This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, December 28, 2013

MKE AKATWA MAPANGA, HAWARA ATAJWA


Stori: Timoth Itembe, TARIME

MAMA mmoja mkazi wa Ronsoti, Kata ya Nyamisangura, wilayani hapa, Eliza Marwa,28, hivi karibuni amenusurika kuuawa na mumewe, baada ya majirani kufika kumuokoa kutokana na kukatwakatwa mapanga.

Mariamu akiugulia maumivu.
Mama huyo aliliambia gazeti hili akiwa katika Hospitali ya Wilaya Bomani, Tarime kuwa mume wake Marwa Ogora alimkatakata mapanga baada ya kumtuhumu kuwa akikwenda kwa hawara yake badala ya kwenda kwenye mazishi ya mjomba wake…

TARIME
MAMA mmoja mkazi wa Ronsoti, Kata ya Nyamisangura, wilayani hapa, Eliza Marwa,28, hivi karibuni amenusurika kuuawa na mumewe, baada ya majirani kufika kumuokoa kutokana na kukatwakatwa mapanga.

Mariamu akiugulia maumivu.
Mama huyo aliliambia gazeti hili akiwa katika Hospitali ya Wilaya Bomani, Tarime kuwa mume wake Marwa Ogora alimkatakata mapanga baada ya kumtuhumu kuwa akikwenda kwa hawara yake badala ya kwenda kwenye mazishi ya mjomba wake huko Bunchari.
Akifafanua zaidi, Eliza alikuwa na haya ya kusema: ‘’Mjomba alifariki na mazishi yake yalifanyika Desemba, kumi na sita mwaka huu ambapo nilihudhuria baada ya kumwarifu mume wangu kuwa nitahudhuria lakini alinijibu kuwa hakuwa na fedha za kunipa ili niende kwenye mazishi.
“Nilichukua jukumu la kwenda kwa kutumia nauli yangu kwa kuwa muda huo mume wangu alikuwa kazini na baada ya mazishi kesho yake asubuhi Desemba kumi na saba mwaka huu nilirudi nyumbani na kumkuta mume wangu ambaye alianza kunipiga kwa mpini wa jembe kisha panga akidai kuwa sikuwa nimeenda kwenye mazishi badala yake nilikuwa nimeenda kwa mpenzi wangu.
“Alinishambulia sehemu mbalimbali za mwili hususani kichwani, kidogo anitoe ubongo, wasingekuwa majirani kuniokoa baada ya kupiga yowe naamini angeniua kwani hivi sasa siwezi hata kuamka na masikio yameziba, miguu ina ganzi, siwezi kutembea.
“Mume wangu Ogora amekuwa akinipiga mara kwa mara lakini kutokana na watoto tuliozaa naye nimekuwa nikivumilia mateso, naogopa kuondoka na kuacha watoto walelewa na mama wa kambo,”alidai mama huyo.
Ogora hakupatikana kuzungumzia tukio hilo kwani anasakwa na dola na afisa mmoja wa polisi wilayani hapa wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema  wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa. Naye daktari wa hospitali aliyolazwa mama huyo, Nega Malico alikiri kumpokea mgonjwa huyo.

Saturday, December 7, 2013

UPEPO MKALI WAEZUA PAA LA SHULE YA MSINGI LUGANGA

1 892ea
Wanafunzi wa shule ya msingi Luganga kata ya Ilolompya Tarafa ya Pawaga Mkoa wa Iringa, wakiangalia sehemu ya paa la chumba cha darasa lililo ezuliwa na upepo mkali hivi karibuni.
2 e40f4
Nyumba ya Mwalimu
4 10483
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Luganga wakicheza nje ya Darasa lililo ezuliwa
5 ff967
Wanafunzi Shule ya msingi Luganga wakiendelea na Masomo ndani ya Darasa lililo ezuliwa na Upepo mkali hivi karibuni,Picha na Said Ng'amilo.(HD)

 Raia wa Afrika Kusini wako kwenye maombolezo kwa siku ya pili hii leo wakiwa kwenye mkesha kwa usiku nzima kwa ajili ya kuomboleza mpendwa wao Kiongozi wa zamani wa taifa hilo Nelson Mandela, aliyeaga dunia siku ya Alhamisi akiwa na umri wa miaka 95.
Watu wamekuwa wakikumbuka mema yake , wakicheza na kuimba Mbele ya makazi yake ya zamani mjini Soweto.
Katika mkutano na Waandishi wa habari , Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma aliainisha matukio ya juma zima kwa ajili ya maombolezo ambapo ametangaza kuwa siku ya jumapili siku maalum ya maombi na ibada maalum.
Siku ya Jumanne, itakuwa ni siku ya shughuli maalum za maombolezo ya kitaifa ambapo shughuli hizo zitafanyika katika uwanja wenye uwezo wa kukusanya watu 95,000 ulio nje kidogo ya mji wa Johannesburg.
Raia wa Afrika kusini wakiwa kwenye maombolezo
Mwili wa Mandela utalala Ikulu ya nchi hiyo jijini Pretoria kuanzia siku ya jumatano mpaka siku ya ijumaa.
Mazishi ya Mandela yatafayika jumapili ijayo tarehe 15 kijijini kwake alikokulia,Qunu.
Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 kabla ya kuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini.
Serikali yake iliondoa utawala wa kibaguzi wa watu weupe ambao ulikuwa na sera za kuwagawa watu wenye asili ya weupe na weusi.
Raia wa Afrika Kusini nchi nzima wamekuwa wakisali, wakiimba nyimbo za kupinga ubaguzi wa rangi na kuwasha mishumaa, wakikumbuka maisha ya Kiongozi wao na namna alivyo wavuta kwa mtindo wa maisha yake.

KINANA AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI PORINI, AOMBOLEZA KIFO CHA NELSON MANDELA


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kusimama njiani akitokea wilayani Makete akielekea wilayani Wanging"ombe, katika ziara yake maalum ya Mkoa wa Njombe kuhusu Chama cha Mapinduzi kilivyopokea kifo cha mpigania uhuru wa Afrika Kusini na mtu aliyeheshimiwa sana duniani Mzee Nelson Mandela kama alivyojulikana kama "Madiba" aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo ijumaa tarehe 6, Kinana amesema CCM inatambua jinsi Nelson Mandela alivyoipigania nchi yake na Afrika kwa ujumla, kuikomboa mikononi mwa ubaguzi wa rangi na kuiweka huru,…

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kusimama njiani akitokea wilayani Makete akielekea wilayani Wanging"ombe, katika ziara yake maalum ya Mkoa wa Njombe kuhusu Chama cha Mapinduzi kilivyopokea kifo cha mpigania uhuru wa Afrika Kusini na mtu aliyeheshimiwa sana duniani Mzee Nelson Mandela kama alivyojulikana kama "Madiba" aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo ijumaa tarehe 6, Kinana amesema CCM inatambua jinsi Nelson Mandela alivyoipigania nchi yake na Afrika kwa ujumla, kuikomboa mikononi mwa ubaguzi wa rangi na kuiweka huru, Ameongeza kwamba CCM na wanachama wake pamoja na watanzania wote watakumbuka mambo mema yote aliyoifanyia nchi yake na Afrika kwa ujumla na kuyaenzi kwa vitendo.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Cchama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana wakati akizungumza nao alipozungumzia kifo cha ayati Nelson Mandela huko Wanging"ombe mkoani Njombe leo.
Katibu Mkuu wa Cchama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mara baada ya kukagua shule ya sekondari ya Makete Girls iliyopo katika kijiji cha Mtweve wilayani Makete leo akiwa njiani kwenda Wilayani Wanging"ombe, kutoka kulia ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi, Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa na wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephin Matiro.
Mkuu wa wilaya ya Makete Mh. Josephin Matiro akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kukagua sekondari ya Makete Girls katika kijiji cha Mtweve akiwa njiani kwenda Wanging"ombe mkoani Njombe, Kutoka kulia ni Toto Timoth ambaye ametoa tani tano ya mifuko ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo,Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.
Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa akiongozana Hosea Mpagike Katibu wa CCM mkoa wa Njombe mara baada ya magari kukwama njiani kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha.
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi, Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana na Hosea Mpagike Katibu wa CCM mkoa wa Njombe wakisubiri magari yaliyokuwa yamenasa kwenye tope wakati msafara ukielekea wilayani Wanging'ombe leo.
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana kutoka kulia na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi wa pili pamoja na waandishi wahabari wakitembea kwa miguu huku magari yakiwafuata mara baada ya kuyanasua kwenye tope.
Mkuu wa Wilaya ya Wanging'ombe Bi.Esterina Kilasi akimkaribisha Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipowasili wilayani Wanging'ombe leo, kulia ni Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi.
"Kweli Bini ana Huruma" Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Bibi Geremana Mrwiro mwanakijiji ambaye alileta jembe ili litumike kwa kusaidia kunasua magari yaliyokuwa yamekwama kwenye tope.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika kijiji cha Usuka kilipo kituo cha Mafunzo ya zana za kilimo kwa wakulima wilayani Wanging'ombe ambapo Katibu mkuu wa CCM alitembelea vijana walioamua kujiunga pamoja na kuendesha kilimo
Baadhi ya vijana hao wakinyanyua kadi zao juu ili kula kiapo cha utii baada ya kukabidhiwa na Ndugu Abdulrahman Kinana leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akimkabidhi kadi kijana Said Mkweta.
Utulivu wa kula kiapo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi kuhuso moja ya Power Tiller itakayotumiwa na vijana hao kulimia shamba lao ili kuwahi mvua zinazonyesha.
Gari lililokuwa likitumiwa na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa likinasuliwa kwenye tope mara baada ya kuteleza na kuingia kandokando ya mtari
Juhudi za kunasua zikiendelea.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akipata kulia Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa kushoto na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi wakitoka nje mara baada ya katibu mkuu huyo kuzindua jengo la kitegauchumi la CCM mkoa wa Njombe leo ambalo limepangishwa na Wizara ya Fedha.

AIRTEL BINGWA KUFUNGUKIA MBAGALA ZAKHIEM LEO

Young killer
Haya sasa mabingwa wote wa Airtel bingwa  kula bata pamoja wikiendi hii Mbagala. Kama wewe ni bingwa wa kusakata kabumbu na kuonyesha umahili wa kumiliki mpira njoo leo tuonyeshe jumamosi hii MBAGALA ZAKHIEM kuanzia saa sita mchana mpaka saa 12 na nusu zawadi kibao kutolewa jezi, tisheti.Wasanii watakaopanda stajini ni Ney wa Mitego, Young killer  na Vinoko shackers ,Pia wadada…
Huku tukishuhudia draw ya Mimi Bingwa watu wanavyojishindia mamilioni na ticket ya kwenda Old Trafford kuangalia live mechi za  Man United  bure. Kama haitoishi sasa screen kubwa ya ukubwa zaidi ya mita  4 itaonyesha live mchezo wa Man United na Newcastle United.
Kiingilio ni BURE.

Saturday, September 28, 2013

Rais Kikwete ahutubia Umoja wa Mataifa New York

1 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia kikao cha 68 cha Baraza kuu la Umoja wa Mataifa leo jijini New York Marekani. 2 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja  na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban- Ki- Moon ofisini kwake. 3Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban- Ki- Moon ofisini kwake muda mfupi kabla ya kuhutubia kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New

MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE AZURU NEBRASKA NCHINI MAREKANI

IMG_2914Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akipokewa na Founder, Benefactor and Chief Executive Officer wa Taasisi ya Opportunity Education Bwana Joe Ricketts kwenye uwanja wa ndege katika mji wa Omaha uliopo katika Jimbo la Nebraska nchini Marekani tarehe 27.9.2013 IMG_2917Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea ua kutoka kwa binti Kate Stephens, 7, mara baada ya Mama Salma kutua kwenye uwanja wa ndege wa Omaha huko Nebraska nchiniMarekani tarehe 27.9.2013. IMG_2976Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akionyeshwa na Bwana James Ricketts, President and Chief Operations Officer, wa Taasisi ya Oppoturnity Education shughuli mbalimbali za kununua na kusafirisha vifaa vya elimu kwenda kwenye shule katika nchi mbalimbali hapa duniani ikiwamo Tanzania wakati Mama Salma alipotembelea Taasisi  hiyo yenye Makao Makuu yake huko Omaha katika Jimbo la Nebraska nchini Marekani tarehe 27.9..2013. IMG_2992Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akipokea zawadi ya ngao kutoka kwa Bwana Joe Ricketts, Founder, Benefactor and Chief Executive Officer wa Taasisi ya Opportunity Education iliyoko huko Omaha nchini Marekani. Bwana Ricketts alitoa zawadi hiyo kwa kutambua mchango mkubwa sana alioufanya Mama Salma binafsi na Taasisi yake ya WAMA Foundation katika masuala ya elimu. Afya na uwezeshaji kwa akina mama..
IMG_3016Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akifanya mazungumzo na uongozi wa juu wa Taasisi ya Opportunies Education kwenye ofisi za taasisi hiyo huko Omaha Nebraska nchini Marekani tarehe 27.9.2013. IMG_3068 IMG_3074Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikaribishwa kwenye Mji Mkuu wa Jimbo la Nebraska, Lincoln, huko Marekani na Dr. Natalie Hahn, Mwanzilishi wa Malaika Foundation na Senior Private Adviser for the United Nations Fund for International Partnership (UNFIP) tarehe 27.9.2013. IMG_3089Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Dr. Marjorie Kastelnik, Dean, College of Education and Human Sciences kwenye Chuo Kikuu cha Nebraska ambapo Mama Salma alishiriki kwenye Gala to support Global Education kwenye Chuo Kikuu cha Lincoln huko Nebraska tarehe 27.9.2013. IMG_3098Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mke wa Bwana Joe Ricketts kwenye gala  to support Global Education .
IMG_3139 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia waalikwa waliohudhuria Gala to support Global Education iliyoandaliwa kwa ajili ya kumtunuku tuzo maalum Bwana Joe Ricketts kwa juhudi zake za kuboresha elimu duniani hasa katika nchi zinazoendelea.

MBUNGE MSIGWA AMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA MKAKATI WAKE WA KUPAMBANA NA UJANGILI , ASEMA YUPO TAYARI KUWATAJA WANAOTUMIA AMBULENCE KUSAFIRISHA PEMBE ZA NDOVU IRINGA

Mwenyekiti wa MANET Bw  Zuberi Mwachura  kulia  akieleza mkakati  wa  kupambana na vitendo vya ujangili katika  hifadhi ya taifa  ya  Ruaha  leo

Mbunge  wa  jimbo la  Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akifafanua  jambo

Mgeni  rasmi  katika warsha ya  siku  moja ya  kujadili  vitendo  vya ujangili katika  hifadhi ya Taifa ya Ruaha ,mbunge  wa jimbo la Iringa mchungaji  Peter Msigwa ( wa pili kushoto) akiwa na viongozi mbali mbali akiwemo mwenyekiti wa taasisi  iliyoandaa warsha hiyo MANET Bw Zuberi Mwachura  na  viongozi  wengine
……………….
Na  Francis  Godwin Blog, Iringa
MBUNGE  wa  jimbo la  Iringa mjini kupitia chama  cha Demokrasia na maendeleo (chadema), Mchungaji Peter Msigwa amempongeza Rais  Jakaya  Kikwete kwa mkakati  wake wa kunusuru vitendo  vya ujangili  katika hifadhi  za  Taifa.
Huku  mbunge  huyo akidai  kuwa anawajua  viongozi  mbali mbali na watu maarufu ambao wanaendelea kuendesha  vitendo vya ujangili katika hifadhi ya  Ruaha  Iringa  ikiwa ni pamoja na kulitumia gari la  wagonjwa (Ambulence) kusafirisha  meno ya tembo na atawataja  wahusika  bungeni.
Msigwa  ambae ni  waziri  kivuli  wa wizara ya maliasili na utalii alitoa   pongezi  hizo  leo mjini Iringa wakati wakati akifungua kikao  cha  kujadili vitendo  vya ujangili  katika  hifadhi ya Taifa  ya  Ruaha Iringa iliyoandaliwa na taasisi  isiyo ya  kiserikali ya Mazingira Netwark Tanzania (MANET).
“Awali  ya  yote  napenda kumshukuru  sana Rais Jakaya Kikwete  kwa  kuja na mikakati ya kweli ya  kupambana na vitendo vya ujangili nchini  kwa  kutumia askari  wa jeshi la lawanchi Tanzania (JWTZ)…huu ni mkakati  mzuri ambao  binafsi  nimempongeza  sana kwa  hatua  hiyo” alisema Msigwa .
Kuwa  ni mara  kadhaa watanzania  wamepata  kusikia viongozi wa Serikali wenye dhamana wakisema kuwa mtandao wa majangili na wafanyabiashara haramu wa wanyamapori ni mpana na mgumu kuumaliza
Pia ni mara  kadhaa pia Serikali imeendelea kukiri kuwa mtandao huu unawahusisha Wafanyabiashara wakubwa, Wanausalama, Wabunge, Wanasiasa na watu wenye dhamana ya uongozi katika taifa letu umekuwa ni  kikwazo  kikubwa katika  vita dhidi ya ujangili.
“….Serikali imeendelea kutoa matamko kuwa itawataja wahusika wa biashara haramu dhidi ya wanyamapori na kuwachukulia hatua lakini cha kushangaza, mara zote hakuna hatua yoyote inayochukuliwa..ni jambo moja la msingi ambalo ningependa kulizungumza na kusisitiza hapa leo ni juu ya wajibu wa kila Mtanzania katika kuhakikisha kuwa tunaungana kwa pamoja katika vita dhidi ya biashara haramu ya wanyamapori
Hivyo  alisema hatua ya  Rais  Kikwete  kuweka mkakati  huo wa  kutumia  askari  wa JWTZ katika kulinda  hifadhi  na kupambana na majangili  ni  jambo la kumpongeza.
Kwani  alisema baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika tamko lake maarufu mwaka 1961 lijulikanalo kama Arusha Manifesto alisema yafuatayo 
          Uhai wa wanyamapori ni jambo muhimu na linalotuhusu sana sisi sote barani Afrika. Viumbe hawa wa porini, wakiwa   katika mapori wanamoishi,sio muhimu tu kwa ajili ya       kuajabiwa na kuvutia lakini pia ni sehemu ya maliasili yetu na pia ndio mustakabali wa maisha yetu ya baadaye.
Alisema  kuwa mwalimu Nyerere alitambua umuhimu wa kutunza wanyamapori kwa wakati huo tukiwa na hazina kubwa ya wanyama, lakini leo viongozi wa Serikali wameshikwa na kigugumizi katika kuhakikisha dira na jitihada za baba wa taifa letu ,vinatimizwa.
Hivyo  alisema kama kiongozi ambaye wananchi wamenipa dhamana ya kuwawakilisha, nawiwa kutumia nafasi hiyo, kuendeleza juhudi zangu na kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anakua mdau nambari moja wa kupinga biashara haramu ya wanyamapori kwani si tu kuwa inalitia hasara taifa letu bali pia inaweka hatarini maisha ya wanyamapori kwa vizazi vijavyo.
Nachukua nafasi hii kuikumbusha na kuitaka Serikali kutimiza wajibu wake kwa kuwafikisha majangili na wafanyabiashara haramu wa wanyamapori katika vyombo vya dola na watendewe ipasavyo kwa mujibu wa Sheria
Kuhusu  watu  maarufu mkoani Iringa  wanaojihusisha na biashar a ya  pembe  za ndovu na hata  kutumia magari ya  umma kama Ambulence  kusafirisha pembe  hizo  za ndovu  alisema kuwa ana idadi  yao ndevu zaidi na kuwa katika kikao cha bunge  kijacho ataweka hadharani majina yao.
 Kiongozi   wa  wanaharakati  wa mtandao  wa  kupambana na vitendo vya ujangili  katika  hifadhi ya Taifa  ya  Ruaha Fundi Mihayo alisema  kuwa mbinu mbali mbali  zinatumika katika kusafirisha pembe za ndovu  ikiwa ni pamoja na usafiri  wa  boda boda kutumika  sasa  kuendeshea  vitendo  vya ujangili .
Alisema  usafiri  huo  umekuwa  ukitumika kuvushia pembe za  ndovu katika  maeneo ya vizuizi na hivyo kutaka  ulinzi  na upekuzi mkubwa unahitajika katika kukomesha vitendo  hivyo.
Kwa upande  wake mwenyekiti wa MANET Zuberi Mwachura alisema  kuwa lengo la mtandao  huo ni kuendelea  kupambana na vitendo vya ujangili  katika maeneo ya  hifadhi nchini .
Kwani  alisema  kuwa usalama wa wanyama pori na mazingira yao ni walazima kwa maendeleo yetu hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kujua na kufahamu eneo ambalo wanatoka au wanaishi watu wanao fanya au kushiriki au kujihusisha na vitendo vya ujangili ni jukumu letu kuhamasisha jamii ya wananchi wote wajione wana wajibu wa kushiliki katika vita dhidi ya ujangili. 
..lazima tukubali kwamba ujangili upo,  Pamoja na changamoto zake,  lakini hatuwezi kukaa kimya tukiacha majangili waendelee kuteketeza tembo wetu. . Mwanzo wa mafanikio katika jambo lolote ni dhamila na nidhamu, ya kupanga na kutekeleza. .. Kwa kukubaliana katika nia hii ya kupambana na ujangili ni vizuri tuwe na tamko la dhamira yetu ya kujinasua katika Lindi Kubwa la ujangili wa Tembo

Ulimboka, Costa na Pawasa wachambua uchezaji Simba

simba_pixWACHEZAJI waliojijengea heshima kubwa wakati wakiichezea Simba wametamka maneno ya moyoni kuhusiana na mwenendo wa timu hiyo.
Wachezaji hao ni Boniface Pawasa, Victor Costa, Selemani Matola na Ulimboka Mwakingwe lakini kocha Talib Hilal alipowasikia naye akaongeza neno.
Pawasa ambaye alikuwa beki kisiki alisema: “Kikosi bado kinahitaji kurekebishwa hasa kwenye kombinesheni ya mabeki na ushambuliaji bado hapako sawa sana. Nafikiri baada ya mwaka Simba wanaweza kuwa kwenye ubora, wakizingatia misingi ya usajili, watu muhimu wakae sehemu muhimu.”
Victor Costa ambaye pia ni beki alisema: “Simba ya sasa si ya kutegemea sana kuleta mafanikio makubwa labda siku za mbele mafanikio yataonekana. Wachezaji wanahitaji muda na kuvumiliwa sana. Waachwe makocha wafanye kazi zao na pia wachezaji waliosajiliwa wapewe muda na si kuwafukuza.”
Kiungo Selemani Matola alisema: “Kikosi cha sasa ni kizuri, tena kina vijana vizuri ingawa wanahitaji kuaminiwa, watachezea timu hiyo kwa muda mrefu kwa kuwa bado ni vijana wadogo.”
Winga matata Ulimboka Mwakingwe alisema: “Sasa si kama zamani, wachezaji wengi wa sasa hawajitambui, hakuna ushindani wowote tofauti na wakati wetu tukicheza kwa kujituma na kushindania namba.
“Viongozi hawaelewi majukumu yao wengine wamekuwa wakifanya kazi ya kutafuta wachezaji wa kusajili na kuishia kusajili wasiofaa kwa kuwa hawana uelewa wa soka.
“Wamekuwa wakijipeleka nje ya nchi na kusajili vibaya, kisha wanaigharimu timu mamilioni ya fedha. Majukumu ya usajili wapewe wachezaji wa zamani kutokana na uzoefu wao,” alisisitiza Mwakingwe.
Kocha wa zamani Talib Hilal aliongeza: “Wachezaji wanatakiwa kujituma na kujiamini zaidi.”

RECHO ATUPIA NUSU UTUPU

 MSANII wa filamu za kibongo, Rachel Haule ‘Recho’ hivi karibuni aligeuka kituko baada ya kutupia picha ya nusu utupu katika mtandao wa kijamii.

Picha hiyo ambayo Recho amevaa shati tupu (inayoonesha ndani) bila kuvaa kitu kingine chochote, aliitupia kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo mashabiki na marafiki zake walichangia huku wakimlaumu kuwa hakufanya vizuri kuiweka picha hiyo ya aibu mtandaoni.

Paparazi wetu alimuuliza Recho kulikoni? Akajibu…
Rachel Haule ‘Recho’
Stori: Gladness Mallya
 MSANII wa filamu za kibongo, Rachel Haule ‘Recho’ hivi karibuni aligeuka kituko baada ya kutupia picha ya nusu utupu katika mtandao wa kijamii.
Picha hiyo ambayo Recho amevaa shati tupu (inayoonesha ndani) bila kuvaa kitu kingine chochote, aliitupia kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo mashabiki na marafiki zake walichangia huku wakimlaumu kuwa hakufanya vizuri kuiweka picha hiyo ya aibu mtandaoni.
Paparazi wetu alimuuliza Recho kulikoni? Akajibu hivi:
“Nawapenda sana marafiki zangu lakini mimi sijaona tatizo la hii picha kwa sababu ni ya kawaida sana sioni ubaya wake.”

MAADHIMISHO YA MIAKA 18 YA KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU YAFANYIKA DAR

Dr. Ringo Tenga ambaye ni mmoja wa waasisi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), akielezea historia ya kituo hicho. (wa kwanza kulia) ni Sengodo Mvungi ambaye pia ni muasisi wa kituo hicho.
 Kwaya iitwayo Mwalusanya inayoundwa na wafanyakazi wa kituo hicho, ikitumbuiza wakati wa maadhimisho hayo.…
Dr. Ringo Tenga ambaye ni mmoja wa waasisi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), akielezea historia ya kituo hicho. (wa kwanza kulia) ni Sengodo Mvungi ambaye pia ni muasisi wa kituo hicho.
Kwaya iitwayo Mwalusanya inayoundwa na wafanyakazi wa kituo hicho, ikitumbuiza wakati wa maadhimisho hayo.
Wanafunzi walihodhuria sherehe hizo wakimsikiliza kwa makini, Dr.Ringo.
Baadhi ya wadau wa kituo hicho wakisikiliza kwa makini historia ya kituo hicho.
Mkurugenzi wa kituo hicho, Dr. Hellen Kijo-Bisimba akilishwa keki na Bumi Mwalusanya. (Nyuma kushoto ni Dr. Sengodo Mvungi na Dr. Ringo Tenga ambao ni miongoni mwa waasisi wa kituo hicho.
Dr. Sengodo Mvungi akilishwa keki na Bumi Mwalusanya kuashiria uzinduzi wa sherehe hizo. (Wa kwanza kushoto ni Mhe. Rozy Kamili Mbunge wa Viti Maalumu Chadema), Mhe, Kamili ni mmoja wa wajumbe wa Bodi ya (LHRC) wa muda mrefu.

Maadhimisho ya miaka 18 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) yalifanyika juzi Septemba 26, jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na waasisi wa kituo hicho, wanachama, wanafunzi wa baadhi ya shule za Sekondari na msingi, viongozi wa dini na serikali na wadau wengine.
Wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika Makao Makuu ya LHRC,  Kijitonyama, mmoja wa waasisi wake, Dr. Ringo Tenga alielezea historia ya kituo hicho kilichoanzishwa 1995 ambapo lengo lake ni kupambana na matukio ya uvunjivu wa haki za binadamu.
Mkurugenzi wa kituo hicho, Dr. Hellen Kijo-Bisimba akizungumza wakati wa maadhimisho hayo alisema licha ya  kukumbana na changamoto nyingi, kituo chao kimepata mafanikio mengi.
Aliyetaja baadhi ya mafanikio hayo kuwa ni kuweza kuwatetea watu ambao kwa namna moja au nyingine hawakutendewa haki.
Mmoja wa watu aliyekuwa wa kwanza kutetewa na kituo hicho alikuwa marehemu Adam Mwaibabile aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Nipashe na Radio One mkoani Ruvuma.
Alisema baada ya mwandishi huyo kufungwa kwa uonevu, walikwenda Ruvuma ambapo walimpigania na kufanikiwa kumtoa katika kifungo alichohukumiwa na matukio mengine.
Kuhusu changamoto wanazokutananazo alisema ni kunyimwa vibali vya kufanya kazi na baadhi ya watendaji wa serikali wanapokwenda mikoani, kuitwa wanasiasa wa Chadema, chama cha kidini nk.
Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio yaliyojiri wakati wa maadhimisho hayo.