collection ya mwanamitindo maarufu duniani , Alexander McQueen katika Topshop Spring 2011 ad campaign.Flaviana matata baada ya kuchukua tuzo ya  “Face of Africa”  aliweza kuwasaidia wanawake wenzake na anaendelea na kampeni yake katika kusaidia wasichana waweze kwenda shule kupitia foundation yake, Flaviana foundation.amekuwa ni kioo cha wanawake na vijana wengi sana hapa Tzee.
January Makamba
January-Makamba
Huwezi kutaja list hii na kumuacha mtu huyu maarufu sana na ni role model wa vijana wengi sana hapa nchini kwa yale aliyoweza ku-achieve katika umri wake huo mdogo,unaambiwa alikuwa msaada mkubwa sana katika serilkali ya Raisi.Kikwete toka mwaka 2005,mbali na hayo aliweza kupata kiti cha ubunge kupitia jimbo lake la Bumbuli kupitia chama chake cha CCM,nafasi aliyoweza kuipata kwa asilimia 80% kati ya wapinzani wake nane,hii inaonyesha kuwa ni moja ya kijana anayeaminika sana na  kupendwa sana na wananchi,huyu ni moja kati ya waheshimiwa wanaopenda ku-socialize sana na watu wa hadhi mbali mbali,na wa aina tofauti kitu kinachozidi kumfanya kukubalika sana na vijana wenzake pia kumsaidia kujua matatizo yao na jinsi yakuwapatia suluhu.
Hashim Thabeet
thabeet_1_120718
Jina lake halisi ni Hashim Thabeet Manka ila maarufu kama Hashim Thabeet tu,ni moja kati ya basketballer professional duniani anayeichezea timu ya Oklahoma City Thunder.ni vigumu sana kuamini kwa mchezaji maarufu wa huko NBA kutoka hapa hapa kwetu Tanzania,huyu ni moja kati ya wachezaji warefu sana maarufu katika ligi ya mpira huu wa kikapu wa huko marekani,ni moja kati ya wanamichezo wanaolipwa kuliko yeyote kutoka hapa Tanzania na hata baadhi ya nchi,za hapa east Africa,na ni moja kati ya celeb wakubwa sana hapa Tzee wanaojishughulisha sana na kazi zakujitolea kwa jamii.
Lady Jay Dee
Jide-3
Ni moja kati ya wanawake wenye majina makubwa sana hapa mjini,ikiwa ni msanii mkubwa sana wa kike anayeheshimika kutokana na kazi zake nzuri za kimuziki, anamiliki biashara mbalimbali hiyo ni mbali kabisa na muziki unaosemekana unamuingizia hela nyingi sana,mbali na muziki pia ni mjasiliamari mkubwa sana,akiwa ni  CEO wa Nyumbani Lounge ,Studios na biashara nyingine nyingi,she is a hustler.ukimuongelea lady jay dee ni msanii wa kike mwenye umaarufu na utajiri mkubwa, anapendwa na kila mtu na kukubalika sana kimuziki na nje ya mziki huu wa Bongo fleva.
Jerry slaa,
slaa1
Huyu ni Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmshauri Kuu ya CCM Taifa ambaye pia ni Mstahiki Meya Manispaa ya Ilala,ni moja kati ya vijana wenye nguvu sana hapa Tzee kwa umri wake tu na kuweza kushikilia cheo kikubwa kama hicho ni very rare hasa kwa mataifa kama yetu ya hapa Africa kuzoea watu wazima tu wakishikilia ngazi za juu ya uongozi,ni moja kati ya vijana wanopendwa sana na wananchi na kukubalikasana na kila mmoja sit u vijana wenzio na hata watu wazima kutokana na jitihada anazozionyesha katika kuleta maendeleo.
Osse Greca Sinare 
Osse-Sinare
Talking about photographers maarufu sana hapa Tanzania na nje ya Tanzania,Osse is the name to be mentioned, Jina lake na kazi yake imeweza kutambulika na mataifa mbali mbali hata nje ya Tanzania,na kuweza kuongelewa na baadhi ya majarida na mitandao mikubwa sana  ikiwemo Africa-vogue,fashion Ghana.com ,FAS mgazine na  Msongo,si tu hapo pia ameweza kufanya interview nyingi sana na media kubwa africca ikiwa inaongelea kazi zake kwa kutambua uwezo wa kazi zake,mwaka 2012 aliweza kupikea tuzo kutoka Swahili Fashion Week tuzo ya Best Fashion Photographer,pia hujishughulisha na kazi za kusaidia jamii katika kuleta mabadiliko katika maisha ya jamii zetu za hapa Tanzania.
Zitto Kabwe
400928_477334872287215_1696426767_n
Jina lake halisi anaitwa Kabwe Zuberi Zitto ila maarufu anajulikana tu kama Zitto Kabwe,huyu ni mmoja wa wanaharakati wanaojitahidi kutetea haki za wananchi bila kuficha lolote lile kwa hadhira,ni moja ya tunda litokalo kwenye chama cha demokrasia,pia ni mheshimiwa mbunge wa jimbo la huko kigoma,ni moja kati ya vijana  wenye umri mdogo na kuweza kutikisa sana nchi haswa kwa hoja zake,umahiri wake kisiasa ndio moja ya vitu vinavyopelekea kuzidi kupendwa sana na wananchi na hasa katika swala zima la kutetea haki za wananchi,ni kijana hodari sana inapokuja kwenye swala zima la siasa.
Patrick Ngowi
Profile-Pic-2013
Ni baada tu ya kuona kuwa kulikuwa na umuhimu wa kupata plan B ya umeme hapa Tzee,Patrick aliamua kuachana na biashara ya kuuza simu na kuanza kuingiza umeme wa solar hapa Tzee kwa mtaji mdogo tu na baadae kuzidi kukua huku wananchi  kuweza kupata suluhisho la tatizo lao la umeme hasa kule kulipokosekana tumaini la kuwa na umeme,hivi ndivyo alivyoanza kujipatia umaarufu mkubwa na biashara kukua sana kupitia kampuni yake inayoitwa Helvetic Solar Contractors,kampuni iliyongezeka thamani na kufikia zaidi ya dola milioni tatu kwa mwaka,hawa ni moja kati ya vijana walioweza kutumia fursa.

Tupe Maoni yako hapo chini

Mbunge Chadema Kortini vurugu za Udiwani Kahama

chadema_25071.jpg
Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki (Chadema), Sylvester Kasulumbayi
Kahama. Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki (Chadema), Sylvester Kasulumbayi na Diwani wa Kata ya Buselesele, Crispian Kagoma na watu wengine 14 wamepandishwa kizimbani kwa tuhuma za kujeruhi katika vurugu zilizoibuka katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Kasulumbayi na wenzake 15, ambao wanaaminika kuwa wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kahama saa 8.00 mchana jana na kusomewa mashtaka sita kila mmoja.
Akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mfawidhi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama, Gadiel Mariki, Mwendesha Mashtaka Shukrani Madulu alisema washtakiwa wote kwa pamoja walitenda makosa hayo Februari 4, mwaka huu.
Madulu aliiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa hao wakiongozwa na mbunge huyo walitenda kosa hilo la kuwashambulia kwa mapanga wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za kuwania udiwani wa Kata ya Ubagwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.
Alisema mashtaka matano ni kushambulia na kujeruhi kwa mapanga, na moja la kuharibu mali, ikidaiwa kuwa katika vurugu hizo washtakiwa waliishambulia gari la CCM la wilaya hiyo na kuliharibu.
Washtakiwa wote walikana mashtaka yote na kuomba mahakama iwape dhamana ili waendelee na kampeni za kumnadi mgombea wao wa nafasi ya udiwani katika kata hiyo ya Ubagwe.
Maombi hayo yalipingwa na Mwendesha Mashtaka, akiiomba mahakama isitoe dhamana kwa kuwa hali za majeruhi watatu ni mbaya kwa kuwa tayari wamepelekwa kwenye Hospitali ya Rufaa na Bugando mkoani Mwanza, baada ya matibabu yao kushindikana wilayani Kahama.
Kutokana na hali hiyo, Hakimu Mariki alikubaliana na hoja hiyo na kuahirisha kesi hiyo hadi leo ambapo kesi hiyo itasikilizwa.
Watuhumiwa wote walipelekwa mahabusu baada ya dhamana hiyo kuzuiliwa.
Waliojeruhiwa kwenye vurugu
Wafuasi watano wa CCM wilayani Kahama akiwamo ofisa mtendaji wa Kata ya Ubagwe walijeruhiwa kwa mapanga kwenye vurugu hizo.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Andrew Emmanuel alisema Masunga, Kamaro na Peter walisafirishwa kwenda Bugando jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.
Chanzo cha vurugu
Vurugu hizo zilitokea juzi saa moja usiku katika Kata ya Ubagwe muda mfupi baada ya wafuasi hao kumaliza kampeni zao za kumnadi mgombea wa CCM, Hamis Majogolo anayewania udiwani kwenye kata hiyo.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, wafuasi hao walikumbwa na mkasa huo wakati wakiwa kwenye gari la CCM ambalo pia lilikuwa na watuhumiwa watatu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema waliokuwa wakipelekwa Kituo Kidogo cha Polisi Bulungwa.
Ilidaiwa watuhumiwa hao nao walidaiwa kufanya fujo kwenye mkutano wa Kampeni wa Chama cha Tadea ambacho pia kina mgombea anayewania nafasi hiyo.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa wanachama wa Chadema waliweka kizuizi kwa kutumia gari la Kasulumbayi kwenye barabara ya kuelekea kituo kidogo cha polisi.
Peter, ambaye ni dereva wa gari la CCM alisimulia kuwa walipofika kwenye kizuizi hicho walisimama, ndipo wafuasi wa Chadema waliposhuka kwenye gari la Mbunge huyo na kuanza kuwashambulia kwa mapanga wakitaka kuwaokoa wenzao watatu.CHANZO MWANANCHI
Watatu wakamatwa Njombe
Pia Jeshi la Polisi wilayani Njombe linawashikilia watu watatu wanaodaiwa kufanya fujo katika ofisi ya CCM ya tawi la Matalawe, Jumatatu iliyopita.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani alisema kuwa watu hao walikwenda kwa gari kwenye maeneo ya tawi hilo na kuanza kuchana picha za mgombea udiwani wa CCM, Menard Mlyuka.
Aliwataja watu waliokamatwa kuwa ni Award Karonga (40), Ally Mhagama (43) na Robert Mabu (24)

FAMILIA KUMINA TANO HAZINA MAHALA PAKUISHI GEREZA PAWAGA


 Ofisi za Gereza Pawaga zilizo ezuliwa na upepo mkali ulio ambatana na mvua juzi jioni.

 Sehemu ya masalia ya bati na matandiko yalio haribiwa na mvua

 SACAP Deusdedit Kamugisha Afisa wa Magereza Mkoa wa Iringa pichani kulia akiongozana na Mkuu wa gereza Pawaga SP.Sosthenes Mwakapala akikagua uharibifu ulio jitokeza katika nyumba za askari na majengo wanayo tarajia kuhamia kwamuda.

 Bustani ikiwa imeharibiwa na Mvua ilionyesha ikiwa na upepo mkari 

Baadhi ya Vyombo vya familia za Askari Magereza vikiwa nje baada ya Mvua kuharibu makazi yao.
Nyumba kumi na tano za Askari Magereza wa Gereza Pawaga wilaya ya Iringa zimeezuliwa na Upepo mkali ulio ambatana na mvua kubwa ya mawe ilionyesha juzi majira ya saa 9 alasiri mpaka saa kumi na moja jioni na kuanza tena saa mbili ya usiku mpaka saa tano usiku.
Akiongea na mwandishi wa habari Mkuu wa Gereza la Pawaga SP.Sosthenes Mwakapala alisema adha hiyo ya mvua imesababisha familia hizo kukosa mahala pa kuishi pamoja na thamani zilizo salia wakati walipokumbwa na mvua hiyo ingawa hakuna madhara kwa binadamu sambamba na hilo kumeezuliwa ofisi za tano za gereza zinazojumuisha Stoo, Bohari, Mapokezi, Utawara pia Bafu ya wafungwa.
 Madhara mengine yaliyo jitokeza ni kuharibiwa vibaya kwa heka tano za Bustani ya gereza yenye mazao mchanganyiko ikiwamo mashina ya Ndizi, Mipapai, Mihogo, Mahindi pamoja na Miwa mimea hiyo imevunjika kabisa haitegemewi  kupona tena.
Mkuu wagareza la Pawaga SP. Sosthenes Mwakapala alisema wao kama uongozi wagereza na viongozi wasaidizi wake wamechukua jukumu la kuhakikisha askari hao na familia zao wanapata mahali pakujihifadhi kwa muda wakati wakisubiri ufumbuzi toka ofisi ya Magereza mkoa wa Iringa. Kwakuwahamishia katika majengo ya Shule ya Msingi, Bwalo la gereza, Ghala la chakula  wakae kwa muda.

MSAMBINUNGWA” by TUNDA MAN feat ALLY KIBA

MSAMBINUNGWA” by TUNDA MAN feat ALLY KIBA
(Photo’s) The Making of music Video “MSAMBINUNGWA” by TUNDA MAN feat ALLY KIBA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/01/photos-making-of-music-video.html#sthash.txPgpp0o.dpuf







Nini hatma ya kesi ya Kenyatta ICC?

KESNYATA_185c0.jpg
Pande zinazohusika katika kesi inayomkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC Mjini The Hague zimekuwa na kikao cha kujadili mstakabali wa kesi hiyo.
Kiongozi wa mashtaka wa ICC Fatou Bensouda amekiri kuwa bado hana ushahidi wa kutosha kuwezesha kesi hiyo kuendelea.
Mawakili wanaomwakilisha Rais Kenyatta wanataka kesi hiyo kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2007 itupiliwe mbali.
Bensouda amesema kuwa bado kuna maswala yanayozua utata na ambayo yanahitaji uchunguzi wa kina. Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mashahidi wengi wamehongwa au kutishwa kiasi cha kujiondoa katika kesi hiyo.
Viongozi wa mashitaka ICC wanasema kuwa Kenyatta aliongoza ghasia hizo lakini kesi dhidi yake imefanywa dhaifu kutokana na baadhi ya mashahidi kujiondoa katika kesi hiyo.
Mawakili wa Kenyatta wanatuhumu upande wa mashitaka kwa kusisitiza kutaka taarifa kuhusu akaunti ya benki ya Rais Kenyatta kuona ikiwa kuna pesa zozote zilizotolewa kwa lengo la kutumika wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007/08
Wakili wa waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi amesisitizia mahakama kuwa kutupiliwa mbali kwa kesi kutawakosesha waathiriwa haki. Mahakama inatarajiwa kutoa uamuzi katika siku chache zijazo.
Rais Kenyatta alifikishwa ICC kutokana na tuhuma kuwa alikuwa mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya mwaka 2007/2008. Anakabiliwa na makosa ya mauaji na uhalifu mwingine dhidi ya binadamu.
Kadhalika Kenyatta alishitakiwa pamoja na makamu wake William Ruto kwa tuhuma sawa. Kesi dhidi ya Ruto inaendelea katika mahakama hiyo.
Watu 1,200 walipoteza maisha yao katika ghasia za uchaguzi mkuu mwaka 2007/08 huku maelfu wakilazimika kutoroka makwao. Wote wamekanusha mashitaka.
Kesi yenyewe ilitarajiwa kuanza Jumatano, lakini ikaahirishwa kwa mara ya nne mwezi jana wakati ambapo wendesha mashitaka waliposema kuwa shahidi mwingine alijiondoa kwenye kesi huku wakiomba mahakama kuwapa muda zaidi kutafuta ushahidi. CHANZO BBC SWAHILI