This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, July 6, 2013

TEMEKE YALIZWA NYUMBANI MABAO 5-2 MICHUANO YA AIRTEL RISING STARS


Timu za Airtel Rising Stars zikiingia kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam tayari kwa ufunguzi rasmi wa ARS ngazi ya Taifa jana Jumanne Julai 2, 2013..

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano – Mallya akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Airtel Rising Stars ngazi ya Taifa uliofanyika kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini  Dar es Salaam jana Jumanne

Mgeni rasmi Naibu Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Kassim Majaliwa akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Airtel Rising Stars ngazi ya Taifa uliofanyika kwenye uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini  Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mheshimiwa Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji


Timu ya Morogoro wavulana leo Jumatano Julai 3, imeifunga timu ya Temeke 5-2 katika fainali za Taifza za Airtel Rising Stars
zinazoendelea kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.

Morogoro waliutawala mchezo na kufanikiwa kupata magoli kupitia kwa mshambuliaji wa machachali Optatus Lupekenya ambaye alifunga magoli matatu peke yake yaani ‘hat trick’ katika dakika za 27 67 na 87.
Magoli mengine ya Morogoro yalifungwa Salum Mohamed dakika ya 72 na Evance Noshan dakika ya 80 wakati magoli ya Temeke yalifungwa na Mohamed Simba dakika ya 10 na Rajab Jumanne dakika ya 83.

Katika mchezo uliochezwa mapema asubuhi timu ya Ilala wasichana ilifanya mauaji ya kutisha baada ya kuifunga bila huruma timu ya Ruvuma 9-0 katika mchezo wa upande mmoja wa fainali za Taifa za Airtel Rising Stars. 
Mchezo huo ulionyesha wazi ya kuwa Ruvuka wanatakiwa
kufanya kazi ya ziada ili kuinua kiwango chao cha soka.

Ilala walifunga magoli yao kupitia kwa Amina Ally (dakika ya 3, 28 na 51), Donisia Daniel (dakika ya 20 na 45), Zuwena Aziz (dakika ya 23 na 35), Madeline Sylvester (dakika ya 8) na Fatuma Bahau (dakika ya 12).

Katika mchezo uliochezwa Jumanne jioni katika uwanja huo huo, timu ya  kombaini ya Mwanza (wavulana) ilitoa onyo kwa timu zinazoshiriki michuano hiyo baada ya kuifunga timu ngumu ya Ilala 3-1.

Huo ulikuwa mchezo rasmi wa ufunguzi wa Airtel Rising Stars Taifa 2013 ambapo mgeni rasmi Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mheshimiwa Kassim Majaliwa aliwataka vijana kuonyesha vipaji vyao.

“Katika dunia ya leo mpira wa miguu ni moja ya vyanzo vya ajira vya kutumainiwa kwa vijana”, alisema Majaliwa na kuwahamasisha vijana hao kucheza kwa kujituma na kutumia mashindano ya Airtel Rising Stars kama fursa ya kuonyesha umahiri wao wa kusakata kabumbu. Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano alisisitiza nia thabiti ya kampuni yake kuendeleza kusaidia programu hii ya vijana.

Mchezo kati ya Mwanza na Ilala ulikuwa wa kuvutia huku timu zote zikionyesha kiwango kizuri kwa kugongeana pasi za uhakika. Mwanza walifanikiwa kupata goli la kwanza dakika ya saba kupitia kwa Nassor ambaye aliwapita walinzi wa Ilala na kutia mpira wavuni. Goli hilo lilidumu hadi mapumziko.

Ilala walianza kipindi cha pili kwa nguvu na kupata goli la
kusawazisha dakika ya 50 kupitia mpira wa adhabu uliopigwa na Omary Hassan baada ya walinzi wa Mwanza kufanya makosa nje kidogo ya eneo la hatari. Mshambuliaji Athanas Adam aliifungia Mwanza goli la pili dakika ya 69 na Kelvin Ntalale kugongelea msumari wa mwisho dakika mbili kabla ya mchezo kumalizika.

ISRAEL YATISHIA KUJENGA HEKALU NDANI YA AQSWA

ISRAEL YATISHIA KUJENGA HEKALU NDANI YA AQSWA

Waziri wa Nyumba wa utawala wa Kizayuni wa Israel amesema kuwa, watajenga hekalu kwa ajili ya Mayahudi ndani ya ua wa msikiti Mtukufu wa al Aqswa. Uri Ariel ambaye ni mwanachama wa chama chenye misimamo mikali cha 'Jewish Home' amesema kwamba, Baraza la Mawaziri la Israel limesimamisha ujenzi wa vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan lakini kwamba atahakikisha kuwa hekalu la Mayahudi linajengwa ndani ya Masjidul Aqswa.
Huku akitoa matamshi ya kufurutu ada na ya kibaguzi waziri huyo wa Israel sambamba na kubainisha kuwa, kuna matakwa ya kuundwa serikali mbili za Palestina na Israel amesema kwamba, njia pekee na ya uhakika eti ni kuwepo serikali moja tu ya Israel katika eneo hilo.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, viongozi wa utawala ghasibu wa Israel wanafanya kila njama ili waweze kuharibu athari na utambulisho wa Kiislamu na Kiarabu katika mji wa Quds kwa lengo la kuuyahudisha mji huo

KENYA YAISUSIA SHEREHE YA UHURU WA MAREKANI

KENYA YAISUSIA SHEREHE YA UHURU WA MAREKANI

Katika kile kinachoonekana ni kuendelea kuzorota uhusiano wa Nairobi na Washington, maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Kenya wamesusia sherehe za uhuru wa Marekani zilizofanyika jana usiku katika ubalozi wa Marekani mjini Nairobi.
Katika hafla hiyo ambayo maafisa wote wa ngazi za juu serikalini walialikwa, rais na naibu wake hawakuhudhuria, aidha hakuna waziri au katibu mkuu wa wizara aliyehudhuria hafla hiyo. Sherehe hizo zimekuja siku mbili tu baada ya Rais Obama kukamilisha safari yake ya kuzitembelea nchi za Afrika pasina kuitembelea Kenya kama Rais Uhuru Kenyatta wa Kenyailivyotarajiwa. Afisa pekee wa serikali ya Jubilee aliyehudhuria sherehe hizo ni Spika wa Senate Ekwe Ethuro na maafisa wa ngazi za chini kutoka Wizara ya Mambo ya Nje.
Hivi karibuni Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema serikali yake haibabaishwi na mitazamo ya nchi za Magharibi ambazo zimekuwa zikimpiga vita. Rais Kenyatta alisema mitazamo ya nchi za Magharibi haitaizuia serikali ya Jubilee kuwahudumia Wakenya.
Chanzo iran swahil radio

WAZIRI MAGUFULI ATAMANI KUWA RAIS WA TANZANIA......ANADAI KWAMBA YUPO TAYARI KUGOMBEA MWAKA 2015 ENDAPO ATAKIDHI MASHARTI


 Katika hali inayoonyesha kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, anautamani urais, amesema anaweza kutangaza nia hiyo kama atakidhi masharti yatakayowekwa kwenye Katiba mpya.

Alisema iwapo Katiba ijayo itakuja na sifa ambazo atakidhi vigezo kuna uwezekano mkubwa wa kuwania nafasi hiyo na kwamba iwapo atapungukiwa sifa zinazohitajika kwa mujibu wa Katiba hataingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Dk. Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Chato alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo kwenye ukumbi wa ‘Mshikamano Saccos’, muda mfupi baada ya mzee Paschal Nyambibo (87) kumsihi agombee nafasi hiyo mwaka 2015 kutokana na sifa zake za uchapakazi ndani ya serikali.

Nyambibo alisema kutokana na uwajibikaji mzuri aliouonyesha Dk. Magufuli tangu mwaka 2000 akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na katika wizara mbalimbali, Watanzania wamekuwa na imani kubwa na uwajibikaji wake na kwamba anastahili kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ifikapo mwaka 2015.

Licha ya kauli hiyo kusababisha minong’ono mingi kwa wazee waliohudhuria kikao hicho, Dk. Magufuli alionekana kutuliza hali hiyo kwa kusema isubiriwe Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano iwapo itakuwa na masharti ambayo yatamfanya kujitathimini iwapo ana sifa za kugombea au vinginevyo.

Hata hivyo, Dk. Magufuli hakusita kuonyesha hisia zake za kukerwa na baadhi ya wananchi wanaobeza maendeleo aliyotekeleza katika jimbo lake tangu alipochaguliwa kuwa Mbunge.

Alimshutumu hadharani aliyekuwa Katibu wa CCM wilaya ya Chato kabla ya kuhamishiwa wilayani Mbogwe, Gervas Stephano, kuwa hana shukrani.

Dk. Magufuli alimwelezea katibu huyo kuwa hana fadhila kutokana na mambo mengi aliyomtendea tangu akiwa katibu wa ofisi yake ya jimbo ambapo alimsaidia kupanda ngazi na kuwa Katibu wa CCM wilaya Chato, Kwimba, Kasulu, Kilosa na kurejea tena Chato kabla ya kuhamishiwa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita  kuendelea na wadhifa huo.

“Tatizo lenu watu wa Chato hamna shukrani…mambo mengi nimefanya hapa Chato, lakini yote mnaona ziro…hata niliowasaidia kama Gervas naye sasa hivi ananiponda…lakini nawashukuru sana wazee wangu kwa kunikumbusha niliyoyafanya kwenye jimbo letu kupitia risala yenu nzuri,
” alisema Dk. Magufuli.

“Kutokana na hali hiyo ninawazawadia Sh. 1,000,000 mfanye sherehe ya kujipongeza kwa kuwa natambua mmejitesa sana mpaka kufanikisha kikao hiki cha leo…na kwa kuwa hamna mradi wowote wa kuwaingizia kipato kama wazee, ninaahidi kuwapa Sh.   3,000,000 kutoka mfuko wa jimbo, ili muanzishe walau saccos ya kukopeshana,” alisema.

Baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakilitaja mara kwa mara jina la Waziri Magufuli miongoni mwa watu wanaodhaniwa kutaka kugombea nafasi ya urais wa Tanzania mwaka 2015, ingawa mwenyewe amekuwa akikanusha uvumi huo.

Mbali na Dk. Magufuli, wengine ndani ya CCM wanaotajwa  ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa; Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, ambaye anajiita mtaji wa urais; Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe; Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Ushirikiano wa Kimataifa –CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano na Mambo ya Nje, Bernard Membe, ambaye alipata kusema anasubiri kuiteshwa na Mungu kuwania nafasi hiyo.



Nipashe:

NELSON MANDELA YUKO KATIKA HALI YA "USINGIZI WA KUDUMU"....NYARAKA ZAFICHUKA



Nelson Mandela ameendelea kuwekwa hai kwa msaada wa mashine za kumsaidia kupumua na  'anakaribia kifo,' nyaraka za mahakama zimefichua.

Afya ya rais huyo wa zamani ni 'yenye hatari kubwa,' kwa mujibu wa nyaraka zilizowasilishwa mahakamani kwenye kesi ambayo imepelekea mabaki ya miili ya watoto wake watatu kuzikwa upya Alhamisi kwenye makaburi yao ya awali.
 
Nyaraka za mahakama za Juni 26 zilisema: "Matarajio hayo ya kukaribia kifo chake yanaegemea katika uhalisia na uthabiti,' zilisema nyaraka hizo za mahakama.
 

Mandela, ambaye alilazwa hospitali Juni 8, ameendelea kuwa mahututi lakini hali inayoimarika, kwa mujibu wa Ofisi ya Rais Jacob Zuma, ambaye alimtembelea kiongozi huyo wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi Alhamisi.


Ikulu ya Afrika Kusini imekanusha kwamba Mandela yuko kwenye 'hali ya kulala tu', na kurejea taarifa zake zilizopita kwamba kiongozi huyo mpendwa yuko mahututi lakini katika hali inayoimarika.


Ikulu hiyo ilitoa taarifa 'inayofafanua' hali ya Mandela, imeripotiwa.

Walisema: "Tunathibitisha taarifa zetu  zilizotolewa awali ... baada ya Rais Jacob Zuma kumtembelea Madiba hospitalini."


Mandela yuko chini ya uangalizi wa karibu wa timu ya wauguzi, ikulu hiyo ilisema, masaa kadhaa baada ya ripoti hizo za kusisimua za mahakama kufichuka.


Nyaraka hizo zilisomeka: Wanasema hali ya rais wa kwanza mweusi wa nchi hiyo ni 'yenye hatari kubwa'. "Matarajio ya kukaribia kifo chake yanaegemea katika uhalisia na uthabiti,'  ziliongeza. 


Nyaraka hizo za kisheria zinahusiana na mapambano makali ya kisheria yenye chuki kati ya makundi yanayopingana kwenye familia kuhusu wapi Mandela atakapozikwa.

Baada ya kumchunguza wiki iliyopita, madaktari waliandika: 
 "Yuko kwenye hali ya kudumu ya kulala tu na anasaidiwa kupumua na mashine ya kuokoa maisha."


Kitabibu, hii inamaanisha hajitambui na yuko kwenye hali katikati ya kuzimia kwa muda mrefu na kifo.

"Kwa kifupi ameshakufa," alisema Charlene Smith, mwandika wasifu wa Mandele aliyethibitishwa.

Taarifa hizo zimekuja huku mabaki ya watoto watatu wa mzee huyo mwenye miaka 94 yakiwa yamezikwa upya kwenye makaburi yao ya awali kufuatia amri ya mahamaka kuirejesha miili hiyo baada ya mjukuu wake, Mandla kuwa ameihamisha.

PICHA ZA LAANA ZA KUNDI LA BAIKOKO - TANGA

Hizi  ni  baadhi  ya  picha  za  kundi  la  wacheza  uchi / nusu  uchi  maarufu  kwa  jina  la  Baikoko  lenye  maskani  yake Tanga....

 
 
 
 


WAZAZI WAUA MTOTO WAKIGOMBANIA CD YA MSANII "DIAMOND"



Vilio  na  simanzi  vilitanda Jumatano iliyopita Mwananyamala Kisiwani, jijini Dar kufuatia mtoto wa mwaka mmoja, Rahim Rajab kufariki dunia kwa kuangukiwa na watu watatu, akiwemo baba yake mzazi, Rajab Said..


Tukio la watu hao kumwangukia mtoto huyo lilitokea Jumatatu iliyopita na lilisababishwa na ugomvi mkubwa wa CD yenye nyimbo za mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ulioibuka ndani ya chumba cha kulala kati ya mama wa marehemu na mpangaji mwenzake aitwaye Aisha.


Akizungumza kwa machungu kuelezea tukio hilo, mama mzazi wa marehemu Rahim, Habiba Ally alikiri kuwa kisa cha kifo cha mwanaye ni CD tu.Akasema: 

" Kwa kweli hakuna kingine zaidi ya CD, naamini hivyo kwa kuwa mimi sikuwa na ugomvi wowote na Aisha. Tulikuwa tunaishi kawaida tu ukiacha mikwaruzo ya hapa na pale.” 

Akaongeza: Jumamosi iliyopita, Aisha alikuja ndani kwangu na CD zake tatu, ya Diamond, Kingwendu na ya Coast Modern Taarab. Alipomaliza kuangalia aliziacha, akaondoka zake.

“Jumapili mimi nikaenda nazo kwa mama zote tatu kwa ajili ya kuziangalia, tulipomaliza na mimi niliziacha huko. 

“Jumatatu usiku Aisha akaja kunidai, nikamwambia zipo kwa mama. Kwa kuwa anapajua anapoishi mama, si mbali akaenda kuzichukua zote tatu. 


Ajabu aliporudi tu, akaja tena kwangu na kusema hajapewa CD ya Diamond kitu ambacho si kweli na ndipo ulipozuka ugomvi wote huo hadi kusababisha kifo cha mwanangu.”

Akizungumza msibani juzi, bibi wa marehemu, Jamima Hassan alisema siku ya tukio alipigiwa simu na mkwe wake (baba wa marehemu) akamwambia kuna ugomvi nyumbani kwake unaohusu CD kati ya mkewe na mpangaji mwenzake ambapo bibi huyo aliamua kwenda kutatua ugomvi huo.

“Niliondoka muda huohuo kwani huyo Aisha alitoka kwangu kuchukua CD zake muda mfupi tu, sasa nilijiuliza ni CD gani wanazogombania?


“Nilipofika nilikuta ugomvi umepamba moto, baba wa mtoto na mume wa Aisha aitwaye Shaban Sangali walikuwa wameungana kumtoa nje ya chumba Aisha bila mafanikio. 

“Wakati naingia, Aisha alikuwa akitukana matusi mazito na tulipojitahidi kumtoa nje alitusukuma kwa nguvu. Ndipo yeye, mume wake na baba wa mtoto waliwaangukia watoto waliokuwa wamelala kitandani,” alisema bibi huyo.


Akaendelea: Tulipowaangalia watoto ambao ni mapacha, hali zao zilikuwa mbaya, tukaamua kwenda kwa mjumbe wa mtaa kuripoti, akatupa barua, tukaenda Kituo cha Polisi Mwinyijuma, pale wakatupa PF3 ya kuwapeleka Hospitali ya Mwananyamala ambako walilazwa kwa matibabu.


Bibi huyo alisema siku iliyofuata, Rahim alifariki dunia, ikabidi waende Polisi Oysterbay ambapo walifungua shitaka lenye faili kwa kumbukumbu No. OB/RB/1150/2013 MAUAJI.

Watuhumiwa katika RB hiyo ni Aisha na mumewe, Sangali ambao walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.


Majirani waliozungumza na mwandishi wetu  walisema wakati ugomvi kati ya Aisha na Habiba unatookea, mume wa Habiba alikuwa anarudi kutoka kazini, akakutana na kimbembe hicho.

Walisema aliingilia kati kuamua bila mafanikio. Wakati huo mume wa Aisha alikuwa chumbani kwake na amefungulia muziki wa redio kwa sauti ya juu hivyo hakujua nini kinaendelea kwenye chumba cha mpangaji mwenzake.


Ikaelezwa kuwa, kuna watu walikwenda kumgongea na kumwambia mkewe anapigwa na mume wa Habiba kwa kushirikiana na mkewe.


Ilibidi mwanaume huyo atoke mbio hadi chumbani kwenye ugomvi ambako alikuta baba wa marehemu akijitahidi kuwaamulia wawili hao bila mafanikio.

Habari zinasema mwanaume huyo aliingilia kati kuongeza nguvu lakini katika hali ya kuwalemea, Aisha aliwasukuma wote na kisha wao kuwaangukia watoto hao mapacha waliokuwa wamelala kwenye kitanda kimoja.


Katika hali ya kusikitisha, marehemu amemuacha pacha mwenzake aitwaye Rahima Rajab ambaye ni kulwa.


Wengi wanaamini kuwa maisha ya Rahima yangekuwa ya furaha zaidi kama Rahimu angekuwepo na kwamba itamsononesha sana akikua na kusikia mwenzake alifariki dunia kwa ugomvi wa mama yake na mpangaji mwenzao kisa ni CD ya nyimbo za mwanamuziki.

GPL

LOWASSA AVIONYA VYOMBO VYA DOLA...!


WAZIRI Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amevitaka vyombo vya dola na wafanyabiashara wakubwa nchini, kujenga mahusiano bora kati yao na wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) ili kuondoa tabaka la matajiri na masikini linaloweza kuathiri uchumi wa taifa.

Lowassa aliyasema hayo jana wakati akizungumza na machinga wa eneo la Makoroboi jijini Mwanza, ambao pamoja na mambo mengine aliwachangia sh milioni 20 kwa ajili ya kutunisha mfuko wao.

Mwanasiasa huyo ambaye pia ni mbunge wa Monduli, aliinyoshea kidole Serikali ya chama chake cha Mapinduzi (CCM) na kuitaka ihakikishe inatekeleza kwa vitendo ilani yake inayosisitiza wananchi kuwezeshwa kiuchumi ili kuondoa matabaka.

Huku akishangiliwa na wafanyabiashara hao, Lowassa ambaye aliongozana na baadhi ya makada wa CCM kutoka ndani na nje ya Mwanza, alisema kila mwananchi wa Tanzania lazima ale, ingawa kwa namna tofauti.

Alisema kuwa ili amani iwepo nchini, lazima Jeshi la Polisi na wafanyabiashara wakubwa wawathamini wafanyabiashara wadogo.

“Tunataka tuwasaidie hawa vijana wetu, maana ni nguzo kubwa sana katika maendeleo ya taifa. Ilani ya CCM inasema lazima watu wawezeshwe kiuchumi.

“Kwa maana hiyo katika nchi yetu kila mtu lazima ale. Na kula kwenyewe tunatofautiana, huyu anakula mkate na huyu anakula hiki. Na ili amani iwepo lazima RPC au OCD na wafanyabiashara wawathamini machinga,” alisema Lowassa.

Pia alitahadharisha kuwa endapo wafanyabiashara hao wadogo watadharauliwa katika nchi, lazima watakula sahani moja na matajiri.

Alitumia pia fursa hiyo kukanusha tuhuma dhidi yake kwamba amejilimbikizia mali.

“Wapo baadhi ya watu wanasema hela ninazotoa hizi ni zangu. Mimi sina fedha, ninazotoa ninapewa na marafiki zangu. Mimi si tajiri wa fedha, ila ni tajiri wa marafiki na ushawishi ninao,” alitamba.

Katika hatua nyingine, Lowassa alikataa kuulizwa maswali na wamachinga hao akisema ameandaa kamati itakayoratibu harambee ya kuwachangia kwa lengo la kupata sh bilioni moja.

“Kwa maandalizi ya harambee nitakayorudi tena kuifanya, na ili mjue kwamba nipo makini natoa hundi ya sh milioni 10 na milioni 10 nyingine nitaitoa leo hii,” alisema Lowassa ambaye baadaye aliondoka kwa kutembea kwa miguu hadi Mwanza Hotel.

Chanzo - Tanzania Daima