This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, April 25, 2013

MTU MMOJA ADAIWA KUFA MAJI COCO BEACH MCHANA HUU


Mwili wa marehemu ukiwa umefunikwa Khanga na wasamaria wema katika fukwe za Coco Beach....
 
Taarifa  zilizotufikia  hivi  punde  zinadai  kuwa  mtu  mmoja  (Pichani)  ambaye  bado  hajafahamika  mara  moja  amekutwa  amekufa  maji  Coco-Beach......

Tunaendelea  kufuatilia   undani  wa  habari hii......
Imetolewa  na Thimothy Shao Koko
 
Mwili ukiwa katika machela

 
Mwili wa Marehemu ukiwa umefunikwa
 
Wasalia wema…
Mwili ukiwa katika machela
 
Mwili wa Marehemu ukiwa umefunikwa
 
Wasalia wema wakiusogeza mwili wa marehemu pembezoni mwa Bahari

LOWASSA CHUPUCHUPU…

Stori: FRANCIS GODWIN, IRINGA

KIJANA ambaye amekuwa ‘akiwaliza’  watu wakiwemo viongozi serikalini kwa kutumia jina la Waziri William Lukuvi aliyejulikana kwa jina moja la Jonathan amenaswa na polisi.
 Mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi baada ya kutiwa mbaro na polisi
Ishu hiyo ilitokea Jumapili iliyopita katika hafla ya Kanisa la Overcomers FM la Askofu Dk. Boaz Sollo kwenye Ukumbi wa St. Dominic…
Stori: FRANCIS GODWIN, IRINGA
KIJANA ambaye amekuwa ‘akiwaliza’  watu wakiwemo viongozi serikalini kwa kutumia jina la Waziri William Lukuvi aliyejulikana kwa jina moja la Jonathan amenaswa na polisi.
Mtuhumiwa akiwa chini ya ulinzi baada ya kutiwa mbaro na polisi
Ishu hiyo ilitokea Jumapili iliyopita katika hafla ya Kanisa la Overcomers FM la Askofu Dk. Boaz Sollo kwenye Ukumbi wa St. Dominic mjini Iringa ambapo kijanna huyo alitaka kumtapeli Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa (pichani) kupitia harambee iliyokuwa ikifanyika kanisani hapo.
Kijana akiwa katika ulinzi mkali wa Askali kanzu wakiwa wana mpeleka kituoni kwa maojiano zaidi

Kijana huyo alipita mbele na MC wa shughuli hiyo alimpa kipaza sauti ambapo alianza kwa kujitambulisha jina na kuongeza yeye ni mtoto wa Lukuvi.
Alisema mara kwa mara amekuwa akimpigia simu Lowassa ili azungumze naye akitaka msaada ambao hakuutaja ukumbini hapo.
Huku Mheshimiwa Lowassa akiwa amesimama wima na kumsikiliza kwa umakini, Jonathan alimwambia siku za nyuma katika mkutano  wa mheshimiwa huyo uliofanyika Viwanja vya Jangwani,  jijini Dar es Salaam alizungumza naye kuhusu shida yake kwa hiyo siku hiyo alitaka atekelezewe.
Kufuatia utambulisho huo, baadhi ya watu waliowahi  kutapeliwa na kijana huyo, akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Teresia Mahongo waliguna, hali iliyosababisha polisi  kujitokeza na kumtia mbaroni kijana huyo ambaye ilionekana alikuwa akiweka mtego wa kumtapeli Lowassa na  viongozi wengine katika hafla hiyo.
Kada wa CCM mkoani Iringa, Godfrey Malenga  Lukuvi alisema kijana  huyo amekuwa akitumia  jina la waziri kuliza  watu. Alisema wengi  wameshalalamika kuhusu  utapeli unaofanywa na Jonathan na kuna wakati alikamatwa na polisi lakini akaachiwa.
Kwa upande wake, Katibu wa Mbunge  Jimbo la Isimani ambaye pia ni familia ya mheshimiwa Lukuvi,  Thom Malenga Lukuvi alisema amekuwa akipokea malalamiko kutoka kwa watu mbalimbali ambao  wamelizwa na Jonathan na ameshaweka mitego ya kumnasa lakini hakuwahi kufanikiwa.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Mahongo alimweleza mwandishi wa habari hizi kuwa Jonathan aliwahi kufika ofisini kwake kwa lengo la kumtapeli lakini alimshtukia na kumpigia simu Waziri Lukuvi ambapo alisema kijana huyo ni tapeli.
Mwandishi wetu alimtafuta Lukuvi kwa simu na alipopatikana alimkana kijana huyo kwamba hamtambui wala hana undugu na ukoo wake.
“Huyu kijana simtambui na wala si ndugu yangu, ila amekuwa akitumia jina langu kutapeli watu na tayari amekamatwa na polisi kwa utapeli huo,” alisema Lukuvi.


ORODHA NZIMA YA WASANII WALIOTAJWA KUWANIA TUZO ZA "KILI MUSIC AWARDS" MWAKA 2013


Majina ya wasanii watakaowania tuzo za Kili mwaka 2013 yametajwa leo. 
WIMBO BORA WA MWAKA
Dear God - Kala Jeremiah
Leka dutigite - Kigoma all star
Mapito - Mwasiti Feat Ally Nipishe
Me n U - Ommy Dimpoz Feat Vanessa Mdee
Pete- Ben pol

MSANII BORA WA KIUME
Ben Pol
Diamond
Linex
Mzee Yusuf
Ommy Dimpoz

MSANII BORA WA KIKE
Isha Mashauzi
Khadija Kopa
Lady Jaydee
Mwasiti
Recho

MSANII BORA WA KIKE - TAARAB
Isha Mashauzi
Khadija Kopa
Khadija Yusuph
Leila Rashid

MSANII BORA WA KIUME - TAARAB
Ahmed Mgeni
Hashim Said
Mzee Yusuf

MSANII BORA WA KIUME - BONGO FLAVA
Ally Kiba
Ben Pol
Diamond
Linex
Ommy Dimpoz

MSANII BORA WA KIKE - BONGO FLAVA
Linah
Mwasiti
Recho
Shaa

MSANII BORA WA HIP HOP
Fid Q
Joh Makini
Kala Jeremiah
Profesa J
Stamina

9. Msanii Bora wa Kiume - Bendi
Chalz Baba
Dogo Rama
Greyson Semsekwa
Jose Mara
Khaleed Chokoraa

Msanii Bora wa Kike - Bendi
Anneth Kushaba
Luiza Mbutu
Mary Lucos
Vumilia

Msanii Bora anayechipukia
Ali Nipishe
Angel
Bonge la Nyau
Mirror
Vanessa Mdee

Video Bora ya Wimbo ya Mwaka
Baadae - Ommy Dimpoz
Kamili gado - Professor J Feat Marco Chali
Marry Me - Rich Mavoko
Nichum - Bob Junior
Party Zone - AY Feat Marco Chali

Mtunzi Bora wa Mashahiri - Taarab
Ahmed Mgeni
Hemed Omary
Khadija Kopa
Mzee Yusuf
Thabit Abdul

Mtunzi Bora wa Mashahiri - Bongo Flava
Ally Kiba
Barnaba
Ben Pol
Linex
Ommy Dimpoz

Mtunzi Bora wa Mashahiri - Hip Hop
Fid Q
Joh Makini
Kala Jeremiah
Mwana Fa
Stamina

Mtunzi Bora wa Mashahiri - Bendi
Chalz Baba
Grayson Semsekwa
Jonico Flower
Jose Mara
Khaleed Chokoraa

Mtayarishaji Bora wa Mwaka - Muziki wa Kizazi Kipya
Bob Junior
Ima the boy
Man Water
Maneke
Marco chali
Mensen Selecta

Mtayarishaji wa Wimbo wa Mwaka - Taarab
Bakunde
Enrico

Mtayarishaji wa Wimbo wa Mwaka - Bendi
Allan Mapigo
Amoroso

Mtayarishaji Chipukizi wa Mwaka
Imma the Boy
Mensen Selecta
Mr T Touch
Sheddy Clever

Rappa Bora wa Bendi
Fagasoni
Greyson Semsekwa
J4
Jonico Flower
Sauti ya Radi

Wimbo wenye vionjo vya asili
Aambiwe - offside trick
Atatamani - AT
Boma la utete - Young D
Chocheeni kuni - Mrisho Mpoto Feat Ditto
Mdundiko - Momba Feat Juma Nature

Wimbo Bora wa Bendi
Chanzo ni sisi - Mapacha watatu
Jinamizi la Talaka - Mlimani Park Orchestra
Risasi kidole - Mashujaa band
Shamba la twanga - African Stars band

Wimbo Bora wa Reggae
Hii si ya waoga - Yuzzo
Kilimanjaro - Warriors from The East
NATAFUTA PARADISE - Mac Malick Simba
Salvation - Delayla Princess
Tunda - Hardmad

Wimbo Bora wa Africa Mashariki
Fresh All Day - Camp Mulla
Make you dance - Keko Feat Madtrax
Maswali ya polisi - DNA
Still a Liar - Wahu
Valu Valu - Jose Chameleone

Wimbo Bora wa - Bongo Pop
Aifola - Linex Feat fundi Samweli
Baadae - Ommy Dimpoz Feat Angel
Chuki Bure - Sharo Milionea Feat Dully Sykes
Marry Me - Rich Mavoko
Me and you - Ommy Dimpoz Feat Vanessa Mdee

Wimbo Bora wa Kushirikiana/kushirikishwa
Chuki Bure - Sharo Millionea Feat Dully Sykes
Mapito - Mwasiti Feat Ally Nipishe
Me and U - Ommy Dimpoz Feat Vanessa Mdee
Sihitaji marafiki - Fid Q Feat Yvonne
Single Boy - Alikiba Feat Lady Jaydee


Wimbo Bora wa Hip Hop
Alisema - Stamina Feat Jux
Bum kubam - Nikki wa Pili Feat G Nako
Dear God - Kala Jeremiah
Nasema Nao - Nay wa Mitego
Sihitaji Marafiki - FID Q Feat Yvonne

Wimbo Bora wa RnB
Amerudi - Belle 9
Kuwa na Subira - Rama Dee Feat Mapacha
Maneno maneno - Ben Pol
Pete - Ben Pol

Wimbo Bora wa Ragga/ Dancehall
Je ni nani - Ras Six
Muda upite - Susu Man
Predator - Dabo
Push Dem - Dr Jahson
Take it down - Chibwa and Tanah

Wimbo Bora wa Taarab
Mjini chuo kikuu - Khadija Kopa
Mpenzi chocolate - Jahazi [Mzee Yusuph]
Si bure una mapungufu - Isha Mashauzi [Mashauzi Classic]
Sina muda huo - Jahazi [Leila Rashid]
Siwasujudii Viwavi jeshi -Isha Mashauzi [Mashauzi Classic]

Wimbo Bora wa Zouk/Rhumba
Gubegube -Barnaba
Mapito - Mwasiti Feat Ally Nipishe
Nashukuru umerudi - Recho
Ni wewe - Amini
Sorry - Barnaba

Bendi Bora ya Mwaka CD1 African Stars Band
Mapacha wa tatu
Mashujaa Band
Mlimani Park Orchestra [Sikinde]
Msondo Ngoma Music band

Kikundi Bora cha Taarab
Dar modern Taarab
Five stars modern Taarab
Jahazi Modern Taarab
Kings modern Taarab
Mashauzi Classic

Kikundi Bora cha Muziki wa Kizazi Kipya
Jambo squad
Makomando
Tip Top Connection
Tmk wanaume family
Weusi

Wednesday, April 24, 2013

GODBLESS LEMA ANASAKWA NA POLISI KWA NGUVU ZOTE....WANADAI KUWA YEYE NDO MWANZILISHI WA VURUGU ZA ARUSHA LEO


Kikosi cha kutuliza ghasia mkoani Arusha kililazimika kutumia Mabomu ya Machozi kuwatuliza wanafunzi waliokuwa wakishinikiza kuandamana baada ya mwanafunzi mwenzao kuuawa kwa kuchomwa kisu na watu wasiojulikana majira ya saa nne usiku wa kuamkia leo.  

 Tukio hilo liliamsha hisia za wanafunzi hao na kuwafanya wakusanyike kuelekea kwa mkuu wa mkoa wa Arusha kwa madai kwamba matatizo yao huwa hayafikishwi ipasavyo, hivyo wanataka kuyawasilisha wenyewe.   

Juhudi za uongozi wa chuo kuwatuliza wanafunzi hao zilishindikana, na ilipofika majira ya saa nne asubuhi, Mbunge wa jimbo la Arusha alifika katika eneo hilo kuwasikiliza wanafunzi hao. 

"Tunatoa dakika thelathini mkuu wa mkoa awe ameshafika hapa, kama hajafika ndani ya muda huo, tunaandamana wote, mimi mbele nyie nyuma mpaka ofisini kwake" alisema 

Mheshimiwa Lema.Baada ya mkuu wa mkoa kufika eneo la tukio aligoma kuzungumza na wanafunzi hao, akidai kwamba hawezi kuongea mpaka Mh.Lema aondoke, ndipo atapanda kuzungumza na pia alilalamika kwamba hamna kipaza sauti kwa hiyo hawez kupaza sauti yake kuzungumza na watu wasio na nidhamu. 
 
Maneno hayo yalipandisha hasira ya wanafunzi hao lakini walitulizwa, na kipaza sauti kikaandaliwa katika ukumbi wa chuo maaruf kama "main cafetaria" ili mkuu huyo azungumze.
Wanafunzi walikusanyika eneo hilo kumsikiliza lakini alivyoanza kuongea, wanafunzi walisikika wakimzomea kwa madai kwamba ameonesha dharau.  
Wanafunzi walianza kuzomea na kumrushia chupa zaa maji na mawe  mkuu wa mkoa na hapo ndipo ilibidi mabomu ya machozi yatumike kuwatuliza wanafunzi wa chuo hicho. 
Kwa muda wa masaa mawili imekuwa ikisikika milio ya mabomu chuoni hapo mpaka hali ilipo tulia kabisa. 
Kwa sasa hali ni shwari chuoni hapo ila polisi wametapakaa huku na kule wakisema wanamtafuta Mbunge wa jimbo la Arusha kwa madai kuwa ndiye anaye chochea mgomo huo wa wanafunzi. 

Mbunge huyo alikimbia kuelekea kusikojulikana na kutelekeza gari yake chuoni hapo, ambayo polisi walilazimika kuivuta kwa "breakdown" car kuelekea kituo cha polisi. kama inavyoonekana katika picha.
Gari ya Mh.Godbless Lema ikiochukuliwa na polisi kutoka eneo la tukio
Polisi wakichukua gari ya mbunge wa jimbo la Arusha

PICHA: HUU NDO UNYAMA WALIOTENDEWA WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

Picha  ya  marehemu  Henry Koga  baada  ya  kuchomwa  kisu  na  kufariki  hapo hapo  jana  usiku  katika  chuo  cha  uhasibu  Arusha.....

Mwanafunzi  huyo  Alikuwa Masomoni Mida Ya Usiku Na Alipomaliza Aliondoka Na Kuelekea Maeneo Ya Esami. Kabla Hajafika Eneo La Malazi (Hostel) alipigiwa Simu na Mwenzake amsubiri Ili Waende Wote Hostel. 
   Marehemu  Henry  katika enzi za uhai wake....

Wakati anamsubiri Rafiki Yake Kwenda Hostel, Kuna Bajaj Ilifika Eneo Hilo Na Watu Hao Wasiojulikana Wakataka Pesa Kutoka Kwa Mwanafunzi Huyo...Wakati  wakiendelea  kuzozana, rafiki  yake  naye  alifika.....
 
Majibu Ya Wanafunzi Hao Hayakuwafurahisha Watu Hao Na Ndio Walipochomoa Kisu Na Kumchoma Mmoja wa Vijana Hao Tumboni Na Shingoni na Kupoteza Maisha Hapo Hapo....

Mauaji  hayo  yamesababisha  vurugu  kubwa  chuoni  hapo  zilizopelekea  kupigwa  mawe  mkuu wa  mkoa

UMEZISOMA HIZI?

VURUGU KUBWA CHUO CHA UHASIBU:....MKUU WA MKOA APIGWA MAWE, GODBLESS LEMA AFICHWA..!!


Vurugu  kubwa  zimeibuka  chuo  cha  uhasibu cha Arusha   baada ya mwanachuo kuchomwa kisu na mwanaakijiji na kufariki dunia....

Baada  ya  tukio  hilo, wanafunzi  walitoa  taarifa  kwa  mkuu wa chuo lakini  hakuwapa msaada wowote.


Walipokosa  msaada,wanafunzi  hao walianza  kuandamana  na taarifa zikafikishwa kwa mbunge  Godbless  lema ....


Mbunge  huyo  bila   hiyana akawasili na kufanikiwa kuwatuliza wanachuo hao maana nyumbani kwa Godbless  lema si mbali na chuo hicho ...

Baada  ya  taarifa  kumfikia Mkuu wa mkoa, ilimbidi  aliwasili na kuanza kuzungumza na wanachuo lakini baada ya kugundua uwepo wa Lema alianza kuongea  kwa  lugha  mbovu  na  ndipo wanachuo walipo kasirika na kuanza kumpiga mawe.


Hali  ilipochafuka,FFU  waliingia kazi  ya  kutuliza  ghasia...Hali ni mbaya sana lakini cha kushangaza askari mmoja aliwatonya wanachuo wamfiche Lema


Godbless  Lema  anasakwa mpaka sasana  hajulikani alipo baada ya wanachuo kumficha kusiko julikana.








Monday, April 22, 2013

RAIS TENGA ATOA MIPIRA YA DOLA 30,000


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ametoa mipira zaidi ya 1,200 yenye thamani ya dola 30,000 za Marekani kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na vituo 21 vilivyo hai vya kuendeleza vijana (academies).
Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) lilimpa Rais Tenga fedha hizo ikiwa ni shukrani kwake kwa kushughulikia mgogoro wa uongozi wa mpira wa miguu nchini Kenya uliodumu kwa miaka miwili; ambapo nchi hiyo kutokana na mgogoro huo ilikuwa na vyama viwili (KFF na FKL).
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mipira hiyo kwenye ofisi za TFF, Dar es Salaam leo (Aprili 22 mwaka huu), Rais Tenga amesema amefanya hivyo kwa vile anaamini kuwa mipira ndiyo kitu muhimu katika kuinua mchezo huo mahali popote.
“Dhamira yangi si kushukuru kwa hafla hii, bali kutoa sababu kwa nini nimefanya hivi. Ninaamini kwa kuanzia mipira ndiyo muhimu, pili kwa kufanya hivi itaonekana kweli mipira imegawiwa,” amesema Rais Tenga.
Amesema amesema mpira wa miguu kwa Tanzania unahitaji sana watu wa kujitolea, na yeye amefanya hivyo kwa kujitolea kutokana na ukweli shughuli anazotumwa na FIFA ni za kujitolea.
Rais Tenga ambaye pia alitumwa na FIFA kutatua matatizo ya uongozi wa mpira wa miguu katika nchi za Uganda, Zambia na Sudan Kusini amesema anaamini anapata fursa hizo kutokana na kuwa kiongozi wa TFF, na kwa kuwakumbuka waliomchagua ndiyo maana hakusita kupeleka fedha hizo kwenye mipira.
Amesema moja ya ndoto zake wakati anaingia kuongoza TFF mwaka 2004 ameshindwa kutimiza ni kusaidia mipira, kwani uwezo wa kununua mipira kwa wanaocheza katika ngazi ya chini hasa watoto haupo.
“Hizi kelele zote za maendeleo ya mpira wa miguu ni kwa sababu shuleni hakuna vifaa. Nia yangu ilikuwa shule zote zipate mipira, lakini hiyo ni moja ya ndoto nilizoshindwa kutekeleza. Vipaji haziwezi kupatikana kama watoto hawachezi.
“Tunashukuru sana kwa Serikali kurejesha mpira shuleni. Hata nitakapoondoka madarakani nikipata nafasi nitaendelea kuomba mipira kwa ajili ya shule,” amesema Rais Tenga.
Vyama vya mikoa ambavyo jumla ni 32 (Tanzania Bara na Zanzibar) kila kimoja kimekabidhiwa mipira 25 (kumi saizi namba tano, 15 saizi namba nne kwa ajili ya vijana). Kwa academies ambazo ni 21 kila moja imepewa mipira 25 (minane saizi namba tano, na 15 saizi namba nne).
Viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Almasi Kasongo, Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) Nassib Mabrouk na Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Riziki Majala.