This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, April 4, 2013

"NALALIA PESA NA NACHAMBIA PESA"......HILI NI DONGO LA MANGE KIMAMBI AKIWA AMETAWANYA MIHELA KITANDANI


Mjasiriamali na blogger maarufu nchini, Mange Kimambi amegeuka Beyonce na kuwaambia wasichana wanaohate mafanikio yake ‘Bowdown bit**es I got lots of money.’
 

Kupitia blog yake yenye wasomaji wengi hasa wanawake, Mange ambaye kwa muda mrefu anaishi nje ya nchi na kurejea hivi karibuni akiuza aina ya nguo yaitwayo Bongolicious, amepost picha hizi na kuandika:

Finally, nimemaliza mahesabu ya leo…..Ngoja niingie kulala sasa… Arusha mmetishaaaaaa, nimewapendajeeeeeeeeee. “BOW DOWN BITCHES”…SHIKAMOO DADA MANGE WILL DO…….LOL. Ps: Nimewazidishiaje hasira????? Hehehehehehe.
Mange 2
And rumor has it that this boss lady is beefing with Sintah.
Katika Moja ya comments zinasema;

“Hahaha ki bibi sintah kimenunaje sasa hahah kusema kweli sintah anajishaua tena sana kama mdogo wake sabra yan wana midomo ya kinafki sana na hawana kitu kaz kujiona matawi na wakat no money in their pocket..

khaaa hiyo mipesa yeye anaipata kwa mwaka..mxxiii..na ndo maana aliolewa Uganda na pia ana mtoto tena mkubwa kamuacha hukohuko..

hv hamjiulizi kwa nin kila xaa yuko huko…anajishaua kwa kipi sasa hicho ki gar chake kimoja hhahha watu wana magar wana change kila siku…kha eti ana kaa sinza ptyuuuu,” ameandika msomaji mmoja.
mange 3
Hata hivyo si kila mmoja aliyekifurajia kitendo hicho.

“I love you so much, I always feel like I am your big sister. Please stop this, this is not classy at all. You are not ignoring them, just leave it alone and do you. I beggo Please. Please let go and let’s just talk about bongolious. Showing off the money and matusi is so unnecessary my sister. Please let’s focus on becoming billionaires,” ameandika mwingine.

MTUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRI MUSHI AFUTIWA MASHITAKA...DPP -ZANZIBAR ADAI KUWA HANA KOSA


Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Zanzibar, Ibrahim Mzee Ibrahim, ametupilia mbali uchunguzi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi uliofanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Maafisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na kusema mtuhumiwa hana kesi ya kujibu mahakamani.

Padri Mushi ambaye alikuwa Paroko wa Kanisa Katoliki Minara Miwili aliuawa kwa kupigwa risasi Febuari 17, mwaka huu katika eneo la Beitrasi mjini hapa akiwa ndani ya gari alipokuwa akielekea kuongoza misa ya Jumapili katika Kanisa la Mtakatifu Theresia, mjini Zanzibar.
Baada ya mauaji hayo, Rais Jakaya Kikwete alitoa kibali cha kukaribisha maafisa wa FBI kushirikiana na Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa mauaji hayo na Machi 17, mwaka huu Jeshi la Polisi lilimkamata Omar Mussa Makame kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo.
Uchunguzi wa NIPASHE umebaini kuwa DPP baada ya kulipitia jalada la uchunguzi wa mauaji hayo, juzi alitoa mwongozo kwa Jeshi la Polisi kuendelea kumtafuta muuaji wa Padri Mushi.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, DPP aliliandikia barua Jeshi la Polisi na kukabidhiwa juzi ikieleza sababu za ofisi yake kutofungua hati ya mashtaka hadi sasa dhidi ya mtuhumiwa wa mauaji hayo.
Jeshi la Polisi limethibitisha kuipokea barua ya DPP ambayo inaeleza kuwa ushahidi uliokusanywa katika jalada la kesi hiyo hauna mashiko na kwamba mtuhumiwa hahusiki na mauaji hayo.
Chanzo cha habari kutoka Jeshi la Polisi kilieleza kuwa DPP hajaridhishwa na uchunguzi wote uliokusanywa dhidi ya mtuhumiwa pamoja na watuhumiwa watatu wanaotuhumiwa kwa mauaji ya askari polisi, Said Abdulrahman aliyeuawa kwa kupigwa mapanga na watu wanaosadikiwa kuwa wafuasi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar Oktoba 17, mwaka jana.
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, alithibitisha hatua ya DPP kutupa uchunguzi wote wa jalada la mauaji ya Padri Mushi na kuwataka waandishi wa habari kumtafuta DPP azungumzie sababu za uamuzi wake wa kutokubaliana na uchunguzi wa Polisi.
Hata hivyo, alisema kwamba Jeshi la Polisi bado linaamini uchunguzi walioufanya kwa kushirikiana na FBI hauna shaka na kwamba mtuhumiwa huyo ana kesi ya kujibu mahakamani na wataendelea kumshikilia.
Alisema kwamba kwa mujibu wa sheria, Jeshi la Polisi jukumu lake ni kuchunguza kesi na ofisi ya DPP jukumu lake ni kufungua hati ya mashtaka na kutetea kesi mahakamani.
Hata hivyo, NIPASHE ilipofika katika ofisi ya DPP, Katibu muhtasi wake alisema amepokea maagizo kutoka kwa bosi wake kuwa waandishi wote wa habari wanaofuatilia suala hilo, wamuone Kamishna wa Polisi kwa vile kazi aliyopewa ya kupitia jalada la uchunguzi kabla ya kufungua kesi ameikamilisha.
“Kamishna ndiye aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari kuelezea hatua iliyofikiwa pamoja na kukamatwa kwa mtuhumiwa, sasa awaite tena amalizie kazi yake ya kuwaeleza hatua iliyofikiwa baada ya Mkurugenzi kurejesha jalada la mauaji,” alisema Katibu muhtasi huyo.
Katika hatua nyingine, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai, Yusuph Ilembo, jana alifika katika Mahakama Kuu ya Zanzibar, kufuatia ombi lililofunguliwa mahakamani na wakili anayemtetea mtuhumiwa wa mauaji, Abdallah Juma Mohamed.
Abdallah Juma amefungua ombi katika Mahakama Kuu kwa kutumia kifungu cha sheria 390 cha sheria namba 7 ya mwenendo wa makosa ya jinai ya mwaka 2004, akitaka Jeshi la Polisi litoe maelezo kwa nini mteja wake hajafikishwa mahakamani ndani ya saa 24 tangu alipokamatwa Machi 17, mwaka huu.
Wakili Abdallah Juma akisaidiwa na mawakili Shaban Juma Bakari na Shaibu Ibrahim Shaibu waliitaka Mahakama Kuu itoe amri ya kuachiwa kwa mteja wao kutoka mikononi mwa Jeshi la Polisi. Hata hivyo, Ilembo alisema kuwa kutokana na uzito wa kesi hiyo, anaomba kupewa muda wa kutayarisha majibu ya hati ya kiapo kwa maandishi na kuuwasilisha kwa upande wa utetezi na mbele ya mahakama hiyo kabla ya ombi hilo kuanza kusikilizwa na kutolewa uamuzi.
“Tunaomba mtuhumiwa aendelee kushikiliwa na Polisi, wakati tukifanya matayarisho ya kujibu hati ya kiapo,” alisema Ilembo.
Kwa upande wake Jaji wa Mahakama Kuu, Mkusa Isaack Sepetu, alisema baada ya kusikiliza pande zote mbili, alimtaka Ilembo awe amejibu kwa maandishi hati ya kiapo ya maombi hayo kabla ya kuanza kusikilizwa kwa shauri hilo Aprili 8, mwaka huu.
Aidha, Jaji alisema wakati wa kusikilizwa kwa shauri hilo, ametaka mtuhumiwa huyo afikishwe mahakamani, baada ya hoja za upande wa mawakili wanaomtetea kutaka dhamana kwa mteja wao, kwa vile bado hajafikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji.
Kutupwa kwa uchunguzi wa jalada la mauaji hayo pamoja na jalada la uchunguzi wa mauaji ya Polisi kunadhihirisha kuwapo kwa mvutano mkubwa baina ya Jeshi la Polisi Zanzibar na ofisi ya DPP.

Wednesday, April 3, 2013

WATUHUMIWA 11 WA GHOROFA LILILOANGUKA DAR WAFIKISHWA MAHAKAMANI...

HABARI  2  MUHIMU:
  • Hakimu aagiza mtuhumiwa wa wa mauaji ya padre Evaristus Mushi
Hakimu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Isaac Sepetu, ameagiza mtuhumiwa Omar Yusuf Makame wa mauaji ya Padre Evaristus Mushi afikishwe mahakamani mara moja siku ya Jumatatu wiki ijayo, ikiwa ni pamoja na nyaraka zinazoeleza ni kwa nini hakupandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka ndani ya saa 24 kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 390 cha mwenendo wa makosa ya jinai, sura na. 7 ya mwaka 2004. Maombi ya kufikishwa mahaknani yametoka kwenye jopo la mawakili watetezi wa mtuhumiwa.
  • Watuhumiwa wa jengo lililoporomoka mtaa wa Indira Gandhi, Dar, wafikishwa mahakamani


Mtuhumiwa namba moja wa mashitaka 24 ya kuua bila kukusudia Raza Hussein Ladha (aliyevaa kanzu nyeupe) na watuhumiwa wenzake 10, wamepandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
Picture
Raza Hussein Ladha (kulia) na watuhumiwa wenzake kumi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Picture
Watuhukiwa wakiondoka mahakamani baada ya kusomewa mashitaka

11 KORTINI KWA MAUAJI YA KUANGUKA KWA GHOROFA

Imeandikwa na  Happiness Katabazi via blog


HATIMAYE mfanyabiashara Razah Hussein Ladha na wenzake 10 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam tarehe 3 Aprili 2013, wakikabiliwa na jumla ya makosa 24 ya kuua bila kukusudia.


Mbali na Razah washitakiwa wengine ni Godluck Mbaga, Wilbroad Mugabisyo, Ibrahim Kisoki, Mohamed Abdubakari, Charles Salu, Zonazea Anage,Vedasto Ferand, Michael Hemed  Hemed, Albert  Jones na Joseph  Ringo ambao waliletwa jana saa  nane mchana chini ya ulinzi mkali wa wanausalama ambao walikuwa wakiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi Ilala (RCO), Duwani Nyanda.


Mbele ya Hakimu Mkazi Devotha Kisoka mawakili waandamizi wa serikali waliokuwa wakiongozwa na Bernad Kongora, Tumaini Kweka, Lasdlaus Komanya, Peter  Mahugo, Kinyeshi waliwasomea mashitaka hayo kwa kupokezana.


Wakili Kongora alidai mashitaka yote hayo 24 yanayowakabili washitakiwa wote yanafanana na kwamba wanakabiliwa na makosa ya kuua bila kukusudia kinyume na kifungu cha 195 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, kuwa   mnano Machi 29 mwaka huu huko katika eneo la Mtaa wa Indira Gandhi waliwaua watu 24 bila kukusudia.


Hata hivyo wakili Kongora aliwataka washitakiwa hao wajibu chochote kwakuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kwamba mahakama yenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ni Mahakama Kuu na kwamba upepelezi bado haujakamilika na kwamba wanaomba mahakama isiwapatie dhamana kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kuwapatia dhamana.


Hata hivyo mawakili wa utetezi zaidi ya saba ambao Jerome Msemwa, Adronicus Byamungu ,John Mhozya waliomba mahakama hiyo iwapatie dhamana na washitakiwa wanao wadhamini wakuaminika kwasababu tayari kuna maamuzi mbalimbali yalishatolewa na mahakama ya Rufaa na mahakama Kuu katika kesi za makosa ya kujaribu kuua. Mahakama hizo zilisema mahakama za chini zina mamlaka ya kutoa dhamana kwa kesi ambazo zinafunguliwa kwanza mahakama ya chini na kisha zinakuja kuamishiwa mahakama kuu kwaajili ya usikilizwaji.


Hata hivyo mawakili wa Serikali walipinga maombi hayo kwa maelezo kuwa maamuzi hayo ya mahakama rufaa yalitolewa kwenye kesi ya kujaribu kuua wakati kesi inayowakabili washitakiwa hao ni kuua bila kukusudia na kusisitiza kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na hivyo haina mamlaka ya kuwapatia dhamana.


“Mheshimiwa hakimu  sisi upande wa Jamhuri tunawasii mawakili wa washitakiwa wawe watulivu na wavumilivu kwani kesi hii ndiyo kwanza imefunguliwa leo, na upelelezi bado haujakamilika na sheria zilizotungwa na bunge zipo wazi kabisa zinasema ni Mahakama Kuu peke yake ndiyo yenye mamlaka ya kusikiliza kesi hii na si mahakama hii hivyo tunasisitiza kuwa mahakama hii haina mamlaka ya kutoa dhamana,” alidai wakili Kongora.


Itakumbukwa kuwa Machi 29 mwaka huu, ghorofa mmoja lililokuwa linajengwa katika mtaa wa Indira Gandhi lilianguka na kusababisha watu  idadi hiyo ya watu 36 kupoteza maisha.


PICHA ZA MATUKIO YA VURUGU HUKO TUNDUMA......DIWANI ( CHADEMA ) NA MCHUNGAJI KKKT WANASAKWA NA POLISI

 

Hii ndiyo hali halisi ya Mji mdogo wa Tunduma leo kuanzia asubuhi

Matairi yanachomwa katikati ya barabara

Mambo hayo 



Mwandishi wetu pamoja na waandishi wenzake walipata shida sana kufika mji wa Tunduma walikutana na vikwazo vingi sana lakini wananchi walikuwa waelewa waliwasaidia kutoa magogo na matairi ili wapite wakapate habari












Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani akiongea na waandishi wa habari
Wanafunzi wakisindikizwa na jeshi la polisi kurudi majumbani mwao
Polisi wakiendelea na kazi yao katika mitaa ya Tunduma
Baadhi ya magari ya IT yaendayo nchini Zambia yakiwa yamepakiwa nnje kidogo ya mji wa Tunduma kuogopa kuharibiwa kwa magari hayo

----------------
Diwani wa kata ya Tunduma Ndugu Frank Mwaijoka (Chadema) pamoja na mchungaji wa kanisa la KKT katika eneo hilo la Tunduma wilayani momba Mkoani mbeya wametakiwa kujisalimisha kituo cha Polisi Tunduma mara baada ya kuhusika na uchochezi wa kidini hali ambayo imepelekea kutokea kwa vurugu  katika eneo hilo.

Vurugu hizo zimeanza majira ya saa 4 asubuhi katika eneo hilo la tunduma mara baada ya kundi la watu wanaodai kuwa wao ni wafuasi wa dini ya kikristo wakidai waruhusiwe kuchinja mifugo na kuuza katika mabucha yao hali iliyo pelekea kuibuka kwa vurugu hizo.

Akizungumza kuhusiana na tukio hilko Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani amesema kuwa kufuatia kuwepo kwa tukio hilo jumla ya watu zaidi ya 40 tayari wamekwisha kamatwa .

Amesema mpaka sasa taarifa walizo zipata kufuatia vurugu hizo zinaeleza kuwa miongoni mwa watu walichochea vurugu hizo ni diwani wa kata hiyo ya Tunduma Ndugu John Mwaijoka pamoja na Mchungaji wa kanisa la kkt ndugu Neema Mwaipusa ambao kwa pamoja wametakiwa kujisalimisha kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.

Amesema suala hilo limegubikwa  na siasa kwani tayari viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa mkoa huo Ndugu Abbas Kandoro amekwisha litolea ufafanuzi Apri 02 mwaka huu wakiwepo pia viongozi wa dini .
Amesema kwa asilimia kubwa mgogoro huo juu ya nani achinje umeingiliwa na mambo ya kisiasa kwani hata baadhi ya wananchi wa maeneo hayo wamekuwa wakilalamika juu ya kutokea kwa vurugu hizo.

Amesema shughuli za kibiashara katika eneo hilo zimeshindwa kufanyika katika eneo hilo hivyo kufanya wananchi kupata adha hasa kwa nchi jirani ya Zambia ambao kwa asilimia kubwa wanategema kupata mahitaji kutoka mpakani mwa Tanzania.

Hata hivyo Diwani amesema kuwa katika vurugu hizo askari mmoja  pamoja na mwananchi wamejeruhiwa kwa kupigwa mawe ambapo tayari wamekwisha fikishwa kituo cha polisi.

Kufuatia hali hiyo Kamanda huyo wa Polisi amesema kwa sasa hali imelejea katika hali yake ya kawaida hivyo amewataka wananchi wa maeneo hayo kuwa watulivu wakati jeshi hilo la Polisi likiendela na msako wa kuwatafuta wahalifu wengine.

HII NDO KAULI YA UCHUNGU ALIYOTOA ABSALOM KIBANDA BAADA YA KUTEKWA NA KUTOBOLEWA JICHO



 

 Kauli  hii  ameitoa  kupitia  ukurasa  wake  wa  facebook:

Si jambo rahisi kibinadamu ingawa kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Japo miye ndiye mwenye maumivu makali na machungu mwilini yanayotokana na majeraha na ulemavu niliotiwa, mke wangu kipenzi al maarufu Mama Joshua alikuwa pembeni mwangu wakati wote nikiwa kitandani hospitalini Dar es Salaam hadi Milipark Afrika Kusini. Pole sana Angela. 

Matendo yanasema zaidi kuliko maneno...umepita nyakati nyingi sana ngumu juu yangu tangu mwaka 2000 tulipokutana na kuwa marafiki na hatimaye mwili mmoja. 

Ni Mungu tu atakayekulipa kile kinachostahili na si mwanadam

KAJALA MASANJA AJICHORA TATTOO YA WEMA SEPETU MGONGONI KAMA ISHARA YA KUMSHUKURU KWA ZILE MILIONI 13



Kajala ameamua kuchora Tattoo yenye jina la WEMA mgongoni mwake  baada ya kutolewa faini ya Shilingi Milioni 13 na msanii mwenzake Wema Sepetu,
 
hii ikiwa kama ishara ya shukrani kwa rafiki yake kipenzi Wema Sepetu.

Kupitia ukurusa wake wa instagram Wema nae ameandika hivi:

BEN POL NA LADY JAYDEE WAZINGUANA....JIDE ANADAI WAMEMTAPELI


So much is happening on Twitter these days. Wengi mnafahamu anachokiandika Lady Jaydee siku za hivi karibuni na sasa kibao kimemuendea Linah na Ben Pol.
 


Lady Jaydee anadai wasanii wa THT wamemsaliti kwa kile anachodai walikatazwa kwenda kuperform Nyumbani Lounge licha ya kuwalipa advance.

“Linah na Ben Pol mnabisha hamkukatazwa? Nisalitini ila hamtapata faida mtatoka kapa pia,” ametweet Jide.

Shutuma hizo zimepolekewa kwa hasira na Ben Pol aliyemjibu Jaydee:

“Hiyo show kulikuwa na wengine pia wakuperform je wali perform? kama nililipwa nanikashindwa ku show up, mbona sidaiwi?? Tafakari.”

Aliongeza, “Ben Pol hana muda wa maneno na majungu. Ombi langu ni mmoja kwako. Put me out of your business. PERIOD.”

“Don’t talk about things you don’t know about. DON’T.”

“Ukiwaza kutumia akili kamwe huwezi kukosea, ila utakapotumia hisia lazima ujikanyage somewhere. Nimekua vya kutosha #Trustme,” alimalizia Ben.

Unazungumziaje hiki kinachooendelea sasa na athari yake kwenye muziki wa Tanzania. Maoni yako tafadhari.