Wafanyakazi
walioajiriwa na shirika la Reli Tanzania (TRL) wakitoa mchanga kwenye
kichwa cha treni ya mizigo kilichopata ajali usiku wa kuamkia katika
stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa. Katika ajali hiyo watu wawili
wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa na kulazwa katika hospital
ya Benjamin Mkapa Wilayani Mpwampwa. Sehemu
ya mabehewa ya mafuta na ngano ambayo hayakusombwa na maji katika ajali
iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika stesheni ya Gulwe, hiyo imetokea
saa 9.15 usiku. Treni hiyo ya Mizigo ilikuwa ikitokea Dar es Salaam na
kuelekea Mkoani Kigoma na ilikuwa na mabehewa yaliyobeba ngano, sukari
na mafuta. Njia
ya Reli iliyoondolewa na maji katika stesheni ya Gulwe Wilaya ya
Mpwampwa kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha maeneno mbambali
nchini.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka akitoka kwenye maji
baada ya kuangalia kichwa cha treni kilichopata ajali na kusombwa na
maji katika stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa, usiku wa kuamkia leo,
0 comments:
Post a Comment