This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Wednesday, September 11, 2013

NJEMBA YAMKUTA MAZITO

NJEMBA moja iliyojulikana kwa jina la Haji Bakari maarufu kama Mchome limekamatwa baada ya kudaiwa kutapeli kiasi cha shilingi 570,000 kwa njia ya simu za mkononi.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, njemba hilo lilifanikisha utapeli huo kwa kutumia majina ya watu wanaofahamiana na washirika kibiashara.

Kijana huyo aliomba pesa hizo kwa madai kuwa gari lake limemharibikia maeneo ya Chalinze mkoani Pwani hivyo alihitaji kiasi hicho ili aweze kulitengeneza. Bila hiyana, aliyeombwa alitoa fedha hizo kwa moyo mmoja ingawa kwa awamu mbili.

Akizungumza na gazeti hili, mtu aliyetapeliwa aliyejitambulisha kwa jina la Godilizen Moshi alisema baada ya kumkamata mtu huyo, alijihami na kusema kuwa aliyefanya mchezo huo ni pacha wake.

Akisimulia mkasa huo, Moshi alidai: “Kijana huyu ni mzoefu na alikuwa…

Haruni Sanchawa na Makongoro Oging'
NJEMBA moja iliyojulikana kwa jina la Haji Bakari maarufu kama Mchome limekamatwa baada ya kudaiwa kutapeli kiasi cha shilingi 570,000 kwa njia ya simu za mkononi.
Haji Bakari akipandishwa kwenye difenda.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, njemba hilo lilifanikisha utapeli huo kwa kutumia majina ya watu wanaofahamiana na washirika kibiashara.
Kijana huyo aliomba pesa hizo kwa madai kuwa gari lake limemharibikia maeneo ya Chalinze mkoani Pwani hivyo alihitaji kiasi hicho ili aweze kulitengeneza. Bila hiyana, aliyeombwa alitoa fedha hizo kwa moyo mmoja ingawa kwa awamu mbili.
...Akiwa ndani ya difenda.
Akizungumza na gazeti hili, mtu aliyetapeliwa aliyejitambulisha kwa jina la Godilizen Moshi alisema baada ya kumkamata mtu huyo, alijihami na kusema kuwa aliyefanya mchezo huo ni pacha wake.
Akisimulia mkasa huo, Moshi alidai: “Kijana huyu ni mzoefu na alikuwa akitumia simu nambari 0655 301646, nilimuamini baada ya kunitajia jina la mtu ambaye nafahamiana na tunashirikiana kibiashara.”
Alisema baada ya kukamilisha kumpatia kiasi hicho cha fedha alizoomba alimpigia simu ili kuhakiki kama amezipata lakini ilipopokelewa, mpokeaji alisema alikuwa mazishini mkoani Kilimanjaro, kitu ambacho kilimshtua na kuhisi kutapeliwa.
Baada ya hapo, Moshi aliwataarifu ndugu zake na mara moja msako mkali dhidi ya tapeli huyo ukaanza.
“Nilipagawa baada ya kujibiwa kuwa niliyemtumia fedha yuko Kilimanjaro, jibu hilo lilinichanganya sana,” alisema Moshi.
Kwa mujibu wa Moshi, alitafuta watu wa kumsaidia kumkamata mtu huyo na hatua yao ya kwanza ilikuwa ni kwenda ofisi za mtandao wa Tigo zilizopo Mlimani City jijini Dar ili kujua sehemu halisi alipo tapeli huyo.
Baada ya kueleza tatizo lao, mfanyakazi wa kampuni hiyo aliwaeleza kuwa mtu mwenye namba hiyo anapatikana eneo la Ubungo Kibangu, jijini Dar es Salaam.
“Na kweli tulipoenda Kibangu tukiwa na wenyeji wa huko tulifanikiwa kumpata kirahisi sana na kumchukua, kutokana na kibano alichopewa alisema sio yeye aliyetapeli bali ni pacha wake,” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, ACP Camilius Wambura alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema mtuhumiwa amekamatwa. “Tunamchunguza kabla ya kumfikisha kortini,” alisema.

DENTI ALIYEDAI KUZAA NA DIAMOND... AUMBUKA, ATISHIA KUJIUA


Video: Sasha siku alipokuwa akiongea na GPL kuhusu madai ya kuzaa na Diamond.
MREMBO Sasha Juma, 20, kwa sasa anapitia kipindi cha majuto, analipia gharama ya kujivalisha ubandidu na kujisingizia kupewa mimba na supastaa, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’.
 Sasha Juma akiongea na…

Video: Sasha siku alipokuwa akiongea na GPL kuhusu madai ya kuzaa na Diamond.
MREMBO Sasha Juma, 20, kwa sasa anapitia kipindi cha majuto, analipia gharama ya kujivalisha ubandidu na kujisingizia kupewa mimba na supastaa, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’.
Sasha Juma akiongea na GPL..
Sasha, akiwa na macho makavu, alitamka mbele ya waandishi wetu kuwa mimba hiyo aliyopewa na Diamond, ilimgharimu kufukuzwa shule akiwa kidato cha nne mwaka jana.
Unadhani Sasha analo tena? Ameshaumbuka na baada ya simulizi yake ya kutunga kushtukiwa, hivi sasa mrembo huyo anatishia kujiua.
Mr. Juma ambaye ni baba mzazi wa Sasha, aliliambia Risasi Mchanganyiko: “Huyu mtoto ametishia kujiua, anajua makosa aliyoyafanya. Anataka kutuvuruga vichwa, ukweli ni kwamba kila alichokisema kuhusu Diamond ni uongo mtupu.
“Nahisi kuna mtu yupo nyuma yake, sasa anataka kumtumia ili kumchafua Diamond, upande mwingine akili yangu inaniambia yule mtoto anataka umaarufu, maana najua yule ni mwigizaji, sasa pengine anataka kutoka.”
Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’.
UONGO WA SASHA
Risasi, lilipata taarifa kuhusu malalamiko ya Sasha ambaye alikuwa akidai kupotezewa dira ya maisha na Diamond kwa sababu alimpa mimba na kumtelekeza na mtoto mwenye umri wa miezi minne.
Baada ya kupata ‘tipu’ hiyo, mwandishi wetu alimsaka kwa udi na uvumba mpaka Septemba 4, mwaka huu (Jumatano ya wiki iliyopita) ambapo mrembo huyo alitia maguu kwenye mjengo mkubwa wa magazeti pendwa nchini Tanzania, Global Publishers Ltd.
Baada ya kuwasili makao makuu ya Global Publishers, Bamaga, Mwenge, Dar es Salaam, Sasha aliingizwa kwenye chumba maalum chenye mitambo ya kurekodi sauti na picha kisha akaanza kumwaga simulizi yake.
Alidai kuwa alikutana na Diamond, Mlimani City, mwaka jana, wakapeana namba za simu kabla ya kuanzisha uhusiano wa kimapenzi ambao uliwafikisha kwenye ‘kategori’ ya kuparamia kitandani na kutenda mchezo wa baba na mama pasipo kutumia na kinga.
“Nilipopata mimba Diamond alinishawishi nisitoe, akaniahidi atanisomesha hata kama nitafukuzwa shule. Baadaye nilifukuzwa shule, akazidi kunipa moyo kwamba atanilinda. Mimba ilipokuwa kubwa akapotea, nilipozaa hakujitokeza.
“Diamond akawa siyo yule ambaye alikuwa ananipa moyo. Alibadilika, hali hiyo ikanifanya nione mwanangu hana baba, hata cheti za kuzaliwa, sijamwandika Diamond, mtoto wangu nimempa ubini wa baba yangu, yaani ya Juma.”
Sasha akiwa na mtoto aliyedai ni wa Diamond.
NI UONGO MTAKATIFU
Ili kukamilisha habari hiyo ambayo ilitoka kwenye gazeti hili, toleo la Jumamosi iliyopita, mwandishi wetu aliwasiliana na baba mzazi wa Sasha (Mr. Juma) ambaye alipoambiwa kuhusu mwanaye kuzaa na Diamond, alishtuka kisha akasema:
“Unajua yule mtoto sikai naye, anaishi na mama yake. Mimi sijui chochote ila nashangaa, inawezekanaje apate mimba mpaka azae mimi baba yake sijui? Ngoja niongee na mama yake.”
Mr. Juma alipiga simu kuzungumza na mama yake Sasha mbele ya mwandishi wetu. Mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo;
MR. JUMA: Habari yako.
MAMA SASHA: Salama tu, za kwako?
MR. JUMA: Namshukuru Mungu, ebwana mbona Sasha kaongea na mwandishi wa habari anasema kapewa mimba na Diamond na amezaa?
MAMA SASHA: Wewe si unajua haya mambo ya vijana?
MR. JUMA: Mambo ya vijana kivipi? Ina maana mtoto anapata ujauzito mpaka anazaa wewe na baba yake hamjui?
MAMA SASHA: Baba nani, si wewe?
MR. JUMA: Mimi baba yake sijui, ndiyo maana nakuuliza wewe, maana nimesikia umekuwa unawasiliana na Diamond kuhusu hili.
MAMA SASHA: Nani kakwambia? Nimeshasema hayo ni mambo ya watoto, naomba umuulize mwanao vizuri, kama hauna namba yake nikutumie.
Katika mazungumzo hayo, Mama Sasha, hakumpa majibu ya moja kwa moja mzazi mwenzake, kuhusu binti huyo kupata mimba, kuzaa na Diamond kuwa mhusika.

RIPOTI YA WIKI HII
Mr. Juma alifika ofisi za Global Publishers na kueleza: “Jana (Jumapili iliyopita), nilimchukua Sasha na kuzungumza naye kwa kirefu, kwa kifupi alikiri kuwa hajawahi kupata mimba na yule mtoto si wa kwake.
“Mtoto imebainika ni wa dada yake, yaani mtoto mkubwa wa Mama Sasha ambaye anaitwa Khadija. Kuna kitu cha kujifunza hapa kuwa Sasha aliwadanganya mpaka watu ambao niliwakabidhi ili wamsaidie kisanii.
“Kabla sijaongea kwa kirefu na Sasha, nilizungumza na Thabit Abdul (mwanamuziki wa Five Stars) ambaye nilimkabidhi kwake kumsimamia kisanii, nikamuuliza inakuwaje mtoto anapata mimba? Akanijibu hata yeye anashangaa. Kwani hata yeye alishangaa kumuona Sasha akiwa na picha nyingi amebeba mtoto kwenye simu yake.
“Akamuuliza umezaa akajibu ndiyo. Hisia zangu zinazunguka katika mambo mawili, ama aliamua kutunga ili kupata umaarufu kupitia jina la Diamond au alitumwa na mtu. Jana wakati nazungumza na Sasha, nilikasirika sana, nikaona hatutafika pazuri.
“Ikabidi nimpigie simu rafiki yangu mmoja ili amwite azungumze naye. Kweli alimwita wakazungumza, baadaye yule rafiki yangu akaniambia Sasha kasema anaona mambo yanazidi kuwa makubwa, kwa hiyo anataka kunywa sumu afe. Namshangaa sana huyu mtoto, sijui ana kichaa gani?”

UKWELI NI HUU
Kwa mujibu uchunguzi wetu usio na shaka, mtoto aliyepigwa picha akiwa amebebwa na Sasha, mama yake halisi ni dada wa mrembo huyo ambaye ni Khadija.
Sasha na Khadija wanaunganishwa na mama yao lakini kila mmoja ana baba yake.
Uchunguzi zaidi ulibaini kuwa kwa sasa Khadija anaishi na mwanaye mkoani Tanga, huku Sasha akiendelea kupuyanga ndani ya Jiji la Dar, akiwa hajui tamu wala chungu ya kunyonyesha, vilevile hajawahi kusikia uchungu wa uzazi wala hatambui sura ya ‘leba’ ilivyo.
Khadija akizungumza kupitia simu ya Mr. Juma, huku mwandishi wetu akifuatilia mazungumzo, alisema: “Nikija Dar nitafika Global, mimi ndiyo mama wa yule mtoto na zile picha Sasha alipiga na mtoto siku ya arobaini yake.
“Sasha anataka kunisababishia matatizo na baba mzazi wa mtoto. Mimi kama mama mzazi wa mtoto, simjui Diamond, kwa hiyo hahusiki chochote na mtoto wangu.”
Aidha, Mr. Juma alisema kuwa alimpigia simu Diamond na kumuweka sawa kuhusiana na tuhuma ambazo binti yake alimsakizia.
“Diamond anajua kila kitu, nimeshaongea naye na nimejaribu kumtaka atulize munkari, maana ni wazi zile taarifa zimemchukiza sana. Kweli zimemchukiza.”

DIAMOND ANASEMAJE?
Gazeti hili lilipozungumza na Diamond, alisema: “Nilishasema simjui huyo Sasha, ahadi yangu ipo palepale, nitampeleka mahakamani. Amenichafua sana.
“Masharti yangu ni haya, kama anataka nimsamehe aende kweye redio na televisheni akatangaze kwamba sijampa mimba.”

ONYO
Aibu ambayo Sasha anakutana nayo sasa na tishio la kuburuzwa mahakamani ambalo analikabili kutoka kwa Diamond ni onyo kwa watu wengine ambao wamekuwa na tabia za kuwasingizia wenzao ili kujipatia umaarufu.
Risasi linazo taarifa kwamba tangu alipoumbuka, Sasha amekuwa mtu wa kujificha, akikwepa kukutana na watu ambao wanajua mkanda mzima wa simulizi yake ya kutunga.

Rais Kikwete azindua miradi ya maji na umeme Sengerema

0L7C0442Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Katika kijiji cha Katunguru/Nyamtelela wilayani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Kulia ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe. 0L7C0638Mwakilishi wa Serikali ya watu wa Marekani Bwana Karl Fickenscher akitoa hati ya kukabidhi mradi wa MCC I kwa waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo wakati wa  hafla ya ufunguzi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambaza umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa wilayani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Katikati akishuhudia ni Afisa mtendaji Mkuu wa Millenium Challenge Account-(MCC)Tanzania Bwana Bernard Mchomvu. 0L7C0665Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya utekelezaji wa mradi wa umeme wa MCC unaotekelezwa katika mikoa ya Mwanza na Geita wakati wa  hafla ya ufunguzi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambaza umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa wilyani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo. 0L7C0717Mwakilishi wa Millenium Challenge Account nchini Tanzania Bwana Karl Fickenscher akipanda mti wa kumbukumbu muda mfupi baada ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua mradi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambazia umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa,Wilayani Sengerema leo. Kushoto ni Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na kulia ni Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo(picha na Freddy Maro)

RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AZURU WILAYA YA SEGEREMA

IMG_1853Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akivishwa skafu kutoka kwa chipukizi mara tu baada ya kuingia wilayani Sengerema kwa ziara ya siku moja tarehe 10.9.2013. IMG_1893Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Katunguru kilichoko wilayani Sengerema alipokwenda kijijini hapo kwa kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Katunguru/ Nyamtelela tarehe 10.9.2013. IMG_1930Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Katungulu/Nyamtelela utakaogharimu shs milioni 734 na utawanufaisha zaidi ya watu elfu kumi. IMG_1981Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Luchili akiwa njiani kwenda katika kijiji cha Bukokwa kuzindua rasmi mradi wa umeme tarehe 10.9.2013. IMG_2008Wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini sherehe za uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini uliofanywa na Rais Kikwete huko Bukokwa wilayani Sengerema tarehe 10.9.2013. IMG_2032 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokea hati ya makabidhiano ya mradi wa umeme wa Bukokwa uliofadhiliwa na Millenium Challenge Co-operation ya Marekani. IMG_2082Rais Jakaya Kikwete akiangalia michoro inayoonyesha usambazaji wa umeme katika mkoa wa Mwanza. IMG_2090Rais Dkt. Jakaya Kikwete akizindua rasmi mradi wa umeme wa Bukokwa tarehe 10.9.2013
PICHA NA JOHN LUKUWI

DIWANI WA TLP :SIASA SI UADUI, AMFAGILIA KINANA KWA BUSARA ZAKE

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa pamoja na diwani wa TLP Ntabo Majabi kata ya MwendaKulima wakati wa uzinduzi wa jengo la kituo cha afya kilichodhaminiwa na mgodi wa Buzwagi kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
……………….
Na Adam Mzee
DIWANI wa Kata Mwendakulima Ntabo Majabi kupitiaTanzania Labour Party (TLP), amesema Katibu Mkuu wa CCM Abdulrhaman Kinana ni kiongozi mwenye busara na hekima kubwa na ndio maana Rais Jakaya Kikwete amemua kumpa nafasi hiyo kwa kuwa atakuwa anamjua vizuri.
Akizungumza katika uzinduzi wa kituo cha afya katika eneo hilo, alisema amefurahishwa na aina ya siasa ambazo zinafanywa na Kinana na yeye binafsi ametambua kuwa Katibu Mkuu huyo wa CCM anaouwezo mkubwa wa kufanya kazi zake.
“Kinana wewe ni jembe, wakati unazungumza nilikuwa nimekaa mbali na kusikiliza lakini maelezo yako yamenifurahisha na ndio maana nimeamua kuja kukupa mkono.Kama nchi hii ingekuwa na makatibu wakuu wengi wa aina yako, tungepiga hatua hasa katika siasa za nchi hii.
“Pia niwaambie wananchi siasa si ugomvi, Kinana ameeleza vizuri, tunatakiwa kushirikiana ili kufanikisha malengo ya kuwatumikia wananchi.Nakupongeza mzee Kinana kwa maelezo yako yamenipa faraja licha ya kwamba mimi ni diwani kupitia TLP,”alisema.
Ndugu Kinana alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wananchi kuwa CCM ndio yenye Serikali na diwani huyo licha ya kuwa TLP bado anatekeleza ilani ya CCM , hivyo wananchi nao wanatakiwa kutambua hakuna sababu ya kulumbana kwasababu tu ya mambo ya siasa.

HODGSON APUMUA INGAWA KAZI IPO, ATOKA 0-0 NA UKRAINE, MECHI DHIDI YA MONTENEGRO NA POLAND NDIO MAHAKAMA YAKE!!

Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
MENEJA wa Timu ya Taifa ya England, maarufu `Simba Watatu`, Roy Hodgson amepumua kidogo katika harakati zake za kuwania kucheza fainali za kombe la Dunia mwakani nchini Brazi baada ya kutoka suluhu dhidi ya Ukraine jana usiku.
England iliingia uwanjani kupambana kwa nguvu bila ya nyota wake Wayne Mark Rooney, Dany Welbeck na Daniel Sturrage kutokana na sababu tofauti.
Sturrage na Rooney ni majeruhi, wakati Welbeck alikuwa anatumikia kadi aliyopewa mechi ya nyuma.
Juni 19, 2012, ilikuwa mara ya mwisho kwa England kushinda mechi ya ushindani, lakini si dhidi ya Moldova au San Marino bali Upinzani wa siku hiyo ulikuwa dhidi ya Ukraine, na toka hapo, England imeshakutana mara mbili na wakali hao na kushindwa kuibuka na ushindi.
England wamebakiwa na mechi dhidi ya Montenegro pamoja na Poland mwezi ujao na wanatakiwa kupata ushindi ili kukata tiketi ya  kcuheza fainali za kombe la Dunia mwakani nchini Brazil.
Na mechi hizo watacheza katika dimba lao la Taifa la Wembley, hivyo kujipa matumaini ya kufanya vizuri.
Late drama: Frank Lampard heads one just past the post in second half stoppage timeDuuh!: Frank Lampard akipiga kichwa na kugonga mwamba dakika za majeruhi kipindi cha pili
Right place right time: Steven Gerrard nips in to stop Yarmolenko as Joe Hart gets ready to make a saveSehemu  na muda sahihi: Steven Gerrard akimdhibiti Yarmolenko huku Joe Hart akiwa tayari kuokoa
Centurion: Frank Lampard (left) gets a header on goal during his 100th capKapiga mechi ya 100: Frank Lampard (kushoto)  akipiga kichwa golini katika mechi yake ya 100
Deep in thought: Roy Hodgson looks to have a lot on his mind on the touchlineDimbwi la mawazo: Roy Hodgson akionekana kutoamini kinachoendeleaDesperate dive: Joe Hart flings himself across goal as Yevhen Konoplyanka's free kick is deflected wideKazi ya nguvu: Joe Hart akijaribu kuokoa mpira wa adhabu uliochongwa na Yevhen Konoplyanka
Kikosi cha Ukraine: Pyatov, Fedetskiy, Khacheridi, Kucher, Shevchuk, Stepanenko, Edmar, Gusev (Bezus 68), Yarmolenko (Khomchenovskiy 90), Konoplianka, Zozulya (Seleznyov 90). Subs: Koval, Dedechko, Tymoschuk, Mandzyuk, Grechyshkin, Morozyuk, Rakitskiy, Devic,
Khudzamov.
Kikosi cha England: Hart, Walker, Cahill, Jagielka, Cole, Lampard, Gerrard, Wilshere (Young 68), Walcott (Cleverley 89), Lambert, Milner. Subs: Ruddy, Smalling, Baines, Caulker, Carrick, Barkley, Defoe, Sterling, Townsend, Forster.

SADC yamuonya Kagame kuhusu mipango yake ya kuivamia Tanzania baada ya kuomba msaada wa kijeshi toka Kenya na Uganda

MZOZO wa kidiplomasia alioibua Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa Rais Jakaya Kikwete, sasa unaonekana kuchukua mwelekeo mpya, baada ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kumuonya kiongozi huyo kuacha mara moja fikra zozote mbaya dhidi ya Tanzania, MTANZANIA Jumatano limedokezwa. 



Habari za uhakika na za kuaminika kutoka miongoni mwa viongozi wa juu wa SADC na maofisa wa Serikali, waliokuwa katika ujumbe wa Rais Jakaya Kikwete aliyekuwa akihudhuria Mkutano wa viongozi wa Maziwa Makuu huko Uganda hivi karibuni, zinaeleza kuwa tayari Jumuiya hiyo imekwisha mpatia ujumbe huo mmoja wa mawaziri aliyekuwa ameandamana na Kagame muda mfupi baada ya kikao chake na Kikwete.

Taarifa ambazo MTANZANIA Jumatano imezinasa, zinaeleza kuwa, kiongozi mmoja wa juu wa Msumbiji ambaye alikuwa pia Uganda, alikaririwa akimueleza Waziri huyo wa Kagame kuacha kabisa fikra za kuishambulia Tanzania, kwa sababu ya uamuzi wake wa kupeleka vikosi vyake Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.

“Uamuzi wa Tanzania na Afrika Kusini kupeleka majeshi DRC, ni msimamo wa pamoja wa SADC. Vitisho vyovyote dhidi ya Tanzania au uvamizi wa kijeshi, utachukuliwa ni uvamizi dhidi ya SADC, hivyo tutakuwa tayari kuingia vitani kupigana upande wa Tanzania,” alikaririwa akisema ofisa huyo wa juu wa Msumbiji.

Inaelezwa kuwa, SADC imetoa msimamo huo baada ya kubaini kuwa hasira ya sasa ya Kagame dhidi ya Rais Kikwete, msingi wake unatokana na hatua ya Tanzania kupeleka vikosi vyake nchini Kongo kwenda kupambana na vikundi vya waasi vikiwemo vile vinavyodaiwa kuwa na ushirika na majeshi ya Rwanda.

Taarifa hizi zinathibitishwa na habari ambazo gazeti hili ilizinasa jana kupitia gazeti la The Namibian la nchini Namibia, ambalo liliandika kuwa Jeshi la nchi hiyo (NDF), ambalo linaunda kikosi maalumu cha SADC, lilikuwa limeanza kushiriki mazoezi huko Jangwani karibu na Walvis Bay. Mazoezi hayo yatadumu hadi Oktoba 15 mwaka huu.

Inaelezwa kuwa wakati mazoezi hayo yakiendelea, Mkuu wa majeshi ya Namibia (NDF), Luteni Jenerali, Epafras Ndaitwah aliwakumbusha washiriki hao kuwa kwa sasa wanachama wenzao kama Wanajeshi wa Tanzania na Namibia, wanapambana na maadui wa amani Kongo na kwamba lazima wajiandae kwa hali yoyote ambayo haitabiriki.

Hatua hiyo ya sasa ya SADC, na sifa ambazo imepata kummwagia Rais Kikwete kwa namna alivyosimamia mizozo wakati akiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi, inaonyesha wazi jinsi Jumuiya hiyo ilivyotayari kuwa upande wa kiongozi huyo.

Kutokana na hilo, baadhi ya wachambuzi na wafuatiliaji wa mambo wanasema kuwa si ajabu basi Kagame na Serikali yake wakawa wanafahamu msimamo huo wa SADC, ambao haujawekwa hadharani hasa kwa kuzingatia uamuzi wake wa kuungana na Uganda na Kenya katika usharika wao wa hivi karibuni.

Pia hatua ya nchi yake kusaini mkataba wa kiusalama na nchi nyingine tano wa kusaidiana kijeshi endapo mmoja wao atavamiwa na nchi nyingine, imeelezwa kuwa na mwelekeo huo huo wa Kagame kuanza kujihami.

Nchi ambazo zimeingia mkataba huo na Rwanda ni pamoja na Ethiopia, Kenya, Uganda na Sudan Kusini.

Hata hivyo wachambuzi na wafuatiliaji wa mambo, wamekosoa muungano huo wa kusaidiana kijeshi na Rwanda, wakidai kuwa ni wa mashaka ukilinganisha na ule unaounda SADC ambao unajengwa na matendo ya kihistoria.

Wameitolea mfano Ethiopia, kwamba ni rahisi kuasi kutokana na mfumo wake wa kijeshi unaoongozwa kwa mkono wa chuma, huku wanajeshi wake wakiwa katika hali mbaya ya kiuchumi.

Wameulinganisha mfano huo na nchi moja tu ya Zimbambwe ambayo inaunda SADC kwamba, pamoja na matatizo yote ya migogoro ya kisiasa na kidiplomasia inayoyakabili, lakini jeshi lake lipo imara na linatunzwa vizuri.

Wakati wadadisi na wachambuzi wa mambo wakiwa na mtizamo huo, hatua ya sasa ya SADC imekuja wakati ambapo tayari Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma aliwahi kuionya Rwanda akisema kuwa endapo nchi hiyo itajaribu kuigusa Tanzania, atakuwa tayari hata peke yake kupeleka jeshi lake kupambana nchini humo.

Nje ya SADC, nchi zinazounda Jumuiya hiyo kama Afrika Kusini, Msumbiji, Zimbabwe, Namibia na Angola zinaguswa moja kwa moja na hisia za Tanzania, kutokana na historia yake ya kushiriki kwenye ukombozi na uhuru wa nchi hizo.

Kutokana na hilo, wachambuzi hao wanasema kuwa si rahisi kwa wao kukaa kando pale watakapoona maslahi ya Tanzania yanachezewa, hasa linapokuja suala la kuichokoza.

Taarifa hizo za SADC zimekuja ikiwa ni siku chache baada ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kuinyooshea kidole cha lawama Rwanda, kitendo hicho kinaonekana kuungwa mkono kwa kasi na makundi mengine ya kimataifa.

Kagame ambaye kwa miaka mingi amekuwa kiongozi kipenzi cha mataifa mengi tangu alipofanikiwa kumaliza mapigano yaliyosababisha mauaji ya halaiki nchini kwake mwaka 1994, katika siku za hivi karibuni taswira yake inaonekana kubadilika na kuchukua mwelekeo wa uadui zaidi kuliko urafiki.

Hilo linatokana na kile kinachodaiwa kuwa Serikali yake imekuwa ikihusika kuwasaidia waasi wa kundi la M23, wanaoendesha mapambano dhidi ya majeshi ya Serikali ya Kongo, jambo linalopingwa na Jumuiya ya Kimataifa pia wanatuhumiwa kwa ubakaji na mauaji ya watu wasiokuwa na hatia.

Tuhuma hizo ndizo ambazo zinamuweka Rais Kagame katika hatari na wingu la mashaka kwa sasa, hasa baada ya uhusiano wake na Tanzania kupita katika wakati mgumu kutokana na kuingia kwenye mgogoro na Rais Kikwete ambaye alimshauri kukaa meza moja ya mazungumzo na waasi wa FDLR.

Thursday, August 29, 2013

TRAFIKI FEKI MAZITO TENA!





MAZITO tena yameibuka kuhusu yule trafiki feki James Hussein, mkazi wa Kimara Matangini, jijini Dar es Salaam ambaye yuko  Gereza la Segerea, Dar akikabiliwa na kesi ya kujifanya askari wa usalama barabarani, Amani lina mpya hiyo.
Trafiki feki James Hussein akiwa kwenye gari baada ya kunaswa.
Habari za ndani kutoka Gereza la Isanga, Dodoma zinadai kuwa, trafiki huyo ana mambo mengi ya kushangaza ambayo Watanzania wengi hawayajui.
JINA HALISI

Mtoa habari wetu alisema kuwa,…
Na Mwandishi Wetu
MAZITO tena yameibuka kuhusu yule trafiki feki James Hussein, mkazi wa Kimara Matangini, jijini Dar es Salaam ambaye yuko  Gereza la Segerea, Dar akikabiliwa na kesi ya kujifanya askari wa usalama barabarani, Amani lina mpya hiyo.
Trafiki feki James Hussein akiwa kwenye gari baada ya kunaswa.
Habari za ndani kutoka Gereza la Isanga, Dodoma zinadai kuwa, trafiki huyo ana mambo mengi ya kushangaza ambayo Watanzania wengi hawayajui.
JINA HALISI
Mtoa habari wetu alisema kuwa, James Hussein si jina halisi la trafiki feki huyo. Alisema jina lake halisi ni Ali Kinanda.
...Mtuhumiwa huyo akiwa na watuhumiwa wenzake.
“Yule jamaa anaitwa Ali Kinanda, sisi kumwona kwenye picha gazetini akijiita James Hussein tulishangaa sana,” kilisema chanzo chetu.
YADAIWA ALIKUWA ASKARI MAGEREZA
Chanzo kikazidi kudai kwamba, kuanzia mwaka 1984 jamaa huyo alikuwa ni askari magereza katika Gereza la Butimba, Mwanza hadi mwaka 1987 alipoacha.

...Akiwa mikononi mwa polisi.
ADAIWA KUNASWA UJAMBAZI, ATUPWA JELA MIAKA 30
Mtoa habari wetu aliendelea kumwanika trafiki feki huyo kuwa, mwaka 2002 mtuhumiwa huyo alidaiwa kupata msala wa tukio la ujambazi lililotokea Mpwapwa, Dodoma ambapo kesi yake iliunguruma hadi mwaka 2003 ambapo hukumu ilitolewa yeye na wenzake kwenda jela miaka 30.
 “Mwaka 2002 mpaka 2003, Kinanda alipata kesi ya ujambazi akiwa na wenzake, sikumbuki idadi yao. Kesi iliisha kwa hukumu ya miaka 30 jela kwenye Gereza la Isanga hapa Dodoma,” alisema mnyetishaji huyo.
“Akiwa gerezani, Kinanda alionekana mtiifu kiasi kwamba alipewa cheo cha kusimamia wenzake, yaani mnyapara wakiamini anaendelea vizuri na kifungo chake hicho.
Trafiki feki katika pozi baada ya kudakwa.
“Hakuna aliyejua kama jamaa anaweza kutoroka. Ama kweli moyo wa mtu anaujua mwenyewe. Hivi hapa (Gereza la Isanga) wafungwa wenzake wameshangaa kusikia jamaa amekuwa trafiki huko Dar es Salaam,” kilidai chanzo.
ADAIWA KUTOROKA JELA
Habari zaidi ziliendelea kudai kwamba, Desemba 10, 2012 akiwa gerezani, mfungwa huyo alitoroka katika mazingira ya kutatanisha akiwa chini ya uangalizi wa askari magereza aliyejulikana kwa jina moja la Shaibu.
Ilidaiwa kuwa, baada ya picha yake kuonekana kwenye gazeti, askari magereza wa Isanga waliutaarifu uongozi mara moja ambapo nao ulituma wachunguzi  jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza mchakato wa kumtia mikononi mfungwa huyo ili akamalizie kifungo chake cha miaka thelathini jela.
Inadaiwa kuwa, wachunguzi hao ambao ni askari magereza  wapo Dar wakisubiri siku ya kesi ya kujifanya trafiki itakapopelekwa kusikilizwa kwa hakimu.

HABARI MPYA, ADAIWA KUFARIKI DUNIA SEGEREA, DAR
Wakati mnyetishaji wetu kutoka gerezani Isanga Dodoma akianika madai ya siri hiyo nzito, Agosti 26, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Mwandishi Wetu, Makongoro Oging’  alipata taarifa kuwa, mtuhumiwa huyo wa kutenda kosa la kujifanya trafiki amefariki dunia ghafla akiwa gerezani Segerea.
Ilibidi mwandishi wetu amtafute Msemaji wa Jeshi la Magereza Tanzania, Meja Mtiga Omar na kumuuliza kuhusu madai hayo ya kifo ambapo alisema:
“Si kweli kwamba amekufa, bali ana tuhuma nyingine ya kutoroka gerezani ambapo tutamfungulia mashitaka mengine  ya kutoroka akiwa gerezani anatumikia kifungo chake.”
Juhudi za kumpata Mkuu wa Gereza la Isanga, Dodoma zilishindikana baada ya simu yake ya mkononi kuita kwa muda mrefu bila kupokelewa.
James Hussein kama ndiye Ali Kinanda yupo Gereza la Segerea, hadi Septemba 5, 2013 kesi yake itakaporudi tena mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Joyce Minde kwa ajili ya kusikilizwa.

MTOTO MIAKA 7 ALEA FAMILIA

Na Imelda Mtema

WAZAZI ambao hawajajulikana walikotokomea wamewatelekeza watoto wao wanne wanaoishi Kata ya Bangulo, Pugu, Ilala, jijini Dar es Salaam, Amani lina mkasa wote.

Mazigira ya nyumba ya watoto hao ni ya kutoa machozi hata kwa mtu mwenye roho ngumu kama jiwe. Nyumba iko hivyo, pa kulala ni chini, wadudu kibao huku wakiwa hawajui hatima yao.

Majirani ndiyo waliowaibua watoto hao baada ya kubaini kuwa baba yao hajaonekana kwa miezi kadhaa nyumbani hapo hali iliyosababisha wengine kulia.

Akizungumza na paparazi wetu juzikati,  Sarah Shija (7) ambaye ndiye anayelea familia hiyo kwa sasa, aliwataja wenzake, Kevin Shija (8), Babu Shija (5) na Brighton Shija (6).

Alisema  mama yao mzazi aliondoka nyumbani hapo miaka miwili iliyopita baada ya kutokea mzozo kati yake na…
Na Imelda Mtema
WAZAZI ambao hawajajulikana walikotokomea wamewatelekeza watoto wao wanne wanaoishi Kata ya Bangulo, Pugu, Ilala, jijini Dar es Salaam, Amani lina mkasa wote.
Mazigira ya nyumba ya watoto hao ni ya kutoa machozi hata kwa mtu mwenye roho ngumu kama jiwe. Nyumba iko hivyo, pa kulala ni chini, wadudu kibao huku wakiwa hawajui hatima yao.
Majirani ndiyo waliowaibua watoto hao baada ya kubaini kuwa baba yao hajaonekana kwa miezi kadhaa nyumbani hapo hali iliyosababisha wengine kulia.
Akizungumza na paparazi wetu juzikati,  Sarah Shija (7) ambaye ndiye anayelea familia hiyo kwa sasa, aliwataja wenzake, Kevin Shija (8), Babu Shija (5) na Brighton Shija (6).
Alisema  mama yao mzazi aliondoka nyumbani hapo miaka miwili iliyopita baada ya kutokea mzozo kati yake na baba yao na kwenda kusikojulikana licha ya kwamba siku hiyo walimsihi sana mama huyo asiondoke.
Sarah aliendelea kuweka wazi kuwa, baada ya mama yao kuingia mitini, baba yao ndiyo akawa kila kitu lakini kumbe  na yeye alikuwa na lake moyoni.
Alisema miezi minne iliyopita, asubuhi baba yao aliamka asubuhi na kuwaachia shilingi 5,000 na kiasi kidogo cha unga kwenye kiroba na kuondoka akisema angerudi jioni.
“Mara ya mwisho baba alipoondoka alituambia angerudi jioni, akatuachia shilingi elfu tano kwa ajili ya kununua mboga na vitu vingine,” alisema Sarah.
Sarah alisema tangu siku hiyo baba yao  hakurudi tena huku wao wakiwa wamebaki wenyewe na elfu tano aliyowaachia ikiwa imeisha.
Alisema hali hiyo iliwalazimisha kusimama masomo kutokana na ugumu wa maisha kwa sababu mara nyingi wanaamka asubuhi wakiwa na njaa hivyo kushindwa kuelewa kinachofundishwa na walimu.
“Tunalala na njaa, tunaamka na njaa, tunashinda na njaa sasa tusingeweza kwenda shule kwa sababu tunakuwa tunatetemeka mwili. Hatujui baba atarudi lini,” alisema Sarah na kuangua kilio.
Alisema imefika hatua nduguze wakishikwa na kiu anawapeleka kunywa maji machafu ya kwenye madimbwi ambayo pia yana chumvi kupita kiasi kwa sababu hawana  fedha (shilingi mia nne) ya kununua maji salama.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Sarah alimuomba baba yao  popote alipo kurudi nyumbani na kuendelea na maisha. Pia walimtaka mama yao akisoma habari hii akawachukue kwani maisha yao ni magumu sana na yeye analazimika kufanya shughuli nyingi za nyumbani ili kuhakikisha uhai wao haukatishwi na njaa.
Ili kujua maisha yao zaidi ya kusikitisha usikose kuangalia Kipindi cha Wanawake Live cha Mtangazaji Joyce Kiria ambacho kitaonesha ‘live’ maisha magumu ya watoto hao.