This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Tuesday, September 24, 2013

TANZANIA MABINGWA WASICHANA MASHINDANO YA KIMATAIFA AIRTEL RISING STARS

Mkurugenzi mkuu wa Airtel Nigeria Segun Ognsanya Katikati akiwakabithi captain wa timu ya wasichana Tanzania na kocha wa timu ya wasichana Rogacian Kaijage zawadi za ushindi mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika
Wachezaji wa timu ya wasichana ya Tanzania ya Airtel Rising stars wakishangilia ushindi
Mwakilishi na kiongozi wa Airtel Tanzania bi Lilian Kibiriti akifurahia ushindi na Wachezaji wa timu ya wasichana ya Tanzania ya Airtel Rising stars mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika
Mwakilishi na kiongozi wa Airtel Tanzania bi Lilian Kibiriti akifurahia ushindi wa kikosi cha timu ya wasichana mara baada ya kuibuka washindi katika michuano ya kimataifa ya Airtel Rising stars
Mkurugenzi mkuu wa Airtel Nigeria Segun Ognsanya akimkabithi kombe captain wa timu ya wasichana Tanzania mara baada ya kuibuka mabigwa wa michuano ya Airtel Rising stars ya Afrika jana jijini Lagos Nigeria
Ni Tanzania
Kikosi cha timu mabigwa ya Airtel Rising stars Afrika cha wasichana cha Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja pichani waliosimama  (wa mwisho kushoto) ni kocha wa timu ya wavulana Abel Mtweve na wa mwisho kulia ni kocha wa timu ya wasichana Rogacian Kaijage
Tanziania mabingwa wasichana mashindano ya kimataifa Air Rising Stars
Timu ya wasichana ya Tanzania imeibuka mabigwa katika michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya kimataifa ya Airtel Rising Stars yaliyokuwa yanafanyika mwaka huu  nchi Nigeria.
Tanzania ilipata ubigwa huo baada ya kuchuana vikali na timu ya Kenya katika mechi ya Fainali  na kuifunga Kenya goli moja bila na kuibuka mabingwa . Donisia Daniel ndio alipeleka furaha kwa upande wa Tanzania.
Tanzania ilikua kundi moja na Sierra-Leone , Malawi , na Uganda. Walishinda mechi moja dhidi ya Sierra-Leone 2-1 , wakapoteza mchezo dhidi ya Uganda na kutoka sare na Malawi 1-1.

Wakashinda 4-2 katika mikwaju ya penati dhidi ya DRC katika robo fainali mechi zilizopigwa katika uwanja wa NIS Sports. Na wakawatoa Uganda kwa mvua ya magoli 8-1.

Mbali na ushindi huo wa wasichana watanzania walijishindia zawadi mbalimbali ikiwemo , Mchezaji bora kwa upande wa wasichana Tatu Iddi, Mfungaji bora wa mashindano kwa upande wa wavulana Athanas Mdam na Mfungaji bora kwa upande wa wasichana Shelda Boniface.

Kwa upande wa wavulana Timu ya Niger wametetea tena ubingwa  baada ya kuifunga Zambia kwa mikwaju ya penati 7-6  katika mechi ya fainali ya Airtel Rising Stars ilifanyika kweny uwanja wa Agege nchini Nigeria.

Niger wamefanya vizuri kuanzia hatua ya makundi  baada ya kushinda michezo yote katika makundi na kufikisha magoli 12 na kuruhusu magili matatu tu katika mechi sita . Jumla ya mechi 58 zimechezwa katika mashinda.

Aidha timu ya wavulana ya Tanzania imeshikilia nafasi ya nne kati ya timu zaidi ya 16 zilizoshiriki michuano hiyo
Michuano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars kwa mwaka huu yamefanyika nchini Nigeria katika viwanja vinne Agege, Township Stadium, Legacy Pitch, National Institute for Sports Fiels na  Main bowl.
Kulianza na “ gala night” jumapili usiku ikafatia  sherehe za ufunguzi , na mechi za ufunguzi za makudi katika uwanja wa AgegeTownship .

Mashindano ya kiamataifa ya umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars yanafanyika kwa mara ya pili , mashindano haya yamekua bora kwa vijana wadogo na kwakuzingatia jinsia.

ILIVYOKUWA SEMINA YA KAMATA FURSA TWENZETU MKOANI SHINYANGA JUMAPILI.


 
 Mbuge wa Jimbo la Shinyanga mjini na Naibu Wa Nishati na Madini,Mh Steven Masele akizungumza na sehemu ya wakazi wa mkoa wa Shinyanga waliofika kwenye semina ya Kamata ya Fursa Twendzetu kwa vijana,iliofanyika leo kwenye ukumbi wa Shinyanga Vijana Center.Mh Steven amewataka vijana wa Shinyanga kuwa na moyo wa kujituma na kuzifanyia kazi ipasavyo fursa wanazokumbana nazo bila kukata tamaa,ameeleza kuwa hivu karibuni mkoa huo,unatarajia kufungua viwanda kadhaa,ambapo anaamini kuanzia fursa ya kupata ajira kwa vijana itaongezeka.
 Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Maxmalipo,Bernard Munubi akizungumza kwenye semina ya Kamata Fursa Twendzetu kwa vijana,kuhusiana na masuala mbalimbali yanayofanywa na kampuni yake katika kusaidia huduma za jamii,ndani ya ukumbi wa Shinyanga Vijana Center.
 sehemu ya wakazi wa mkoa wa Shinyanga waliofika kwenye semina ya Kamata ya Fursa Twendzetu kwa vijana,iliofanyika leo kwenye ukumbi wa Shinyanga Vijana Center. 
 Mkurugezi  wa Vipindi na Uzalishaji Kutoka Clouds Media Groug,Ruge Mutahaba akizungumza sehemu ya wakazi wa mkoa wa Shinyanga waliofika kwenye semina ya Kamata ya Fursa Twendzetu kwa vijana,iliofanyika leo kwenye ukumbi wa Shinyanga Vijana Center.Ruge pia amefunga semina hiyo ya fursa kwa vijana mapema loe mchana,ambayo imekuwa ikiandaliwa na kampuni ya Clouds Media,Semina hiyo imefanyika  ndani ya mikoa takribani zadi ya kumi  ikiwemo   Kigoma,Singida,Tabora,Mtwara,Morogoro,Dodoma,Mbeya,Iringa,Bukoba na sasa ndani ya mkoa wa Shinyanga.

 sehemu ya wakazi wa mkoa wa Shinyanga waliofika kwenye semina ya Kamata ya Fursa Twendzetu kwa vijana,iliofanyika leo kwenye ukumbi wa Shinyanga Vijana Center.  

 Wengine tena ndio hivyo teena,fursaaa fursaaaaa. 
 Sehemu ya meza kuu ikifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa ukumbini humo.

 Wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini.

 Mtangazaji wa Clouds FM,Shaffih Dauda akitoa mada ya fursa ndani ya michezo na changamoto zake,lakini pia namna ya kukabiliana nazo kiasi hata kupata mafanikio kwa namna moja ama nyingine,
Mwakalilishi kutoka TPSF,Jane Gonsalves akizungumza kwenye semina ya Kamata Fursa Twendzetu kwa vijana,kuhusiana na masuala mbalimbali ya ujasiliamali kwa vijana ikiwa ni sehemu pia kujiongezea kipato,semina hiyo imefanyika mapema leo ndani ya ukumbi wa Shinyanga Vijana Center. 
Baadhi wakazi wa mkoa wa Shinnyanga wakifuatila mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa ndani ya semina ya kamata fursa twendzetu,semina hiyo imefanyika mapema leo ndani ya ukumbi wa Shinyanga Vijana Center.Picha na Michuzijr wa MICHUZI MEDIA GROUP-SHINYANGA.

MKUU WA MKOA WA MWANZA AWASHANGAA WANAOPINGA PENDEKEZO LA UWANJA WA NDEGE WA MWANZA KUITWA SERENGETI



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Wiki ya Utalii Jijini Mwanza ambapo yanaanza rasmi leo kwa ufunguzi na kumalizika tarehe 27/09/2013 uwanja wa Nyamagana.

Saturday, September 14, 2013

IRENE UWOYA "SHIGONGO ANANICHAFUA KWENYE MAGAZETI YAKE SABABU NINA KESI NAYE MAHAKAMANI"


Ukurasa wa mbele wa gazeti la Risasi la leo Jumamosi (Sept 14) umetawaliwa na habari inayomhusu msanii wa Bongo Movie Irene Uwoya yenye kichwa cha habari “UWOYA MBARONI KWA WIZI WA SIMU!!”.


“MSANII aliyewahi kutamba kisha kuporomoka kwa kasi katika tasnia ya filamu nchini Tanzania kwa sababu ya tabia zake chafu, Irene Uwoya, amefikishwa Kituo cha Polisi Msimbazi kwa wizi wa simu aina ya iPhone 5.

MAMBO yanaendelea kumwendea kombo mwigizaji huyo huku akiwa ameanza kuporomoka vibaya kwenye sanaa na kujikuta akiingia matatani kwa tuhuma za aibu.

Uwoya ambaye siku hizi anajitutumua kwa kuanzisha kipindi kwenye runinga moja ya Bongo baada ya kushindwa kwenye filamu, alidakwa na askari wa Kituo cha Polisi Msimbazi, Dar baada ya kusakwa usiku na mchana kwa kutumia kumbukumbu ya jalada la kesi namba MS/RB/8522/13 WIZI KUTOKA MAUNGONI.”

Katika kujibu tuhuma zilizoripotiwa na gazeti hilo, Uwoya kupitia akaunti yake ya Instagram leo amepost picha ya ukurasa wa mbele wa gazeti hilo wenye habari hiyo pamoja na maneno yafuatayo:


“Minimti wenye matunda milele siogop kupigwa mawe…shigongo kamua kunichafua coz nakes nae mahakaman…anadhan ntaiacha never yeye aponde anavyoweza ila mwisho wasiku sheria iatafata mkondo wake….minayake mengi nayajua ila ngoja ninyamaze nisimwagiwe tindikali”

Maafisa Mawasiliano waaswa kuhabarisha na kuelimisha shughuli za Serikali;

_MG_3914_521be.png
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga akiongea na Maafisa Mawasilino Serikalini (hawamo pichani) wakati akifungua mkutano wa tathmini wa awamu ya kwanza ya utaratibu wa Maafisa Mawasiliano kuzungumza na waandishi wa habari, ambapo aliwataka kutekeleza utaratibu huu kama ulivyopangwa ili kuweza kutoa taarifa mbalimbali za utekelezaji wa Sera na Miradi inayoratibiwa na Ofisi zao kwa wananchi kupitia waandishi wa habari, katika mkutano uliofanyika jana Ukumbi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa.
_MG_3939_7e9a1.png
Baadhi ya Maafisa Mawasilino Serikalini waliohudhuria mkutano huo wa tathmini uliofanyika jana katika Ukumbi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es Salaam.(P.T)

_MG_3945_574df.png
MKURUGENZI Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa Akiwasilisha ripoti ya utekelezaji Mikutano ya awamu ya kwanza ya utaratibu wa maafisa mawasiliano kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu Sera na Mipango pamoja na ujibuji wa hoja mbalimbali zinazohusu Ofisi zao, kwenye katika mkutano uliofanyika jana Ukumbi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es Salaam.
_MG_3963_f8c94.png
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Innocent Mungy Akiwasilisha kwa Maafisa Mawasilino Serikalini juu ya namna bora ya kuandaa na kuboresha taarifa kwa vyombo vya habari, katika mkutano uliofanyika jana Ukumbi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dar es Salaam.
IMG_3896_ac1df.png
IMG 3896- MKURUGENZI wa Idara ya Habari na Msemaji wa Serikali Assah Mwambene akiongea na Maafisa Mawasilino Serikalini (hawamo pichani) jana wakati mkutano wa tathmini wa awamu ya kwanza ya utaratibu wa maafisa mawasiliano kuzungumza na waandishi wa habari, ambapo alisisitiza utoaji wa taarifa za utekelezaji wa Sera na Mipango pamoja na kujibu hoja mbalimbali zinazohusu Ofisi zao. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga na katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Bi. Zamaradi Kawawa.
PICHA ZOTE NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
HOTUBA YA BI SIHABA NKINGA, KATIBU MKUU, WIZARA YA HABARI VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO KUFUNGUA KIKAO CHA TATHMINI YA MZUNGUKO WA KWANZA WA MIKUTANO YA WASEMAJI SERIKALINI NA WAANDISHI WA HABARI, DAR ES SALAAM, SEPTEMBA 13, 2013
Ndugu Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO,
Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi na Mameneja mliopo hapa,
Maafisa Mawasiliano,
Waandishi wa Habari,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana Habari za Asubuhi!!!
Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kumshukuru mungu kuweza kunikutanisha nanyi siku hii ya leo tukiwa na afya njema. napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwenu kwa kuhudhuria mkutano huu muhimu kwa ajili ya kufanya tathmini ya utekelezaji wa ratiba ya mzunguko wa kwanza wa mikutano ya Waandishi wa Habari na Wasemaji Serikalini.
Ndugu Washiriki,
Kama mnavyofahamu Wizara ambayo ina jukumu la kusimamia masuala ya Habari na Uratibu wa Mawasiliano ya Serikali, iliandaa ratiba kwa ajili ya Ofisi za Serikali kujitangaza kwa umma kupitia vyombo mbalimbali vya mawasiliano nchini.
Ratiba hiyo ilianza rasmi Tarehe 4, Julai,2013 na kumalizika Septemba 3,2013 ambapo Wasemaji wa Taasisi/Wakuu wa Idara/Vitengo vya Mawasiliano Serikalini walitakiwa kuzungumza na vyombo vya Habari katika siku na muda uliopangwa . Mikutano 75 ilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Idara ya Habari-MAELEZO na mkutano mmoja wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kitengo kipya cha magonjwa ya moyo cha Hospitali hiyo iliyopo Upanga, Dar es Salaam.
Nimeambiwa kuwa Jumla ya Taasisi za Serikali 88 zilitakiwa kushiriki katika mikutano hiyo, kati ya Taasisi hizo, Taasisi 75 sawa na asilimia 85 zilishiriki katika mikutano hiyo na Taasisi 14 sawa na asilimia 15 hazikushiriki.
Kwa mara nyingine tena natoa pongezi kwa Taasisi zote zilizoshiriki katika mikutano hiyo. Mikutano hii ni muhimu na imeleta tija kwa kuwa wananchi kupitia Vyombo vya Habari nchini walipata fursa ya kuelewa masuala mengi ya msingi yanayotekelezwa na Serikali kwa lengo la kupunguza umaskini na kukuza uchumi wa wananchi. Ni ukweli usiopingika kuwa maswali yaliyoulizwa na wananchi kupitia Waandishi wa Habari wakati wa mikutano hiyo kunaonesha shauku kubwa iliyokuwepo ya kutaka kujua Serikali inafanya nini kwa ajili ya wananchi wake.
Aidha, napenda kutoa wito kwa Taasisi ambazo hazikuhudhuria mzunguko wa kwanza wa mikutano hii wajiandae kwa ajili ya kushiriki mzunguko wa Pili.
Ndugu Washiriki,
Kama mnavyofahamu, jukumu kubwa mlilopewa ni kuwezesha Serikali kupitia Ofisi zenu kufanya mawasiliano na umma kupitia Vyombo vya Habari kuhusu masuala mbali mbali yanayohusu Sera na Miradi inayotekelezwa na Serikali yenye lengo la kustawisha maendeleo ya watanzania. Kwa kufanya hivyo, Serikali inatimiza wajibu wake wa kutoa haki ya msingi ya wananchi ya kupata habari hususan zinazohusu utekelezaji wa shughuli mbali mbali za Serikali.
Kumekuwa na malalamiko ya kutokuridhika na namna ambavyo Serikali haitoi taarifa kwa umma ili kuweza kutosheleza kiu ya wananchi ya kupata habari zinazohusu utekelezaji wa shughuli za maendeleo ambazo kwa kiasi fulani huchangiwa na fedha za walipa kodi.
Ndugu Washiriki,
Nitumie nafasi hii kuwaasa kuwa tumieni fursa za ratiba za mikutano zinazoandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO ili kukidhi kiu ya jamii ya kuhabarishwa na kuelimishwa shughuli za Serikali.
Pamoja na mikutano hiyo inayoratibiwa na Wizara, napenda pia kuwakumbusha kuwa Taasisi kupitia Ofisi zenu kuandaa Mkakati wa Mawasiliano Serikalini kwa wale ambao hawana na wale ambao tayari wameshaandaa Mkakati huo utekelezeni kwa dhati ili kufanikisha malengo yaliyokusudiwa.
Aidha, natoa wito kwenu kama daraja la mawasiliano ya Serikali kwa umma kuelewa Sera na shughuli zote zinazotekelezwa na Taasisi zenu ili muweze siyo tu kuwa wasemaji wazuri wa Serikali lakini pia kuwa washauri wazuri wa viongozi katika ngazi mbali mbali kuhusiana na masuala ya mawasiliano ya Serikali kwa umma.
Nasisitiza kuwa toeni ushauri ulio sahihi, kwa haraka na wakati ili kutoa majibu mwafaka kwa umma pale ambapo Vyombo vya Habari vinakuwa vimetoa taarifa zisizo sahihi. Hili lifanyike kwa vyombo vyote vya Habari vikiwemo Radio, Televisheni, Magazeti na Mitandao ya Kijamii pale inapolazimu ili kuondoa upotoshaji wa taarifa za Serikali unaosababishwa na ukuaji wa teknolojia ya Habari na Mawasiliano ambapo kila mtu anaandika kile anachokijua bila kufuata weledi wa taaluma ya uandishi wa habari. na utangazaji. Taarifa zisizosahihi zikiachwa bila kujibiwa zinaweza kuleta uchonganishi kati ya Serikali na umma na hivyo kusababisha sintofahamu isiyokuwa na ulazima.
Aidha, napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru Waandishi wa Habari walioshiriki katika zoezi hili kwa mchango mkubwa wa kutoa taarifa kwa umma kuhusu utekelezaji wa shughuli mbali mbali za Serikali hususan kwa kazi kubwa mliyoifanya wakati wa mikutano ya Waandishi wa Habari na Wasemaji wa Taasisi za Serikali iliyoanza Julai 4,2013 na kumalizika Septemba 3, 2013.
Ndugu Washiriki ,
Wizara sasa imeandaa ratiba ya awamu ya Pili ya Mikutano ya Waandishi wa Habari na Wasemaji wa Taasisi ambayo inaanza Septemba 16, 2013. Naomba mshiriki kwa kikamilifu na mjiandae vizuri zaidi kama mlivyofanya awali. Aidha, mkitumie vizuri kikao cha tathmini kwa kufahamu mafanikio na upungufu uliokuwepo wakati wa utekelezaji wa awamu ya Kwanza ya Mikutano hiyo ili muweze kujirekebisha na kuboresha zaidi mikutano hii ya Awamu ya Pili.
Ni matumaini yangu kuwa wenzetu Waandishi wa Habari wataendelea kutoa Ushirikiano kwa Serikali katika kutoa taarifa wakati wa mikutano hii.
Ndugu Washiriki ,
Mwisho niwatakie maandalizi mema, mfanye kazi vizuri kwa kuhabarisha jamii yale yote yanayofanywa na Serikali yetu. Wizara itaendelea kushirikiana nanyi ili kufanikisha majukumu yetu sote.
Naomba sasa nitamke kuwa mkutano wenu umefunguliwa rasmi. Nawatakia kila la heri na mafanikio katika tathmini ya kazi kubwa mliyoifanya katika Awamu ya Kwanza ya kukutana na waandishi wa Habari pamoja na kujibu maswali yote kwa usahihi na kwa kutumia takwimu sahihi.
Ahsanteni.

Mume amsamehe mkewe aliyepanga kumuua

mke_3e033.jpg
Mwanamke mmoja mfanyabiashara mjini Nairobi, Kenya, ambaye alikiri kosa la kupanga njama ya kumuua mumewe, ameachiliwa na mahakama
Bi Faith Wairimu Maina, aliachiliwa huru baada ya mumewe kuitaka mahakama kufuta kesi yake kwani amemsamehe.(P.T)
Bi Faith alikiri kuwa aliwakodi mamluki kumuangamiza mumewe. "Nataka kumsamehe kwa sababu ya watoto na familia yetu," mumewe Faith aliambia mahakama.
Mwanamke huyo alikiri makosa ya kupanga njama ya kutaka kumuua mumewe baada ya kukamatwa ingawa baadaye alibadili msimamo wake na kukanusha madai hayo na alitarajiwa kushtakiwa.
Polisi walitibua njama ya mwanamke huyo baada ya majasusi waliokuwa wanajidai kuwa mamluki kupokea malipo ya shilingi 40,000 kuitekeleza njama hiyo.
Mwendesha mkuu wa mashtaka alisema kuwa alifahamishwa wanandoa hao walikubali kusameheana na kuwa bwana Muthee ambaye ni mumewe mwanamke huyo akataka kesi hiyo kufungwa.
Wakili wa mwanamke huyo alisema kuwa hakuwa na pingamizi zozote kutupilia mbali kesi hiyo. Bwana Muthee alisema kuwa mwanamke huyo ni mkewe na alimsamehe kwa sababu ya familia, jambo linaloruhusiwa na mahakama.
Mwanamke huyo tayari alikuwa amewalipa mamluki kumuua mumewe na kisha kuwataka wamletee nguo zake zenye damu ili aweze kuwalipa pesazitakazokuwa zimesalia ambazo ni shilingi 160,000 na pia aweze kuthibitisha kuwa mumewe ameuawa.
Majajusi walisema kuwa ilikuwa mara ya pili kwa mwanamke huyo kujaribu kumuua mumewe baada ya njama ya kwanza kukosa kufaulu licha ya kuwalipa mamluki waliomwambia kuwa walishikwa na uoga.
Mwanamke huyo alipanga njama ya kumuua mumewe kutokana na madai kuwa alikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine.

Rais Dk. Shein amtembelea Padri aliyemwagiwa Tindikali Mjini Unguja


IMG_4338
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui, alipofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole Mjini Unguja,baada ya kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana katika Mtaa wa Mlandege Mkoa wa Mjini Magharibi jana jioni, Padri alimwagiwa Tindikali alipokuwa akitoka kupata huduma ya Mtandao.
IMG_4342
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimsikiliza Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,akitoa maelezo jinsi alivyopata mkasa wa kutiwa  Tindikali jana na watu wasiojulikanwa,katika mtaa wa Mlandege Mjini Unguja, alipofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole,ambapo amelazwa na kuapatiwa matibabu.
IMG_4349 (1)
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwafariji jamaa  na ndugu wa Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,waliofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole Padri huyo baada ya kumwagiwa Tindikali na Watu wasiojulikanwa jana jioni Mtaa wa Mlandege Mjni.
IMG_4360
Mmoja wa Ngugu wa Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui akimueleza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,hisia zake kwa Uchungu kutokana na kitendo hicho cha kumwagiwa Tindikali na watu wasiojulikanwa  kwamba zilichukuliwe hatua za kisheria na kukomeshwa Vitendo kama hivyo.
IMG_4370
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifafanua jambo wakati akiwafariji jamaa na ndugu wa Padri Joseph Monesmo Magamba wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,waliofika kumuangalia Padri huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja baada ya kumwagiwa Tindikali na Watu wasijulikanwa jana jioni katika Mtaa wa Mlandege Mjini Unguja.(Picha na Ramadhan Othman wa Ikulu, Zanzibar).