This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, August 29, 2013

TRAFIKI FEKI MAZITO TENA!





MAZITO tena yameibuka kuhusu yule trafiki feki James Hussein, mkazi wa Kimara Matangini, jijini Dar es Salaam ambaye yuko  Gereza la Segerea, Dar akikabiliwa na kesi ya kujifanya askari wa usalama barabarani, Amani lina mpya hiyo.
Trafiki feki James Hussein akiwa kwenye gari baada ya kunaswa.
Habari za ndani kutoka Gereza la Isanga, Dodoma zinadai kuwa, trafiki huyo ana mambo mengi ya kushangaza ambayo Watanzania wengi hawayajui.
JINA HALISI

Mtoa habari wetu alisema kuwa,…
Na Mwandishi Wetu
MAZITO tena yameibuka kuhusu yule trafiki feki James Hussein, mkazi wa Kimara Matangini, jijini Dar es Salaam ambaye yuko  Gereza la Segerea, Dar akikabiliwa na kesi ya kujifanya askari wa usalama barabarani, Amani lina mpya hiyo.
Trafiki feki James Hussein akiwa kwenye gari baada ya kunaswa.
Habari za ndani kutoka Gereza la Isanga, Dodoma zinadai kuwa, trafiki huyo ana mambo mengi ya kushangaza ambayo Watanzania wengi hawayajui.
JINA HALISI
Mtoa habari wetu alisema kuwa, James Hussein si jina halisi la trafiki feki huyo. Alisema jina lake halisi ni Ali Kinanda.
...Mtuhumiwa huyo akiwa na watuhumiwa wenzake.
“Yule jamaa anaitwa Ali Kinanda, sisi kumwona kwenye picha gazetini akijiita James Hussein tulishangaa sana,” kilisema chanzo chetu.
YADAIWA ALIKUWA ASKARI MAGEREZA
Chanzo kikazidi kudai kwamba, kuanzia mwaka 1984 jamaa huyo alikuwa ni askari magereza katika Gereza la Butimba, Mwanza hadi mwaka 1987 alipoacha.

...Akiwa mikononi mwa polisi.
ADAIWA KUNASWA UJAMBAZI, ATUPWA JELA MIAKA 30
Mtoa habari wetu aliendelea kumwanika trafiki feki huyo kuwa, mwaka 2002 mtuhumiwa huyo alidaiwa kupata msala wa tukio la ujambazi lililotokea Mpwapwa, Dodoma ambapo kesi yake iliunguruma hadi mwaka 2003 ambapo hukumu ilitolewa yeye na wenzake kwenda jela miaka 30.
 “Mwaka 2002 mpaka 2003, Kinanda alipata kesi ya ujambazi akiwa na wenzake, sikumbuki idadi yao. Kesi iliisha kwa hukumu ya miaka 30 jela kwenye Gereza la Isanga hapa Dodoma,” alisema mnyetishaji huyo.
“Akiwa gerezani, Kinanda alionekana mtiifu kiasi kwamba alipewa cheo cha kusimamia wenzake, yaani mnyapara wakiamini anaendelea vizuri na kifungo chake hicho.
Trafiki feki katika pozi baada ya kudakwa.
“Hakuna aliyejua kama jamaa anaweza kutoroka. Ama kweli moyo wa mtu anaujua mwenyewe. Hivi hapa (Gereza la Isanga) wafungwa wenzake wameshangaa kusikia jamaa amekuwa trafiki huko Dar es Salaam,” kilidai chanzo.
ADAIWA KUTOROKA JELA
Habari zaidi ziliendelea kudai kwamba, Desemba 10, 2012 akiwa gerezani, mfungwa huyo alitoroka katika mazingira ya kutatanisha akiwa chini ya uangalizi wa askari magereza aliyejulikana kwa jina moja la Shaibu.
Ilidaiwa kuwa, baada ya picha yake kuonekana kwenye gazeti, askari magereza wa Isanga waliutaarifu uongozi mara moja ambapo nao ulituma wachunguzi  jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza mchakato wa kumtia mikononi mfungwa huyo ili akamalizie kifungo chake cha miaka thelathini jela.
Inadaiwa kuwa, wachunguzi hao ambao ni askari magereza  wapo Dar wakisubiri siku ya kesi ya kujifanya trafiki itakapopelekwa kusikilizwa kwa hakimu.

HABARI MPYA, ADAIWA KUFARIKI DUNIA SEGEREA, DAR
Wakati mnyetishaji wetu kutoka gerezani Isanga Dodoma akianika madai ya siri hiyo nzito, Agosti 26, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Mwandishi Wetu, Makongoro Oging’  alipata taarifa kuwa, mtuhumiwa huyo wa kutenda kosa la kujifanya trafiki amefariki dunia ghafla akiwa gerezani Segerea.
Ilibidi mwandishi wetu amtafute Msemaji wa Jeshi la Magereza Tanzania, Meja Mtiga Omar na kumuuliza kuhusu madai hayo ya kifo ambapo alisema:
“Si kweli kwamba amekufa, bali ana tuhuma nyingine ya kutoroka gerezani ambapo tutamfungulia mashitaka mengine  ya kutoroka akiwa gerezani anatumikia kifungo chake.”
Juhudi za kumpata Mkuu wa Gereza la Isanga, Dodoma zilishindikana baada ya simu yake ya mkononi kuita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
James Hussein kama ndiye Ali Kinanda yupo Gereza la Segerea, hadi Septemba 5, 2013 kesi yake itakaporudi tena mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Joyce Minde kwa ajili ya kusikilizwa.

MTOTO MIAKA 7 ALEA FAMILIA

Na Imelda Mtema

WAZAZI ambao hawajajulikana walikotokomea wamewatelekeza watoto wao wanne wanaoishi Kata ya Bangulo, Pugu, Ilala, jijini Dar es Salaam, Amani lina mkasa wote.

Mazigira ya nyumba ya watoto hao ni ya kutoa machozi hata kwa mtu mwenye roho ngumu kama jiwe. Nyumba iko hivyo, pa kulala ni chini, wadudu kibao huku wakiwa hawajui hatima yao.

Majirani ndiyo waliowaibua watoto hao baada ya kubaini kuwa baba yao hajaonekana kwa miezi kadhaa nyumbani hapo hali iliyosababisha wengine kulia.

Akizungumza na paparazi wetu juzikati,  Sarah Shija (7) ambaye ndiye anayelea familia hiyo kwa sasa, aliwataja wenzake, Kevin Shija (8), Babu Shija (5) na Brighton Shija (6).

Alisema  mama yao mzazi aliondoka nyumbani hapo miaka miwili iliyopita baada ya kutokea mzozo kati yake na…
Na Imelda Mtema
WAZAZI ambao hawajajulikana walikotokomea wamewatelekeza watoto wao wanne wanaoishi Kata ya Bangulo, Pugu, Ilala, jijini Dar es Salaam, Amani lina mkasa wote.
Mazigira ya nyumba ya watoto hao ni ya kutoa machozi hata kwa mtu mwenye roho ngumu kama jiwe. Nyumba iko hivyo, pa kulala ni chini, wadudu kibao huku wakiwa hawajui hatima yao.
Majirani ndiyo waliowaibua watoto hao baada ya kubaini kuwa baba yao hajaonekana kwa miezi kadhaa nyumbani hapo hali iliyosababisha wengine kulia.
Akizungumza na paparazi wetu juzikati,  Sarah Shija (7) ambaye ndiye anayelea familia hiyo kwa sasa, aliwataja wenzake, Kevin Shija (8), Babu Shija (5) na Brighton Shija (6).
Alisema  mama yao mzazi aliondoka nyumbani hapo miaka miwili iliyopita baada ya kutokea mzozo kati yake na baba yao na kwenda kusikojulikana licha ya kwamba siku hiyo walimsihi sana mama huyo asiondoke.
Sarah aliendelea kuweka wazi kuwa, baada ya mama yao kuingia mitini, baba yao ndiyo akawa kila kitu lakini kumbe  na yeye alikuwa na lake moyoni.
Alisema miezi minne iliyopita, asubuhi baba yao aliamka asubuhi na kuwaachia shilingi 5,000 na kiasi kidogo cha unga kwenye kiroba na kuondoka akisema angerudi jioni.
“Mara ya mwisho baba alipoondoka alituambia angerudi jioni, akatuachia shilingi elfu tano kwa ajili ya kununua mboga na vitu vingine,” alisema Sarah.
Sarah alisema tangu siku hiyo baba yao  hakurudi tena huku wao wakiwa wamebaki wenyewe na elfu tano aliyowaachia ikiwa imeisha.
Alisema hali hiyo iliwalazimisha kusimama masomo kutokana na ugumu wa maisha kwa sababu mara nyingi wanaamka asubuhi wakiwa na njaa hivyo kushindwa kuelewa kinachofundishwa na walimu.
“Tunalala na njaa, tunaamka na njaa, tunashinda na njaa sasa tusingeweza kwenda shule kwa sababu tunakuwa tunatetemeka mwili. Hatujui baba atarudi lini,” alisema Sarah na kuangua kilio.
Alisema imefika hatua nduguze wakishikwa na kiu anawapeleka kunywa maji machafu ya kwenye madimbwi ambayo pia yana chumvi kupita kiasi kwa sababu hawana  fedha (shilingi mia nne) ya kununua maji salama.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Sarah alimuomba baba yao  popote alipo kurudi nyumbani na kuendelea na maisha. Pia walimtaka mama yao akisoma habari hii akawachukue kwani maisha yao ni magumu sana na yeye analazimika kufanya shughuli nyingi za nyumbani ili kuhakikisha uhai wao haukatishwi na njaa.
Ili kujua maisha yao zaidi ya kusikitisha usikose kuangalia Kipindi cha Wanawake Live cha Mtangazaji Joyce Kiria ambacho kitaonesha ‘live’ maisha magumu ya watoto hao.