This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Friday, February 28, 2014

Benki ya Dunia yaisimamishia Uganda msaada

S_77135.png
Benki ya dunia imesitisha mkopo wa dola milioni 90 kwa Uganda wa kuimarisha sekta ya afya kufuatia kupitishwa kwa sheria inayoharamisha ushoga na kutoa adhabu kali kwa watakaopatikana na hatia
Hatua hiyo ya benki ya dunia haikutarajiwa na wengi kwani taasisi hiyo mara nyingi hujiepusha kuingilia masuala ya ndani ya kisiasa ya nchi wanachama au kuhusiana na masuala kama haki za mashoga, kuepuka kuzishurutisha nchi wanachame wake 188.
Hata hivyo msemaji wa benki hiyo David Theis amesema katika barua pepe kuwa wamesitisha mradi huo wa kuboresha sekta ya afya ya Uganda hadi watakapoufanyia tathmini na kuhakikisha malengo yake ya maendeleo hayataathiriwa na sheria hiyo mpya ya kuharamisha ushoga.
Rais wa benki hiyo Jim Yong Kim amewatumia wafanyakazi wake barua akisema benki ya dunia inapinga ubaguzi na itawalinda wafanyakazi wake wote na kuongeza kupitishwa kwa sheria hiyo ya Uganda sio nchi ya kwanza kufanya hivyo kwani ushoga umeharamishwa katika nchi 83 na zaidi ya nyingine 100 zinawabagua wanawake.
Mkopo ulikuwa uimarishe sekta ya afya
Licha ya kusimamishwa kwa mkopo huo wa dola milioni 90,benki ya dunia bado ina miradi mingine nchini Uganda ya kiasi cha dola bilioni 1.56. Mkopo huo ulitarajiwa kuidhinishwa hapo jana na ulipaswa kuangazia miradi ya kuboresha afya ya uzazi,afya ya watoto wachanga na uzazi wa mpango
Kutiwa saini kwa sheria hiyo ya kuharamisha ushoga Uganda na Rais Yoweri Museveni mapema wiki hii kumeibua shutuma kali kutoka kwa nchi za magharibi na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Norway,Denmark na Uholanzi zimetangaza kuwa zitasitisha misaada kwa serikali ya Uganda kutokana na sheria hiyo na nchi nyingine wafadhili ikiwemo Marekani pia zimetishia kusitisha misaada na kutafakari upya uhusiano kati yao na Uganda.
Ghadhabu hiyo ya nchi za magharibi kuhusu kuharamishwa kwa ushoga ambayo adhabu yake ni kifungo cha maisha gerezani kwa watakaokutikana na hatia imeporomosha thamani ya shilingi ya Uganda na kusababisha Benki nchini humo kuingilia kati kwa siku mbili mfululizo
Kutiwa saini kwa sheria hiyo ya kuharamisha ushoga Uganda na Rais Yoweri Museveni mapema wiki hii kumeibua shutuma kali kutoka kwa nchi za magharibi na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
Norway,Denmark na Uholanzi zimetangaza kuwa zitasitisha misaada kwa serikali ya Uganda kutokana na sheria hiyo na nchi nyingine wafadhili ikiwemo Marekani pia zimetishia kusitisha misaada na kutafakari upya uhusiano kati yao na Uganda.
Ghadhabu hiyo ya nchi za magharibi kuhusu kuharamishwa kwa ushoga ambayo adhabu yake ni kifungo cha maisha gerezani kwa watakaokutikana na hatia imeporomosha thamani ya shilingi ya Uganda na kusababisha Benki nchini humo kuingilia kati kwa siku mbili mfululizo
Serikali ya Uganda haina wasiwasi
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Uganda Ofwono Opondo amesema Uganda inaweza kujiendeleza bila ya misaada kutoka nchi za magharibi na kuongeza Uganda haina wasiwasi na hatua hizo kwani ni wakati kwa Afrika kupinga ukoloni, utumwa na ubabe kutoka magharibi.
Mwanaharakati ambaye amekuwa katika mstari wa mbele kuwatetea mashoga nchini Uganda Frank Mugisha alikutana na maafisa wa ngazi ya juu wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani mjini Washington hapo jana kuomba usaidizi utakaowalinda mashoga.
Ofisi ya kutetea haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa umelaani kuchapishwa kwa majina ya watu wanaodaiwa kuwa mashoga nchini Uganda katika gazeti moja la udaku nchini humo na kuonya hatua hiyo inakiuka haki ya kuwa na faragha na kuonyesha wazi kuwa maisha ya mashoga yamo hatarini.
Kiongozi wa upinzani Uganda Kizza Besigye ameishutumu serikali kwa kutumia suala hilo kuwahadaa raia wa nchi hiyo ili wasiangalie masuala muhimu kama ufisadi au kuwepo kwa jeshi la Uganda Sudan Kusini.(E.L)

BANZA: NILIANZA SIGARA, BANGI, UNGA ILA SASA…

MWIMBAJI mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ amefunguka mazito juu ya matumizi mabaya ya bangi na madawa ya kulevya ikiwa ni pamoja na jinsi alivyokuwa akiyatumia.
Akizungumza kupitia Kipindi cha Mtu Kati cha Global TV Online mwanzoni mwa wiki hii, Banza alikiri kutumia madawa ya kulevya na kusema; “Nilianza kuvuta sigara ya kawaida, nikaja bangi na baadaye madawa ya kulevya aina ya Heroin ambapo alikuwa akiyatumia kwa…
MWIMBAJI mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ amefunguka mazito juu ya matumizi mabaya ya bangi na madawa ya kulevya ikiwa ni pamoja na jinsi alivyokuwa akiyatumia.
Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ kabla ya kufanya mahojiano na Global TV Online.
Akizungumza kupitia Kipindi cha Mtu Kati cha Global TV Online mwanzoni mwa wiki hii, Banza alikiri kutumia madawa ya kulevya na kusema; “Nilianza kuvuta sigara ya kawaida, nikaja bangi na baadaye madawa ya kulevya aina ya Heroin ambapo alikuwa akiyatumia kwa kuchanganya na sigara au bangi.
“Ujana ulisababisha nikajiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya ila sasa nimeacha kabisa na nawashauri vijana wenzangu kuwa mbali na kilevi hicho kwani kama huna kipato cha kutosha unaweza kugeuka kibaka maana mwili ukizoea ni vigumu kuacha.”

Real Madrid yaisulubu Schalke 04

ronaldo_8e1ea.jpg
Na Fadhy Mtanga
REAL Madrid imejihakikishia kucheza robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya kuitandika Schalke 04 ya Ujerumani mabao 6-1. Mchezaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo, mchezaji aliyevunja rekodi ya usajili ulimwenguni Gareth Bale pamoja na mchezaji mahiri Karim Benzema walihakikisha kila mmoja wao anatupia nyavuni magoli mawili ili kuifanya Real Madrid, vinara wa ligi kuu nchini Hispania, kuisulubu vilivyo Schalke 04 tena kwenda dimba lake la nyumbani, Veltins-Arena. Bao la kufutia machozi la Wajerumani hao lilifungwa na Klaas Jan Huntelaar katika dakika ya 90.
Alikuwa Karim Benzema katika dakika ya 13 tu alipopokea mpira kutoka kwa Cristiano Ronaldo na kuutumbukiza wavuni kama ishara ya ufunguzi rasmi wa karamu ya magoli ya miamba hao wa soka nchini Hispania. Kisha, panapo dakika ya 21, mchezaji aghali zaidi aliyesajiliwa kutoka Tottenham Hotspur ya Uingereza, Gareth Bale akautia mpira kimiani baada ya kupokea pasi kutoka kwa Karim Benzema.

Mwamuzi Howard Webb, anayetajwa kuwa mwamuzi bora zaidi duniani kwa sasa alipopuliza kipenga kuashiria mapumziko, Real Madrid wakarejea vyumba vya mapumziko wakiwa tayari na magoli mawili nunge.

Timu hizo ziliporejea dimbani kwa ngwe ya mwisho, ilimchukua Cristiano Ronaldo dakika saba tu kuibadili pasi kutoka kwa Gareth Bale kuwa goli la tatu. Dakika tano baadaye, dakika ya 57, Karim Benzem akafungua awali ya pili ya ufungaji kwa wasukuma ndinga hao machachari alipofunga bao la nne dhidi ya Schalke 04. Kama ilivyo kanuni ya hesabu za pythagoras, Karim alifunga goli hilo kwa kupata usaidizi kutoka kwa yule yule aliyempa pasi awali, Cristiano Ronaldo.

Dakika ya 69 ya mchezo, ikawa zamu tena ya Gareth Bale kuutia mpira wavuni baada ya kupokea pasi nzuri ya Sergio Ramos. Ubao wa matokeo ukasoma Schalke 04 0 Real Madrid 5. Matokeo hayo yalidumu kwa dakika 20 tu kwani panapo dakika ya 89 ya mchezo krosi ya Karim Benzema ikamfikia Cristiano Ronaldo. Naye hakufanya ajizi, akaitia wavuni na kuwafanya mashabiki wa Real Madrid kote ulimwenungi kushangilia kwa tambo na kujidai kwa kila namna.

Dakika iliyofuata, Klaas Jan Huntelaar aliyekuwa tayari amelimwa kadi ya njano panapo dakika ya 72, akafunga bao la kuwafutia machozi wenyeji wa mchezo huo.

Kwa matokeo hayo, Schalke 04 inahitaji miujiza ili isonge mbele. Timu hizo zinatarajia kukwaana tena katika mchezo wa pili utakaokimbizwa dimbani Santiago Bernabeu jijini Madrid, Hispania majuma matatu yajayo.

Kwingine barani Ulaya, Galatasaray iliikaribisha Chelsea, vinara wa ligi kuu ya Uingereza. Dakika ya 9 tu ya mchezo huo uliopigwa katika dimba la Turk Telekom, Fernando Torres akaifungia Chelsea goli la kuongoza. Chelsea ikawa timu ya kwanza kutoka Uingereza kufunga goli katika hatua hiyo ya 16 ya michuano ya UEFA. Timu zingine kutoka Uingereza, Machester City, Arsenal na Manchester United ziliambulia kichapo cha magoli 2-0 kutoka kwa Barcelona, Bayern Munich na Olympiakos.

Chelsea iliendelea kuongoza ikiwa ugenini hadi dakika ya 65 pale Aurelien Chedjou alipofunga akisaidiwa na Wesley Sneijer. Matokeo hayo yanaipa ahueni ya goli la ugenini Chelsea. Timu hizo zinatarajia kutimuliana vumbi tena wiki tatu zijazo pale mitaa ya Fulham, London katika dimba la Stamford Bridge.

STEVE NYERERE AMWAGIA SIFA LULU

Stori: Mayasa Mariwata

RAIS wa Bongo Movie Unit, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amemmwagia sifa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuwa ni binti mdogo lakini sasa anajitambua tofauti na wasanii wengine wakubwa.
Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Akipiga stori na Ijumaa Steve alisema kuwa, mbali na umakini katika kazi zake za kisanii, sasa hivi yuko makini sana na maisha yake kiasi kwamba ni nadra sana kumkuta na skendo za kijingajinga.…

RAIS wa Bongo Movie Unit, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amemmwagia sifa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kuwa ni binti mdogo lakini sasa anajitambua tofauti na wasanii wengine wakubwa.
Akipiga stori na Ijumaa Steve alisema kuwa, mbali na umakini katika kazi zake za kisanii, sasa hivi yuko makini sana na maisha yake kiasi kwamba ni nadra sana kumkuta na skendo za kijingajinga.
Steve Nyerere.
“Achilia mbali hao mastaa wote unaowajua wewe, mimi nikiwa kama kiongozi wa Bongo Movie siwezi kusema uongo, namkubali sana Lulu kwani ni binti mdogo na anajitambua na sasa siyo mtu wa kuendekeza mambo ya starehe kama wengine, pia huwezi kumuona viwanja kirahisi, katulia anafanya kazi,” alisema rais huyo.

RED HANDED! NJEMBA AUVAA MTEGO AKIWA NA MKE WA RAFIKI YAKE GESTI

 
MAANDIKO yanasema ‘usitamani mali ya mtu mwigine’! Ni kweli kabisa, onyo hilo lilichukua fursa yake kufuatia njemba mmoja aliyejulikana kwa jina la Anton John Mwaweje kunaswa laivu gesti na mke wa rafiki yake aliyefahamika kwa jina moja la Chalz.

Mke wa mtu sumu: Anton John Mwaweje baada ya kunaswa akiwa na mke wa rafiki yake gesti.
Tukio hilo lilijiri mwanzoni mwa wiki hii kwenye gesti moja maarufu (jina tunalo) iliyopo Buguruni- Malapa jijini Dar es Salaam.
Katika sakata hilo ilidaiwa kuwa, Mwaweje alikuwa akiifahamu vyema familia ya Chalz sambamba na mke wake (jina lipo) lakini hilo hakulijali na kumtokia mke wa Chalz ambaye kwa utamaduni wa Kiafrika ni shemejiye.
Mshangao: Anton John akishangaa baada ya kuba
Habari zikazidi kudai kwamba, ilifika mahali katika kumtaka shemejiye huyo ambaye alikuwa akimkatalia katakata, Mwaweje alitumia gia nyingine ikiwemo ya kumuahidi mambo manono kama angekubali kuivunja amri ya 6 ya Muumba na yeye.
Chanzo cha habari kiliendelea kudai kuwa,  ‘Mungu si Athuman wa Lucas’ siku isiyo na jina jamaa alimtumia ujumbe (SMS) mke wa mwenzake kwa kutumia maneno ya kumtoa nyoka pangoni kumbe muda huo bwana simu alikuwa nayo mwenye mke.
Misosi na mitungi: Baadhi ya misosi na vinywaji vilivyokutwa chumbani humo.
Chalz alimwita mkewe na kumuuliza ni nani aliyemtumia ujumbe huo? Ndipo mke akaanika ukweli akisema:
“Mume wangu, wala usikonde. Aliyetuma ujumbe huo si mwingine, ni Anton…”
Mume:  “(akihamaki) Anton huyuhuyu?”
Mke: “Huyuhuyu mume wangu. Amekuwa akinitaka kimapenzi kwa muda mrefu sana, namkatalia lakini hasikii.”
Za mwizi 40: Bwana Anton John akiwa na pingu mkononi baada ya kunaswa na kamanda wa OFM pamoja na wanausalama.
Pia, mwanamke huyo alimwonesha mumewe meseji kibao ambazo jamaa huyo amekuwa akimtumia na zile ambazo yeye amekuwa akimkatalia.
“Sasa sikia, mkubalie,” mwanaume huyo alimwambia mke wake huku midomo ikimcheza kwa hasira.
Chini ya usimamizi wa mumewe, mwanamke huyo aliwasiliana na Anton na kumwambia alikuwa na nafasi wanaweza kukutana kwa ajili ya kumsaliti Chalz.
Baada ya kupanga mipango ya kukutana, mume huyo alipiga simu Global Publishers kwenye kitengo cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) na kuomba msaada wa fumanizi ambapo alibahatika kukuta kuna kamera mpya zimewasi tayari kwa kazi kama hizo.
Baada ya kupata maelezo ya Chalz, OFM ilishirikiana na Jeshi la Polisi Buguruni –Kwamnyamani jijini Dar na kuandaa mtego ambapo Jumatatu iliyopita, saa nane na ushee mchana, Anton ambaye naye inasemekana ana mke aliuingia mtego na kunasa kwenye chumba namba 5 akiwa na mke mwema huyo.
Ndani ya chumba hicho, Anton alikutwa na boksa  tayari kwa mlo wa wizi ambao alibakia kuendelea kusikia njaa. Mezani, kulikuwa na chipsi kuku na pombe ambazo zingewapa stimu kabla ya mchezo.
Kitendo cha Chalz kumnasa jamaa huyo na mkewe kitandani kilimpandisha munkari ambapo nusura afanye ndivyo sivyo lakini alitulizwa na polisi waliokuwa eneo hilo kwa ajili kulinda usalama.
Kilichofuata baada ya hapo, mgoni huyo akiwa na pingu mkononi alipelekwa kwenye kituo hicho cha polisi ambapo awali, Chalz alitoa ripoti ya malalamiko baada ya kugundua  jamaa huyo anataka kumtumbukiza mkewe kwenye mstari wa usaliti.
Mpaka OFM wanaondoka kituoni hapo, taratibu za kisheria kuhusiana na kesi hiyo zilikuwa zikiendelea huku mgoni huyo akiwa chini ya ulinzi mkali.


WASANII WAZINDUA KAMPEINI KUHAKIKISHA MAPENDEKEZO YAO KIKATIBA YANASIKILIZWA

Wasanii mbalimbali wakifuatilia kuhusiana na katiba iliyokataliwa kusikilizwa.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la sanaa (BASATA), Godfrey Lebejo Mngereza akihutubia wasanii.…
Wasanii mbalimbali wakifuatilia kuhusiana na katiba iliyokataliwa kusikilizwa.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la sanaa (BASATA), Godfrey Lebejo Mngereza akihutubia wasanii.
Wana Hip hop kutoka kushoto, Danny Msimamo, Quick Racka, Profesa Jay, Nikki wa Pili na Kala Pina.
Batuli (kulia) na Monalisa wakiwa katika pozi leo Uwanja wa Vijana, Kinondoni.
Wasanii mbalimbali walikuwepo.
WASANII mbalimbali katika nyanja za sanaa leo wameungana katika ukumbi wa Vijana, Kinondoni  katika kuzindua rasmi kampeni ya kuhakikisha mapendekezo yao kikatiba yanasikilizwa na kupitishwa.
Akizindua kampeni hizo, Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Godfrey Lebejo Mngereza alisema:
“Tupo pamoja na wasanii wote, tutahakikisha wasanii wetu wanasikilizwa na kutekelezewa. Haiwezekani msanii kukosa haki zake za msingi kwa muda mrefu.” Alisema.
Awali, Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) wakishirikiana na Mtandao wa Wanamuziki Tanzania (TAMUNET) waliandaa na kupeleka mapendekezo mawili yaliofikishwa kwenye Tume ya Katiba. Pamoja na kupokelewa hapakuwepo na jambo lolote lililotokana na mawazo hayo ambalo lilichukuliwa na kuingizwa kwenye Rasimu ya Katiba.
Mapendekezo mawili waliokuwa wameyatoa awali ni pamoja na kutaka wasanii kutambuliwa katika Katiba kama moja ya makundi maalum, kama vile walivyotajwa wavuvi, wakulima, wafugaji na kadhalika.
Pendekezo la pili lilikuwa ni kuweka kipengele cha kulinda na kuendeleza Haki za Miliki Bunifu katika Katiba mpya.

WANACHAMA WA SACCOS YA WALIMU KILOLO WATAKIWA KUREJESHA MADENI


Afisa  ushirika mkoa  wa Iringa John Kiteve  akifungua mkutano huo
 
Mwakilishi wa CRDB Iringa akifuatilia matukio  katika mtandao huu 

Mwakilishi wa benk ya CRDB Iringa Bw Bruno  akiwahamasisha  kujiunga na bima mbalimbali  


Afisa ushirika mkoa wa Iringa John Kiteve akifungua mkutano mkuu wa Saccos ya  Walimu Kilolo leo
Na  Francis Godwin Blog
WANACHAMA wa  chama cha   kuweka na kukopa  cha  Kilolo Teacher’s  Saccos wilayani  Kilolo  mkoani  Iringa  wametakiwa  kujenga  uaminifu  katika  kulipa madeni ya  mikopo  ambayo  wamekopeshwa badala ya  kugeuza ni  sadaka  kwao.
Wito  huo  umetolewa na afisa  ushirika  wa  mkoa wa Iringa  John  Kiteve  wakati  akifungua  mkutano mkuu  wa mwaka  leo  mjini  Kilolo.
Kiteve  alisema  kuwa  wapo  baadhi ya  wanachama  wasio  waaminifu ambao  wamekuwa  wakiomba mikopo na mara  baada ya  kupewa  mikopo  hiyo wamekuwa  wakishindwa  kurejesha  mikopo   hiyo  jambo  ambalo  linachangia  vyama  vingi  vya  ushiriki na mikopo  kuyumba hapa nchini.
“ wapo  baadhi  ya  wanachama  ambao  si  waaminifu  wamekuwa  wakichukua  mikopo  na wakati  wakihama  wamekuwa  wakihama na madeni  ya  saccos  bila kufika  ofisini  za  Saccos na kueleza  jinsi ambavyo atarejesha  mikopo  hiyo.
Hivyo  aliwataka  wanachama hao  kujenga utamaduni  wa  kurejesha  mikopo kwa  wakati  ikiwa ni  pamoja na  kutumia  mikopo  hiyo  kwa maendeleo  badala ya  kutumia  mikopo kwa anasa  ambazo  zitakwamisha  urejeshaji wa madeni ya mikopo  yao.
Pia  Kiteve  alisema  kuwa  Saccos  hiyo  ya walimu  wilaya ya  kilolo ni moja kati ya  Saccos  ambazo  zimekuwa  zikifanya  vema na kuwa  tofauti na  saccos  nyingine za  walimu  nchini  kutokana na utaratibu mzuri  wa Saccos  hiyo kuwaunganisha  walimu wa  shule za msingi na  sekondari.
Hata  hivyo  alisema ili kuondoa matabaka katika Saccos  hiyo ni  vema  wanachama  wote  kuwa  kitu kimoja  badala ya  kuwepo kwa matabaka  kati ya  walimu wa  shule za msingi na Sekondari jambo ambalo litaua nguvu ya  Saccos  hiyo.
  katibu  wa  chama  hicho  Fabian  Chavala alisema  kuwa  chama   hicho  kilianzishwa  mwaka 2007 na  kupata  usajili wake  IR 465 kikiwa na  wanachama  60 wakiwemo  wanaume 36 na  wanawake 24 ila  kwa  sasa  kina  wanachama 516  kati yao ni  walimu wa   shule za msingi ni 416 na  wengine  waliobaki ni  kutoka  shule za sekondari.
Hata  hivyo  alisema  kumekuwepo  na mafanikio makubwa katika  chama hicho  kwa chama  kuongeza wanachama kwa kasi na kuwa na jengo lake pamoja na  kuwa na mahusiano mazuri na taasisi za kifedha  hasa benk ya CRDB
Mwenyekiti  huyo  alisema kuwa wanachama  wa chama  hicho  wameendelea  kunufaika na mikopo  na kuwa hadi sasa  wanachama 35  wamekopeshwa  mikopo ya ununuzi wa vyombo  vya usafiri yakiwemo  magari  manne na pikipiki 31,wanachama 343 wamepewa  mikopo ya ujenzi wa nyumba za kisasa ,wanachama 156 wamekopeshwa mikopo ya masomo ya  watoto  wao na wanachama 28  wamepewa  mikopo ya biashara na  kilimo .(P.T)

Wednesday, February 26, 2014

Al Ahly watua Dar na vyakula, maji




WAPINZANI wa Yanga katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri wameonyesha wamepania kuhakikisha hawapotezi mchezo wa Jumamosi baada ya kutua nchini na maji na baadhi ya vyakula ambavyo watapikiwa wachezaji wao.
Habari za uhakika kutoka Cairo, zimeeleza Ahly wamebeba chupa za maji, baadhi ya vyakula na kazi hiyo itafanywa na mpishi wao maalum raia wa…

WAPINZANI wa Yanga katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri wameonyesha wamepania kuhakikisha hawapotezi mchezo wa Jumamosi baada ya kutua nchini na maji na baadhi ya vyakula ambavyo watapikiwa wachezaji wao.
Habari za uhakika kutoka Cairo, zimeeleza Ahly wamebeba chupa za maji, baadhi ya vyakula na kazi hiyo itafanywa na mpishi wao maalum raia wa Ujerumani ambaye amekuwa akisafiri na timu hiyo kwa misimu miwili sasa, kila inapotoka nje ya Misri.
Mmoja wa Watanzania wanaoishi jijini Cairo, amesema waliondoka na vifaa hivyo jana usiku na wanatarajia kuwasili Dar leo alfajiri na ndege ya Egypt Air.

“Wamebeba kila kitu, wakati wanapita hapa airport, baadhi ya vitu vyao vilishapita. Kwa kuwa sisi tuko hapa kazini, tulisikia wakisema kuwa ni maji na vyakula kwa ajili ya wachezaji wa Ahly.
“Wachezaji walifuatia baadaye sana, hapa walikuja na basi maalum na baadaye wakaingia ndani ya uwanja wa ndege. Wanaonekana wako fiti na walikuwa wakitumia muda mwingi kutaniana na walionekana kuwa na furaha tu,” alisema mpashaji huyo ambaye ameishi nchini humo kwa zaidi ya miaka 10 na anazungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha.
Timu hiyo imekuwa ikibeba maji na vyakula ikiwa ni sehemu ya kujiwekea tahadhari ya kuhujumiwa au kuhofia ubora wa maji katika nchi husika wanayokwenda kucheza mechi yoyote ya kimataifa. Mfumo huo hutumiwa pia na timu ya taifa ya Misri.
Hii si mara ya kwanza kwa timu za Kiarabu kufanya hivyo, Ahly iliwahi kufanya hivyo ilipocheza na Yanga na kuifunga bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, mwaka 2008, pia Zamalek nayo ilifanya hivyo lakini ikapigwa bao 1-0 na Simba, mwaka 2003.

Alphonce Mawazo Meneja Kampeni wa Mgombea wa Chadema Kalenga, Achukua Nafasi ya Lema



Alphonce Mawazo, Kamanda wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Picha na Arusha Times)
Arusha255 inaweza kuthibitisha uteuzi mpya wa Ndugu Alphonce Mawazo kama meneja kampeni za kumnadi mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bi Grace Tengega Mvanga katika uchaguzi mdogo wa ubunge unaotarajiwa kufanyika Machi 16, 2014 katika Jimbo la Kelenga Mkoani Iringa kwa lengo la kumpata mbunge atakayewakilisha wana Kalenga baada ya kufariki kwa aliyekuwa M<bunge wa Jimbo hilo Marehemu Profesa Mgimwa, ambaye pia alikuwa Waziri wa Fedha.
Awali alikuwa ameteuliwa Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema kuwa meneja kampeni, lakini kutokana na majukumu ya Bunge la Katiba imeonekana hatakuwa na muda wa kutosha kufanya kazi hiyo.
Mawazo na lemaAlphonce Mawazo (kushoto) na Gobless Lema latika moja ta tukio la kisiasa.  Hapa chini ni maelezo binafsi ya Mawazo kufuatia uteuzi huo kama alivyoandika kwenye ukufasa wake wa Facebook
“Nakishukuru chama changu cha chadema kwa kuniamini na kunipa heshima kuu ya kuwa kampeni meneja wa hapa Kalenga panapofanyika uchaguzi mdogo wa ubunge baada kifo cha aliyekuwa Mbunge Wa jimbo hili Dr. Mugimwa.
Mikoba hii nimeirithi kutoka kwa Mh: Lema Mbunge wa Arusha Mjini kutokana na wabunge kushiriki moja kwa moja kwenye Bunge la Katiba hivyo kuwa na muda mfinyu sana aa kufanya shughuli zingine nje ya Bunge.
Natambua sio kazi ndogo na wala sio mteremko.  Ninchoweza kuwaahidi ni mapambano yasiyo na simile. Dhamira yangu ni dhabiti mno, utayari wangu kutimiza adhima ya mioyo ya watanzania na ile ya chama changu haipimiki. Hakuna gharama itakayo kuwa ngumu kwangu kuilipa kwa ajili ya ukombozi wa taifa langu, nina maanisha HAKUNA. Nitajie gharama yoyote nitakuambia am ready to pay ili mradi niwe na uhakika ya kwamba kama ni damu yangu inatakiwa haimwagiki bure kwa faida ya wachache.
Namwamini Benson Kigaila ambaye ni operation kamanda, Mimi humwita General wa vita. Namwamini Dr:slaa kipenzi cha watanzania na MTU shupavu sana. Namwamini Mbowe Mwenyekiti ambaye ni chachu kubwa ya mabadiliko Tanzania na inspirational kwa vijana. Naiamini Kamati Kuu ya Chadema.
Nilipokea kwa mshituko kidogo taarifa za wasaliti wawili kule Shinyaga lakini baada ya kusikia majina yao nikapumua maana nawafahamu fika na kwa wakati mmoja nilishawahi kuwaonya kuwa chama kingewashinda. Yametimia, sina sikitiko hata chembe waacheni waondoke lilikuwa bomu hatari sana. Nimemwambia Dr Slaa asipoteze muda kuwafikiri. Kkwa mila za kiafrika hatuombolezei mimba iliyo haribika.
Mwisho naomba mtuombee sisi tulioko vitani Kalenga, vijana wenu wengi wamejitoa na wako huku, wengi wao wamekuja kwa kusukumwa na matamanio ya mabadiliko na hawajui watakula au kunywa nini. Kama una chochote waweza kutuma kupitia namba yangu 0756039703 au kama unamjua yoyote aliyeko field huku tafadhali msaidie. ALUTA CONTINUA.”

SLAA AWANG'AKIA VIONGOZI WA SERIKALI!!


Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa amesema tatizo la umaskini linalowakabili Watanzania, linatokana na viongozi walioko madaraka kutokuwa waadilifu.
Alisema Tanzania ni nchi iliyojaaliwa rasilimali nyingi ambazo kama zikisimamiwa vyema taifa haliwezi kuwa na watu maskini kama ilivyo hivi sasa.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza kwenye mikutano ya kampeni iliyofanyika katika Vijiji vya Igula katika Kata ya Luwota na Magulilwa mkoani Iringa.
“Nchi hii siyo maskini, imejaliwa rasilimali nyingi ambazo kama zikisimamiwa ipaswavyo, taifa lisingekuwa na umaskini kama ilivyo sasa,” alisema Dk Slaa na kuongeza:
“Leo hii viongozi wa CCM wamekosa uadilifu ndiyo maana magogo kutoka katika misitu yetu yanaibiwa na kupelekwa nje ya nchi.
Dk Slaa alisema hayo yanatokana taifa kuongozwa na watu wasio waadilifu, huku Amiri Jeshi Mkuu ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete akishindwa kukabiliana na hali hiyo. Katika mikutano hiyo, Dk Slaa aliwataka wakazi wa Kalenga kumchagua mbunge wao ili kuongeza idadi ya wabunge wake
 
 
 

Tuesday, February 25, 2014

MAJAMBAZI WAUWAWA ARUSHA

Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Watu wanne ambao bado hawajafahamika wanaume wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 35 wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wameuawa baada ya kupigwa risasi na askari Polisi. Tukio hilo lilitokea jana tarehe 21.02.2014 muda wa saa 1:00 jioni katika bar moja iitwayo Pama iliyopo maeneo ya Makao Mapya jijini hapa.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas alisema kwamba, tukio hilo lilitokea mara baada ya jeshi la polisi Mkoani hapa kupata taarifa toka kwa raia wema kwamba watu hao walikuwa wanapanga kwenda kufanya tukio la uhalifu katika kituo kimojawapo cha kuuzia mafuta kilichopo jijini hapa ambapo ufuatiliaji wa taarifa hiyo ulianza.

Ilipofika muda huo askari hao walikwenda katika bar hiyo na mara baada ya majambazi hao kuwaona askari hao walihisi wanafuatiliwa ndipo mmojawao ghafla alitoa bastola  na kufyatua risasi tatu ambapo moja ilimparaza askari mmoja aitwaye F. 1416 D/Ssgt Richard katika mkono wake wa kushoto

 “Kufuatia hali hiyo askari nao waliamua kujibu mapigo kwa kupiga risasi ambapo wanne kati ya watano walijeruhiwa na mmojawao alifanikiwa kukimbia akiwa na silaha inayosadikiwa kuwa ni SMG”. Alisema Kamanda Sabas.

Kamanda Sabas alisema kwamba, majambazi hao walifariki dunia wakiwa njiani kuelekea hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya matibabu na miili yao imehifadhiwa hospitalini hapo kwa ajili ya utambuzi toka kwa ndugu na jamaa wa karibu.

Aidha Kamanda Sabas alisema, katika eneo la tukio askari hao walipata bastola moja aina ya Star yenye namba 42640 FNH PISTOLE MODEL KAL 7.65 ikiwa na risasi tatu katika magazine, maganda matatu ya risasi pamoja na begi moja dogo la mgongoni lenye rangi nyekundu likiwa na risasi nne hivyo kufanya jumla ya risasi saba kupatikana.

Bado Jeshi la Polisi Mkoani hapa linaendelea na upelelezi kuhusiana na tukio hilo ikiwa ni pamoja na kumtafuta mtuhumiwa mmoja aliyekimbia.

Kufuatia tukio hilo Kamanda Sabas aliendelea kuwashukuru wananchi wa Arusha kwa ushirikiano wao mkubwa wanaoutoa kwa jeshi la Polisi Mkoani hapa na kuwasihi waendelee kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu hali itakayosaidia kukomesha matukio ya uhalifu mkoani hapa.

MREMBO AFARIKI GHAFLA GUEST ARUSHA

MREMBO mmoja ambaye alihu-dumu kwenye nyumba ya kulala wageni na baa (jina tunalo) iliyopo Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha, Blandina Michael (33) amekutwa amekufa kwenye moja ya vyumba vya nyumba hiyo huku chanzo cha tukio hilo kikihusishwa na vitendo vya ushirikiana.
Taarifa za awali zilimtuhumu mmiliki wa nyumba ya wageni moja ambaye pia anajihusisha na biashara za madini (jina tunalo) kwamba alimtoa kafara mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa, kila mwaka mtu mmoja katika biashara zake hupoteza maisha ghafla. 
Hata hivyo, mfanyabiashara huyo alipoongea na Uwazi juzikati alikanusha vikali tuhuma hizo na kueleza kuwa yeye ni muumini mzuri wa imani yake. 
‘’Hao watu wanapotosha sana, unajua kuna mwaka mwanaume mmoja alikufa ghafla kwenye nyumba yangu ya kulala wageni, alikuja na mpenzi wake ila alimeza Viagra ambazo hata polisi walizikuta mezani. 
“Sasa watu wasio na nia njema na mimi tukio hilo wanaliunganisha na hili kwamba nawatoa kafara,” alisema. 
Kifo cha Blandina kilitokea ndani ya chumba huku mtu mmoja anayedaiwa kuwa mpenzi wake aliyejulikana kwa jina moja la Timo, mkazi wa eneo hilo akihojiwa na polisi. 
Marehemu Blandina ambaye ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga, anaelezwa na bosi wake huyo kwamba alikuwa kama mtoto wa familia yake kwa vile alimwamini sana. Alifanya kazi hapo kwa miaka 8 na hakuwa na tatilo la kiafya. Bosi huyo alisema mwili wa marehemu uligundulika baada ya mfanyakazi mwenzake wa kiume kumpigia simu saa 2 asubuhi ambapo simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa ndipo alipoamua kwenda kumgongea katika chumba hicho. Alisema baada ya kufika alishangaa kukuta mlango wa chumba chake uko wazi na alipochungulia alibaini kwamba Blandina alikuwa amefariki dunia. Hata hivyo, polisi baada ya kufika na kuufanyia uchunguzi wa awali mwili huo hawakugundua kuwepo kwa jeraha lolote linaloashiria kuuawa, ingawa mwili huo ulipelekwa kufanyiwa uchunguzi wa kitaalam katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru 
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali hiyo.

TASWIRA MBALIMBALI TOKA KATIKA VIWANJA VYA BUNGE MJINI DODOMA




ameir
Wajumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Ismail Aden Rage na Kheri Ameir wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuaharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma hadi Ijumaa.
 dovutwa
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama (UPDP), Fahmi Dovutwa  na Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia Mwenyekiti wa Chama cha TLP Augustino Mrema wakibadlishana…
ameir
Wajumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Ismail Aden Rage na Kheri Ameir wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuaharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma hadi Ijumaa.
 dovutwa
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama (UPDP), Fahmi Dovutwa  na Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia Mwenyekiti wa Chama cha TLP Augustino Mrema wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma. fedh
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Ismail Aden Rage (kulia) na Mjumbe mwezie na Naibu Waziri wa Fedha Mwingulu Nchemba (kushoto) wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma.
hamis
Wajumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Dkt Khamis Kigwangalla (kulia) akisalimiana na Mjumbe mwezie ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta (kushoto)  nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma. 
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba na Mwenyekiti wa Chama cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba(kulia) alisamiana na mwandishi na Mpiga picha wa Kampuni ya Mwananchi Emmanuel Helman jana mjini Dodoma mara baada ya kuharishwa kikao cha Bunge.
jenista
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia ni NaibuWaziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Jenista Mhagama (kushoto) na Mjumbe mwezie Lediana Mung’ong’o wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma. kissu
Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) Shaban Kissu (koshoto) na Naibu Waziri wa Habari , Vijana , Utamaduni na Michezo Juma Mkamia (kulia) wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma. mapalala
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge la Katiba  ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta (kushoto)  akisalimiana na Mjumbe mwezie James Mapalala nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma. nagu
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji ) Dkt Mary Nagu (kushoto) akibadilishana mawazo na Mjumbe mwenzie Paul Kimiti  jana mjini Dodoma mara baada ya kuharishwa kikao cha Bunge hilo.
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia ni Waziri wa Fedha  Mwingulu Nchemba akiteta jambo na Mjume wa Bunge hilo Philemon Ndesamburo jana mjini Dodoama mara baada ya kuharishwa kikao cha Bunge. simba
Wajumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba ambao pia ni wapenzi na wananchama wa Timu ya Simba wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma. Kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Juma Mkamia, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta (katikati)  na Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage. oWajumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba wakibadlishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuharishwa kwa kikao jana mjini Dodoma.

NI AIBU ILIOJE BUNGE LA KATIBA!

NYALANDU APANGUA WAKURUGENZI MALIASILI


nyalandupx_745e8.jpg
Dar es Salaam. Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amewaondoa katika nyadhifa zao, Wakurugenzi mbalimbali kwa sababu zilizoelezwa kushindwa kutekeleza majukumu yao.
Hatua ya Nyalandu imekuja ikiwa ni utekelezaji wa azimio la Bunge la Desemba 22, 2013 lililotaka Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori kuwajibishwa kutokana na tuhuma za uzembe na ukiukwaji wa haki za binadamu katika Operesheni Tokomeza.
Nyalandu alisema: "Namwondoa Prof Alexander Songorwa (Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori) na kumteua Paul Sarakikya kukaimu nafasi hiyo."

Alisema pia kuwa amemwondoa Mkurugenzi Msaidizi wa Matumizi Endelevu ya Wanyamapori, Profesa Jafari Kidegesho kwenye nafasi hiyo na Dk Charles Mulokozi ameteuliwa kushika wadhifa huo.
Mwingine aliyeteuliwa ni Julius Kibebe kuwa Mkurugenzi Msaidizi Uzuiaji-Ujangili, nafasi iliyoachwa wazi na Sarakikya wakati Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo, Utafiti na Takwimu, Nebbo Mwina anabaki kwenye nafasi yake.
Nyalandu alisema Herman Keiraryo anaendelea kuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Uendelezaji wa Wanyamapori na kwamba waliotangazwa kuondolewa kwenye nyadhifa, kazi zao mbadala zitatangazwa baadaye.
Waziri Nyarandu alitoa siku 30 kwa Wakurugenzi Wakuu wa kila Idara, Shirika na Taasisi za Wizara ya Maliasili na Utalii, kutengeneza viashiria vya utendaji kazi (Key Performance Indicators) na kuvikabidhi kwake.
Alisema hatua hiyo itafanikisha kufikiwa malengo ya wizara hiyo, kwani uwajibikaji na ufanisi wa kazi za kila siku utapimwa katika hali ya uwazi ili mikakati ya wizara itekelezwe katika mifumo inayopimika na hatimaye kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Waziri huyo aliagiza kila mtumishi akiwamo yeye mwenyewe, kutekeleza majukumu yaliyopangwa kwa kuzingatia kanuni za mwenendo (code of conduct), zitakazopendekezwa na kupitishwa na Baraza la Wafanyakazi la wizara hiyo.

HATIMAYE MTOTO MWENYE UVIMBE WA AJABU AKATWA MGUU NCHINI INDIA


Mtoto mwenye uvimbe wa ajabu, Hamis Liyuga akiwa anaandaliwa kupelekwa katika chumba cha upasuaji.
 
 Hamis Liyuga akipelekwa katika chumba cha upasuaji.…
 
Mtoto mwenye uvimbe wa ajabu, Hamis Liyuga akiwa anaandaliwa kupelekwa katika chumba cha upasuaji.
 

...Akiwa ndani ya chumba cha upasuaji.
...Akiwa chini ya uangalizi wa madaktari.
Mwandishi wa Global Publishers, Imelda Mtema (kushoto) aliyeambatana na mtoto Hamis Liyuga nchini India.