This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, February 6, 2014

Nini hatma ya kesi ya Kenyatta ICC?

KESNYATA_185c0.jpg
Pande zinazohusika katika kesi inayomkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC Mjini The Hague zimekuwa na kikao cha kujadili mstakabali wa kesi hiyo.
Kiongozi wa mashtaka wa ICC Fatou Bensouda amekiri kuwa bado hana ushahidi wa kutosha kuwezesha kesi hiyo kuendelea.
Mawakili wanaomwakilisha Rais Kenyatta wanataka kesi hiyo kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya mwaka 2007 itupiliwe mbali.
Bensouda amesema kuwa bado kuna maswala yanayozua utata na ambayo yanahitaji uchunguzi wa kina. Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mashahidi wengi wamehongwa au kutishwa kiasi cha kujiondoa katika kesi hiyo.
Viongozi wa mashitaka ICC wanasema kuwa Kenyatta aliongoza ghasia hizo lakini kesi dhidi yake imefanywa dhaifu kutokana na baadhi ya mashahidi kujiondoa katika kesi hiyo.
Mawakili wa Kenyatta wanatuhumu upande wa mashitaka kwa kusisitiza kutaka taarifa kuhusu akaunti ya benki ya Rais Kenyatta kuona ikiwa kuna pesa zozote zilizotolewa kwa lengo la kutumika wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007/08
Wakili wa waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi amesisitizia mahakama kuwa kutupiliwa mbali kwa kesi kutawakosesha waathiriwa haki. Mahakama inatarajiwa kutoa uamuzi katika siku chache zijazo.
Rais Kenyatta alifikishwa ICC kutokana na tuhuma kuwa alikuwa mmoja wa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya mwaka 2007/2008. Anakabiliwa na makosa ya mauaji na uhalifu mwingine dhidi ya binadamu.
Kadhalika Kenyatta alishitakiwa pamoja na makamu wake William Ruto kwa tuhuma sawa. Kesi dhidi ya Ruto inaendelea katika mahakama hiyo.
Watu 1,200 walipoteza maisha yao katika ghasia za uchaguzi mkuu mwaka 2007/08 huku maelfu wakilazimika kutoroka makwao. Wote wamekanusha mashitaka.
Kesi yenyewe ilitarajiwa kuanza Jumatano, lakini ikaahirishwa kwa mara ya nne mwezi jana wakati ambapo wendesha mashitaka waliposema kuwa shahidi mwingine alijiondoa kwenye kesi huku wakiomba mahakama kuwapa muda zaidi kutafuta ushahidi. CHANZO BBC SWAHILI

Wednesday, February 5, 2014

Utata kesi ya Mtanzania Afrika Kusini

Kesi ya Mtanzania Stephen Ongolo anayeshikiliwa na polisi Afrika Kusini akituhumiwa kutishia kutoa siri za mke wa pili wa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma, Nompumelelo Ntuli Zuma (MaNtuli), imeibua mabishano ya kisheria ya kuhusu mahali anapotakiwa kushtakiwa.
Gazeti la The Star la Afrika Kusini liliripoti kuwa baada ya Ongolo kupandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Camperdown jijini Durban, Jumatatu wiki hii, ilibainika kuwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ndoda January hakueleza ni wilaya gani ya kimahakama ambayo Ongolo alitenda kosa hilo. January alisema kuwa walishindwa kujua eneo alilofanya makosa Ongolo, kwani alikuwa akitumia ujumbe mfupi wa simu alioutuma kwa vyombo vya habari vya nchi hiyo.
"Tunashindwa kuelewa eneo gani ambalo mshtakiwa amefanya kosa kwa sababu mlalamikaji anaweza kuwa sehemu yeyote kati ya Camperdown na Nkandla ambako alipeleka ujumbe huo," alisema January.
Kukamatwa kwa Ongolo
Ongolo alikamatwa na polisi jijini Durban mwezi uliopita kwa madai ya kumtishia mke wa pili wa Rais Zuma kuwa angetoa siri zake. Siri hizo zinahusiana na kifo cha mlinzi wa Rais Zuma, Phinda Thomo, ambaye alidaiwa kujiua bafuni kwake mwaka 2009.
Ongolo alikaririwa na Gazeti la Sunday Independent la Afrika Kusini akieleza kuwa Thomo hakujiua bali kifo chake kilipangwa baada ya siri kati yake na MaNtuli kubainika.
Gazeti la The Star la nchini humo, jana liliripoti kuwa hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Thys Talijaard wa Camperdown alisema ili Ongolo apate dhamana hapo Camperdown, alitakiwa awe ameshtakiwa kwa makosa aliyofanya kwenye mahakama ya wilaya ambayo kosa limetendeka.
Ongolo alitakiwa kuomba dhamana Jumatatu lakini mwanasheria anayemtetea, Lekoa Le-koko hakuwapo mahakamani, na hivyo mashtaka kupangwa kusikilizwa tena jana.
Wakati mshtakiwa huyo akiwa mahakamani hapo ulizuka mjadala mzito kati ya January na Mdu Thuketana ambaye alishika nafasi ya Le-koko, wakijadiliana ni wapi mshtakiwa anaweza kushikiliwa wakati kesi yake ikiendelea kusikilizwa.
Thuketana aliomba Ongolo awe chini ya ulinzi wa polisi kutokana na afya yake kwani anasumbuliwa na maradhi ya pumu na pia walikuwa wakihofia usalama wake.
Wiki iliyopita, Ongolo alishindwa kwenda mahakamani baada ya kuugua pumu na kupelekwa hospitali.
Hata hivyo, January alisema mshtakiwa anaweza kuwekwa chini ya ulinzi wa polisi kwa siku saba tu, na baada ya hapo atapelekwa kwenye mahabusu za kawaida, jambo ambalo liliafikiwa na Hakimu Talijaard.
Kuhusu uraia wa Ongolo, Msemaji wa Ofisi ya Uhamiaji nchini Tanzania, Kamishna Abbas Irovya alisema suala la uraia wake linatakiwa lianzie Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ambako yuko, badala ya kuanzia hapa nchini.
"Kama ubalozi haumtambui, hata sisi inakuwa shida kwetu kuthibitisha." alisema.
JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BIFU NA WEMA, NA KUMSAPRISE SH. 600,000/= JUKWAANI WALIPOKUWA ARUSHA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/02/jokate-akieleza-jinsi-alivyo-maliza.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29#sthash.aA38eZ3M.dpuf
JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BIFU NA WEMA, NA KUMSAPRISE SH. 600,000/= JUKWAANI WALIPOKUWA ARUSHA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/02/jokate-akieleza-jinsi-alivyo-maliza.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29#sthash.aA38eZ3M.dpuf
JOKATE AKIELEZA JINSI ALIVYO MALIZA BIFU NA WEMA, NA KUMSAPRISE SH. 600,000/= JUKWAANI WALIPOKUWA ARUSHA - See more at: http://onelovetz.blogspot.com/2014/02/jokate-akieleza-jinsi-alivyo-maliza.html?utm_source=feedburner&utm_medium=feed&utm_campaign=Feed%3A+blogspot%2FhgdRs+%28Onelove+Tz%29#sthash.aA38eZ3M.dpuf

Tanzania yakamata dawa za kulevya

Polisi nchini Tanzania wamekamata shehena ya dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa kilo 201 katika eneo la bahari kati ya Dar es Salaam na Zanzibar nchini humo.
Kamanda wa kikosi maalum cha kuzuia dawa za kulevya Godfrey Nzowa ameiambia BBC kuwa Watu 12 wanashikiliwa kuhusiana na shehena hiyo.
Kamanda Nzowa amesema dawa hizo za kulevya zimekamatwa na Polisi wa doria baharini muda wa saa sita usiku wa kuamkia Jumanne zikisafirishwa katika Jahazi.
Kwa mujibu wa Kamanda Nzowa Shehena hiyo ilikuwa ikitoka nchini Iran kuelekea nchi au eneo ambalo mpaka sasa bado halijafahamika.
Hivi karibuni kumekuwa na matukio ya kukamata dawa za kulevya aina mbalimbali kupitia viwanja vya ndege,nchi kavu na baharini, ambapo mwaka jana kiasi kikubwa cha dawa za kulevya zilizokamatwa ziliteketezwa.
CHANZO:BBC

Friday, January 17, 2014

MJAMZITO ANASWA KWA UKAHABA

Stori: ISSA MNALLY NA DUSTAN SHEKIDELE

OPARESHENI ya Polisi wa Mkoa wa Morogoro na kikosi maalum cha kufichua Maovu cha Magazeti ya Global Publishers (OFM), imemnasa mwanamke mjamzito katika kamatakamata ya machangudoa.
Polisi akimkagua changudoa mwenye mimba aliyenaswa akijiuza.
Katika oparesheni hiyo ya aina yake iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Msamvu (Kambi ya Itigi), wanawake 30 waliodaiwa kujihusisha na biashara hiyo walikamatwa.
Waandishi wetu wakiwa na askari wa mkoa huo…

OPARESHENI ya Polisi wa Mkoa wa Morogoro na kikosi maalum cha kufichua Maovu cha Magazeti ya Global Publishers (OFM), imemnasa mwanamke mjamzito katika kamatakamata ya machangudoa.
 
Polisi akimkagua changudoa mwenye mimba aliyenaswa akijiuza.
Katika oparesheni hiyo ya aina yake iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Msamvu (Kambi ya Itigi), wanawake 30 waliodaiwa kujihusisha na biashara hiyo walikamatwa.
Waandishi wetu wakiwa na askari wa mkoa huo walimnasa mjamzito huyo anayedaiwa kuwa na mimba ya miezi sita akiwa mawindoni eneo hilo.
Changudoa huyo mwenye mimba akiwa chini ya ulinzi.
Mara baada ya mjazito huyo kukamatwa alitoa yake ya moyoni kwa kusema kwamba anafanya biashara hiyo ili kupata fedha za kujikimu na ujauzito wake haumpi shida yoyote.
“Jamani natafuta pesa za kujikimu na maisha hapa mjini sasa mnatukamata tukale wapi? Hii mimba ni yangu na ninayefanya ukahaba ni mimi niacheni,” alisema mdada huyo.
Pamoja na maneno yake, polisi walimbeba msobemsobe na kumfikisha kituoni pamoja na makahaba wengine.

Thursday, January 16, 2014

DIAMOND, NI BUSARA KUACHA NYODO!

Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz'.
JINA lake lipo juu mno, pengine kuliko msanii mwingine yeyote kati ya vijana wanaotingisha anga ya muziki wa kizazi kipya kwa sasa. Siyo jambo la busara hata kidogo, kubeza uwezo wake katika kumiliki jukwaa, jinsi anavyojituma na zaidi, tungo zake zinazoendelea ‘kubamba’ kila kukicha, ingawa zina ujumbe unaofanana, kuhusu mapenzi!
Hapa ninamzungumzia Nasibu Abdul maarufu kwa mashabiki kama Diamond, yule kijana aliyeibuka akitokea mitaa ya Tandale, jijini Dar es Salaam, ambaye sasa anakula kuku kwa mrija katika maeneo ambayo miaka mitano nyuma ilikuwa ni sawa na kumdhihaki mtu aguse mbingu!
Wakati flani nilipata kuandika habari zake, muda ambao rafiki yangu Said Mdoe alikuwa akimtumia katika baadhi ya maonyesho yake, akimchanganya na Mzee Yusuf wa Jahazi Modern Taarab. Kutokana na ugeni wake katika fani, nilipata taabu sana kulijua jina lake, kila siku nilikuwa nikiuliza, anaitwa nani vile?!!
Hivi sasa habari imegeuka, dogo anatisha na sidhani kama Mdoe anaweza tena kumpandisha katika jukwaa, sijui! Binafsi sijawahi kukutana na supastaa huyu, si kikazi wala bahati mbaya. Ninamsikia kama wengi wanavyomsikia, ingawa tofauti yetu ni kwamba mimi sina mzuka naye!
Nimekuwa nikipata simu na sms nyingi katika safu hii, zikimlalamikia, kwamba anaringa na kujisikia. Kama nilivyosema awali, sijawahi kukutana naye, sijawahi kuzungumza naye na sitaki dhambi ya kumjaribu mtu. Kwamba nijaribu kulazimisha nafasi ya kukutana naye ili nithibitishe madai dhidi yake, naona nitakuwa sitendi haki.
Lakini nimejikuta nikilazimika kusema naye baada ya baadhi ya waandishi wenzangu, nao kujiunga na mashabiki juu ya lawama za nyodo za Diamond. Eti sasa hapokei simu zao, hajibu sms zao, hata kama zitakuwa ni kwa ajili ya kuzungumzia kazi zake mwenyewe.
Wanapojaribu kuniambia kuhusu jinsi alivyokuwa anahangaika kuwatafuta wakati ule akipanda mlima, sishangai kwa sababu ninayo orodha ndefu ya wasanii wa aina hiyo. Baadhi yao walikaa kwenye maboksi nje ya ofisi, wakisubiri tumalize kazi ili tufanye nao mahojiano, na walipiga simu kila mara kuulizia kuhusu kutoka kwa habari zao.
Lakini hata walipofanikiwa, heshima iliendelea kuwepo. Ingawa sasa hawawezi kukaa tena kusubiri kwenye maboksi, lakini angalau walipiga simu kusalimia na mara zote walikuwa wepesi kupokea tulipowapigia na kama walikuwa bize, hawakusita kueleza.
Tunao wasanii wa aina hiyo, hadi leo tuko nao pamoja wakiendeleza harakati, bila kujali wana mafanikio kiasi gani. Diamond ni kijana mdogo, aliyepata mafanikio ghafla. Ingawa mwenyewe amekuwa akielezea jinsi alivyosota, akitaka tuamini kwamba amehangaika sana, lakini kwa umri wake, nadhani haelewi nini hasa maana ya msoto.
Kama leo anawadharau waandishi, kwa maana labda sisi tunaoandika magazetini, ambao tulitumia muda mwingi kumpamba ili atoke, huenda pia hivi sasa anaweza kuwa anamdharau mama ntilie, aliyekuwa akimkopesha ukoko wakati ule. Na ni jambo la kutegemea pia kwamba, huenda anawadharau washkaji aliokuwa akishinda nao ghetto!
Nimshauri tu kuwa kelele dhidi yake zimekuwa nyingi, na bahati mbaya zingine zinatoka kwa baadhi ya mashabiki wake. Maringo, kujisikia na kujisifu ni hulka ya mtu, haizuiliki, lakini unapojaribu kutaka kuwa mtu wa watu, ni vyema kuepuka baadhi ya tabia kwa manufaa yako na wadau wako.
Nimkumbushe tu kuwa wapo wasanii ambao walianza kuwika tokea kuanza kwa game na bado hadi leo wako levo za juu, lakini ushirikiano wao kwa wanahabari, mashabiki na wadau ni wa hali ya juu!

BABY MADAHA

Baby Joseph Madah.
AMA kweli maovu yanazidi kuongezeka, shetani naye mbioni siku zote kunasa waliyo wake, kauli hizo zote ziko sambamba na staa wa sinema za Kibongo na mkali wa muziki wa Kizazi Kipya, Baby Joseph Madaha amenaswa baada kuingia mkenge mtego wa kujiuza, Ijumaa limesheheni.

Kumekuwa na skendo kuwa baadhi ya mastaa wa kike Bongo hujihusisha na biashara ya kujiuza ili kujipatia kipato na kufanya sanaa kuwa kama chambo cha kunasa wanaume.
OFM MZIGONI
Oparesheni Fichua Maovu (OFM) chini ya Global Publishers, mwaka jana ilinasa mastaa wawili kwenye mtego wake, mke wa mtu, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ na Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’.
Mwaka huu, OFM imeanza kazi zake ambapo kwa kuanzia iliamua kumtega Baby Madaha aliyejaa kwenye kumi na nane zake.
Mmoja wa wadau wa OFM alijifanya mfanyabiashara kutoka Mwanza ambaye ni mgeni wa jiji a.k.a Ngosha akijipachika jina la Frank ambapo baadaye katika mazungumzo, Baby Madaha alimbana na kutaka ampatie majina matatu ndipo mwana-OFM Frank (feki) akajipatia jina Frank Michael Lugwisha.
ILIKUWAJE?
Mchezo mzima ulianza Januari 13, mwaka majira ya saa 11:52 jioni kwa kuchati kwenye simu ya kiganjani ambapo Baby Madaha aliingia kichwakichwa bila kujua anachati na ‘sumu’ wa OFM kama ifuatavyo;
Frank/OFM: Mambo vipi Baby Madaha? Nilikuwa naomba tuonane.
Baby Madaha: Kuhusu nini?
Frank/OFM: Niwe mkweli, Madaha nimekupenda, nilipofika hapa Dar ndo nikaona nikutafute.
Baby Madaha: Unampendaje mtu usiyemjua?
Frank/OFM: Jamani nakuonaga magazetini na video zako.
Baby Madaha: Safi, so unataka kuniambia nini ambacho sijakisikia?
 Frank/OFM:  Nataka tu-meet (kukutana) Madaha nimetokea kukupenda sana lakini Alhamisi (jana) narudi mkoani Mwanza.
Baby Madaha: Huwezi ku-manage kuwa na mimi, baki kuwa shabiki wangu tu.
Frank/OFM: N’take radhi Madaha, kwa nini nisiweze, kikubwa kipi?
Baby Madaha: Huh! Tuma vocha tuone how worth are you? (Tuma vocha tuone utajiri wako)
Frank/OFM: Acha utani bwana, vocha kitu gani, ongea mambo makubwa Madaha
Baby Madaha: Hahaha…yote ninayo-except vocha tajiri.
Frank/OFM: Acha bwana. Vocha ndo kikwazo kwako?
Baby Madaha: Yap! Kama hutaki acha au unadhani natumia wireless kuchati na wewe?
Frank/OFM: Madaha wewe ni mkatili kiasi hicho?
MAMBO YASIMAMA KWA MUDA
Masuala ya kuchati yalisimama kwa muda lakini ilipofika saa 2:22 usiku, mazungumzo yaliendelea ambapo siku iliyofuata Frank wa OFM aliamua kuendelea kumtengenezea mtego ili kujiridhisha kama ni kweli baadhi ya mastaa wa Bongo wanafanya biashara hiyo haramu.
Januari 14, mwaka huu, majira ya saa 5:00 asubuhi, Frank wa OFM alianza tena kuchati na Baby Madaha kama ifuatavyo;

Frank/OFM: Mambo Madaha? Mi Frank
(akaamua kumpigia simu Frank wa OFM, ilikuwa mshtuko kwa Frank kwa sababu hakujipanga kuongea naye kwa hiyo hakupokea simu ya Baby Madaha ambayo ilipigwa saa 6: 30 mchana.
Dakika moja baadaye, Baby Madaha alituma meseji ya kumtoa hofu Frank wa OFM;
Baby Madaha: Frank ‘am calling you in vain uh afraiding of me (Frank nakupigia kwa nia njema unaniogopa?)
Frank/OFM: Sorry nilikuwa tight, naweza kupiga?
Baby Madaha: Yap!
Frank/OFM: Frank wa OFM aliongea na Baby Madaha na kuanza kumchomekea ambapo alitoa ushirikiano wa kutosha na kuonesha nia ya kujenga uhusiano huku akimtaka staa huyo kuwa ‘siriaz’ akimuahidi kuwa atakuwa naye na kuwa ajenti wake wa muvi jijini Mwanza.
Baada ya maongezi ya kutongozana kwenye simu, Frank wa OFM alimtumia tena meseji Baby Madaha kama ifuatavyo;

Frank/OFM: Nimefurahi sana kuongea nawe, sijui itakuwaje tukionana?
Baby Madaha: Wait, you I’ll see.
Frank/OFM: Eti ee, nimetokea kukupenda sana.
Baby Madaha: Thanks.
Baada ya hapo Frank wa OFM alimaliza kumtumia ‘sms’ siku hiyo, ilikuwa saa 9:12 alasiri.
Hata hivyo, Frank wa OFM aliamua kumhoji zaidi kupitia sms akitaka kujua hasa akiwa naye hata kwa saa tatu atataka shilingi ngapi?
Frank/OFM: Sasa hivi nataka kutoka niende ATM kuchukua pesa, sasa hebu kuwa muwazi tu wangu, kuwa na wewe kwa kama saa tatu utakuwa poa nikupe Sh. ngapi? Mtu mzima nisije nikaumbuka si unajua tena kwa staa kama wewe?
Baby Madaha: Milioni 10!
Frank/OFM: Baby usinikomoe, mimi na wewe tuna safari ndefu, kila nikija Dar tutakuwa pamoja.
Baby Madaha: (...anapiga simu lakini Frank wa OFM hapokei).
Baada ya kuona hivyo, Baby Madaha alituma sms hii “Call” (piga).

MAONGEZI YA SIMU
Frank/OFM: Mambo vipi Baby, habari za muda tena?
Baby Madaha: Salama tu, kwani wewe ulikuwa unataka kutoa sh. ngapi ATM?
Frank/OFM: Mimi ndiyo nilikuwa njiani naelekea ATM natoka hapa hotelini nilipofikia nina Shilingi Mil.4 kwa usiku mmoja, hapo vipi?
Baby Madaha: Katoe 5 fresh, sasa benki gani utaenda kutoa wakati benki zote zimeshafungwa na ATM mwisho kutoa ni Mil.1, sasa hapo itakuwaje?
Frank/OFM: Nitatoa kwa ATM, hata hivyo, nina master-card, naweza kutoa Mil.1 hadi mara 5, usijali kwani pesa kitu gani, cha msingi mimi ni kuwa na wewe!
Baby Madaha: Okay, fine unaweza kuja Kijitonyama (Dar) hapa kwenye hoteli ya (anaitaja jina)?
Frank/OFM: Nimefikia hapa hotelini (jina kapuni), sasa kutoka ni vigumu.
Baby Madaha: Okay, poa nitakuja hapo hotelini saa 1:00 usiku.
Frank/OFM: Usijali karibu sana, nakupenda sana Baby Madaha yaani niko tayari kwa lolote, sema unataka nikupe nini?
Baby Madaha: Hahaha....(anachekaaa) nikija nitakwambia vyote ninavyotaka kwani unafanya biashara gani?
Frank/OFM: Nauza nguo, mara nyingi nafuata Jakarta, Indonesia mara kwa mara lakini natumia muda mwingi kufanya kazi zangu Mwanza.
Baby Madaha: Wee Msukuma eti? Mimi mwenyewe Msukuma kwani unadhani jina Madaha ni la nini hilo, mimi mwenyewe Msukuma.
Frank/OFM: Nimefurahi sana kusikia hivyo, unaweza kuongea Kisukuma?
Baby Madaha: Naweza, wewe nisemeshe tu!
Frank/OFM: Nakutogilwe gete Madaha (Frank anaongea Kisukuma kwamba anampenda sana Madaha)
Baby Madaha: Tukuhoya ntondo nduhu tabu (anajibu kwa Kisukuma kuwa hakuna tatizo tutaongea kesho).
Ulipofika muda waliokubaliana na Frank wa OFM, Madaha alisema kuna foleni kubwa hivyo kuna sababu ya kubadilisha hoteli hiyo iliyoko maeneo ya Ubungo alipopanga Frank wa OFM waonane, Baby Madaha akataka wakutane nyingine iliyoko Kijitonyama.
“Siwezi kuja huko, kwanza kuna mifoleni isitoshe ni vizuri ukafika mwenyewe maeneo haya ya hoteli ya… (anataja), ni sehemu nzuri kwangu hivyo kama huna nia mbaya na mimi ni vizuri ukaja maana kesho nasafiri kwenda Kenya kwenye shughuli zangu za muvi, kwa hiyo unaweza kuja wewe tu maeneo haya,” alisema Madaha.
Frank aliendelea kumbana kwamba tayari alikuwa ameshaandaa pesa shilingi Mil.5, kama walivyokubaliana lakini asingeweza kubeba mfuko wa fedha wote huo isitoshe ni hoteli ambayo ameizoea kwa muda mrefu.
“Ujue Dar mimi siyo mzoefu, achilia mbali kuogopa kutapeliwa hivyo nakuomba uje kwenye hii hoteli nitafurahi sana dear, nakuomba unielewe ujue nakupenda sana mpenzi wangu Baby Madaha, tulia tuyajenge maisha,” alisema Frank wa OFM.
Msanii huyo alimkomalia Frank wa OFM wakutane siku ya Jumanne usiku ambapo alimwambia pia kuwa amepata dharura anakwenda kumuona mfanyabiashara mwenzake kwenye hoteli moja iliyopo Masaki (jina tunalo) ambapo Baby Madaha alitaka waonane na Frank wa OFM kwenye hoteli hiyohiyo.
“Nimepata dharura sitaweza kuonana na wewe, naenda kumuona mfanyabiashara mwenzangu maeneo ya hoteli…(jina tunalo), tuonane kesho muda wa asubuhi,” alisema Frank.
Baadaye Frank alimjulisha mteja wake kuwa yuko njiani anafuata mzigo bandarini akitoka wataonana na Baby Madaha kesho yake asubuhi ya Jumatano iliyopita, alituma sms hii;
Baby Madaha: Kuna stage tano in anything, nakupa tatu, coz uko siku ya tatu, denying, bargaining, accepting..... tomorrow if you be still on game, i give you the remained good day, enjoy Mr Frank, ukitoka cargo call me, we meet!
Frank/OFM: Okay, siku njema nitakutafuta.
Baby Madaha: Matajiri wengine hawana maneno kama wewe kwa mfano…(anataja jina la pedeshee mmoja maarufu Dar). Wanatuma pesa na siyo maneno, wee tuma hela (-)-pesa ipo kila sehemu we tuma ndo nitaweza kujiongeza kama nakuja au laa.
Frank/OFM: Nakutumia muda siyo mrefu, usijali.
IJUMAA LAMBANA BABY MADAHA
Hata hivyo, Baby Madaha hakutumiwa pesa alizotaka ili kukamilisha zoezi badala yake, OFM walitua mzigo wa ushahidi kwenye dawati la Ijumaa ambalo lilikuwa na jukumu la kutafuta mzani wa ishu hiyo.
Ijumaa lilipomtafuta Baby Madaha alikiri kuwa kwenye mawasiliano na mwanaume aliyemtaja kwa jina la Frank Michael Lugisha ambaye alisema alikuwa akifanya naye makubaliano ya kusambaza filamu yake ya The Gal Bladder.
Alipobanwa juu ya makubaliano ya kujiuza kwa mwanaume huyo kwa Sh. milioni 5 alikataa pamoja na kwamba alielezwa kuwa kuna ushahidi wa meseji na sauti.
Alipotakiwa kufika kwenye ofisi za gazeti hili ili kusikilizishwa sauti na kuoneshwa meseji zake, Baby Madaha alisema hawezi kwa kuwa alikuwa na safari ya kwenda nchini Kenya muda mfupi

Saturday, December 28, 2013

MKE AKATWA MAPANGA, HAWARA ATAJWA


Stori: Timoth Itembe, TARIME

MAMA mmoja mkazi wa Ronsoti, Kata ya Nyamisangura, wilayani hapa, Eliza Marwa,28, hivi karibuni amenusurika kuuawa na mumewe, baada ya majirani kufika kumuokoa kutokana na kukatwakatwa mapanga.

Mariamu akiugulia maumivu.
Mama huyo aliliambia gazeti hili akiwa katika Hospitali ya Wilaya Bomani, Tarime kuwa mume wake Marwa Ogora alimkatakata mapanga baada ya kumtuhumu kuwa akikwenda kwa hawara yake badala ya kwenda kwenye mazishi ya mjomba wake…

TARIME
MAMA mmoja mkazi wa Ronsoti, Kata ya Nyamisangura, wilayani hapa, Eliza Marwa,28, hivi karibuni amenusurika kuuawa na mumewe, baada ya majirani kufika kumuokoa kutokana na kukatwakatwa mapanga.

Mariamu akiugulia maumivu.
Mama huyo aliliambia gazeti hili akiwa katika Hospitali ya Wilaya Bomani, Tarime kuwa mume wake Marwa Ogora alimkatakata mapanga baada ya kumtuhumu kuwa akikwenda kwa hawara yake badala ya kwenda kwenye mazishi ya mjomba wake huko Bunchari.
Akifafanua zaidi, Eliza alikuwa na haya ya kusema: ‘’Mjomba alifariki na mazishi yake yalifanyika Desemba, kumi na sita mwaka huu ambapo nilihudhuria baada ya kumwarifu mume wangu kuwa nitahudhuria lakini alinijibu kuwa hakuwa na fedha za kunipa ili niende kwenye mazishi.
“Nilichukua jukumu la kwenda kwa kutumia nauli yangu kwa kuwa muda huo mume wangu alikuwa kazini na baada ya mazishi kesho yake asubuhi Desemba kumi na saba mwaka huu nilirudi nyumbani na kumkuta mume wangu ambaye alianza kunipiga kwa mpini wa jembe kisha panga akidai kuwa sikuwa nimeenda kwenye mazishi badala yake nilikuwa nimeenda kwa mpenzi wangu.
“Alinishambulia sehemu mbalimbali za mwili hususani kichwani, kidogo anitoe ubongo, wasingekuwa majirani kuniokoa baada ya kupiga yowe naamini angeniua kwani hivi sasa siwezi hata kuamka na masikio yameziba, miguu ina ganzi, siwezi kutembea.
“Mume wangu Ogora amekuwa akinipiga mara kwa mara lakini kutokana na watoto tuliozaa naye nimekuwa nikivumilia mateso, naogopa kuondoka na kuacha watoto walelewa na mama wa kambo,”alidai mama huyo.
Ogora hakupatikana kuzungumzia tukio hilo kwani anasakwa na dola na afisa mmoja wa polisi wilayani hapa wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema  wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa. Naye daktari wa hospitali aliyolazwa mama huyo, Nega Malico alikiri kumpokea mgonjwa huyo.