This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, April 2, 2013

VODACOM FOUNDATION YASAIDIA UJENZI WA KITUO CHA AFYA PEMBA

Mkuu wa Mfuko wa Vodacom wa Kusaidia Jamii - (Vodacom Foundation), Yessaya Mwakifulefule, akikabdhi kwa mmoja wa wazee wa Shehia ya Michenzani Mkoa wa Kusini Pemba mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. milioni 30. Fedha hizo zimetolewa kumalizia ujenzi wa jengo la kituo cha afya cha Michenzani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya katika eneo hilo. Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa (wa pili kulia) na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim wakishuhudia.…
Mkuu wa Mfuko wa Vodacom wa Kusaidia Jamii - (Vodacom Foundation), Yessaya Mwakifulefule, akikabdhi kwa mmoja wa wazee wa Shehia ya Michenzani Mkoa wa Kusini Pemba mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. milioni 30. Fedha hizo zimetolewa kumalizia ujenzi wa jengo la kituo cha afya cha Michenzani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya katika eneo hilo. Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa (wa pili kulia) na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim wakishuhudia.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa akielezea kwa  Mkuu wa Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule na Meneja Uhusiano wa Nje wa Kampuni ya Vodacom, Salum Mwalim (mwenye fulana nyekundu) ujenzi wa jengo jipya la kituo cha Afya cha Michenzani Mkoa wa Kusini Pemba muda mfupi kabla ya Vodacom Foundation kukabidhi hundi yenye thamani ya Sh. milioni  30 kumalizia ujenzi wa jengo hilo.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa, akiongoza kikundi cha ngoma ya kibati kutoka Chokochoko Mkoa wa Kusini Pemba kucheza ngoma hiyo wakati wa hafla ya kupokea hundi yenye thamani ya Sh. milioni  30 kumalizia ujenzi wa kituo cha Afya cha Michenzani Kisiwani humo zilizotolewa na Mfuko wa Vodacom wa kusaidia Jamii - (Vodacom Foundation). Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mfuko huo, Yessaya Mwakifulefule akifurahia burudani hiyo.
---
WAKAZI wa Shehia ya Michenzani, Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba na maneo ya jirani sasa wana kila sababu ya kuwa na uhakika wa huduma za afya kwa ukaribu zaidi kufuatia msaada wa Sh 30 Milioni uliotolewa na kampuni ya Vodacom kupitia mfuko wake wa kusaidia Jamii – Vodacom Foundation kwa ajili ya kuamlizia ujenzi wa jengo jipya la kituo hicho.
Jengo hilo ambalo kwa sasa lipo katika hatua ya linta linajengwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Tenknolojia Profesa Makame Mbarawa akishirikiana na nguvu za wananchi.
Kutolewa kwa fedha hizo ambazo zitanunulia vifaa vya ujenzi vinavyohitajika kwa ajili ya kazi ya kuezeka pamoja na vifaa vingine vya kumalizia ujenzi ni matokeo ya juhudi za makusudi za mfuko huo za kusaidia miradi ya kijamii yenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa wananchi hapa nchini.
Akikabidhi mfano wa hundi kwa wakazi wa Mkanyageni katika hafla iliyoongozwa na Waziri Profesa Mbarawa, Mkuu wa Mfuko huo Yessaya Mwakifulefule amesema Vodacom Foundation imekuwa na dhamira ya dhati ya kusaidia maisha ya watanzania mijini na vijijini ili kuboresha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya na uwezeshaji wanawake  kiuchumi.
“Tunajisikia furaha sana leo kuona Vodacom Foundation ipo hapa Michenzani kuendeleza azma yake ya kuunga mkono juhudi za maendeleo, tutachangia fedha ambazo zitatumika kununulia vifaa vya ujenzi kumalizia ujenzi wa kituo cha afya katika eno hilli.”Alisema Mwakifulefule.
Hata hivyo Mwakifulefule aliwapongeza wakazi wa Shehia ya Michenzani na jimbo zima la Mkanyageni hususan vijana kwa namna wanavyojitolea kushiriki katika miradi ya maendeleo jambo ambalo amesema huenda limechangia kwa kiasi kikubwa kumpa nguvu Waziri Prof;Mbarawa ambae ni mweneyeji  wa eneo hilo kusaidia maendeleo.
“Nimezunguka sehemu mbalimbali hapa nchini hamasa na ari niliyoiona hapa ni ya kipekee jinsi ambavyo wananchi mnavyojitolea katika miradi ya maendeleo hili ni jambo zuri na linawapa moyo wahisani wa maendeleo.”Alisema Mwakifulefuke na kuongeza. “Na sisi katika fedha tutakazozitoa kumalizia ujenzi zinahusisha fedha za kulipia gharama za mafundi na vibarua mbao ni miongoni mwenu. Kwa namna hiyo tunaamini kuwa tutakuwa pia tunaimarisha hali ya uchumi wa vijana wa eneo hili.”
Kwa upande wake Waziri Profesa Mbarawa ameishukuru Vodacom Foundation kwa kukubali kusaidia kumalizia ujenzi wa kituo hicho,
“Nawashukuru Vodacom Foundation kwa kuja hapa na kusaidia maendeleo yetu ila nataka niwaambie wananchi kwamba haya yote hayaji tu hivihivi bali hutafutwa.”   Alisema Profesa Mbarawa
Waziri huyo wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  aliwashukuru vijana na wakazi wa Mkanyageni kwa jinsi wanavyojitoa na kuwaeleza kuwa hiyo ni silaha muhimu ya maendeleo hivyo waupeke kudanganywa na badala yake waangalie namna gani ya kuleta maendeleo na kiwanga mkono wale wanaowaletea maendeleo badala ya kukubalia hila za kuwabeza.
Vodacom Foundation imekuwa ikichangia miradi mbalimbali ya maendeleo Zanzibar ambapo pia hivi karibuni imeahidi kutoa boti mbili za uvuvi kwa vikundi vya vijana Pemba na Unguja kusaidia juhudi za serikali ya Zanzibar za kutengeza ajira kwa vijana.
Mbali na mchango huo, Mwishoni mwa mwaka jana, Vodacom Foundation ilisaidia wanawake wajasiriamali zaidi ya 300 kwa kuwaptia mikopo nafuu isiyo na riba wala dhamana yenye thamani ya zaidi ya Sh. 27 Milioni katika kisiwa cha Unguja pamoja na kuahidi kuchangia Sh 15 Milioni kwenye mfuko wa maendeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar.

TASWIRA MBALIMBALI ZA MAKAMUZI YA TMK FAMILY NA TMK HALISI NDANI YA DAR LIVE


Bi. Cheka akikamua sambamba na Mhe. Temba.
Mhe. Temba akiwapa hi fans wake.
Juma Kassim Nature 'Kiroboto' nae akisema na wanae.
Mashabiki wakiwa wamekolea na shoo za Dar Live.
TMK Halisi mzigoni.
TMK Family wakilishambulia jukwaa.
Juma Nature 'Sir Nature' akiwapagawisha mashabiki wake.
Profesa J akiwapa raha mashabiki.
Inspekta Haroun wa Gangwe Mob naye alikuwepo kutoa burudani.
Malkia wa mipasho nchini, Khadija Kopa, akiwapa raha mashabiki.
Chegge kutoka TMK Family akionyesha cheche zake.
KR Mullar wa TMK Halisi akimwaga nyuki.
...Mapanga shaaa...
...Ilikuwa ni full burudani ndani ya viunga vya Dar Live.
DJ JD akimtangaza Juma Nature kuwa ndiye kinara wa Temeke.
...Mikono juuuu kwa Sir Nature!

UKWELI KAMILI NI HUU

Na Waandishi Wetu

JENGO lenye urefu wa ghorofa 16, lililoanguka katikati ya Jiji la Dar es Salaam na kusababisha vifo, ulemavu wa watu pamoja na uharibifu wa mali, lilikuwa lazima lianguke.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mke wake Mama Salma Kikwete wakiwa katika wodi ya Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam wakimpa pole kijana  Mohamed Ally Dhamji ambaye ni miongoni mwa  majeruhi walionusurika katika jengo lililoporomoka katikati ya jiji Ijumaa iliyopita na kusababisha vifo vya watu 34. (PICHA NA…

Tathmini iliyoratibiwa kisayansi na timu ya waandishi wetu, ikihusisha baadhi ya wataalamu wa majengo, inaonesha kwamba aina ya ujenzi wa jengo hilo, ulikuwa haukidhi hata kwa ghorofa tano.
Jengo lililopo jirani na lile lililoporomoka.
Machi 29, mwaka huu (Ijumaa iliyopita), jengo hilo, lililopo kwenye makutano ya Barabara ya Morogoro na Mtaa wa Indira Ghandhi, lilianguka na kuibua wasiwasi mkubwa.
Kwa mujibu wa mhandisi wa majengo, Abel Kadali, anayemiliki kampuni yake, akiwa ni msomi mwenye shahada mbili, ujenzi wa jengo hilo, ulizungukwa na utani mwingi.
“Kwanza jengo refu kama lile linapokatika na kubomoka kisha eneo kugeuka kifusi kama hivi, maana yake ujenzi ulikuwa dhaifu kuanzia mwanzo hadi mwisho.
“Kama ujenzi ungekuwa mzuri, hili jengo hata kama lingeanguka, lisingesambaratika kama hivi. Hapa kuna kasoro za kiweledi. Ujenzi wa namna hii, huwa unatufanya tuonekane hatuwezi kazi,” alisema.

Wananchi wakiondoa kifusi eneo la ajali.
KASORO KATIKA SARUJI
Macho ya waandishi wetu yaliona lakini Kadali akafafanua kwamba ni kosa kubwa kujenga ghorofa, halafu ukabana saruji.
“Nikishika tofali, naona ni mchanga mtupu. Kwa kadirio la kitaalamu, inaonekana kila mfuko mmoja  wa saruji, ulitengeneza matofali 90. Maana ni mchanga mtupu.
“Kwa hiyo kosa la kwanza kabisa ninaloweza kuliona hapa ni matumizi ya saruji,” alisema Kadali.

NONDO DHAIFU
Kadali alifafanua kuwa nondo zilizotumika siyo za kujengea ghorofa lenye urefu huo.
“Nikiziangalia hizi nondo, naona kabisa hili jengo lilijengwa chini ya kiwango kuanzia kwenye msingi wake mpaka hapo lilipofikia na kuanguka. Sasa ni kwa nini lisianguke?
“Tunacheza na maisha ya watu. Nondo ni nyembamba sana, nikiziangalia, zinaonesha kuwa pamoja na wembamba wake, hazina ubora,” alisema Kadali.

TATIZO LA MALIGHAFI
Kuhusu ubora wa nondo, Kadali alisema kuwa inashangaza kuona zikikunjwa zinakatika.
“Hili ni tatizo la malighafi, lazima ukaguzi wa kina ufanyike kwenye viwanda vyetu, kuona ubora wa bidhaa zinazotengenezwa.
“Ni kweli nondo ni nyembamba lakini ukweli usipindishwe kuwa hata ubora wenyewe haupo. Ina maana zilitengenezwa kwa malighafi zisizokidhi viwango.
“Viwanda vyetu vinaunda nondo kwa kuyeyusha vyuma chakavu. Ni kosa kubwa. Wakati mwingine inakuwa siyo vyuma peke yake, bali ni mchanganyiko na ‘Alminiamu’,” alisema Kadali na kuongeza:
“Kama nondo inatengenezwa kwa kuchanganya chuma na Alminiamu, unatarajia kweli kupata nondo imara? Ifahamike kwamba kila madini na kazi yake.”

KOSA LA TBS
Kadali alisema kuwa kiwango dhaifu cha nondo na bidhaa mbalimbali nchini, ni matokeo ya Shirika la Viwango Tanzania  (TBS) kutofanya kazi zake ipasavyo.
“Kuruhusu nondo kama zile kuingia sokoni na kuuzwa kwa ajili ya ujenzi, ni tatizo. TBS lazima wasimame imara kuhakikisha wanafanya kazi yao kisheria, hivyo kuokoa maisha ya Watanzania,” alisema Kadali.

KOSA LA NHC
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), nalo limeingia lawamani kwa sababu kisheria, lenyewe lina haki katika umiliki wa jengo hilo lililoanguka.
NHC, linamiliki asilimia 25 ya hisa za jengo hilo, hivyo kitendo cha kuacha ujenzi holela, siyo tu kwamba limeshindwa kutimiza wajibu wake, bali pia linachezea rasilimali za Watanzania.

MAITI ZAFIKIA 34
Mpaka gazeti hili linaingia mtamboni, maiti zilizokuwa zimepatikana ni 30 na jitihada za kuendelea kusaka maiti zaidi zilikuwa zinaendelea.
Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema: “Uokoaji bado unaendelea, vyombo vyote vya dola vipo, pamoja na zana zote.”

WANANE WAKAMATWA
Kova alisema: “Mpaka sasa, polisi kanda maalum imeshawakamata watu wanane kuhusiana na kuanguka kwa ghorofa hilo.
“Waliokamatwa ndiyo waliohusika moja kwa moja, kuanzia michoro mpaka ujenzi. Kwa sasa nisingependa kuwataja majina kwa sababu uchunguzi unaendelea,” alisema Kova.
Kwa upande mwingine, Kova alisema: “Kipindi hiki tunaendelea na uokoaji, hatutarajii kupata majeruhi. Tunachofanya ni kuhakikisha tunapata maiti wote ili waweze kuzikwa kwa heshima zote kama binadamu.”

KUHUSU JENGO PACHA
Habari zinasema kuwa jengo hilo lililoanguka, lilikuwa na pacha wake, jirani kabisa na ilipo Hospitali ya Burhani. Kova amesema kuwa ujenzi wake umesimamishwa mara moja.
“Tuligundua kuwa mmiliki na mjenzi ni yuleyule, kwa hiyo tumechukua hatua za haraka sana kuzuia shughuli zote za ujenzi wa jengo hilo pacha,” alisema Kova.
Na Waandishi Wetu
JENGO lenye urefu wa ghorofa 16, lililoanguka katikati ya Jiji la Dar es Salaam na kusababisha vifo, ulemavu wa watu pamoja na uharibifu wa mali, lilikuwa lazima lianguke.

KIJIJI CHA MISUKULE CHAFUMULIWA


INATISHA na hofu kubwa imetanda katika Kijiji cha Kimange, Wilaya ya Bagamoyo  mkoani Pwani kufuatia baadhi ya viongozi  wa dini kuwatumia vijana wa hapo kama misukule ili wapelekwe kanisani.

Msukule.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa nia ya viongozi hao wa dini kuteua kijiji hicho na kuwatumia vijana wa hapo kama misukule ni kuwalaghai waumini kwamba wana uwezo wa kufufua watu wanaodaiwa kufa na kuchukuliwa kimazingara.

Gazeti hili limebaini kuwa viongozi hao wa dini wamekuwa wakifanya udanganyifu huo lengo lao likiwa ni kupata waumini wengi katika makanisa yao ambao wamekuwa wakiamini kwamba kweli misukule inarejeshwa katika maisha…
Na Makongoro Oging', Bagamoyo
INATISHA na hofu kubwa imetanda katika Kijiji cha Kimange, Wilaya ya Bagamoyo  mkoani Pwani kufuatia baadhi ya viongozi  wa dini kuwatumia vijana wa hapo kama misukule ili wapelekwe kanisani.

Msukule.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa nia ya viongozi hao wa dini kuteua kijiji hicho na kuwatumia vijana wa hapo kama misukule ni kuwalaghai waumini kwamba wana uwezo wa kufufua watu wanaodaiwa kufa na kuchukuliwa kimazingara.
Gazeti hili limebaini kuwa viongozi hao wa dini wamekuwa wakifanya udanganyifu huo lengo lao likiwa ni kupata waumini wengi katika makanisa yao ambao wamekuwa wakiamini kwamba kweli misukule inarejeshwa katika maisha ya kawaida.
Habari kutoka kijijini hapo zinadai kwamba viongozi wa dini wanaofika katika kijiji hicho wamekuwa wakiwalipa watu wanaojitokeza kuwa misukule bandia kati ya shilingi 200,000  hadi 250,000  kwa kila mtu.
Msukule.
Imegundulika kuwa viongozi hao wa dini  hufanya zoezi hilo kwa siri kubwa na kuna  nyumba ya mchungaji mmoja, nje kidogo ya kijiji hicho ambapo misukule hao feki  hupewa mafunzo ya nini cha kufanya kabla ya kusafirishwa kuelekea Dar es Saalam.
Imeelezwa kuwa misukule husafirishwa kwenye magari yenye vioo vyeusi ‘tinted’ wakiwa wamepakwa matope mwili mzima  na kuvalishwa nguo zilizochanika.
“Wapo wachungaji waliofanya hivyo kwa kuwalaghai waumini wao kwamba wana uwezo wa kufufua watu huku wakijua kwamba lengo lao ni kuwavutia watu wajazane kwenye makanisa yao ili wapate  sadaka nyingi,” kilisema chanzo chetu.
 Uchunguzi  umebaini  kwamba  kuna makanisa  ambayo  yana wafuasi wengi wa kufanya mazingaombwe ya namna hiyo na wamekuwa wakijipatia fedha nyingi ambapo kwa Jumapili moja, hujikusanyia kati ya shilingi 7,000,000 hadi 7,500,000.
Aidha, ‘hukomba’ sadaka wakati wa maombi ya katikati ya wiki kwa kutumia mbinu mbalimbali za kuvuta waumini.
Baadhi ya vijana wa kijiji hicho ambao  waliwahi kurubuniwa na wachungaji baada ya kufuatwa kijijini hapo ni pamoja na Ziada Mlanga (33) na Shakila Ayubu (29).
Katika  mahojiano  na mwandishi wetu kijijini hapo, Ziada alikuwa na haya ya kusema:
“Machi 21, 2011 kaka mmoja (jina tunalihifadhi) anayeishi Kijiji cha Makore jirani na chetu, alinifuata na kunieleza kwamba anahitaji vijana wanne, wa kike  wawili na wa kiume wawili ili wajiunge katika shughuli za sanaa, yaani kuigiza.
“Hata hivyo, alifanikiwa kunipata mimi na Shakila, akatuahidi kutulipa shilingi 350,000 kila mmoja na wazazi wetu kupewa shilingi 100,000 kila mmoja.
“Tulikubali  kufanya hivyo, walituchukua kwa pikipiki hadi Kijiji cha Makore  nyumbani kwa mtu mmoja aliyemtaja kuwa ni mchungaji.
“Tulipofika huko walituweka katika chumba maalum katika nyumba ya huyo mchungaji  ambayo ipo porini, wakatueleza kwamba  tusubiri kuna watu wanakuja kutupa  mafunzo.
“Baada ya muda mfupi walifika watu ambao tulipoongea nao, walitueleza tuvue nguo zote tubaki na za ndani. Tulifanya hivyo, wakatupaka majivu, wakatuvuruga nywele  na kutuvalisha nguo chakavu na ilipofika saa moja usiku, walikuja watu wengine wakiwa kwenye gari yenye vioo vya tinted.
“Walitueleza kwamba tunaelekea jijini Dar es Salaam ambako tukifika tujifanye mazezeta. Tulifika usiku sana na kupelekwa katika kanisa moja (jina linahifadhiwa).
“Ndani ya gari lile kulikuwa na bastola, hatukujua ni ya nini, pale kanisani tulitengenezewa chai. Hata hivyo, tulikataa  kuinywa.
“Baadaye walitueleza kwamba wametufanya vile ili tuonekane kama watu  waliokuwa wamechukuliwa kimazingara na kufanywa misukule na sasa tumeokolewa na mchungaji wa kanisa hilo.
“Kesho yake ilikuwa Jumapili, tuliambiwa tutasimama mbele ya waumini kanisani na tusiseme kitu chochote ili tuje kuanza kuongea kidogo baada ya kuombewa na mchungaji.
 “Hata hivyo, tulipewa majina ya watu mashuhuri waliokufa lakini mimi nilikataa kwa kuwa aliyetajwa kuwa nijifanye ndiyo mimi alikuwa mtu maarufu.
 “Nilijiuliza ndugu zake wangenielewaje? Kitu cha pili ni kwamba nilikataa kwa kuwa fedha tulizokubaliana walikuwa hawajatupatia na tukaona kuwa huo ni udhalilishaji.
“Baada ya kuona tumekataa, walitusihi  tusitoe siri na baadaye tulipewa nguo  nyingine tukavaa na tukapewa shilingi elfu hamsini kila mmoja kama nauli ya kurudia kijijini kwetu Kimange.
“Tulipofika tuliwaeleza wazazi wetu  mambo tuliyofanyiwa wakaona tumedhalilishwa, ikabidi tuje nao Dar es Salaam  tukaenda hadi Kituo cha Polisi  Magomeni na kufungua  kesi.
  “Tuliwaambia polisi kuwa simu na nguo zetu ziko kwa watu hao lakini hadi leo kesi tuliyofungua hatujui ilipofikia na tuliambiwa polisi wamewasiliana na wenzao wa Mkoa wa Pwani.
“Polisi wa Pwani walikuja Dar na kutuchukua hadi Kibaha ambako tulitoa maelezo na tukaenda nao Kijiji cha Makore lakini  hatukumkuta mchungaji huyo, tukaambiwa kuwa alihama baada ya kupata habari kuwa anatafutwa na polisi,” alisema Ziada akiungwa mkono na Shakila.

BABA  WA  ZIADA
Baba wa Ziada aliyejitambulisha kwa jina la Sijali Musini Mlanga, alisema kwamba kitendo walichofanyiwa watoto hao ni cha udhalilishaji na anaiomba serikali kuchukua hatua.
“Hatuwezi kukubaliana na hali hiyo, huo ni utapeli na udhalilishaji mkubwa, hakuna dini  inayoweza kufanya mambo kama hayo, wahusika wachukuliwe hatua,” alisema Mlanga.

MWENYEKITI  WA  KIJIJI
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kimange, Juma Issa  Madinga amekiri kufahamu suala hilo na kukemea kitendo hicho.
“Hao wachungaji hawawezi kuachwa wakifanya mambo hayo na kusababisha kijiji kupakaziwa kuwa ni cha misukule, sasa wananchi wasilaghaiwe na matapeli hao, wakija tena watoe taarifa kwangu,” alisema  mwenyekiti huyo.