This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, July 24, 2014

Mlipuko waua 40, Nigeria

Watu wapata 40, wameuawa katika milipuko mikubwa miwili iliyotokea katika mji wa Kaduna, kaskazini mwa Nigeria. Katika mlipuko wa kwanza wa kujitoa mhanga watu 25 waliuawa, huku wengine 15 wakiuawa katika eneo lililokuwa na msongamano wa watu katika mji wa Kawo.
Shambulio hilo pia lilimlenga kiongozi wa upinzani na kiongozi wa zamani wa kijeshi Jenerali Muhammadu Buhari.
Shambulio la kwanza lilimlenga kiongozi mashuhuri wa kiislam aliyeambatana na wafuasi wake alipokuwa akitoka katika eneo la katikati ya Kaduna alikomaliza kufanya muhadhara kwa ajili ya mwezi mtukufu wa ramadhani. Maelfu ya watu walihudhuria tukio hilo la mwaka.
Kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo, watu 25 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa. Shambulizi la pili lilimlenga kiongozi wa juu wa upinzani ambaye pia ni rais wa zamani Jenerali Muhammadu Buhari ambako nako wamekufa watu 19. Wote wawili, kiongozi wa kiislam na kiongozi wa upinzani wamenusurika bila kujeruhiwa.
Mwanahabari wa BBC amesema aliona viungo vya binadamu vikiwa vimetapakaa katika eneo kubwa la mlipuko. Kamishina wa polisi wa jimbo la Kaduna Alhaji Umar Usman Shehu amesema mlipuko ulisababishwa na anayehisiwa kujitoa muhanga.
Hakuna kundi lolote lililojitokeza kuhusika na mlipuko huo. Kundi la Boko Haram ambalo bado linawashikilia wanafunzi wasichana 200 kwa takribani siku 100 sasa, limeshafanya matukio ya kulipua mabomu kwa kujitoa muhanga katika miji mingi kaskazini mwa naijeria ukiwamo mji mkuu Abuja.
CHANZO BBC,(A.I).

FILAMU YA 'THE KARATE KID' HATI HATI KUTOKA

Filamu ya The Karate Kid iliyoigiwa na Jaden Smith na Jackie Chan imepata pigo baada ya muongozaji wa filamu hiyo kujitoa katika mradi huo.

Waandaaji wa filamu hiyo wameeleza kuwa muongozaji Breck Eisner ametoka kwenye mradi wa filamu hiyo kutokana na mgongano/mgogoro wa ratiba. Filamu hiyo bado haijampata muongozaji mpya.

Hata hivyo filamu hiyo imeongeza waandishi wengine wawili kwenye timu yake, ambao ni Jeremiah Friedman na Nick Palmer.

Filamu ya kwanza ya The Karate Kid ya mwaka 2010 ilifanikiwa kufikia mauzo ya $343 millioni duniani kote.

Wednesday, July 23, 2014

Thamani ya pesa ya Tanzania inazidi kushuka thamani, hii inasababishwa na material inayotengenezewa, kwa mfano noti ya shili mia tano imekosa muonekano wake kabisa. kwa maelezo zaidi www.zacott.blogspot.com


 
 

Tuesday, July 15, 2014

Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Hague atangaza kujiuzulu.



 Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Bw.William Hague akizungumza na waandishi wa habari mjini London.

 Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague alisema  jumatatu kuwa anajiuzulu kama mwanadiplomasia wa juu baada ya miaka minne katika kazi hiyo, ikiwa ni sehemu ya  mabadiliko makubwa yaliofanywa na waziri mkuu David Cameron tangu kuchaguliwa kwake 2010.
Hague aliandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba anajiuzulu na hatagombea ubunge katika uchaguzi mkuu ujao unaotarajiwa kufanyika Mei mwakani.Vyombo vya habari vya Uingereza vinasema nafasi yake huenda ikachukuliwa na Phillip Hammond waziri wa sasa wa Ulinzi.
Mkuu wao  Bw.Cameron ambaye ni kiongozi wa chama cha Conservative anafanya kile kinachotarajiwa kuwa mabadiliko ya mwisho ya baraza lake la mawaziri  kabla ya uchaguzi huo mkuu wa kitaifa. Anatarajiwa kutangaza majina kadhaa ya mawaziri wapya Jumanne.