This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Wednesday, July 31, 2013

MBUNGE WENJE ATUHUMIWA KWA UTAPELI MWINGINE WA HARAMBEE NAYE MBUNGE LAMECK AMTAKA ASHINDANE NAYE KWA VITENDO NA SIYO MATUSI JUKWAANI


Mbunge wa Rorya Mhe. Lameck Airo akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari jijini Mwanza akimtaka Mbunge wa Nyamagana Mhe. Ezekiel Wenje, kushindana naye kwa kuwaletea wananchi maendeleo na siyo matusi jukwaani.
MBUNGE wa Jimbo la Rorya Mkoani Mara Lameck Airo (La-Kairo) amesikitishwa na kitendo cha Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje kumtapeli kiasi cha fedha shilingi milioni moja alizozitoa ili zikatangazwe kama sehemu ya mchango kwa lengo la kuchangia harambee aliyoiendesha katika kijiji cha Buchile Kata ya Mkoma Mjini Shirati Mkoani Mara alikozaliwa Wenje.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya tukio la hivi karibu la Bw. Wenje kutumia jukwaa la harambee hiyo ya kuchangia elimu katika kijiji cha Buchile kumkashifu kwa maneno yasiyofaa Mbunge wa jimbo la Rorya na kusema kuwa mbunge huyo hajafanya maendeleo yoyote kwa watu wa jimbo lake licha ya kusaidiwa kuongea Bungeni. 
Bw. Airo alisema kwamba kitendo alichokifanya Bw. Wenje cha kushindwa kuwasilisha mchango wa shilingi milioni moja alioutoa Airo katika harambee hiyo, kumchafua kwa kutumia lugha chafu pamoja na kushindwa kutambua thamani ya kazi mbalimbali ambazo amekuwa akizifanya katika kijiji hicho alikozaliwa Mbunge Wenje ni kitendo kisicho na uungwana na hakipaswi kufanywa na mtu wa hadhi yake anayetizamwa kama mfano wa kuigwa na jamii.
"Nadhani Bw.Wenje anapaswa kushindana nami kwa kwa vitendo katika kuwaletea maendeleo wananchi wa majimbo yetu badala ya kuhangaika na maneno jukwaani bila vitendo, hili haliwasaidii wananchi ila ninaamini mwisho wa siku tutakapokwenda kwenye tathimini tutaona ni nani aliwatumikia wananchi wake waliomchagua kikamilifu" "Mimi sitafuti umaarufu kwa wananchi wa Rorya na wao wanatambua hilo bali ni mimi niko kwaajili ya kutekeleza nilichowaahidi" alisisitiza Bw.Airo.
Mbunge Ezekiel Wenje.
Alieleza kwamba ni matukio yanayojirudia na anahisi huu ni mfumo na aina mpya ya utapeli aliobuniwa na Wenje wa kujipatia fedha toka kwa wadau na marafiki wanaokubali kumchangia, naye kuacha kuwasilisha michango hiyo au kuichakachua kwa kutoa kiduchu na kwamba siajabu hata Mwenyekiti wake Bw. Freeman  Mbowe naye alimchangia lakini hakumtaja kwa wananchi zaidi ya kusema yeye anatoa milioni moja zake kwa ujenzi wa darasa hilo la shule ya msingi aliyosomea.
“Nimeshangazwa kuona hata michango yetu mimi shilingi milioni moja na Mwenyekiti wangu wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Bw.Charles Ochele aliyetoa laki tano hazikutajwa zaidi ya Bw. Wenje kutoa milioni moja tu kwenye harambee hiyo fedha aliyodai imetoka mfukoni mwake, hii inaonyesha kuwa hakuwa na harambee ya kweli bali lengo lilikuwa kuwachafua na kuwakashifu kwa maneno yasiyofaa viongozi wenzake ili kujitafutia umaarufu wa kisiasa” alisema Airo. 
Bw. Airo amesisitiza kwamba kamwe hatomjibu kwa matusi mbunge Wenje na badala yake atamjibu kwa vitendo kwenye utekelezaji shughuli za maendeleo kupitia ilani ya CCM. 
Jimboni Rolya ahadi nyingi zilizoainishwa kwenye ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2010-2015 hadi sasa miradi mingi inatajwa kukamilika kwa asilimia 90 huku mbunge wa jimbo hilo akiahidi kukamilisha miradi mingine iliyoainishwa mapema zaidi hata kabla ya kumalizika kwa msimu.
Hii ni mara ya pili sasa kwa Bw.Wenje kushutumiwa na Bw.Airo kwa kutoweka wazi michango ya fedha anazoomba kuchangiwa kwenye harambee mbalimbali alizoendesha akidai kusaidia maendeleo lakini imekuwa tofauti kwani michango kuwasilishwa pungufu ya idadi iliyotolewa na zaidi Wenje amekuwa akimshambulia kutumia mikutano ya hadhara na majukwaa ya kisiasa akidai kuwa hajatoa mchango wowote japo amemuomba kufanya hivyo.

MIKUTANO WA MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA MWANZA NA WANANCHI WA MTAA WA MALIMBE WATOA SULUHISHO KWA KERO ZAO


Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza  ambaye pia ni diwani wa kata ya Mkolani (wa pili kutoka kushoto) akisikiliza kero za wananchi wa mtaa wa Malimbe ikiwa ni sehemu ya utaratibu aliouweka kufanya mikutano ya kila mara katika maeneo ya kata yake, wengine katika picha kushoto kabisa ni Mwenyekiti wa Mtaa Bi Zenaida Musiba, Mtendaji wa kata ya Mkolani Evarist Mtaki, Afisa Ardhi Idara ya Urasimishaji Makazi holela jijila Mwanza Bw. Maduhu Kazi Ilanga, pamoja na Mhandisi wa barabara  halmashauri ya jiji la Mwanza Bw. Malulu.

Mwananchi ambaye ni mkazi wa mtaa wa Malimbe kata ya Mkolani mkoani Mwanza akitoa hoja ya kuitaka Halmashauri ya jiji iwapatie hati baadhi ya wananchi waliopimiwa viwanja na kufanikisha upimaji wa maeneo ambayo hayajapimwa ili kuwa na uhakika wa makazi yao.

Sehemu ya wananchi wa mtaa wa Malimbe kusanyikoni.

Afisa Ardhi Idara ya Urasimishaji Makazi holela jijila Mwanza Bw. Maduhu Kazi Ilanga, akijibu hoja motomoto za wananchi zilizowasilishwa.

Mhasibu wa Wananchi Mwalimu mstaafu Mzee Mahola aliwasilisha 

Akinamama.

Mwananchi akitoa hoja ya ukarabati wa barabara ya Malimbe - Saut - Mnangani hadi Mkolani Centre ili kupitika kiurahisi. 

Mwananchi huyu alimuomba Mstahiki Meya kuwasiliana na SUMATRA na kuwabana baadhi ya wamiliki wa vyombo vya Usafiri wanaokatiza ruti huku magari yao yakiwa yamesajiliwa kuihudumia njia yote.

Mwalimu Crecency Njogopa aliwakilisha akina mama kwa kulizungumzia suala la uhaba wa maji.

Mdau huyu alimuomba Mstahiki Meya kuwabana Tanesco kuongeza juhudi za kutandaza nguzo za umeme bila urasimu ambapo suala hilo limekuwa kero ya muda mrefu, suala ambalo limechangia kuwaficha wahalifu walioleta maafa ya ujambazi na ubakaji hasa kwa wakazi wapangao maeneo hayo wengi wakiwa ni wanafunzi wa Chuo cha SAUT.

Mhandisi wa barabara wa Halmashauri ya jiji la Mwanza Bw. Malulu akijibu hoja na maswali yaliyojitokeza kwenye mkutano wa wananchi waishio mtaa wa Malimbe. 

Mstahiki Meya akitoa majibu na ufafanuzi kwa yaliyowasilishwa.

Kumalizika kwa mkutano eneo la mtaa wa Malimbe.

Wananchi wakimpongeza Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza mara baada ya mkutano kumalizika huku akitoa majibu mazuri yakitaalamu kupitia safu ya wataalamu alioongozana nao. 

Akina mama nao hawakuwa nyuma kutoa pongezi ambapo ndani yake waliahidi kutoa ushirikiano kwake na wataalamu hao wakati wa utekelezaji.

KUFUATIA kutupiwa skendo za kuhusika na usafirishaji wa madawa ya kulevya nje ya nchi, Mbunge wa Kinondoni jijini Dar, Idd Azzan ametinga polisi Julai 29, mwaka huu na kuwataka wamchunguze kwa kina.
Madawa ya kulevya.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Idd Azzan alifika katika Kituo Kikuu cha Polisi Posta jijini Dar na kukutana na Kamanda wa Kanda Maalumu, Kamishna, Suleiman Kova.

“Kikubwa Azzan amemwambia Kova kwamba anataka jeshi la polisi limchunguze na kisha liwaambie wananchi kama yeye…
Na Mwandishi Wetu
KUFUATIA kutupiwa skendo za kuhusika na usafirishaji wa madawa ya kulevya nje ya nchi, Mbunge wa Kinondoni jijini Dar, Idd Azzan ametinga polisi Julai 29, mwaka huu na kuwataka wamchunguze kwa kina.
Madawa ya kulevya.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Idd Azzan alifika katika Kituo Kikuu cha Polisi Posta jijini Dar na kukutana na Kamanda wa Kanda Maalumu, Kamishna, Suleiman Kova.
“Kikubwa Azzan amemwambia Kova kwamba anataka jeshi la polisi limchunguze na kisha liwaambie wananchi kama yeye anahusika na biashara hiyo au la,” kimesema chanzo chetu.
Baada ya kupata habari hizo, Risasi Mchanganyiko lilimpigia simu Azzan ambaye alikiri kufika polisi na kuwataka wamchunguze kwa kina.
Mbunge wa Kinondoni jijini Dar, Idd Azzan.
“Kila kinapofika kipindi kama hiki huwa kuna vuguvugu la uchaguzi, hivyo maneno kama haya husemwa ili kuharibiana sifa, nimewataka polisi wanichunguze na watakachokipata watoe taarifa kwa wananchi,” alisema.
Hivi karibuni Mbunge huyo alitajwa katika habari zilizosambazwa mtandaoni kwamba anahusika na biashara hiyo baada ya mfungwa mmoja wa gereza moja nchini Hong Kong kumtaja kwamba ndiye anayewatuma vijana nje ya nchi kupeleka madawa ya kulevya.
Hata hivyo, Mbunge huyo amekanusha taarifa hizo kwa kusema kuwa hausiki kwa njia moja ama nyingine na kutaka mfungwa huyo atajwe jina lake kamili, namba yake ya ufungwa na hata ndugu zake waliopo hapa nchini ili ukweli ujulikane.
Barua zilizosambazwa mtandaoni ambapo jina la Mhe. Idd Azzan lilitajwa kuhusika na dawa za kulevya:


ROSE NDAUKA ANASWA AKIPAPASWA NDANI YA GARI KABLA YA KUPELEKWA HOTELINI


 
Rose Ndauka  au  Aisha  anaweza  kuwa  ameitia  najisi  funga  yake  baada  ya  kunaswa akiingia  hotel  moja   iliyoko  kinondoni  jijini  Dar  kwa  kile  kilichoelezwa  ni  kwenda  kuivunja  amri  ya  sita  na  mwanamziki wa  bongo  fleva  Nassoro  Ayoub  "Nasry"   au  Tajiri Boy
 
Rose ambaye alisilimu mwaka jana  na  kupewa  jina  la  Aisha  baada  ya  kuchumbiwa  na mwanamziki  mwasisi  wa  kundi  wa  TNG Squad, Malik Bandawe, alifumwa na  kamera  za wakazi wa jirani na  hoteli  hiyo  mwishoni  mwa  wiki  iliyopita.....

Shuhuda  wa  tukio  hilo  amedai  kwamba  majira  ya  mchana  kweupe  gari  aina  ya  Toyota Mark  X lenye  rangi  nyeusi  liliwasili  kwenye  viunga  vya  hoteli  hiyo  na  kusimama  kwa  takribani  dakika  10  kisha  likaondoka  na  kwenda  kupaki  sehemu  nyingine  ambapo  ni  umbali  mfupi  toka  hotelini  hapo...
  Kitendo  hicho  kiliibua  mashaka  miongoni  mwa  watu  hasa  kutokana  na  vioo  vya  gari  hilo  kuwa  tinted  hivyo  kutowaonesha  waliokuwemo  ndani...

"Walipoondoka  na  kupaki  palipojificha  tuliamua  kuwasogelea  ili  tujue  ni  akina  nani

"Baada  ya  muda, kioo  cha  dereva  kilishushwa kidogo, tukamuona  dogo  anayefanana  na Diamond  akiwa  anampapasa  demu  aliyekuwa  pembeni  yake...

"Tulipoona  hivyo, tulidhana  mnyamwezi  ameamua  kumaliza  mambo  yake  ndani  ya  gari, hivyo  tukaziweka  simu  zetu  standby  kwa  ajili  ya  kushuhudia" alisema shuhuda  huyo

Baada  ya  muda, mlango  wa  kulia  ulifunguliwa  kisha  wakamuona  dogo  aliyetambuliwa  kwa  jina  la  Nasry

"Kumbe  hakuwa  Diamond,alikuwa  ni  dogo  Nasry.Tulipotupa  jicho  ndani, tulihamaki  kumuona  Rose  Ndauka  akibadili  nguo  na  kujitanda  baibui.

"Nadhani  alifanya  hivyo  ili  watu  wasimjue  pindi  atakaposhuka  kwenye  gari  maana  aliposhuka  tu, waliongozana  na  dogo  Nasry  kwa  mwendo  wa  kasi  hadi  ndani...

"Toka  walipoingia  ndani  hadi  walipotoka  iliwachukua  kama  masaa  matatu  hivi.Wakati  wa  kutoka, Nasry  alilifuata  gari  hadi  mlangoni  na  kisha  Rose  akaingia  na  kutokomea"...Kilimalizia  kusimulia  chanzo  hicho

SHEIKH PONDA ISSA PONDA APENDEKEZWA KUGOMBEA URAIS MWAKA 2015



Ikiwa  imebakia  miaka  miwili  kabla  ya  kufanyika  kwa  uchaguzi  mkuu wa  Rais  na  wabunge  hapa  nchini,baadhi  ya  waumini  wa  kiislamu  wameanza  kupendekeza  wagombea  wa  urais  wanaoona  kuwa wanafaa  ambapo  jina  la Sheikh  Ponda Issa Ponda  limeongoza....

Mapendekezo  hayo  yamedhihirika   katika  mihadhara kadhaa  anayoifanya Ponda  katika  mikoa  mbalimbali  nchini,ambako  amekuwa  akipendekezwa  na  kushauriwa  na  waumini  agombee  nafasi hiyo.....

Walianza  waumini  wa  msikiti  mkuu  wa  Ijumaa  wa  Arusha  alipokuwa  kwenye  ziara  mkoani  humo  ambapo  muumini  mmoja  alisimama  na  kusema  kwamba  kwa  mawazo  yake  anaona  Ponda  anafaa  kugombea  nafasi  ya  urais  kwa  vile  anaamini  kuwa  uwezo  wa   kuongoza  anao..

Alisema  mbali  na  uwezo pia  yuko  makini  katika  kusimamia  jambo lolote  lenya  maslahi  kwa  waislam  na  kwamba  mtu  wa  namna  hiyo  atafanya  vyema  zaidi  akipewa  dhamana  ya  kuongoza  nchi....

Inaelezwa  kuwa Ponda  alipotembelea  Zanzibar  alipata  wakati  mgumu  wa  kuwakataa  waislam  waliojitokeza   kumlaki  katika  misikiti  ya  Mpendae na  Mbuyuni  ambako  alifanya  mihadhara  na  kupendekezwa kugombea  urais  kwa  kura  nyingi  na  waumini  ....

Kufuatia  kusikika  kwa  mapendekezo  hayo,Kisiwa  lilimtafuta  Ponda  ili  kusikia  maoni  yake  juu  ya  maombi  ya  waislam  kumtaka  agombee  urais.

"Sikuwa  na  fikra  hiyo  hata  mara  moja,lakini  maadam limeletwa  nami  ni  kiongozi  wa  taasisi  ninawashukuru  waliofikiria  hivyo...

"Kwa  sasa  siwezi  kuzungumza  lolote  kuhusu  hilo, ntalifikisha  katika  taasisi  na  maulana  ndio  watakaolitazama  na  kutoa  uamuzi." Alisema  Sheikh Ponda

Ponda  alisema  kuwa  inawezekana  waumini  wakawa  na  mtazamo  huo  lakini  viongozi  wakawa  na  mtazamo  tofauti  kabisa,hivyo  akawataka  waumini  kuwa  na   subira  katika  hilo.

-KISIWA.

AGNESS MASOGANGE AMPONZA MADEE NA KUSABABSHA AVULIWE NGUO AIRPORT



Kwenye Exclusive interview na millardayo , Madee amehadithia kila kitu kilichomtokea wakati anaingia tu Afrika Kusini siku kadhaa zilizopita ambapo hii imetokea kutokana na ukubwa wa habari, uzito wa tukio la wale Watanzania wawili wasichana (Akina Masogange )  waliokamatwa kwenye kiwanja cha ndege Johannesburg wakiwa na dawa za kulevya wakitokea Tanzania.


Madee anakwambia alipotua kwenye kiwanja cha ndege, kawaida huwa kuna utaratibu wa kuchekiwa hati ya kusafiria na ukaguzi mwingine ambao hufanywa na mitambo maalum kwa kila abiria anaeingia Afrika kusini, ni ukaguzi ambao unafanywa Airport kabla ya abiria kuruhusiwa kuingia kwenye nchi yenyewe.


Kilichomfanya Madee kusachiwa na kuhojiwa karibu dakika 60 ni pale tu aliposema anatokea Tanzania, kuna wazungu wawili wenye sare tofauti za kipolisi wakaanza kumsachi mpaka kufikia kumwambia avue t shirt yake, alivua t shirt na kubakiwa na nguo nyepesi ya ndani wakati huo abiria wenzake aliokwenda nao walikua wameruhusiwa.


Kati ya abiria wote waliokuja pamoja kwenye ndege, Madee na Mzimbabwe mmoja ndio walikaguliwa sana ila huyo mwingine alikaguliwa kidogo tu kama dakika 10 na wala hakuambiwa avue nguo.


Sehemu yenyewe Madee aliyoambiwa avue nguo sio kwenye chumba maalum, ni palepale kwenye foleni wanaposimama watu ila kwa pembeni kidogo, ni sehemu ambayo imezibwa na kioo kinacholingana na usawa wa tumbo kushuka chini…. Madee anakwambia jamaa walinong’onezana sana wakati wanamkagua.


Hata hivyo baada ya Askari hao kumuweka sana msanii huyu wa bongofleva kutoka kundi la TipTop Connection walimuomba radhi baada ya kumaliza ukaguzi wao ambao pia ulihusika kulivuruga sana begi lake.

Friday, July 26, 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWA WILAYANI MULEBA

Rais Kikwete akivikwa skafu na skauti baada ya kuwasili Muleba.

Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wageni.…

Rais Kikwete akivikwa skafu na skauti baada ya kuwasili Muleba.
Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wageni.
Rais Kikwete akisalimiana na mama wa Profesa Anna Tibaijuka.
Waziri wa Ardhi Profesa Anna Tibaijuka akishiriki katika ngoma ya utamaduni wakati wa mapokezi ya Rais Kikwete wilayani Muleba.
Wananchi wa Muleba wakimshangilia Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipowasili wilayani humo akiwa katika ziara yake ya siku sita Mkoani Kagera.
Rais Kikwete akiongea na viongozi wa wilaya ya Muleba baada ya kupokea taarifa ya maendeleo, akiwa na mawaziri watano anaoongozana nao katika ziara hiyo.
Mbunge wa Muleba akitoa  maoni na kero za jimbo lake.
Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe akiwahakikishia viongozi wa Muleba juu ya mipango ya serikali kuleta meli za abiria mpya mbili katika ziwa Victoria.
Rais Kikwete akipata maelezo ya mpango kabambe wa maji wilaya ya Muleba.
Rais Kikwete akizindua mradi mkubwa wa maji wilayani Muleba.
Rais Kikwete akikata utepe kuzindua mradi wa maji.
Rais Kikwete akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa wananchi wa Muleba baada ya kuzindua mradi mkubwa wa maji kwa wilaya hiyo.
Mwananchi mwingine akitwishwa maji.
Ngoma ya utamaduni ikimlaki Rais Kikwete alipowasili katika mkutano wa hadhara.
Rais Kikwete akisalimia wananchi.
Rais Kikwete akiangalia mazao yatokanayo na uzalishaji mbegu ya kampuni ya Itente ya Muleba.
Rais Kikwete akipozi na wafanyakazi wa kampuni ya uzalishaji mbegu ya Itente.
Rais Kikwete akifurahia ngoma.
Umati wa wananchi Muleba ukimsikiliza Rais Kikwete.
Rais Kikwete akiongea na wananchi wa Muleba.
Rais Kikwete akihutubia wana Muleba.
Sehemu ya umati mkutanoni.
Rais Kikwete akiendelea kungea na wananchi.
Umati  katika mkutano wa hadhara.
Umati katika mkutano wa hadhara.
Rais Kikwete akijiunga na waumini wa Muleba kusali swala ya Magharibi kabla ya kufuturu.
Dua ikisomwa baada ya futari aliyoandaa Rais Kikwete kwa wananchi wa Muleba.
Dua ikiombwa baada ya futari.
Dua.
Wananchi wa Muleba katika futari aliyoandaa Rais Kikwete wilayani Muleba.