This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, February 6, 2014

Mbunge Chadema Kortini vurugu za Udiwani Kahama

chadema_25071.jpg
Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki (Chadema), Sylvester Kasulumbayi
Kahama. Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki (Chadema), Sylvester Kasulumbayi na Diwani wa Kata ya Buselesele, Crispian Kagoma na watu wengine 14 wamepandishwa kizimbani kwa tuhuma za kujeruhi katika vurugu zilizoibuka katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Kasulumbayi na wenzake 15, ambao wanaaminika kuwa wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kahama saa 8.00 mchana jana na kusomewa mashtaka sita kila mmoja.
Akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mfawidhi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Kahama, Gadiel Mariki, Mwendesha Mashtaka Shukrani Madulu alisema washtakiwa wote kwa pamoja walitenda makosa hayo Februari 4, mwaka huu.
Madulu aliiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa hao wakiongozwa na mbunge huyo walitenda kosa hilo la kuwashambulia kwa mapanga wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za kuwania udiwani wa Kata ya Ubagwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu.
Alisema mashtaka matano ni kushambulia na kujeruhi kwa mapanga, na moja la kuharibu mali, ikidaiwa kuwa katika vurugu hizo washtakiwa waliishambulia gari la CCM la wilaya hiyo na kuliharibu.
Washtakiwa wote walikana mashtaka yote na kuomba mahakama iwape dhamana ili waendelee na kampeni za kumnadi mgombea wao wa nafasi ya udiwani katika kata hiyo ya Ubagwe.
Maombi hayo yalipingwa na Mwendesha Mashtaka, akiiomba mahakama isitoe dhamana kwa kuwa hali za majeruhi watatu ni mbaya kwa kuwa tayari wamepelekwa kwenye Hospitali ya Rufaa na Bugando mkoani Mwanza, baada ya matibabu yao kushindikana wilayani Kahama.
Kutokana na hali hiyo, Hakimu Mariki alikubaliana na hoja hiyo na kuahirisha kesi hiyo hadi leo ambapo kesi hiyo itasikilizwa.
Watuhumiwa wote walipelekwa mahabusu baada ya dhamana hiyo kuzuiliwa.
Waliojeruhiwa kwenye vurugu
Wafuasi watano wa CCM wilayani Kahama akiwamo ofisa mtendaji wa Kata ya Ubagwe walijeruhiwa kwa mapanga kwenye vurugu hizo.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Andrew Emmanuel alisema Masunga, Kamaro na Peter walisafirishwa kwenda Bugando jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.
Chanzo cha vurugu
Vurugu hizo zilitokea juzi saa moja usiku katika Kata ya Ubagwe muda mfupi baada ya wafuasi hao kumaliza kampeni zao za kumnadi mgombea wa CCM, Hamis Majogolo anayewania udiwani kwenye kata hiyo.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, wafuasi hao walikumbwa na mkasa huo wakati wakiwa kwenye gari la CCM ambalo pia lilikuwa na watuhumiwa watatu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema waliokuwa wakipelekwa Kituo Kidogo cha Polisi Bulungwa.
Ilidaiwa watuhumiwa hao nao walidaiwa kufanya fujo kwenye mkutano wa Kampeni wa Chama cha Tadea ambacho pia kina mgombea anayewania nafasi hiyo.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa wanachama wa Chadema waliweka kizuizi kwa kutumia gari la Kasulumbayi kwenye barabara ya kuelekea kituo kidogo cha polisi.
Peter, ambaye ni dereva wa gari la CCM alisimulia kuwa walipofika kwenye kizuizi hicho walisimama, ndipo wafuasi wa Chadema waliposhuka kwenye gari la Mbunge huyo na kuanza kuwashambulia kwa mapanga wakitaka kuwaokoa wenzao watatu.CHANZO MWANANCHI
Watatu wakamatwa Njombe
Pia Jeshi la Polisi wilayani Njombe linawashikilia watu watatu wanaodaiwa kufanya fujo katika ofisi ya CCM ya tawi la Matalawe, Jumatatu iliyopita.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani alisema kuwa watu hao walikwenda kwa gari kwenye maeneo ya tawi hilo na kuanza kuchana picha za mgombea udiwani wa CCM, Menard Mlyuka.
Aliwataja watu waliokamatwa kuwa ni Award Karonga (40), Ally Mhagama (43) na Robert Mabu (24)

FAMILIA KUMINA TANO HAZINA MAHALA PAKUISHI GEREZA PAWAGA


 Ofisi za Gereza Pawaga zilizo ezuliwa na upepo mkali ulio ambatana na mvua juzi jioni.

 Sehemu ya masalia ya bati na matandiko yalio haribiwa na mvua

 SACAP Deusdedit Kamugisha Afisa wa Magereza Mkoa wa Iringa pichani kulia akiongozana na Mkuu wa gereza Pawaga SP.Sosthenes Mwakapala akikagua uharibifu ulio jitokeza katika nyumba za askari na majengo wanayo tarajia kuhamia kwamuda.

 Bustani ikiwa imeharibiwa na Mvua ilionyesha ikiwa na upepo mkari 

Baadhi ya Vyombo vya familia za Askari Magereza vikiwa nje baada ya Mvua kuharibu makazi yao.
Nyumba kumi na tano za Askari Magereza wa Gereza Pawaga wilaya ya Iringa zimeezuliwa na Upepo mkali ulio ambatana na mvua kubwa ya mawe ilionyesha juzi majira ya saa 9 alasiri mpaka saa kumi na moja jioni na kuanza tena saa mbili ya usiku mpaka saa tano usiku.
Akiongea na mwandishi wa habari Mkuu wa Gereza la Pawaga SP.Sosthenes Mwakapala alisema adha hiyo ya mvua imesababisha familia hizo kukosa mahala pa kuishi pamoja na thamani zilizo salia wakati walipokumbwa na mvua hiyo ingawa hakuna madhara kwa binadamu sambamba na hilo kumeezuliwa ofisi za tano za gereza zinazojumuisha Stoo, Bohari, Mapokezi, Utawara pia Bafu ya wafungwa.
 Madhara mengine yaliyo jitokeza ni kuharibiwa vibaya kwa heka tano za Bustani ya gereza yenye mazao mchanganyiko ikiwamo mashina ya Ndizi, Mipapai, Mihogo, Mahindi pamoja na Miwa mimea hiyo imevunjika kabisa haitegemewi  kupona tena.
Mkuu wagareza la Pawaga SP. Sosthenes Mwakapala alisema wao kama uongozi wagereza na viongozi wasaidizi wake wamechukua jukumu la kuhakikisha askari hao na familia zao wanapata mahali pakujihifadhi kwa muda wakati wakisubiri ufumbuzi toka ofisi ya Magereza mkoa wa Iringa. Kwakuwahamishia katika majengo ya Shule ya Msingi, Bwalo la gereza, Ghala la chakula  wakae kwa muda.

MSAMBINUNGWA” by TUNDA MAN feat ALLY KIBA

MSAMBINUNGWA” by TUNDA MAN feat ALLY KIBA
(Photo’s) The Making of music Video “MSAMBINUNGWA” by TUNDA MAN feat ALLY KIBA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/01/photos-making-of-music-video.html#sthash.txPgpp0o.dpuf







Nini hatma ya kesi ya Kenyatta ICC?

KESNYATA_185c0.jpg
Pande zinazohusika katika kesi inayomkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC Mjini The Hague zimekuwa na kikao cha kujadili mstakabali wa kesi hiyo.
Kiongozi wa mashtaka wa ICC Fatou Bensouda amekiri kuwa bado hana ushahidi wa kutosha kuwezesha kesi hiyo kuendelea.
Mawakili wanaomwakilisha Rais Kenyatta wanataka kesi hiyo kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2007 itupiliwe mbali.
Bensouda amesema kuwa bado kuna maswala yanayozua utata na ambayo yanahitaji uchunguzi wa kina. Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mashahidi wengi wamehongwa au kutishwa kiasi cha kujiondoa katika kesi hiyo.
Viongozi wa mashitaka ICC wanasema kuwa Kenyatta aliongoza ghasia hizo lakini kesi dhidi yake imefanywa dhaifu kutokana na baadhi ya mashahidi kujiondoa katika kesi hiyo.
Mawakili wa Kenyatta wanatuhumu upande wa mashitaka kwa kusisitiza kutaka taarifa kuhusu akaunti ya benki ya Rais Kenyatta kuona ikiwa kuna pesa zozote zilizotolewa kwa lengo la kutumika wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007/08
Wakili wa waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi amesisitizia mahakama kuwa kutupiliwa mbali kwa kesi kutawakosesha waathiriwa haki. Mahakama inatarajiwa kutoa uamuzi katika siku chache zijazo.
Rais Kenyatta alifikishwa ICC kutokana na tuhuma kuwa alikuwa mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya mwaka 2007/2008. Anakabiliwa na makosa ya mauaji na uhalifu mwingine dhidi ya binadamu.
Kadhalika Kenyatta alishitakiwa pamoja na makamu wake William Ruto kwa tuhuma sawa. Kesi dhidi ya Ruto inaendelea katika mahakama hiyo.
Watu 1,200 walipoteza maisha yao katika ghasia za uchaguzi mkuu mwaka 2007/08 huku maelfu wakilazimika kutoroka makwao. Wote wamekanusha mashitaka.
Kesi yenyewe ilitarajiwa kuanza Jumatano, lakini ikaahirishwa kwa mara ya nne mwezi jana wakati ambapo wendesha mashitaka waliposema kuwa shahidi mwingine alijiondoa kwenye kesi huku wakiomba mahakama kuwapa muda zaidi kutafuta ushahidi. CHANZO BBC SWAHILI

Wednesday, February 5, 2014

Utata kesi ya Mtanzania Afrika Kusini

Kesi ya Mtanzania Stephen Ongolo anayeshikiliwa na polisi Afrika Kusini akituhumiwa kutishia kutoa siri za mke wa pili wa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma, Nompumelelo Ntuli Zuma (MaNtuli), imeibua mabishano ya kisheria ya kuhusu mahali anapotakiwa kushtakiwa.
Gazeti la The Star la Afrika Kusini liliripoti kuwa baada ya Ongolo kupandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Camperdown jijini Durban, Jumatatu wiki hii, ilibainika kuwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ndoda January hakueleza ni wilaya gani ya kimahakama ambayo Ongolo alitenda kosa hilo. January alisema kuwa walishindwa kujua eneo alilofanya makosa Ongolo, kwani alikuwa akitumia ujumbe mfupi wa simu alioutuma kwa vyombo vya habari vya nchi hiyo.
"Tunashindwa kuelewa eneo gani ambalo mshtakiwa amefanya kosa kwa sababu mlalamikaji anaweza kuwa sehemu yeyote kati ya Camperdown na Nkandla ambako alipeleka ujumbe huo," alisema January.
Kukamatwa kwa Ongolo
Ongolo alikamatwa na polisi jijini Durban mwezi uliopita kwa madai ya kumtishia mke wa pili wa Rais Zuma kuwa angetoa siri zake. Siri hizo zinahusiana na kifo cha mlinzi wa Rais Zuma, Phinda Thomo, ambaye alidaiwa kujiua bafuni kwake mwaka 2009.
Ongolo alikaririwa na Gazeti la Sunday Independent la Afrika Kusini akieleza kuwa Thomo hakujiua bali kifo chake kilipangwa baada ya siri kati yake na MaNtuli kubainika.
Gazeti la The Star la nchini humo, jana liliripoti kuwa hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Thys Talijaard wa Camperdown alisema ili Ongolo apate dhamana hapo Camperdown, alitakiwa awe ameshtakiwa kwa makosa aliyofanya kwenye mahakama ya wilaya ambayo kosa limetendeka.
Ongolo alitakiwa kuomba dhamana Jumatatu lakini mwanasheria anayemtetea, Lekoa Le-koko hakuwapo mahakamani, na hivyo mashtaka kupangwa kusikilizwa tena jana.
Wakati mshtakiwa huyo akiwa mahakamani hapo ulizuka mjadala mzito kati ya January na Mdu Thuketana ambaye alishika nafasi ya Le-koko, wakijadiliana ni wapi mshtakiwa anaweza kushikiliwa wakati kesi yake ikiendelea kusikilizwa.
Thuketana aliomba Ongolo awe chini ya ulinzi wa polisi kutokana na afya yake kwani anasumbuliwa na maradhi ya pumu na pia walikuwa wakihofia usalama wake.
Wiki iliyopita, Ongolo alishindwa kwenda mahakamani baada ya kuugua pumu na kupelekwa hospitali.
Hata hivyo, January alisema mshtakiwa anaweza kuwekwa chini ya ulinzi wa polisi kwa siku saba tu, na baada ya hapo atapelekwa kwenye mahabusu za kawaida, jambo ambalo liliafikiwa na Hakimu Talijaard.
Kuhusu uraia wa Ongolo, Msemaji wa Ofisi ya Uhamiaji nchini Tanzania, Kamishna Abbas Irovya alisema suala la uraia wake linatakiwa lianzie Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ambako yuko, badala ya kuanzia hapa nchini.
"Kama ubalozi haumtambui, hata sisi inakuwa shida kwetu kuthibitisha." alisema.
JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BIFU NA WEMA, NA KUMSAPRISE SH. 600,000/= JUKWAANI WALIPOKUWA ARUSHA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/02/jokate-akieleza-jinsi-alivyo-maliza.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29#sthash.aA38eZ3M.dpuf
JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BIFU NA WEMA, NA KUMSAPRISE SH. 600,000/= JUKWAANI WALIPOKUWA ARUSHA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/02/jokate-akieleza-jinsi-alivyo-maliza.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29#sthash.aA38eZ3M.dpuf
JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BIFU NA WEMA, NA KUMSAPRISE SH. 600,000/= JUKWAANI WALIPOKUWA ARUSHA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/02/jokate-akieleza-jinsi-alivyo-maliza.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29#sthash.aA38eZ3M.dpuf

Tanzania yakamata dawa za kulevya

Polisi nchini Tanzania wamekamata shehena ya dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa kilo 201 katika eneo la bahari kati ya Dar es Salaam na Zanzibar nchini humo.
Kamanda wa kikosi maalum cha kuzuia dawa za kulevya Godfrey Nzowa ameiambia BBC kuwa Watu 12 wanashikiliwa kuhusiana na shehena hiyo.
Kamanda Nzowa amesema dawa hizo za kulevya zimekamatwa na Polisi wa doria baharini muda wa saa sita usiku wa kuamkia Jumanne zikisafirishwa katika Jahazi.
Kwa mujibu wa Kamanda Nzowa Shehena hiyo ilikuwa ikitoka nchini Iran kuelekea nchi au eneo ambalo mpaka sasa bado halijafahamika.
Hivi karibuni kumekuwa na matukio ya kukamata dawa za kulevya aina mbalimbali kupitia viwanja vya ndege,nchi kavu na baharini, ambapo mwaka jana kiasi kikubwa cha dawa za kulevya zilizokamatwa ziliteketezwa.
CHANZO:BBC

Friday, January 17, 2014

MJAMZITO ANASWA KWA UKAHABA

Stori: ISSA MNALLY NA DUSTAN SHEKIDELE

OPARESHENI ya Polisi wa Mkoa wa Morogoro na kikosi maalum cha kufichua Maovu cha Magazeti ya Global Publishers (OFM), imemnasa mwanamke mjamzito katika kamatakamata ya machangudoa.
Polisi akimkagua changudoa mwenye mimba aliyenaswa akijiuza.
Katika oparesheni hiyo ya aina yake iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Msamvu (Kambi ya Itigi), wanawake 30 waliodaiwa kujihusisha na biashara hiyo walikamatwa.
Waandishi wetu wakiwa na askari wa mkoa huo…

OPARESHENI ya Polisi wa Mkoa wa Morogoro na kikosi maalum cha kufichua Maovu cha Magazeti ya Global Publishers (OFM), imemnasa mwanamke mjamzito katika kamatakamata ya machangudoa.
 
Polisi akimkagua changudoa mwenye mimba aliyenaswa akijiuza.
Katika oparesheni hiyo ya aina yake iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Msamvu (Kambi ya Itigi), wanawake 30 waliodaiwa kujihusisha na biashara hiyo walikamatwa.
Waandishi wetu wakiwa na askari wa mkoa huo walimnasa mjamzito huyo anayedaiwa kuwa na mimba ya miezi sita akiwa mawindoni eneo hilo.
Changudoa huyo mwenye mimba akiwa chini ya ulinzi.
Mara baada ya mjazito huyo kukamatwa alitoa yake ya moyoni kwa kusema kwamba anafanya biashara hiyo ili kupata fedha za kujikimu na ujauzito wake haumpi shida yoyote.
“Jamani natafuta pesa za kujikimu na maisha hapa mjini sasa mnatukamata tukale wapi? Hii mimba ni yangu na ninayefanya ukahaba ni mimi niacheni,” alisema mdada huyo.
Pamoja na maneno yake, polisi walimbeba msobemsobe na kumfikisha kituoni pamoja na makahaba wengine.