This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Monday, March 25, 2013

JAMABAZI SUGU LAUWAWA KWA KUPIGWA RISASI MLIMA NYOKA JIJINI MBEYA



Mwili wa Jambazi sugu  Emanuel Blasius Mdendemi ukiwa umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa Mbeya

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya  Diwani akiangalia mwili jambazi lililouwawa na kikosi cha polisi Mbeya



Baadhi ya polisi na waandishi wa habari wakiwa nje yajengo la kuhifadhia maiti katika hospitali ya rufaa Mbeya

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika Mkutano alioufanya na waandishi wa Habari Ofisini kwake ambapo alisema tukio hilo lilitokea  jana majira ya Saa 10(kumi) Alfajiri

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani akionyesha baadhi ya siraha alizokutwanazo jamabazi huyo aliyeuwawa



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani akionyesaha hirizi iliyofungwa katika bunduki aliyokuwa anatumia jambazi huyo kama kinga katika matukio yake 

Hii ndiyo hirizi iliyofungwa katika bunduki aliyokuwa anatumia jamabazi huyo jamani waganga wakienyeji acheni hizo kuwadanganya watu matokeo yake ni kuongeza uhalifu nchini hakika nao tutawashughulikia kwani wamekuwa chanzo cha uhalifu nchini hayo yamesemwa na kamanda Diwani





Kamanda Diwani akiongea na waandishi wa habari

MTU mmoja ambaye anasadikiwa kuwa ni jambazi ameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Jeshi la Polisi akiwa kwenye harakati za kuteka magari katika Eneo la Mlima Nyoka Jijini Mbeya baada ya kutokea kwa majibizano ya kurushiana risasi.
  
Jambazi huyo ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Polisi Mkoani hapa akituhumiwa kuhusika na mauaji ya Askari Polisi mwenye namba G 68 PC Jafari yaliyotokea  Februari 6, Mwaka huu  katika eneo la Matundasi Wilayani Chunya.
  
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika Mkutano alioufanya na waandishi wa Habari Ofisini kwake ambapo alisema tukio hilo lilitokea  jana majira ya Saa 10(kumi) Alfajiri .
  
Kamanda Diwani alisema kabla ya tukio majambazi wapatao wanne  tayari walikuwa wameweka mawe barabarani kwa nia ya kuteka magari ili wafanye uporaji katika eneo hilo la Mlima Nyoka ambalo limekuwa na matukio kadhaa ya watu kuporwa mali zao.
  
Alisema Jeshi la polisi baada ya kupata habari za kutegwa mawe, askari walifika kwa wakati kwa kuwa polisi walikuwa jirani na eneo hilo na kuweka mtego kwa kuwa majambazi hawakuwa wameonekana kwa wakati ule.
  
Aliongeza kuwa baada ya muda majambazi walipoona taa za gari walijitokeza tayari kushambulia lakini kabla ya hapo polisi walitoa amri ya kujisalimisha kinyume chake wakaanza kupiga risasi ovyo ndipo mashambulizi ya polisi yakafanywa.
  
Diwani alisema katika mapambano hayo alijeruhiwa jambazi mmoja kwa risasi kiunoni na ubavuni kulia na wengine watatu walifanikiwa kutoroka ambapo Marehemu alipowahishwa hospitali kwa matibabu daktari alibaini kuwa amekwisha fariki.
  
Alisema  jambazi huyo alikutwa na silaha moja SMG yenye namba  AB huku namba  nyingine zikiwa zimefutwa na magazine yake ikiwa na risasi ishirini na mbili (22) pamoja na mapanga mawili([2).
  
Aliongeza kuwa baada ya  Marehemu kufanyiwa upekuzi maungoni mwake jambazi huyo alikutwa na kitambulisho cha mkazi chenye namba B.0010453 chenye jina la Emanuel Blasius Mdendemi aliyezaliwa mwaka 1984 eneo la Matamba wilayani Makete Mkoa wa Iringa makazi yake ni Uwemba Mkoani Njombe.
  
“Jambazi huyu amebainika kuwa ni miongoni mwa majambazi waliokuwa kwenye mtandao wa majambazi uliokamatwa hivi karibuni kuhusiana na matukio waliyofanya Mikoa mbalimbali ikiwemo Mbeya,Njombe na Iringa.aidha amebainika kushiriki katika tukio la mauaji ya askari polisi PC Jafari wa kituo cha Mkwajuni – Chunya tarehe 06.02.2013.” Alisema Kamanda Diwani.
  
Aliongeza kuwa  ufuatiliaji wa majambazi waliotoroka unaendelea kufanywa ambapo pia  anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za wahalifu hao azitoe bila kuchelewa kwa jeshi la polisi ili zifanyiwe kazi.

Pia  amewatahadhalisha majambazi na wahalifu wa makosa yeyote kuachana na uhalifu kwa kuwa ni biashara isiyo na faida badala yake wafanye shughuli halali kupata maendeleo ambazo fursa zake ni nyingi.

"SIKUONA HAJA YA KUFIKIRIA MARA MBILI KUMSAIDIA KAJALA MILIONI 13 ILI ATOKE SEGEREA"...WEMA SEPETU AFUNGUKA


Mrembo Wema Sepetu leo amemake headline baada ya kutoa mfukoni mwake shilingi milioni 13 kulipa faini aliyopigwa muigizaji mwenzie Kajala Masanja aliyehukumiwa leo kwenda jela miaka mitano ama kulipa kiasi hicho cha fedha.
Kajala na Wema wakikumbatianaKajala na Wema wakikumbatiana
Akiongea  kwa  kujiamini, Wema amesema hakufikiria mara mbili kutoa kiasi hicho cha fedha.

“Kusema kweli wanasemaga kwamba kutoa ni moyo so naamini what I did is best, nimetoa kwasababu I had to do it and sikuthink twice kuhusu kufanya hivyo,” amesema Wema.
Wema akwa na KajalaWema akwa na Kajala
“Nimefanya kama namsaidia rafiki yangu kama namsaidia ndugu yangu na sidhani kama ingekuwa ni kitu kizuri kumuona mwenzako anaingia kwenye dhahama, kwenye tabu, kwenye mateso na wakati nina uwezo wa kumsaidia kwahiyo I just did what I had to do.”

Kuachiwa kwa Kajala kumepokelewa kwa furaha kubwa na mastaa mbalimbali nchini.

Cpwaa

So I hear Kajala is out! Good news..Hongereni sana wana BOngoMovies! Bongoflava tujipangeni..tutaendelea kupigwa bao kila siku while we are sitting on a Multi-Billion Industry, it’s time to stop fantasizing posing in front of camera poppin bottles of Champagne,Rented Fancy cars,Cheap Wardrobe n ( No..The Ladies are fine,I love them too sitaki ubaguzi)… Tufikirie kibiashara zaidi na sio sifa tu.

Rio Pol

It’s a blessed Monday I say this because finally someone stood up and did something right and righteous. I’ve worked in the entertainment industry for the past seven years and no star or their glam team or entourage would do what Miss Wema Abraham Sepetu did. Thank you god both my girls Elizabeth Michael and Kajala Masanja are free. God bless you wema.
Kajala akikumbatiana na ZamaradiKajala akikumbatiana na Zamaradi
Mboni Masimba
KAJALA outtttttttttt# Mungu mkubwa # WEMA mwokozi wa KAJALA # Mwenyez Mungu akuzdishie na akupe ulipo pungukiwa. Una moyo wa pekee. Lov u always my Dogo

Saturday, March 23, 2013

Taswira Kutoka Unyaluni


222 ca02e
Mambo ya Analogia+Digitali , Picha ni mtaa wa Mwembetogwa mkoani Iringa
111 619ab
Inyeshe isinyeshe ulanzi utaletwa tu mjini Iringa

444 a6e46
Matunda Kwa afya:--Pichani ni mjasiriamali  na mteja wa matunda eneo la miyomboni mkoani Iringa
PICHA NA SAID  NG’AMILO  IRINGA.

Inyeshe isinyeshe ulanzi utaletwa tu mjini Iringa kama uonavyo mpanda baiskeli  akirejea kwao Tanangozi kijijini  kishauza nimoja ya ujasiliamali.

Magazeti Leo jumamosi


.


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

.
.






































































Waziri Sitta awaanika wabunge wa Afrika Mashariki kuhusu posho


Na: Gustav Chahe, Iringa
MTU mmoja amenusurika katika ajali baada ya gari alilokuwa akisafiria kuacha njia na kutumbukia kwenye mtaro wa maji. Ajali hiyo imetokea majira ya saa 11 alfajiri katika barabara ya Iringa – Dodoma maeneo ya Sabasaba katika Manispaa ya Iringa ambapo gari lenye namba za usajili T 287 AAG Prado limetumbukia kwenye mtaro kwa kile kilichoelezwa kuwa chanzo cha ajali hiyo ni
hitilafu katika maungio ya tairi (boll joint).
Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na kikosi cha uokoaji (K.B. WORKSHOP) zinasema kuwa baada ya kupata hitilafu katika tairi moja, gari lilipoteza mwelekeo na kuhama njia kasha kutumbukia kwenye mtaro.
Imeelezwa kuwa katika gari hilo alikuwemo dereva pekee ambapo hata hivyo hakupata majeraha makubwa.
Gari hilo lilikuwa likitokea mjini Iringa kuelekea Kihesa ambapo mara baada ya ajali hiyo imeelezwa kuwa dereva alikwenda kupumzika kutokana na maumivu ya majeraha aliyopata japo kuwa jina lake halikutajwa.
Mtandao huu umeshuhudia gari lenye namba za usajili T 332 AKP mali ya K.B.WORKSHOP wakiokoa gari hilo lililokuwa kwenye mtaro.