This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, July 11, 2013

RAIS KIKWETE AWASHANGAA CHADEMA KUTAKA KAMBI YA KUJILINDA...DR. SLAA NAYE AWATAKA POLISI WAYAVUNJE MAKAMBI YA CCM


Rais wa Tanzania amewashangaa na kuwalaani CHADEMA kwa kutangaza kufundisha vijana namna ya kujilinda na kusema kuwa ni watu wa ajabu kama wamefikia huko.

Mh. Rais kayasema hayo katika kuhitimisha kongamano la amani  huku bwana Cheyo  nae akisema  kuwa  hata kama  ni kutaka kuwa rais wa nchi CHADEMA wamefika kubaya....


Wakati  mh. Rais  akiwashangaa CHADEMA,Katibu Mkuu wa chama  hiyo,  Dr Wilbroad Slaa amelitaka jeshi la polisi kuvunja mara moja makambi yote ya CCM nchini yanayotoa mafunzo kwa vijana wanaoitwa Green Guards.
 

Kauli  hiyo  ya Dr. Slaa  imekuja  baada  ya  polisi  kuwazuia  CHADEMA kuanzisha  kambi  yoyote  ya  kujihami  na  kwamba  hatua  kali  za kisheria  zitachukuliwa  dhidi  yao  endao  watakaidi  agizo  hilo

Dk. Slaa, amesema kauli ya Jeshi la Polisi inadhihirisha namna wahusika wasivyofahamu sheria kwa kile alichoeleza kuwa wao hawaundi majeshi bali vikundi vya ukakamavu.

Alisema ni heri msemaji wa jeshi hilo angekaa kimya kuliko kulifedhehesha Jeshi la Polisi kwa tamko lisilokuwa na ushawishi wa kisheria.


“Nawashauri hawa waanze na Tendwa…ila kwanini wameanza leo sisi tulishayalalamikia makundi ya CCM kwa barua na hata walipomaliza mafunzo yao kule Igunga tukapiga na picha wao hawakuinua mdomo kuliongelea,” alisema Dk. Slaa.

Alisema katika miaka minne iliyopita CHADEMA ilikuwa ikionyesha kwa ushahidi namna vijana wa CCM wanavyopewa mafunzo ya kijeshi, ikwamo silaha kutoka nje ya nchi huku wahusika wakiendelea kukaa kimya.

Aliongeza kuwa hali hiyo ya kuamka baada ya kauli ya CHADEMA inatia nguvu shaka yao, aliyodai kuwa makundi ya CCM yanafanya mafunzo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi.

Dk. Slaa alitolea mfano kundi la vijana wa CCM walioweka kambi katika shule ya wazazi katika Kata ya Ivumwe, Mbeya mjini na kisha kuwateka katibu wa CHADEMA Mbeya mjini na baadhi ya wanachama wake.

Alisema katika tukio la Ivumwe wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani wa hivi karibuni, CHADEMA walitoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi wa Mbeya ambaye aliwajibu kuwa wapeleke ushahidi kama vijana hao ni wahalifu.

Alibainisha kuwa CCM imekuwa na kawaida ya kukusanya vijana kutoka maeneo tofauti na kisha kuwapa mafunzo ya kijeshi na silaha kwa ajili ya kuwadhuru wapinzani na kutolea mfano Kambi ya Ulemo aliyosema ilikuwa na vijana waliopewa mafunzo ya kijeshi.

“Tunawasubiri tuone hatima yao ni nini, sisi tunajua Jeshi la Polisi limeshajitoa  kulinda viongozi wa CHADEMA sasa kwanini tusijilinde wenyewe,” alisema Dk. Slaa.

Source: BBC, Tanzania Daima,Jamii Forum

PICHA YA MREMBO AKIWA KATIKA POZI LA NUSU UCHI YADAKWA

 Katika  hali  ya  kushangaza, mrembo huyu   anayejiita  Emmy  alijikuta   akitupia  picha  yake  ya  uchi ( kifua wazi ) katika  mtandao  wa Badoo....

Haijafahamika  mara  moja  kama  picha  hiyo  iliwekwa  makusudi  au  kimakosa  maana  iliondolewa  ndani  ya  dakika  chache  tangu iwekwe......
 Profile  ya mrembo huyo  katika mtandao huo  inaonesha  kwamba  yupo Arusha.

MWANAMKE AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MITANO JELA BAADA YA KUMTUPA MTOTO WAKE CHOONI

Mwanamke mmoja mkazi wa Manga A Jijini Mbeya amehukumiwa kifungo cha miaka 5 jela kwa kosa la kutupa mtoto wake chooni.
Tukio hilo lilitokea Juni 14, Mwaka huu katika eneo hilo baada ya watoto waliokuwa wakicheza kugundua kuwepo kwa Mtoto katika choo cha shimo.
 
Mtuhumiwa baada ya kukamatwa amekiri kutenda kosa hilo na kwamba alifanya hivyo baada ya mzazi mwenzie kumkataa.
Ameongeza kuwa amelazimika kutupa katika choo cha jirani kwa sababu ni cha shimo tofauti na chao ambacho asingeweza kutupa mtoto huyo.
  
Rukia Haruna (31)  akitolewa nje  na Askari wa Jeshi la Polisi akitolewa nje ya  Mahakama kwenda Gerezani kutumikia kifungo cha miaka 5 Jela  
 
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Zabibu Mpangula, amemtaja Mtuhumiwa kuwa ni Rukia Haruna (31) mkazi wa Manga A Jijini Mbeya na kwamba kosa lake ni kinyume cha kifungu  218 kifungu kidogo cha 35 sura ya 16 ya mwaka 2002.
Na  Mbeya yetu

Tuesday, July 9, 2013

HUYO NDO "MELLIS EDWARD" ALIYEKAMTWA NA MADAWA YA KULEVYA AKIWA NA "AGNESS MASOGANGE

Picha  ya  Mrembo Mellis Edward  aliyedakwa  na  madawa  ya  kulevya  Afrika  kusini  akiwa  na  Agness Masogange
Mellis Edward
Inahisiwa kuwa  huyu mwanamke wa pili aliyetajwa na Kamanda Nzowa kwa jina la “Melisa Edward”  ni mdogo wake na Agnes ambaye katika akaunti ya facebook anayo tumia jina la (MELLIS EDWARD) , Agnes amemuweka katika orodha ya family kama ‘sister’ katika akaunti yake ya Facebook.
 Kamanda  Gofrey  Nzowa - Kitengo  cha  Madawa ya Kulevya


 Agness Masogange  akiyahesabu  "MAPESA" yake.Picha  hii aliiweka  siku  chache  zilizopita

"NASUBIRI WAKATI MWAFAKA WA KUMUONYESHA KIKWETE YA KWAMBA MIMI NI NANI".....HILI NI TISHIO LA KIHUNI LA RAISI KAGAME WA RAIS KIKWETE

Nikiwa  katika  upekuzi  wangu, nimeshtushwa sana na kauli za  KIHUNI  za Rais  Paul Kagame  dhidi ya  Rais wetu Kikwete na nchi yetu kwa ujumla....

Rais Kikwete ameepuka malumbano na Kagame kwa  kukaa  kimya , lakini inaelekea Kagame  anadhani ukimya wa Kikwete ni uoga kwake  au labda anatafsiri kuwa anadharauliwa.....

Nadhani  huu  ni  wakati  mwafaka  kwetu  sisi  watanzania  kuungana  na  kumuunga  mkono  rais  wetu  juu  ya  huu  UPUMBAVU  wa  Kagame....

Kagame  ni  lazima  atambue  kwamba  watanzania  tupo  tayari  kuilinda  nchi  yetu  kwa  gharama  yoyote  na  kamwe  hatuwezi  kuwa  VIBARKA  wa  Rwanda...

Ifuatayo  ni  Kauli  ya  Kihuni  aliyoitoa  Rais  Kagame  Kwa  Taifa  letu:
-------------------------------------------------------------

.....“Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR and urging negotiations… negotiations? 


 Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete] did not deserve my answer.


 I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…”“


It is in these ominous terms that the Rwandan dictator General Paul Kagame threatened to get even with Tanzanian President Jakaya Kikwete, while addressing Rwandan Youth on June 30, 2013 during a summit called “Youth Konnect”“, sponsored by his wife, Janet Kagame.


Relations between Tanzanian President Jakaya Kikwete and Rwandan leaders have soured in the last weeks. On several occasions Rwandan leaders called the Tanzanian President “a genocide and terrorist sympathizer”, “ignorant”, “arrogant”, and “mediocre leader”. 

The relations have deteriorated following the recommendation by President Jakaya Kikwete of open negotiations between Rwandan, Ugandan and Congolese leaders and their respective armed opposition in order to bring durable peace and security in the African Great Lakes region....
 


source..I will Just Wait For You At the Right Place And I will Hit You, Rwandan General Paul Kagame Threatens Tanzanian Jakaya Kikwete

MANDELA BASI TENA

Johannesburg, Afrika Kusini

MADAKTARI wanaomtibu Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, wanakubali kuwa kiongozi huyo basi tena kwani hali yake ni tata na sasa wanasubiri kiungo kimojawapo cha mwili wake kishindwe kufanya kazi ndipo wazime mashine inayomsaidia kupumua.
Nelson Mandela.
Kutokana na subira hiyo madaktari hao sasa wamebadili msimamo wao wa awali wa kuiondoa mashine hiyo inayomsaidia kupumua.

“Madaktari hao, wameishauri familia yake kuachana na ushauri wa awali wa kuiondoa mashine hiyo hadi tu pale moja ya kiungo chake muhimu cha mwili…
Johannesburg, Afrika Kusini
MADAKTARI wanaomtibu Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, wanakubali kuwa kiongozi huyo basi tena kwani hali yake ni tata na sasa wanasubiri kiungo kimojawapo cha mwili wake kishindwe kufanya kazi ndipo wazime mashine inayomsaidia kupumua.
Kutokana na subira hiyo madaktari hao sasa wamebadili msimamo wao wa awali wa kuiondoa mashine hiyo inayomsaidia kupumua.
“Madaktari hao, wameishauri familia yake kuachana na ushauri wa awali wa kuiondoa mashine hiyo hadi tu pale moja ya kiungo chake muhimu cha mwili kitakaposhindwa kufanya kazi,” alisema rafiki wa Mandela, Denis Goldberg ambaye alikuwa mpigania uhuru aliyewahi kufungwa pamoja na Mandela.
Amesema madaktari hao waligusia kuhusu suala la kuondoa mashine lakini baadaye walikataa kwa kuwa kiongozi huyo aliweza kusogeza baadhi ya viungo na kutambua sauti.
“Ni kweli kuwa hali ya Mandela ni mbaya lakini si kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika,” alisema Goldberg.
Juzi vyombo vya habari vya hapa nchini vilitoa hati ya kiapo ya mahakama, ikionyesha kuwa madaktari hao waliishauri familia ya Mandela kuondoa mashine ya kumsaidia kupumua kwani asingeweza kuendelea kuishi.
Hata hivyo, msemaji wa Rais Jacob Zuma,Mac Maharaj alikataa kuzungumzia kuhusu hati ya mahakama ambayo ilieleza kuwa Mandela mwenye miaka 94 yupo mahututi.

WATOTO WAWILI WALIOKUWA WAMEPELEKWA "JANDONI" WAMEFARIKI WA AJALI YA MOTO HUKO LINDI

 Lindi- Watoto wawili wamekufa na mmoja wao kunusurika mauti, baada ya kuungua kwa moto uliosababishwa na kibatari kilichounguza nyasi za kijumba walichokuwemo.

Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga amesema ajali hiyo ilitokea mwishoni mwa wiki jana katika


mtaa wa Mitwero, katika kata ya Rasbura ya Manispaa ya Lindi na kuwataja waliokufa kuwa ni Maliki Kasimu (7) na na Selemani Fadhili (5) wakati aliyenusurika ni Juma Abdallah.

Mzinga amesema watoto hao watatu waliofika kwa mzee mmoja wa jadi, walikuwa wakijenga nyumba kwenye michezo yao wakati wakiwasubiri wenzao wafike siku za usoni, tayari kwa shughuli ya jando.

Siku ya tukio, moto huo ulishika nyasi zilizokuwa ndani ya shimo na kuwaka na kuwachoma Maliki na Selemani ambapo mwenzao, Juma alifanikiwa kukimbia na kujiokoa.

Wanakijiji wanasema mwangalizi wa jando hilo alikuwa mbali na eneo la tukio na hivyo kushindwa kuwaokoa


-Via Wavuti