This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Monday, June 24, 2013

BARNABA APOTEZA FAHAMU WAKATI WA MAZISHI YA MAMA YAKE

Mwanamuziki Elias Barnabas 'Barnaba' akiweka udongo katika kaburi la mama yake mzazi, Mariamu  Arubeth.
Baada ya kuweka udongo Barnaba akaishiwa nguvu.
Barnaba akiwa kapoteza fahamu wakati wa mazishi ya mama yake.
Akipatiwa huduma ya kwanza.
Baada ya kuzinduka.
Akipelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu.
Mwanamuziki Elias Barnabas 'Barnaba' jana alipoteza fahamu wakati wa mazishi ya mpendwa mama yake mzazi, marehemu Mariamu Arubeth katika makaburi ya Mburahati jijini Dar es Salaam. Hali ya Barnaba ilibadilika baada ya kuweka udongo katika kaburi la mama yake ndipo alipopoteza fahamu na kupatiwa huduma ya kwanza kisha kupelekwa hospitali. GPL inampa pole msanii Barnaba na wanafamilia wote kwa msiba huu.
(Picha kwa hisani ya This is Diamond)

SUGU AGOMA KUOMBA RADHI BAADA YA KUDAI KUWA WAZIRI MKUU NI MPUMBAVU


Juzi, mbunge  wa  mbeya  mjini  alitoa  tusi  zito  kwa  waziri  mkuu  wa  Tanzania  na  kudai  kuwa  Tanzania  haijawahi  kuwa  na  waziri  mkuu  mpumbuvu  kama  yeye...

Kupitia  account  yake  ya facebook, Sugu, ambaye  ni  mbunge  wa  mbeya  amezidi  kusisitiza  kuwa  hawezi  kuomba  msamaha wala  kuifuta  kauli  yake....

Hii   ni  post  yake  facebook:

"...naskia kuwa watu wanasema kwamba eti nimefuta kauli yangu kuhusu waziri mkuu na amri yake kwa polisi kupiga wananchi?!...

Sina sababu ya kufuta wala kuomba radhi, na nasimamia kauli yangu to the end...kwanza 'upumbavu' sio tusi,upumbavu kwa kiingereza ni stupidity-which is lack of knowledge and understanding...

So hata uwe na cheo gani kama ukishindwa kuwa na 'understanding' juu ya madhara ya kauli zako kwa taifa then u r 'stupid'...ambapo kwa kiswahili ndio 'mpumbavu'..."

KIJIJI CHA NGONO CHAFICHULIWA HUKO SINZA,MAKAHABA WAAHIDI KUTOACHA KAZI HIYO

 


NI hakika ‘mtaa wa ngono’ umefumuliwa! Sakata hilo lilijiri saa tisa usiku, Ijumaa iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori jijini Dar eneo ambalo makahaba wameligeuza chumbani

Kwa mujibu wa takwimu za kiserikali, eneo hilo
(kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori) limekubuhu kwa wasichana kujiuza nyakati za usiku huku makao yao makuu yakiwa eneo la Afrika Sana hasa pembezoni mwa Corner Bar.
 

Mmoja wa viongozi wa serikali ya mtaa ya eneo hilo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe , alisema:
 

“Tumejitahidi sana kushirikiana na polisi ili kutokomeza ukahaba eneo hilo lakini wapi! Hawa mabinti ni wabishi, mbaya zaidi wamelifanya eneo hili kuwa la ngono.

“Watoto wetu wanapita usiku pale wanawaona wanavyofanya, wanatuharibia kizazi kijacho, kama wao wamejishindwa wasiwaambukize wengine.”
Siku ya tukio, saa tisa usiku,  askari wa ulinzi shirikishi walijipanga kwa ajili ya kuufumua mtaa huo huku wakiwa na tahadhari kufuatia habari za kiintelijensia kudai kuwa, makahaba hao walipanga kuua mtu punde watakapovamiwa.
 

Askari hao wakiwa kwenye doria ya kila usiku, waliwavamia makahaba hao eneo lenye majani madogo katikati ya Afrika Sana na Mapambano upande wa yadi ya Mwanamboka wakiwa na wateja wao wakifanya ngono hadharani.


Katika hali iliyoonesha makahaba wamejiimarisha kwa ulinzi siku hizi, wakati wa zoezi hilo, machangu hao sanjari na vibaka  wanaowaunga mkono wakisemekana ni ‘walinzi’ wao, waliokota mawe na kuwarushia askari hao hali iliyozua tafrani zaidi.


Ndipo piga nikupige ilipozuka ambapo askari walionesha umahiri wao wa kupambana na wahalifu kwa kuwadhibiti kwa vichapo vya hapa na pale na kufanikiwa kuwaweka wengi chini ya ulinzi.


Kuona hivyo, baadhi ya makahaba na wateja wao walifanikiwa kuwachoropoka askari bila nguo na kutokomea gizani hivyo kulifanya eneo hilo kuwa jeupe.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya makahaba waliokimbia walijikuta wakiacha kwenye majani nguo zao za ndani na kuzua maswali kwamba ni kwa nini hawakuwa wamezivaa!


“Jamani hizi si nguo zao za ndani? Ina maana wakiwa kazini hawavai siyo? Wanakuwa tayaritayari kwa kazi? Jamani!” alisema kwa mshangao mkubwa mmoja wa askari hao.
 
Licha ya kuwa chini ya ulinzi mkali, baadhi ya makahaba walionaswa walikuwa wakiwalalamikia askari hao kwamba wanawafuatafuata wakati kila mtu siku hizi anaangalia atakulaje!
 

“Mnatuonea bure, nyie mnakula kivyenu na sisi mngetuacha tule kivyetu, hao watoto wenu mnaosema tunawaharibu usiku huu wao wanatokea wapi na wanakwenda wapi?” alisikika akisema kahaba mmoja aliyekuwa mtata kuwekwa chini ya ulinzi.


Mwingine akadakia: "Kama mnataka tuwape uroda si mseme, mnatukamata kila siku kwani tunawatibulia nini majumbani mwenu? Lini tumekuja kuwaghasi wakati mmelala na wake zenu?”
 

Uchunguzi wa kawaida ulibaini kuwa muda rasmi wa 
makahaba hao kuwasili eneo la Corner Bar ili kuanza ‘kazi’ ni saa mbili usiku japokuwa wapo wanaoripoti mapema na kufanya biashara hiyo kwa wizi kulingana na wateja wenye ‘kiu’ nyakati hizo.

Licha ya kuwa chini ya ulinzi, makahaba hao waliahidi endapo watapelekwa polisi na kutoka watarejea eneo hilo kujiuza kwani ndiyo ajira inayowafanya waendelee kuishi katika Jiji la Dar es Salaam, kusomesha watoto vijijini kwao na kuwasaidia wazazi wao mahitaji mbalimbali.
 

“Hata kama mtatupeleka polisi, tutarudi tu hapa, sisi tunasomesha watoto, tunasaidia wazazi wetu vijijini, pia tunaishi Dar kwa sababu ya kipato hiki cha kuuza miili yetu, acheni hizo,” mmoja wa makahaba hao alisema bila kumung’unya maneno.

WABUNGE NA MASHOGA WATETA.....HOFU YA KUWA NA RAIS SHOGA TANZANIA YATANDA


WABUNGE wanachama wa Chama cha Kupambana na Ukimwi (TAPAC), wiki iliyopita walikutana na kujadiliana mambo mbalimbali na mashoga katika mkutano wa mwaka wa chama hicho uliofanyika kwa muda wa siku tatu mjini  Dodoma. Katika mkutano huo, baadhi ya wabunge walionyesha wasiwasi wa taifa kupata rais shoga katika miaka ijayo kutokana na ongezeko la mashoga hapa nchini.

Mbali na wasiwasi ulioonyeshwa na wabunge, mashoga waliokuwa wakihudhuria mkutano huo, walilalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na wanajamii wenzao na kudai watambulike na wapatiwe huduma za msingi za kibinadamu.

Akizungumza katika mkutano huo uliomalizika jana, Mbunge wa Nkasi, Ally Kessy (CCM), alitahadharisha uwezekano wa nchi kupata rais shoga katika miaka ijayo, iwapo hatua za makusudi za kudhibiti hali hiyo hazitachukuliwa.

“Tabia ya kuwapeleka watoto kwenye shule za mabweni wangali wadogo wa umri wa miaka hadi miwili, itatuletea matatizo baadaye.

“Katika shule nyingi za bweni vitendo vichafu vinafanyika, vikiwamo vya ushoga. Katika vyuo vikuu hivi sasa kuna mashoga wasiopungua 40,000. Hii ni hatari, tusipojihadhari tutakuwa na rais shoga katika miaka ijayo,” alisema Kessy huku akishangiliwa na wabunge.

Mbunge huyo alitaka elimu dhidi ya ushoga na athari zake ienezwe nchini kupitia vyombo vya habari na nyumba za ibada.

Naye, mmoja wa mashoga waliohudhuria mkutano huo aliyejitambulisha kwa jina la Abdilah Ally, alieleza kuwa yeye ni shoga mwenye wanaume watatu lakini amekuwa akikutana na vitendo vya unyanyasaji kutoka ndani ya jamii inayomzunguka.

“Tunataka haki zetu. Tunanyanyaswa katika jamii hasa na polisi. Na sisi tunastahili huduma bora za afya na nyingine tuweze kujikinga na Ukimwi,”
alisema Ally, mkazi wa Dar es Salaam.

Wakati huo huo, taarifa iliyotolewa na Mshauri wa Masuala ya Ufundi wa Kampuni ya Jhpiego, Dk. Augustine Hellar, ilieleza kuwa kuna wanaume 397,458 waliotahiriwa nchini hadi Mei, mwaka huu katika mpango maalumu wa tohara kwa ajili ya kupambana na maradhi ya Ukimwi.

Dk. Hellar alitoa takwimu hizo alipowasilisha mada kuhusu tohara ya hiari kwa wanaume katika kukabili maambukizi ya Ukimwi nchini.

Alisema lengo la mpango huo ulioanza kutekelezwa Oktoba, 2011 katika baadhi ya mikoa nchini ni kutoa tohara kwa wanaume milioni 2.8 kila mwaka mmoja.

Alisema mpango huo umekabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwamo ya watu wazima ambao ndiyo walengwa kutojitokeza kwa wingi na baadhi ya watu kuhusisha hatua hiyo na upotevu wa nguvu za kiume.

Sunday, June 23, 2013

ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUGONGA NYUMBA AKIJIFUNZA KUENDESHA GARI MORO



Gari hilo baada ya kugonga nyumba na kuingia mpaka chumbani.
Chumba ambapo gari hilo liliingia.…
Gari hilo baada ya kugonga nyumba na kuingia mpaka chumbani.
Chumba ambapo gari hilo liliingia.
Baadhi ya mashuhuda wakiwa eneo la ajali.
Wananchi wakilifunga gari hilo tayari kuondolewa na winchi.
Likinyanyuliwa na winchi.
Likitolewa eneo la ajali.
NA DUSTAN SHEKIDELE, MOROGORO
MWANAMKE mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja jana usiku alinusurika kifo baada ya kugonga nyumba wakati akijifunza kuendesha gari aina ya Prado lenye namba za usajili T 952 BTJ.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa tatu usiku maeneo ya uwanja wa ndege jirani na Chuo cha Ujenzi njia panda ya kuelekea gereji ya Msuya.
Mbali na mwanamke huyo kunusurika kifo, pia familia iliyokuwa ikiishi kwenye nyumba iliyogongwa nayo ilinusurika baada ya gari hilo kuvunja ukuta wa nyumba na kuingia mpaka chumbani ambako familia ilikuwa inajianda kulala.
Mashuhuda wa tukio hilo walipohojiwa na mtandao huu walidai kwamba mwanamke huyo ambaye bado hajaiva kwenye udereva alikata kona iliyo eneo hilo kwa mwendo kasi.
"Huyu mama anajifunza kama unavyoona kibao cha 'L' kwenye gari yake, uzembe alioufanya alikata kona hii kwa mwendo wa kasi na kwamba badala ya kukanyaga breki alikanyaga moto na kuzidisha kasi ndipo alipogonga nyumba hii." Alisema shuhuda mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Jumanne Athuman.

TASWIRA ZA KILI MUSIC TOUR NDANI YA DODOMA


Hatimaye ile ziara ya Muziki Tanzania iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu imeanza rasmi leo kwa show baab kubwa katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma. Katika onyesho hilo lililohusisha wasanii waliofanya vizuri mwaka 2012 kwa utangulizi wa waendeshaji wake Dulla na Zembwela kutoka East Africa TV kugawa zawadi kwa mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwa kuendesha mashindano mbali mbali.
Hakuna ubishi kuwa Ben Pol ndiye mfalme wa R&B na alilithibitisha hilo alipoponda jukwaani na kuwaimbisha…
Hatimaye ile ziara ya Muziki Tanzania iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu imeanza rasmi leo kwa show baab kubwa katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma. Katika onyesho hilo lililohusisha wasanii waliofanya vizuri mwaka 2012 kwa utangulizi wa waendeshaji wake Dulla na Zembwela kutoka East Africa TV kugawa zawadi kwa mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwa kuendesha mashindano mbali mbali.
Hakuna ubishi kuwa Ben Pol ndiye mfalme wa R&B na alilithibitisha hilo alipoponda jukwaani na kuwaimbisha mashabiki wake mwanzo hadi mwisho kwa nyimbo zake kali Pete, Jikubali, Samboira huku kivutio kikiwa pale uwanja mzima ulipoimba pamoja nae wimbo wa Nikikupata.
Malkia wa Bongo Flava, Lady Jaydee ambaye ni mwanamke pekee katika wasanii waliokuja Dodoma alithibitisha kwamba habahatishi baada ya kulishambulia jukwaa kwa nyimbo zake zote zililizompa umaarufu. Jide nae kama wasanii wengine alianza kwa kumkumbuka marehemu Albert Mangwea kwa kuimba chorus ya wimbo wa "Sikiliza" ambao ni ushirikiano wake, MwanaFalsafa na Mangwair kisha kuanza kuimba nyimbo zake kali na kumalizia na Joto Hasira alioshirikiana na Profesa Jay aliepanda jukwaani kuungana nae.
Profesa Jay anapenda kuitwa The Heavy Weight MC na alililithibitisha hilo wakati alipokabidhiwa jukumu la kufunga show, kwa zaidi ya nusu "Jay wa Mitulinga" kama anavyojulikana aliwaimbisha mashabiki nyimbo zake kali toka Bongo Dar es Salaam, Chemsha Bongo, Piga Makofi nk. Kivutio kilikuwa pale alipoimba wimbo wake wa zari la mentali na kumpandisha jukwaani moja ya mashabiki kuimba mistari ya "Zubeda" huku akishangiliwa na wengi kabla ya kuendelea kuchana nyimbo zake nyingine zilizompatia umaarufu.
Alipotajwa kuwa zamu yake imefika ulitokea mtafaruku wa mashabiki kusukumana kila mmoja akitaka kuwa mbele ili amuone vizuri, lakini huyu ndiye Mfalme wa Hip Hop kwa mwaka 2012, Kala Jeremiah ambaye alilishambulia jukwaa kwa zaidi ya nusu saa huku akwadatisha maelfu waliojitokeza huku kama kawaida wimbo wake wa Dear God ukionekana kumgusa kila mtu.
Wa kwanza kupanda kwenye steji alikuwa Linex "Mjeda" alieimba nyimbo zake zilizotamba kwenye vituo mbalimbali vya redio na televisheni. Wimbo ulioonekana kuwakonga wengi ulikuwa "Aifola".
Wa pili jukwaani alikuwa ni Ommy Dimpoz aliepanda jukwaani na madansa wake wanaosifika kwa uhodari wao wa kumiliki jukwaa na kuimba nyimbo zake mbili za Baadae na Me and You kabla ya kushuka na kumpisha Ben Pol.
Roma! Roma! Roma! ndio kelele zilizopigwa na mashabiki wakati akipanda jukwaani na kama ilivyo kawaida ilikuwa ni michano mwanzo hadi mwisho. Roma ambaye mwaka jana alishinda tuzo mbili alizidi kuonyesha ubora wake pale alipoimba nyimbo zake kama "Pastor", "Tanzania", "Kidole cha mwisho juu" na "2030" huku akitumia dakika kadhaa kumkumbuka marehemu Albert Mangwair.

CHEKA NAO YAZIDI KUPOKELEWA VIZURI NA WAKAZI WA MBAGALA‏


Baadhi ya watoto wakiwa tayari kushindana katika mbio za Vodacom Cheka Nao zilizofanyika Dar Live, Mbagala siku ya kifamilia iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya Promosheni ya Cheka Nao inayowawezesha wateja kupiga simu kwa bei nafuu kwenda mitandao yote nchini na kujishindia shilingi milioni 2 kila mmoja kwa mwezi, ili kujiunga na kufaidika na ofa  piga…
Baadhi ya watoto wakiwa tayari kushindana katika mbio za Vodacom Cheka Nao zilizofanyika Dar Live, Mbagala siku ya kifamilia iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya Promosheni ya Cheka Nao inayowawezesha wateja kupiga simu kwa bei nafuu kwenda mitandao yote nchini na kujishindia shilingi milioni 2 kila mmoja kwa mwezi, ili kujiunga na kufaidika na ofa  piga *149*01#.
Ofisa wa Voacom Tanzania Alfani Mdachi (katikati) akimwandikisha Mustafa Mustafa mkazi wa Mbagala ili kumpatia kadi ya simu tayari kwa matumizi halali, zoezi hilo lilifanyika wakati wa kampeni ya Cheka Nao inayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kupiga simu kwa bei nafuu kwenda mitandao yote nchini na kujishindia shilingi milioni 2 kwa mwezi, ili kujiunga na kufaidika nayo piga *149*01#. Anaeshuhudia ni Meneja wa kanda ya Mbagala, Idd Mawe.
Ofisa wa Vodacom Tanzania, Bi. Rehema William (aliyeketi) akimwelezea jambo mkazi wa Mbagala Dar es Salaam, wakati Promosheni ya Cheka Nao iliyofanyika Mbagala hapo jana inayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kupiga simu kwa bei nafuu kwa mitandao yote nchini na kujishindia shilingi milioni 2 kwa mwezi, ili kujiunga na kufaidika nayo piga *149*01#.
Bi.Tumu Said ambaye ni mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam akimsikiliza Ofisa wa Vodacom Tanzania jinsi anavyomfafanulia faida za kujiunga na Promosheni ya Cheka Nao inayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kupiga simu kwa bei nafuu kwa mitandao yote nchini na kujishindia shilingi milioni 2 kwa mwezi, ili kujiunga na kufaidika nayo piga *149*01#. Wanaoshuhudia kushoto ni Meneja wa kanda ya Mbagala, Idd Mawe na kulia ni Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo, Bw. Matina Nkurlu.
Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bw. Matina Nkurlu (kulia) akimwelezea Bi.Tumu Said ambaye ni mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam manufaa na faida za kujiunga na Promosheni ya Cheka Nao inayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kupiga simu kwa bei nafuu kwenda mtandao wowote na kujishindia shilingi milioni 2 kwa mwezi, ili kujiunga na kufaidika nayo piga *149*01#.

"TUNAJIANDAA KUIPINDUA NCHI ENDAPO SERIKALI HAITAWASHUGHULIKIA WATU WALIOFICHA MABILIONI USWISWI"...ZITTO KABWE


Zitto  Kabwe  amefunguka  na  kudai  kuwa  kwa  sasa  wanajiandaa  kufanya  mapinduzi  ya  nchi  endapo   watu  walioficha    mabilioni  uswiswi    hawatashughulikiwa  ipasavyo....

Suala la baadhi ya Watanzania kuhifadhi mabilioni ya fedha nchini Uswisi limechukua sura mpya, baada ya tume maalumu kuwahoji vigogo 200 wakiwamo wabunge, wanasiasa na wafanyabiashara.
  
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa tume hiyo inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema tayari imeshafanya kazi hiyo kwa miezi miwili sasa.
 
Tume hiyo maalumu iliyoundwa na Serikali kwa Azimio la Bunge lililotolewa mwishoni mwa mwaka jana, inatarajiwa kukamilisha uchunguzi huo wakati wowote kuanzia sasa na kuwasilisha ripoti hiyo katika kikao kijacho cha Bunge.

Zitto  Kabwe  anatoa  angalizo  katika  hatua  hiyo  ya jaji Werema   kwa  kusema  kuwa  hatua  hii  isiwe  "zima  moto"   na  daganya  toto  ili  kuwafumba  macho  watanzania...

Ubabaishaji  wowote  kwa  mujibu  wa  Zitto  Kabwe  utasababisha  mapinduzi  ya  nchi.....

Hii  ni  post  yake  aliyoweka  katika  mtandao  wa  twitter

OMMY DIMPOZ APIGWA CHUPA NA MASHABIKI AKIWA JUKWAANI HUKO DODOMA

Kuna tetesi kuwa Ommy dimpoz amepigwa mawe jukwaaani dodoma na kushindwa kufanya show ya kilimanjaro music award dodoma. 
Wadau toka  Dodoma wasema  msanii yoyote atakaye mdiss msanii wa dodoma hawatamruhusu kufanya show Dodoma  na watamshusha jukwaani kama walivyo fanya leo  kwa  Ommy

Tunafuatilia  undani  wa  habari  hii

Saturday, June 22, 2013

MCHUNGAJI AZAA NA HAUSIGE

Stori:Gladness Mallya na Harun Sanchawa
HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.

Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.…
Stori:Gladness Mallya na Harun Sanchawa
HAYA ni madai mazito! Mchungaji wa Kanisa la Kiroho la Kijito cha Utakaso au Healing Centre International lililopo Kimara-Mwisho, Dar, Thomas Mariki anadaiwa kuvuliwa kofia ya uchungaji baada ya kutuhumiwa kuzaa na ‘hausigeli’ wake, Sessy Mwambashi.

Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa masikitiko, mke wa ndoa wa Mariki, Joyce Thomas Mariki alidai kuwa yeye na mchungaji huyo walioana mwaka 2004 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Lungai Mwika, Moshi.
Alisema walijaliwa kupata watoto watatu lakini mmoja hakuwa bahati.
MATESO YAANZA
Mwanamke huyo alidai amani katika ndoa yake ilipotea baada ya kujifungua mtoto wa pili (marehemu), mumewe alianza kumtuhumu kuwa alitoka nje ya ndoa na huyo mtoto hakuwa wake.
Aliendelea kudai kuwa, mtoto alipofikisha mwaka mmoja na miezi nane, walishauriana watafute hausigeli ili mama huyo afanye biashara ya kuwaongezea kipato.
Mama mchungaji alisema alimpata Sessy akiwa na miaka 15, mkazi wa Mbozi, Mkoa wa Mbeya.
Alisema yeye alianza biashara ya genge maeneo ya Kimara-Mwisho ambapo alikuwa akiwahi sokoni saa 11:00 alfajiri na kumwacha msichana huyo akiendelea na kazi za nyumbani.

VISA VYAANZA
Mama mchungaji aliendelea kudai: Baada ya miezi michache, mchungaji alibadilika tabia, alikuwa mkali, wakati mwingine alinifuata sokoni na kunipiga akinishutumu nina uhusiano na wanaume ndiyo maana nachelewa kurudi nyumbani.

MUMEWE AMFICHULIA SIRI
Akadai: “Siku moja mchungaji alinifichulia siri kuwa hausigeli wetu ni mjamzito na mimba ilikuwa yake hivyo akataka iwe siri kati yetu watatu.”
Mama Mariki alisema alikubaliana na mumewe ambapo alivumilia kwa kipindi kirefu lakini uzalendo ulimshinda baada ya msichana huyo kuwa na tabia ya kuwatesa watoto huku akisema aachwe kwani ni mjamzito.

MKE NAYE AFICHUA SIRI
Alisema kuwa baada ya kuona mumewe anamjali zaidi hausigeli kuliko yeye na watoto aliamua kwenda kutoa siri kwa wasimamizi wa ndoa, wakaitwa na kusuluhishwa ambapo waliamua kuwa msichana huyo arudishwe nyumbani kwao Mbeya jambo ambalo mtumishi huyo wa Mungu alilitekeleza, yeye mwenyewe alimrudisha msichana huyo kwao.

NDOA YATIBUKA
Mwanamke huyo alidai mumewe huyo aliporudi Dar, alianza visa akisema kuwa hausigeli alikuwa akimpa ‘mambo’ kuliko yeye ambaye amezeeka huku vitisho na vipigo vikiongezeka maradufu!
“Wasimamizi wa ndoa walituita kwa mara nyingine wakatusuluhisha lakini tulipofika nyumbani, mateso yakawa palepale ndipo wasimamizi waliponiambia nirudi kwa wazazi wangu kwani ni aibu kubwa kwa mtumishi wa Mungu kufanya vile,” alisema na kuongeza:
“Kweli nilirudi kwetu Moshi, wazazi wangu walimpigia simu mume wangu kuhusu matatizo yetu, lakini aliwajibu hanitaki na ataniletea talaka nyumbani.”
Alisema miezi mitatu baadaye, wasimamizi wa ndoa walimtaka arudi Dar kwa ajili ya kujua hatima ya ndoa yake.
Aliambatana na kaka yake hadi nyumbani kwa mumewe, cha ajabu walimkuta hausigeli akiwa na mtoto mchanga. Aliwazuia kuingia ndani akidai hawakuwa na mamlaka hayo.
Alisema kaka yake alimtaka hausigeli ampigie simu mchungaji amwambie shemeji yake anamhitaji, alifanya hivyo na mchungaji alifika lakini alipowaona alitoka nduki.

WAZEE WA KANISA WAINGILIA KATI
Aliendelea kudai kuwa ulifika wakati wazee wa kanisa waliingilia kati, wakamuweka mchungaji kikao na kumuuliza kulikoni hawamuoni mke nyumbani badala yake  msichana wa kazi tena akiwa na kichanga.
“Cha kushangaza mchungaji alipandwa na hasira, akawafanyia fujo wazee hao, alimpiga na kiti mzee mmoja ambaye alikuwa msaidizi wake anayeitwa Kisaka na kumjeruhi,” alisema mama mchungaji.
Alisema sakata la kujeruhiwa kwa Kisaka liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Mbezi Kwayusuf na kufunguliwa jalada namba KMR/RB/2125/2013- SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI.

AVULIWA UCHUNGAJI
Alisema katika kikao hicho, wazee hao walifikia uamuzi wa kumvua rasmi uchungaji kwa kumwandikia barua na kumkabidhi.
Mchungaji aliipokea barua hiyo lakini hadi sasa anaendelea na huduma kwani wapo waumini wachache walio upande wake huku wengine wakidaiwa kulikimbia kanisa hilo.

BOFYA HAPA UMSIKIE MCHUNGAJI
Baada ya kuzinyaka habari hizo, Juni 18, mwaka huu, mapaparazi wetu walimtafuta Mchungaji Mariki na kufanikiwa kumkuta nyumbani kwake Kimara-Mwisho ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Siwezi kuzungumzia lolote kuhusu habari alizosema mke wangu kwa sababu suala hili lipo kwenye Baraza la Usuluhishi wa Ndoa na lipo kwa maandishi, naweza kuwaambia kuwa kuna watu wanataka kunipindua, wanapanga hila na njama ili walichukue kanisa na ndiyo wanamtumia mke wangu lakini hawawezi, wameshindwa.
“Kuhusu kuzaa na hausigeli wangu ni kweli na mtoto ana miezi saba sasa, lakini hizo shutuma kwamba alikuwa na miaka 15 siyo kweli, alikuwa na miaka 17 na sasa ana miaka hiyohiyo.”

HAUSIGELI VIPI?
Risasi Jumamosi lilizungumza pia na hausigeli ambaye anaishi na mchungaji huyo kwa sasa kama mke ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Anayesema nilikuwa na miaka 15 ana ushahidi? Wanaoweza kujua umri wangu ni wazazi wangu na ukweli ni kwamba mwezi wa kumi mwaka huu natimiza miaka kumi na nane.
“Kuhusu kwamba nilikuja kufanya nini Dar, nilikuja kwa mume wangu mwenye ushahidi kuwa nilimfukukuza mke wake alipokuja nyumbani aniletee.”
Hata hivyo, Risasi Jumamosi linaendelea kufuatilia sakata hili ili kukujuza nini hatima yake.

SHOW YA MIAKA 13 YA KIKOSI CHA MIZINGA JANA VIWANJA VYA MSASANI CLUB DAR

Mashabiki wakiwa mzukaa mbaya
Chidi Benz akifanaya yake
Ilikuwa aibu Babu…
Mashabiki wakiwa mzukaa mbaya
Chidi Benz akifanaya yake
Ilikuwa aibu Babu
hayaaaa
afande Sele akikinukisha kwa hisia stegini
Mashabiki waki enjoy show ya miaka 13 ya kikosi cha mizinga
Songa akiwa kwa steji akifanya yake
Kalapina akifanya mambo kwenye stegi
Tabla akifanya yake kwa steji            Mashuati kwenye stage wakionyesha ujuzi wa karate raha kwelii                       Haya sasa Man 2 Man Battle nichane nikupasue                             Ohhh usiogope jamaa hapigwiiii ila ni mizuka ya battle man 2 man
Kundi la Kiokosi cha Mizinga limefanya show ya kutimiza miaka 13 tangu lianzishwe
Show hiyo iliyo hudhuliwa na mashabiki kibao wa hip hop wa Jijini Dar es salaam.
Onyesho hilo lilifanyika usiku wa kuamkia leo na kuhudhuliwa na wasanii wa muda mrefu sana waliopotea katika mziki huo wakiwemo Member wa Kundi la Wateule,Mark 2 Be aka Simba wa kundi la Big Dogg Poz