This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Monday, March 25, 2013

KAULI YA RAIS KIKWETE KUHUSU UCHAWI KWENYE SOKA LA TANZANIA


Moja kati ya kauli ambazo zimeingia kwenye headlines za michezo kwa wiki iliyokwisha ni kauli ya President Jakaya Kikwete, kauli kuhusu ushirikina kwenye soka la bongo aliyoitoa wakati akizindua uwanja mpya wa club ya soka ya Azam Chamazi Dar es salaam.

  Namkariri akisema “najua mtapata tabu sana mkiwaleta hapa watasema kiwanja hiki kina namna, yote ni ushirikina tu…. ni wale ambao hawataki kuwekeza kwenye maendeleo ya mchezo, wanataka kuwekeza kwenye mambo ya kipuuzi… we tangu lini uchawi ukacheza mpira? ingekua uchawi unacheza mpira Afrika ingekua ina kombe la dunia na hatunyang’anywi, nyie hamjajua kwamba jambo hili la kipuuzi? mnawekeza pesa nyingi kwenye kamati ya ufundi hakuna chochote, haiwafikishi kokote”

  Rais aliongeza  kwa  kusema “wekeza kwa kocha mzuri, vifaa vizuri, mafunzo mazuri, wachezaji walale mahali pazuri, Uwanja wa Azam Complex ni mzuri na wa kisasa, kuna sehemu ya mazoezi, vijana wanalala sehemu nzuri… ndio maana naamini nyinyi hakuna sababu ya kutofanikiwa"

AFYA YA KIBANDA ALIYETOBOLEWA JICHO YAANZA KUIMARIKA


Hope all is well.
Salamu nyingi saaana toka JBG!
I could not resist! Yes I cried! But Absalom is the same person I knew last two months! Amesimama! Mungu ni Mwema!!!
Anaomba watanzania wamwombee na amesema anaendelea vizuri kwa sasa…

BINTI MIAKA 7 ABAKWA NA KUHARIBIWA VIBAYA




BINTI wa miaka saba  amefanyiwa ufirauni wa kutisha baada ya kijana mmoja wa kiume aliyetambulika kwa jina moja la Justin kudaiwa kumuingilia kimwili na kumharibu vibaya sehemu za siri kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.
 
Akisimulia mkasa huo wa kusikitisha, binti huyo anayesoma darasa la pili katika shule moja iliyopo Sanawari jijini hapa, alisema kuwa mara ya kwanza alipelekwa nyumbani kwa mwanaume huyo na msichana mmoja ambaye kiumri ni mkubwa kuliko yeye .

“Alikuwa ananipa pipi kisha ananipaka mafuta na kuni… (anaeleza alichokuwa anafanyiwa). Mara kwa mara alikuwa ananisubiri njiani ninapotoka shuleni na kunipeleka chumbani kwake,” alisema binti huyo mdogo kwa masikitiko.





 Mwanaume mmoja aliyekuwa miongoni mwa walioshtukia mchezo huo, amesema baada ya majirani kumuona mtoto huyo akiingia mara kwa mara kwenye chumba cha Justin anayesoma kidato cha nne kwenye shule moja ya sekondari jijini hapo, walienda kumtonya mama yake anayemlea mtoto huyo peke yake baada ya mumewe kuoa mke mwingine.

“Mama yake alipomchunguza mwanaye, alishtuka sana kwa jinsi alivyokuwa ameharibika, akampeleka hospitali ambapo daktari alimchukua vipimo na majibu yalipotoka, ilithibitika kuwa ni kweli mtoto huyo amekuwa akifanyiwa ukatili huo kwa kipindi kirefu.


Baada ya taarifa hizo kulifikia jeshi la polisi, kijana huyo alikamatwa na kupelekwa kwenye Kituo cha Polisi cha Mjini Kati alikofunguliwa kesi.


 Hata hivyo, katika hali iliyozua utata, Justin alitolewa kinyemela kituoni hapo na baadaye ikadaiwa kuwa wazazi wa binti huyo na wazazi wa Justin, walifikia makubaliano ya wazazi wa mtuhumiwa kulipa kiasi cha shilingi laki saba kama fidia.

ISHA MASHAUZI AKIRI KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA


STAA wa muziki wa taarab na mkurugenzi wa Mashauzi Classic, Aisha Ramadhan ‘Isha Mashauzi’ ameibua gumzo na kushangaza mashabiki baada ya kukiri kuwa yeye ni mtumiaji wa pombe kali na madawa ya kulevya aina ya mirungi

Ishu hiyo ilijiri Alhamisi ya wiki iliyopita wakati akihojiwa na mtangazaji wa Redio Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’ kupitia kipindi chake cha Mitikisiko ya Pwani ambapo alisema mirungi na pombe kali ndiyo starehe yake kwani inampa stimu kabla hajapanda jukwaani na katika maisha yake ya kawaida nje ya usanii.

Mashauzi alifunguka hayo baada ya Dida kumtaka atoe ufafanuzi juu ya skendo ya kuvuta bangi inayomkabili ambapo alisema siyo kweli kwamba anavuta bangi ila akakiri kuwa anakula sana mirungi na kugida ulabu. Aliongeza kwamba kwa kuwa hana mume, mtoto wala hataki kuwa na familia, mirungi na pombe ndiyo vitu vinavyompa furaha maishani mwake.


CHID BENZ " AMCHAPA MAKOFI " NGWAIR


Mkali wa vina na mashairi kutoka pande za Ilala anayefahamika kwa jina maarufu la 'Chid Benz' ameanza kupata sifa mbaya baada ya kumpiga mwanamuziki mwenzake 'Ngwea' nje ya ukumbi wa  Ambassador Lounge ulioko kwenye jengo la Benjamini Mkapa tower Posta usiku wa kuamkia Machi 22.

Kupigwa kwa
'Ngwea' kulikuja baada ya 'Chid' kumzingua 'Dully' alipokua akiingia ambapo mwisho wake aliamua kuondoka.
 
 Alipoondoka 'Dully', 'Ngwea' akamuuliza inakuaje unamzingua kubwa lao, ndipo 'Chid' alipopaniki na kuanza kutoa lugha chafu huku akitaka kutokumsikiliza 'Ngwea', inasemekana 'Ngwea' aliamua kukaa kimya lakini 'Chid' aliendelea kungea kwa hasira na kusema "ndio nimemzingua kwani yeye nani" na kumbadilikia 'Ngwea'.
 
'Ngwea' aliamua kuondoka kwenye ukumbi huo lakini alipofika chini ya ghorofa ndipo 'Chid' alipomfuata na kuanza kumshambulia mwanamuziki mwenzake huyo na baadaye kumjeruhi kwa chupa mkononi. 

Lakini baada ya hapo 'Ngwea' aliweza kufika hospitali na kuweza kupatiwa matibabu ya jeraha hilo la chupa.

JAMABAZI SUGU LAUWAWA KWA KUPIGWA RISASI MLIMA NYOKA JIJINI MBEYA



Mwili wa Jambazi sugu  Emanuel Blasius Mdendemi ukiwa umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa Mbeya

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya  Diwani akiangalia mwili jambazi lililouwawa na kikosi cha polisi Mbeya



Baadhi ya polisi na waandishi wa habari wakiwa nje yajengo la kuhifadhia maiti katika hospitali ya rufaa Mbeya

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika Mkutano alioufanya na waandishi wa Habari Ofisini kwake ambapo alisema tukio hilo lilitokea  jana majira ya Saa 10(kumi) Alfajiri

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani akionyesha baadhi ya siraha alizokutwanazo jamabazi huyo aliyeuwawa



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani akionyesaha hirizi iliyofungwa katika bunduki aliyokuwa anatumia jambazi huyo kama kinga katika matukio yake 

Hii ndiyo hirizi iliyofungwa katika bunduki aliyokuwa anatumia jamabazi huyo jamani waganga wakienyeji acheni hizo kuwadanganya watu matokeo yake ni kuongeza uhalifu nchini hakika nao tutawashughulikia kwani wamekuwa chanzo cha uhalifu nchini hayo yamesemwa na kamanda Diwani





Kamanda Diwani akiongea na waandishi wa habari

MTU mmoja ambaye anasadikiwa kuwa ni jambazi ameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Jeshi la Polisi akiwa kwenye harakati za kuteka magari katika Eneo la Mlima Nyoka Jijini Mbeya baada ya kutokea kwa majibizano ya kurushiana risasi.
  
Jambazi huyo ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Polisi Mkoani hapa akituhumiwa kuhusika na mauaji ya Askari Polisi mwenye namba G 68 PC Jafari yaliyotokea  Februari 6, Mwaka huu  katika eneo la Matundasi Wilayani Chunya.
  
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika Mkutano alioufanya na waandishi wa Habari Ofisini kwake ambapo alisema tukio hilo lilitokea  jana majira ya Saa 10(kumi) Alfajiri .
  
Kamanda Diwani alisema kabla ya tukio majambazi wapatao wanne  tayari walikuwa wameweka mawe barabarani kwa nia ya kuteka magari ili wafanye uporaji katika eneo hilo la Mlima Nyoka ambalo limekuwa na matukio kadhaa ya watu kuporwa mali zao.
  
Alisema Jeshi la polisi baada ya kupata habari za kutegwa mawe, askari walifika kwa wakati kwa kuwa polisi walikuwa jirani na eneo hilo na kuweka mtego kwa kuwa majambazi hawakuwa wameonekana kwa wakati ule.
  
Aliongeza kuwa baada ya muda majambazi walipoona taa za gari walijitokeza tayari kushambulia lakini kabla ya hapo polisi walitoa amri ya kujisalimisha kinyume chake wakaanza kupiga risasi ovyo ndipo mashambulizi ya polisi yakafanywa.
  
Diwani alisema katika mapambano hayo alijeruhiwa jambazi mmoja kwa risasi kiunoni na ubavuni kulia na wengine watatu walifanikiwa kutoroka ambapo Marehemu alipowahishwa hospitali kwa matibabu daktari alibaini kuwa amekwisha fariki.
  
Alisema  jambazi huyo alikutwa na silaha moja SMG yenye namba  AB huku namba  nyingine zikiwa zimefutwa na magazine yake ikiwa na risasi ishirini na mbili (22) pamoja na mapanga mawili([2).
  
Aliongeza kuwa baada ya  Marehemu kufanyiwa upekuzi maungoni mwake jambazi huyo alikutwa na kitambulisho cha mkazi chenye namba B.0010453 chenye jina la Emanuel Blasius Mdendemi aliyezaliwa mwaka 1984 eneo la Matamba wilayani Makete Mkoa wa Iringa makazi yake ni Uwemba Mkoani Njombe.
  
“Jambazi huyu amebainika kuwa ni miongoni mwa majambazi waliokuwa kwenye mtandao wa majambazi uliokamatwa hivi karibuni kuhusiana na matukio waliyofanya Mikoa mbalimbali ikiwemo Mbeya,Njombe na Iringa.aidha amebainika kushiriki katika tukio la mauaji ya askari polisi PC Jafari wa kituo cha Mkwajuni – Chunya tarehe 06.02.2013.” Alisema Kamanda Diwani.
  
Aliongeza kuwa  ufuatiliaji wa majambazi waliotoroka unaendelea kufanywa ambapo pia  anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za wahalifu hao azitoe bila kuchelewa kwa jeshi la polisi ili zifanyiwe kazi.

Pia  amewatahadhalisha majambazi na wahalifu wa makosa yeyote kuachana na uhalifu kwa kuwa ni biashara isiyo na faida badala yake wafanye shughuli halali kupata maendeleo ambazo fursa zake ni nyingi.

"SIKUONA HAJA YA KUFIKIRIA MARA MBILI KUMSAIDIA KAJALA MILIONI 13 ILI ATOKE SEGEREA"...WEMA SEPETU AFUNGUKA


Mrembo Wema Sepetu leo amemake headline baada ya kutoa mfukoni mwake shilingi milioni 13 kulipa faini aliyopigwa muigizaji mwenzie Kajala Masanja aliyehukumiwa leo kwenda jela miaka mitano ama kulipa kiasi hicho cha fedha.
Kajala na Wema wakikumbatianaKajala na Wema wakikumbatiana
Akiongea  kwa  kujiamini, Wema amesema hakufikiria mara mbili kutoa kiasi hicho cha fedha.

“Kusema kweli wanasemaga kwamba kutoa ni moyo so naamini what I did is best, nimetoa kwasababu I had to do it and sikuthink twice kuhusu kufanya hivyo,” amesema Wema.
Wema akwa na KajalaWema akwa na Kajala
“Nimefanya kama namsaidia rafiki yangu kama namsaidia ndugu yangu na sidhani kama ingekuwa ni kitu kizuri kumuona mwenzako anaingia kwenye dhahama, kwenye tabu, kwenye mateso na wakati nina uwezo wa kumsaidia kwahiyo I just did what I had to do.”

Kuachiwa kwa Kajala kumepokelewa kwa furaha kubwa na mastaa mbalimbali nchini.

Cpwaa

So I hear Kajala is out! Good news..Hongereni sana wana BOngoMovies! Bongoflava tujipangeni..tutaendelea kupigwa bao kila siku while we are sitting on a Multi-Billion Industry, it’s time to stop fantasizing posing in front of camera poppin bottles of Champagne,Rented Fancy cars,Cheap Wardrobe n ( No..The Ladies are fine,I love them too sitaki ubaguzi)… Tufikirie kibiashara zaidi na sio sifa tu.

Rio Pol

It’s a blessed Monday I say this because finally someone stood up and did something right and righteous. I’ve worked in the entertainment industry for the past seven years and no star or their glam team or entourage would do what Miss Wema Abraham Sepetu did. Thank you god both my girls Elizabeth Michael and Kajala Masanja are free. God bless you wema.
Kajala akikumbatiana na ZamaradiKajala akikumbatiana na Zamaradi
Mboni Masimba
KAJALA outtttttttttt# Mungu mkubwa # WEMA mwokozi wa KAJALA # Mwenyez Mungu akuzdishie na akupe ulipo pungukiwa. Una moyo wa pekee. Lov u always my Dogo