Monday, June 24, 2013

BARNABA APOTEZA FAHAMU WAKATI WA MAZISHI YA MAMA YAKE

Mwanamuziki Elias Barnabas 'Barnaba' akiweka udongo katika kaburi la mama yake mzazi, Mariamu  Arubeth.
Baada ya kuweka udongo Barnaba akaishiwa nguvu.
Barnaba akiwa kapoteza fahamu wakati wa mazishi ya mama yake.
Akipatiwa huduma ya kwanza.
Baada ya kuzinduka.
Akipelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu.
Mwanamuziki Elias Barnabas 'Barnaba' jana alipoteza fahamu wakati wa mazishi ya mpendwa mama yake mzazi, marehemu Mariamu Arubeth katika makaburi ya Mburahati jijini Dar es Salaam. Hali ya Barnaba ilibadilika baada ya kuweka udongo katika kaburi la mama yake ndipo alipopoteza fahamu na kupatiwa huduma ya kwanza kisha kupelekwa hospitali. GPL inampa pole msanii Barnaba na wanafamilia wote kwa msiba huu.
(Picha kwa hisani ya This is Diamond)

0 comments: