This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Friday, July 26, 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWA WILAYANI MULEBA

Rais Kikwete akivikwa skafu na skauti baada ya kuwasili Muleba.

Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wageni.…

Rais Kikwete akivikwa skafu na skauti baada ya kuwasili Muleba.
Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wageni.
Rais Kikwete akisalimiana na mama wa Profesa Anna Tibaijuka.
Waziri wa Ardhi Profesa Anna Tibaijuka akishiriki katika ngoma ya utamaduni wakati wa mapokezi ya Rais Kikwete wilayani Muleba.
Wananchi wa Muleba wakimshangilia Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipowasili wilayani humo akiwa katika ziara yake ya siku sita Mkoani Kagera.
Rais Kikwete akiongea na viongozi wa wilaya ya Muleba baada ya kupokea taarifa ya maendeleo, akiwa na mawaziri watano anaoongozana nao katika ziara hiyo.
Mbunge wa Muleba akitoa  maoni na kero za jimbo lake.
Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe akiwahakikishia viongozi wa Muleba juu ya mipango ya serikali kuleta meli za abiria mpya mbili katika ziwa Victoria.
Rais Kikwete akipata maelezo ya mpango kabambe wa maji wilaya ya Muleba.
Rais Kikwete akizindua mradi mkubwa wa maji wilayani Muleba.
Rais Kikwete akikata utepe kuzindua mradi wa maji.
Rais Kikwete akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa wananchi wa Muleba baada ya kuzindua mradi mkubwa wa maji kwa wilaya hiyo.
Mwananchi mwingine akitwishwa maji.
Ngoma ya utamaduni ikimlaki Rais Kikwete alipowasili katika mkutano wa hadhara.
Rais Kikwete akisalimia wananchi.
Rais Kikwete akiangalia mazao yatokanayo na uzalishaji mbegu ya kampuni ya Itente ya Muleba.
Rais Kikwete akipozi na wafanyakazi wa kampuni ya uzalishaji mbegu ya Itente.
Rais Kikwete akifurahia ngoma.
Umati wa wananchi Muleba ukimsikiliza Rais Kikwete.
Rais Kikwete akiongea na wananchi wa Muleba.
Rais Kikwete akihutubia wana Muleba.
Sehemu ya umati mkutanoni.
Rais Kikwete akiendelea kungea na wananchi.
Umati  katika mkutano wa hadhara.
Umati katika mkutano wa hadhara.
Rais Kikwete akijiunga na waumini wa Muleba kusali swala ya Magharibi kabla ya kufuturu.
Dua ikisomwa baada ya futari aliyoandaa Rais Kikwete kwa wananchi wa Muleba.
Dua ikiombwa baada ya futari.
Dua.
Wananchi wa Muleba katika futari aliyoandaa Rais Kikwete wilayani Muleba.

ALIYETIMULIWA KANIKASI AKIWA NA VAZI LA NUSU UCHI ADAI KUWA KANISA LIMEMUONEA, WALIMSUKUMA AKAANGUKA NA WAMEHARIBU VIATU VYAKE VYA "UINGEREZA"..!!!


 
Wakati mwanamke wa kivazi kilichositisha ndoa kanisani kwa dakika kadhaa akidai hakuwa na tatizo kuvaa vile, Katekista wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Peter, Yohane Maboko, amesisitiza kuwa alikiuka maadili ya Kanisa.

Mwanamke huyo ambaye ameendelea kukataa kutaja jina lake, huku njia zingine zikimtaja kwa jina la Restituta Kalemera, alidai juzi kuwa kivazi hicho cha mabega wazi hakikuwa tatizo kanisani, bali ni unyanyasaji tu wa Katekista huyo.

Akizungumza  juzi, alidai kuwa Katekista Maboko alimsukuma na kumwangusha katika ngazi ndefu za Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam.

"Wakati Katekista akinitaka nitoke nje, ghafla alinisukuma nikaanguka kwenye ngazi na kudakwa na mtu mwingine aliyeniokoa, la sivyo ningeumia vibaya," alidai.

Alidai kilichomsikitisha ni kudaiwa kutaka kuingia kanisani akiwa amevaa nguo zilizoacha mwili wazi, jambo ambalo si la kweli, kwa kuwa alikwenda kanisani hapo akiwa na kitambaa kilichofunika mwili.

"Nilipofika kanisani, nilikutana na Katekista akimrudisha mtu mwingine, ghafla alitokea bibi harusi aliyevalia nguo ambazo hazikuruhusiwa kanisani, akaniomba skafu niliyokuwa nayo, nikampa nami kubaki wazi mabegani,"
alidai.

Baada ya kuvua kitambaa hicho, alidai alitaka kuingia kanisani ili kuchukua funguo za gari, lakini alikutana na Katekista kwenye ngazi, ambaye alimwamuru atoke nje naye akaendelea kumsihi kuwa anakwenda kuchukua funguo za gari ndani, hata hivyo hawakukubaliana.

Aliendelea kudai, kuwa Katekista alipomsukuma na kuanguka, baada ya kudakwa alichanganyikiwa akidhani kanisani ni sehemu ya malumbano, akakimbilia ndani kutafakari, huku kiatu chake alichonunua nje ya nchi (Uingereza) kikiwa kimeharibika.

Alidai kuwa akiwa kanisani, Katekista alimfuata tena na kumsihi atoke nje, jambo lililosababisha ndugu zake wamzingire kiongozi huyo wa Kanisa na kumhoji kwa jazba, sababu ya kumsukuma ndugu yao na kuhatarisha maisha yake.

Baada ya malumbano huyo, alitoka nje ya Kanisa na kuacha utaratibu mwingine ukiendelea, huku akilalamika kwamba Kanisa ni sehemu takatifu hivyo hapatakiwi kuwa uwanja wa mapigano na kwamba limeacha kazi ya kufundisha na kuomba ielezwe wazi watu wavae nini.

Akijibu tuhuma hizo, Katekista Maboko alimpongeza mwandishi kwa kushuhudia tukio hilo na kutoa habari yake na kuongeza kuwa utaratibu wa jinsi ya kuingia kanisani kwa maharusi, umekuwa ukifundishwa tangu kuandikishwa kwa ndoa hadi mafundisho ya ndoa.

Alisema dada huyo alipofika kanisani hapo, alikuwa na wanawe wawili waliokuwa na mavazi yaliyoacha sehemu za miili yao wazi, na aliwaelewesha lakini yeye akabisha.

"Niliwashika mikono na kuwapeleka uliko ubao ili wasome maelekezo ya kinachotakiwa kuvaliwa, lakini yeye alilazimisha kuingia huku akisema Mungu haangalii mavazi, bali roho," alisema Katekista Maboko na kuongeza kuwa wakati akieleza hayo, ndipo wanandugu walipofika na kumhoji.

Kuhusu miwani yake kuvunjwa, alisema wakati akiwa amezungukwa na watu kama 30 kwa lengo la kumchanganya, aliendelea kujenga hoja kuwa kanisani zipo taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa, lakini mmoja wao alitumia nguvu na kuvunja miwani hiyo.

Hata hivyo, alisema mtu huyo aliomba samahani na kulipa kiasi cha fedha, ambapo walipeana mikono kama ishara ya kusameheana.

Katekista Maboko alisema kwa ufupi kilichotokea, ni kukosekana kwa busara kwa waumini hao, kwani vipo vibao vinavyotoa maelekezo juu ya utaratibu unaotakiwa na unaopaswa kufuatwa.

MWANAMKE E ALIYEPANGA KUMUUA MUMEWE AFIKISHWA MAHAKAMANI HUKO ARUSHA



Mwanamke anayedaiwa kupanga njama za kumuua mumewe wa ndoa na mtoto wa mume huyo, amepandishwa mahakamani akiwa na mtuhumiwa mwingine wa mauaji hayo.

Janeth Jackson (32), mkazi wa Moshono, Arusha na Novatus Elias, walifikishwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha /Arumeru, Devotha Kamuzora, wakisomewa makosa mawili ya kula njama ya kutaka kumuua Simon Jackson ambaye ndiye mume wa Janeth.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Edna Kasala, alidai mahakamani hapo kuwa washtakiwa wote walitenda kosa la pili la kula njama na kutaka kumuua Desderi Sabas, ambaye ni mtoto wa mke mwingine kwa mume huyo anayeishi Bukoba, mkoani Kagera.


Washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu lolote kwa sababu Mahakama hiyo kisheria haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji.


Kasala iliomba mahakama kuwanyima dhamana washtakiwa, kwa sababu watuhumiwa wengine wawili wanatafutwa hivyo na upelelezi haujakamilika.


Alidai kutokana na uzito wa tuhuma hizo, maombi hayo ya kuwanyima dhamana washtakiwa yameambatana na hati ya kiapo ya Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha.


“Mheshimiwa tunafahamu kwamba dhamana ni haki ya washtakiwa kikatiba, lakini kutokana na mazingira ya kesi hii kuwa magumu, tunaomba dhamana isitolewe ili kuwatafuta watuhumiwa wengine wa kesi hii,” alidai Kasala.


Kwa upande wake,Wakili wa utetezi, Fidelis Peter, alipinga maombi hayo na kutaka mahakama itoe dhamana kwa washtakiwa kwa sababu ni haki yao ya kikatiba na kwamba hilo ni kosa lao la kwanza.


Sababu nyingine ya kupinga maombi ya upande wa mashtaka, ni kwamba washtakiwa wanaweza kuvuruga upepelezi wakiachiwa siyo za msingi kwani ni watu wanaoaminika katika jamii.


“Mheshimiwa sababu za kuwanyima dhamana washtakiwa hazina uzito wowote, pia mshtakiwa wa kwanza (Janeth) ana mtoto wa miezi sita na tangu akamatwe alhamisi iliyopita hajamwona wala kumnyonyesha hivyo anastahili kupewa dhamana,”alidai Wakili Peter.


Hata hivyo, baada ya kusikiliza maombi ya pande zote mbili, Hakimu Kamuzora, alikubaliana na maombi ya upande wa mashtaka na kuamuru watuhumiwa wapelekwe mahabusu hadi Agosti 5, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.


Katika kesi hiyo iliyovuta hisia za watu wengi jijini hapa, inadaiwa Janeth alitaka kumuua mumewe ambaye ni mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite na mwanaye wa kiume, ili arithi mali na utajiri alionao mfanyabiashara huyo.

Akiwa amejifunika uso muda wote alipokuwa mahakamani, Janeth alionekana kuwa na mawazo mengi na macho mekundu kwa sababu ya kulia baada ya njama hizo kugonga mwamba.


Awali kabla ya kukamatwa kwa mwanamke huyo, taarifa zilieleza kuwa, mwanamke huyo alitumia fedha nyingi kulipa majambazi waliotakiwa kutekeleza tukio hilo lakini mmoja wa majambazi hao aliamua kuvujisha siri hiyo polisi iliyofanikisha kukamatwa kwa wahusika kabla ya kutenda mauaji hayo.

Mume wa mwanamke huyo alinukuliwa awali akisikitika na kuhoji kwa nini mke huyo alifikia kupanga hilo.

VAI WA UKWELI AMTAKA MUME WA AUNT EZEKIE


KATIKA hali isiyo ya kawaida msanii anayechipukia katika filamu za Kibongo, Isabella Fransis ‘Vai wa Ukweli’ anamtafuta ubaya gwiji katika tasnia hiyo, Aunt Ezekiel kwa kusema anamtamani mumewe.
Isabella Fransis ‘Vai wa Ukweli’.
Vai wa Ukweli bila ya kupindisha maneno amedai kuwa hapati usingizi kutokana na kumzimia Sunday Demonte ambaye ni mume wa Aunt.

Akizungumza na mwandishi wetu, Vai alisema ili kuonesha kuwa anachokisema kinatoka moyoni mwake, amekata vipande vya picha za Dimonte na…
Na Imelda Mtema
KATIKA hali isiyo ya kawaida msanii anayechipukia katika filamu za Kibongo, Isabella Fransis ‘Vai wa Ukweli’ anamtafuta ubaya gwiji katika tasnia hiyo, Aunt Ezekiel kwa kusema anamtamani mumewe.
Isabella Fransis ‘Vai wa Ukweli’.
Vai wa Ukweli bila ya kupindisha maneno amedai kuwa hapati usingizi kutokana na kumzimia Sunday Demonte ambaye ni mume wa Aunt.
Akizungumza na mwandishi wetu, Vai alisema ili kuonesha kuwa anachokisema kinatoka moyoni mwake, amekata vipande vya picha za Dimonte na kuvibandika chumbani kwake.
“Kusema ukweli nampenda sana Sunday na sijaanza kumpenda leo wala jana kwani namfahamu tangu zamani alipokuwa Kariakoo,” alisema Vai.
Aunt Ezekiel.
Msanii huyo chipukizi alisema anamuonea wivu Aunt kwa kuamini kuwa anafaidi sana kwa kuwa na mwanaume huyo.
Kwa upande wake Aunt alishangazwa na taarifa hizo na akaomba atafutwe baada ya kumalizika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili ajue cha kufanya.
“Haya mambo ni makubwa jamani, sijawahi kusikia mtu akimpenda mume wa mtu na kusema hadharani, lakini ngoja nimalize Ramadhani, nitamtafuta aniambie vizuri,” alisema Aunt. Dimonte ni mume wa Aunt ambaye kwa sasa anaishi Duba

DANGURO LA MAKAHABA LAFUMULIWA


 Hili ni sakata la  kikongwe mmoja anayedaiwa kumiliki idadi kubwa ya madanguro katika uwanja wake na kuwapangisha makahaba katika eneo maarufu kwa jina la Kijiji cha Makahaba.


Mwandishi wetu alipokea ujumbe mfupi ulioelezea ufuska unaofanywa na mabinti ambao hupewa eneo na kujenga vibanda kisha kujiuza kwa bei chee katika kijiji hicho maeneo ya Kigamboni jijini Dar.


Bada ya simu hiyo, uchunguzi wetu  ulibaini kwamba, eneo hilo linalofanyiwa ufuska huo linamilikiwa na kikongwe aliyejitambulisha kwa jina la mzee Matutu akidaiwa kuendesha maisha kwa biashara hiyo ya madanguro.
 
Baada ya kujiridhisha na uchunguzi kuwa ni kweli jambo hilo linafanyika eneo hilo,waandishi walivamia eneo la tukio wakiwa na mjumbe wa mtaa huo aliyefahamika kwa jina la Abbas na kujionea madanguro yaliyojengwa kwa mstari ambapo milango yake iliachwa wazi huku ndani wakionekana mabinti wakiwa wamejilaza kihasarahasara wakiwatega wateja wanaopita katika mtaa huo.
 
Madanguro hayo ambayo kwa hesabu ni takriban kumi na nane, yamejengwa kwa aina yake ambapo mengi kati ya hayo yana ukubwa wa kutosha kuingia kitanda kidogo pekee.

 
Baada ya kujionea hayo, kikosi kazi sambamba na mjumbe huyo kilimtafuta mzee Matutu na kufanikiwa kuzungumza naye kuhusu madanguro hayo na namna anavyoyaendesha ambapo alikiri kuwa yeye ni mmiliki wa eneo hilo na huwa anapokea shilingi 30,000 kwa mwezi kwa kila mwanamke na fedha hiyo ndiyo inayomsaidia kuendesha maisha.

“Sina kazi nyingine ya kuniingizia kipato zaidi ya hii ya wasichana licha ya kwamba sijawaruhusu wafanye biashara hiyo. Fedha hiyo ndiyo inanisaidia kwa mahitaji yangu,” alisema kwa tabu mzee Matutu huku akimtaja msimamizi wa madanguro hayo kuwa ni mpwa wake.
 Kwa upande wake mjumbe wa mtaa huo, Kassim alisema kuwa serikali ya mtaa imejitahidi kwa kadiri ilivyoweza kuwaondoa mabinti hao lakini wamekuwa wakirudi kila mara.

Alipoulizwa hatua waliyoichukua kwa mmiliki wa madanguro hayo ambaye ni mzee Matutu, kiongozi huyo alibakia kusikitika asijue hatua gani ya kumchukulia mzee huyo ambaye hata wakimpeleka kwenye vyombo vya sheria anahisi itakuwa ni uonevu kwa kuwa hana msaada mwingine wa kifedha zaidi ya fedha kutoka kwa mabinti hao.

HII NDO HALI HALISI YA MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTER ALIYEMWAGIWA TINDIKALI


MFANYABIASHARA maarufu na Mmiliki wa maduka ya Home Shopping Center (HSC), Said Mohamed Saad, ambaye wiki iliyopita alimwagiwa tindikali maeneo ya Msasani City Mall, jijini Dar es Salaam, sasa yuko Afrika Kusini kwa matibabu zaidi. 


Wiki iliyopita majira ya saa moja jioni, mfanyabiashara huyo alimwagiwa tindikali na mtu mmoja ambaye hakufahamika na mara baada ya kutenda tukio hilo, mhusika alikimbia huku mlinzi wa eneo hilo akijaribu kumkimbiza pasipo mafanikio baada ya kuteleza na kuanguka.

 Hatua hiyo ilitoa mwanya kwa mtuhumiwa kutoroka eneo la tukio kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki. Hapo awali ilidaiwa kuwa Saad alikuwa anaweza kuzungumza japo amefungwa mashine sehemu ya pua kwa ajili ya kumsaidia kupumua.

 Matukio ya watu kumwagiwa tindikali yameonekana kushamiri nchini katika siku za hivi karibuni.

 Tukio la kumwagiwa tindikali mmiliki huyo wa Home Shopping Centre, limekuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Said Juma Makamba naye ajeruhiwe vibaya usoni kwa kumwagiwa maji maji yanayosadikiwa kuwa ni tindikali majira ya usiku akiwa nyumbani kwake