This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Friday, September 13, 2013

RIPOTI YA (UNODC) YASEMA TANZANIA SASA NI KINARA DAWA ZA KULEVYA


*Umoja wa Mataifa wasema Tanga ni hatari
*Yaongoza Afrika Mashariki ikifuatiwa na Kenya
Na Mwandishi Wetu RIPOTI mpya ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Mihadarati na Uhalifu (UNODC), imesema Tanzania ni kinara wa kupitisha dawa za kulevya katika nchi za Afrika Mashariki.

Ripoti hiyo, imesema jumla ya tani 64 za dawa za kulevya aina ya Heroine, zilisafirishwa bila kukamatwa kwenda au kupitia Afrika Mashariki, ikiwamo Tanzania kati ya mwaka 2010 na 2013.

Ripoti hiyo, imesema nchini Tanzania mji wa Tanga, ndio kinara na njia kuu ya kusafirishia dawa hizo kwani tangu mwaka 2010, ukamataji uliongezeka kutoka kilo 145 hadi kilo 813 mwaka huu. 

“Tanga ni njia kuu ya usafirishaji wa dawa hizi, kumekuwa na ongezeko kubwa mno tofauti na miji mingine katika ukanda wa Afrika Mashariki,” ilisema ripoti hiyo. Wastani wa ukamataji wa shehena za dawa za kulevya eneo hilo, uko katika kilogramu 1,011 mwaka 2013 kutoka 145 kilo za awali.

Takwimu zinaonyesha kwa pamoja Watanzania na Wakenya, wanaongoza kwa utumiaji na usafirishaji dawa za kulevya aina ya Cocaine, huku wakitumia dola milioni 160 kila mwaka. Lakini katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, kati ya mwaka 2010 na 2013, shehena zilizokamatwa na maofisa husika nchini Tanzania, Kenya, Shelisheli na Mauritius zilikuwa tani 1.6 tu. 

Takwimu hizo za kushtusha, zinatoa picha kwamba sehemu kubwa ya shehena za dawa za kulevya hupitishwa bila kugundulika au kukamatwa na vyombo vya dola. Eneo la Afrika Mashariki, linaonekana kuwa kimbilio la wasafirishaji kutoka Asia hususani wa Afghanistan, Iran na Pakistan. 

Ripori hiyo, imesema Pwani ya Mashariki mwa Afrika imekuwa kitovu cha biashara na upitishaji dawa za kulevya, kwa sababu ya kukua kwa mahitaji ya ndani na kuchagizwa na hatua zilizochukuliwa kudhibiti dawa hizo katika eneo la Balkan, lililokuwa likiongoza kwa biashara hiyo.

Kwa mfano mwaka 2011, kilogramu 102 za dawa za kulevya zilikamatwa mjini Mombasa, lakini kufikia mwaka 2013, kiwango hicho kiliongezeka kuwa kilo 194.

Ripoti ililinganisha ukanda huo na njia ya Balkan, ambayo inaunganisha nchi za Pakistan, Iran na Uturuki kabla ya kuvusha kwenda kusini mashariki mwa Ulaya. Katika njia hiyo, ukamataji ulishuka hadi kilogramu 679 mwaka 2010, kutoka kilogramu 1,804 mwaka 2006 ikichangiwa pamoja na mambo mengine na kupungua kwa soko la Heroine barani Ulaya.

Hata hivyo, Umoja wa Mataifa unasema wasafirishaji wamebuni njia nyingine ambazo bado hazijulikani kuingia Ulaya. “Mtiririko wa biashara mashariki mwa Afrika kwa hakika umeongezeka, kutokana na ukuaji wa mahitaji ya ndani au ukuaji wa matumizi katika ukanda huo kama soko au eneo la kupitisha mihadarati. 

Iwapo mashariki mwa Afrika itakuwa ‘Balkan mpya’ athari zake kwa ukanda huo, zitakuwa kubwa kama zile zilizoikumba Afrika Magharibi, ripoti ilionya.

“Hatua ya hivi karibuni ya kukamatwa kwa dawa za kulevya, zinachukuliwa uzito kimataifa, lakini pia ongezeko la matumizi ndani ya mashariki mwa Afrika si jambo la kupuuza.”

Wakati dawa za kulevya zinapoondoka Afghanistan, husafirishwa kwa njia ya barabara hadi Pwani ya Makran, ukanda wa jangwani uliotambaa kutoka Pakistan hadi Iran katika mwambao wa Bahari ya Arabu na Ghuba ya Oman ambako wakazi wake wengi ni Waafrika Magharibi na Waasia.

Wasafirishaji hao wana watu wao Mashariki mwa Afrika, ambao wengi wao ni Watanzania na Wakenya wanaoendesha shughuli mpakani.

Mwaka 2011, kwa mfano, Nyakiniywa Naima Mohamed maarufu kama Mama Lela, msafirishaji maarufu wa biashara hiyo raia wa Kenya kutoka kitongoji cha Majengo mjini Nairobi, alikamatwa nchini Tanzania baada ya Rais wa Marekani, Barack Obama kumtaja kuwa mmoja wa vigogo wa ‘unga’. Vigogo wa ‘unga’, hata hivyo huajiri watu wanaowabebea kutoka mataifa mbalimbali yakiwamo Waafrika Kusini na Waafrika Magharibi.

Inaelezwa wabebaji huhusika wa kusafirisha dawa za kulevya, hupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole nchini Ethiopia. Lakini imekuwa kawaida kwa Waafrika Magharibi kutumia hati za kusafiria za Afrika Kusini, wanazopata kwa njia ya kuhonga au kufunga ndoa na raia. 

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, baada ya Watanzania na Wakenya, raia wa Nigeria wanashika nafasi ya pili kama wabebaji maarufu zaidi, huku idadi yao kubwa wakiishi nchini Kenya. Mmoja wa Wanigeria hao, Anthony Chinedu kutimuliwa kwake nchini Kenya, kidogo kusababishe mgogoro wa kidiplomasia baina ya Kenya na Nigeria.

Kesi ya Ruto na Sang yaanza ICC

 
 
 


Naibu rais wa Kenya William Ruto pamoja na mshukiwa mwenzake Joshua Arap Sang wamesomewa mashtaka yanayowakabili katika mahakama ya kimataifa ya ICC
12:24 Wakili Stenberg ambaye anaendelea kuelezea mahakama kuhusu ushahidi wao amesema kuwa Ruto alisambaza silaha kwa vijana ambao wangefanya mashambulizi dhidi ya watu wa kabila hasimu waliokuwa wanaishi katika mkoa wa Rift Valley

12:13 Wakili Steynberg wa upande wa mashtaka amesema kuwa Ruto aliahidi kuwazawadi wale ambao wangefanya uhalifu katika mikutano ambayo vijana walihudhuria kwa wengi wakati wakipangia vurugu baada ya uchaguzi
12:01 Upande wa mashtaka unasimulia ambavyo unapanga kuthibitisha kuwa kesi yao ni ya uhakika, ushahidi utakaotolewa , na nani atakayetoa ushahidi huo. Mashahidi inasemekana watawataja wahusika wengine kwenye kesi hiyo hasa walioshirkiana na washtakiwa kufanikisha mipango yao.
11:55 Upande wa mashtaka kupitia kwa wakili Steynberg umeiambia mahakama kuwa kila mshukiwa anakabiliwa na mashtaka matatu ya kuwalazimisha watu kuondoka makwao kwa lazima, mauaji na kuchochea ghasia

11:51 Bensouda aambia mahakama kuwa amekuwa na wakati mgumu sana kukusanya ushahidi wa kesi yake akisema kuwa wengi wa mashahidi wamejiondoa katika kesi hiyo wakisema wanahofia maisha yao na kuongeza kuwa baadhi pia wamehongwa ili wasitoe ushahidi wao

11:41 Fatou Bensuda mwendesha mkuu wa mashtaka katika mahakama hiyo aelezea mahakama kuhusu tuhuma zinazowakabili Ruto na Sang kwa kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007-2008. Bansuda amesema kuwa Ruto alifanya mauaji kwa sababu za kisiasa huku Sang akimsaidia kuchochea ghasia ili kumsaidia kufanikisha ajenda yake ya kuingia mamlakani

11:35 Joshua Sang pia amekanusha mashtaka yote dhidi yake
11:33 Ruto amekana mashtaka yote aliyosomewa na upande wa mashtaka kuwa alihusika na uhalifu dhidi ya binadamu , mauaji, dhulma na kuwaondosha watu makwao kwa lazima

Ruto akiwa na Joshua Arap Sang wakati kesi dhidi yao ilipowasilishwa katika mahakama ya ICC
11:24 Naye Joshua alisomewa mashtaka dhidi yake ya kuchochea ghasia katika mkoa wa Rift Valley kwa kutumia kituo cha redio alichokuwa anafanyia kazi kueneza chuki na ukabila
11:23 Ruto asomewa mashtaka dhidi yake na kuambiwa kuwa alihusika na mauaji ya watu katika mkoa wa Rift Valley

11:20 Kesi dhidi ya mshukiwa mkuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya Naibu Rais William Ruto imeanza kusikilizwa katika mahakama ya kimataifa ya ICC .
11:00 Wahusika wote kwenye kesi hii kutoka upande wa naibu rais Ruto, mshukiwa mwengine Joshua Arap Sang na upande wa mashtaka wake Fatou Bensauda walijitambulisha mahakamani kwa ombi la mmoja wa majaji kwenye jopo la majaji

NDOA YA H. BABA NA FLORA MVUNGI IMEJIBU.


Hatimaye ile ndoa iliyofungwa miezi michache iliyopita kati ya Super Star wa TAKEU Bongo Fleva H. Baba na mwigizaji maarufu nchini wa Bongo Movie mwanamama Flora Mvungi imejibu kwa wawili hao kupata mtoto wa kike. 

Kwa mujibu wa Mwanamuziki huyo anayetoka familia ya 'MWANZA KWANZA', Leshontek  H. Baba anasema kuwa anaendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa mkewe kujifungua salama mtoto wa kike ambaye tayari kesha mpa jina la Tanzanite, akijivunia kuwa Mtanzania na kuzitukuza rasilimali zake zilizopo.
WAKUTWA CHOONI WAKILAWITIANA...BOSI AJITETEA ALIKUWA ANATAKA KUNYOLEWA MAV***I NA MFANYAKAZI WAKE. - See more at: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2013/09/mbongo-anaswa-akitaka-kulawitiwa-na.html#sthash.bmDSJchT.dpuf

SHILOLE BALAAAAAAAA

MWENYEKITI wa Kamati ya Umoja wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania, Kimela Billa, ameutaka uongozi wa Shirikisho la Muziki Tanzania, kumchukulia hatua ya kinidhamu, msanii wa muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kosa la kukiuka maadili ya Tanzania katika tamasha la Serengeti Fiesta, mkoani Iringa.

Shilole alipanda jukwaani akiwa anacheza wimbo wake wa ‘Nakomaa na jiji’ huku akiwa amevaa nguo ambazo zinaonesha maumbile yake yote ya mwili.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Billa alisema Shirikisho la muziki chini ya rais wake, Addo Novemba wanatakiwa kuchukua hatua zaidi juu ya shilole kwa kosa la kuwadhalilisha wanawake ikiwa ni pamoja na kukiuka maadili ya Tanzania.

“Hatukatai hayo mambo yapo lakini kwa staili ile sisi kama viongozi wa sanaa hatutaweza kuvumilia, shirikisho la muziki wakishindwa kutekeleza hili lazima kamati ilivalie njuga swala hilo, kiukweli wanalidhalilisha taifa hawa wasanii, mbona wanaume hafanyi shoo zao uchi,? Alihoji Billa.

Alisema shirikisho la muziki liige mfano wa shirikisho la filamu kama lilivowaonya Wema Sepetu na Aunt Ezekiel kwa makosa kama hayo, ambapo anamini kwaasilimia kubwa kunachangia kuwa na nidhamu wanapopanda jukwaani.


“Angekua ameenda kwa shughuli za filamu wangelifanya wao lakini hili shirikisho la muziki wanatakiwa wakae meza moja na Shilole kulizungumzia hilo, wao wanakua wazito kuwachukulia hatua
- See more at: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2013/09/chupi-na-shanga-alizoonyesha-shilole.html#sthash.EdxLF8Zq.dpuf
MWENYEKITI wa Kamati ya Umoja wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania, Kimela Billa, ameutaka uongozi wa Shirikisho la Muziki Tanzania, kumchukulia hatua ya kinidhamu, msanii wa muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kosa la kukiuka maadili ya Tanzania katika tamasha la Serengeti Fiesta, mkoani Iringa.

Shilole alipanda jukwaani akiwa anacheza wimbo wake wa ‘Nakomaa na jiji’ huku akiwa amevaa nguo ambazo zinaonesha maumbile yake yote ya mwili.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Billa alisema Shirikisho la muziki chini ya rais wake, Addo Novemba wanatakiwa kuchukua hatua zaidi juu ya shilole kwa kosa la kuwadhalilisha wanawake ikiwa ni pamoja na kukiuka maadili ya Tanzania.

“Hatukatai hayo mambo yapo lakini kwa staili ile sisi kama viongozi wa sanaa hatutaweza kuvumilia, shirikisho la muziki wakishindwa kutekeleza hili lazima kamati ilivalie njuga swala hilo, kiukweli wanalidhalilisha taifa hawa wasanii, mbona wanaume hafanyi shoo zao uchi,? Alihoji Billa.

Alisema shirikisho la muziki liige mfano wa shirikisho la filamu kama lilivowaonya Wema Sepetu na Aunt Ezekiel kwa makosa kama hayo, ambapo anamini kwaasilimia kubwa kunachangia kuwa na nidhamu wanapopanda jukwaani.


“Angekua ameenda kwa shughuli za filamu wangelifanya wao lakini hili shirikisho la muziki wanatakiwa wakae meza moja na Shilole kulizungumzia hilo, wao wanakua wazito kuwachukulia hatua
- See more at: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2013/09/chupi-na-shanga-alizoonyesha-shilole.html#sthash.EdxLF8Zq.dpuf
 
 
MWENYEKITI wa Kamati ya Umoja wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania, Kimela Billa, ameutaka uongozi wa Shirikisho la Muziki Tanzania, kumchukulia hatua ya kinidhamu, msanii wa muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kosa la kukiuka maadili ya Tanzania katika tamasha la Serengeti Fiesta, mkoani Iringa.

Shilole alipanda jukwaani akiwa anacheza wimbo wake wa ‘Nakomaa na jiji’ huku akiwa amevaa nguo ambazo zinaonesha maumbile yake yote ya mwili.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Billa alisema Shirikisho la muziki chini ya rais wake, Addo Novemba wanatakiwa kuchukua hatua zaidi juu ya shilole kwa kosa la kuwadhalilisha wanawake ikiwa ni pamoja na kukiuka maadili ya Tanzania.

“Hatukatai hayo mambo yapo lakini kwa staili ile sisi kama viongozi wa sanaa hatutaweza kuvumilia, shirikisho la muziki wakishindwa kutekeleza hili lazima kamati ilivalie njuga swala hilo, kiukweli wanalidhalilisha taifa hawa wasanii, mbona wanaume hafanyi shoo zao uchi,? Alihoji Billa.

Alisema shirikisho la muziki liige mfano wa shirikisho la filamu kama lilivowaonya Wema Sepetu na Aunt Ezekiel kwa makosa kama hayo, ambapo anamini kwaasilimia kubwa kunachangia kuwa na nidhamu wanapopanda jukwaani.


“Angekua ameenda kwa shughuli za filamu wangelifanya wao lakini hili shirikisho la muziki wanatakiwa wakae meza moja na Shilole kulizungumzia hilo, wao wanakua wazito kuwachukulia hatua
- See more at: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2013/09/chupi-na-shanga-alizoonyesha-shilole.html#sthash.EdxLF8Zq.dpuf
MWENYEKITI wa Kamati ya Umoja wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania, Kimela Billa, ameutaka uongozi wa Shirikisho la Muziki Tanzania, kumchukulia hatua ya kinidhamu, msanii wa muziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kosa la kukiuka maadili ya Tanzania katika tamasha la Serengeti Fiesta, mkoani Iringa.

Shilole alipanda jukwaani akiwa anacheza wimbo wake wa ‘Nakomaa na jiji’ huku akiwa amevaa nguo ambazo zinaonesha maumbile yake yote ya mwili.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Billa alisema Shirikisho la muziki chini ya rais wake, Addo Novemba wanatakiwa kuchukua hatua zaidi juu ya shilole kwa kosa la kuwadhalilisha wanawake ikiwa ni pamoja na kukiuka maadili ya Tanzania.

“Hatukatai hayo mambo yapo lakini kwa staili ile sisi kama viongozi wa sanaa hatutaweza kuvumilia, shirikisho la muziki wakishindwa kutekeleza hili lazima kamati ilivalie njuga swala hilo, kiukweli wanalidhalilisha taifa hawa wasanii, mbona wanaume hafanyi shoo zao uchi,? Alihoji Billa.

Alisema shirikisho la muziki liige mfano wa shirikisho la filamu kama lilivowaonya Wema Sepetu na Aunt Ezekiel kwa makosa kama hayo, ambapo anamini kwaasilimia kubwa kunachangia kuwa na nidhamu wanapopanda jukwaani.


“Angekua ameenda kwa shughuli za filamu wangelifanya wao lakini hili shirikisho la muziki wanatakiwa wakae meza moja na Shilole kulizungumzia hilo, wao wanakua wazito kuwachukulia hatua
- See more at: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2013/09/chupi-na-shanga-alizoonyesha-shilole.html#sthash.EdxLF8Zq.dpuf
 

 
a kosa la kuwadhalilisha wanawake ikiwa ni pamoja na kukiuka maadili ya Tanzania.

“Hatukatai hayo mambo yapo lakini kwa staili ile sisi kama viongozi wa sanaa hatutaweza kuvumilia, shirikisho la muziki wakishindwa kutekeleza hili lazima kamati ilivalie njuga swala hilo, kiukweli wanalidhalilisha taifa hawa wasanii, mbona wanaume hafanyi shoo zao uchi,? Alihoji Billa.

Alisema shirikisho la muziki liige mfano wa shirikisho la filamu kama lilivowaonya Wema Sepetu na Aunt Ezekiel kwa makosa kama hayo, ambapo anamini kwaasilimia kubwa kunachangia kuwa na nidhamu wanapopanda jukwaani.


“Angekua ameenda kwa shughuli za filamu wangelifanya wao lakini hili shirikisho la muziki wanatakiwa wakae meza moja na Shilole kulizungumzia hilo, wao wanakua wazito kuwachukulia hatua wasanii wa muziki kuliko filamu lakini kwa hili haitawezekana, ,” alisema.
- See more at: http://vitukovyamtaa.blogspot.com/2013/09/chupi-na-shanga-alizoonyesha-shilole.html#sthash.EdxLF8Zq.dpuf
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

NDOA YA MZEE MAJUTO YAVUNJIKA

MWANAMKE anayedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchekeshaji mahiri Bongo, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto au King Majuto, Rahma Abdallah (20), ameibuka na kudai kutelekezwa na mumewe huyo.

Mzee Majuto akiwa na mkewe Rahma Abdallah siku ya ndoa yao.
Ndoa hiyo ambayo ilifungwa kwa siri jijini Dar Julai 28, mwaka huu na kudumu siku 44, inaonekana imevunjika rasmi baada ya Mzee Majuto kutoa talaka kupitia kwa msanii wa…
Na Imelda Mtema
MWANAMKE anayedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchekeshaji mahiri Bongo, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto au King Majuto, Rahma Abdallah (20), ameibuka na kudai kutelekezwa na mumewe huyo.
Mzee Majuto akiwa na mkewe Rahma Abdallah siku ya ndoa yao.
Ndoa hiyo ambayo ilifungwa kwa siri jijini Dar Julai 28, mwaka huu na kudumu siku 44, inaonekana imevunjika rasmi baada ya Mzee Majuto kutoa talaka kupitia kwa msanii wa filamu aitwaye Rehema Omary.
Akizungumza na gazeti hili katika ofisi zetu, Bamaga-Mwenge, Dar, Septemba 9, mwaka huu, Rahma alidai kuwa alikutana na Mzee Majuto jijini Tanga na kuanzisha uhusiano wa kimapenzi kwa miezi sita kabla ya kufunga ndoa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani uliopita.
“Tulifahamiana Tanga, mimi ni mwenyeji wa huko kama ilivyo kwa Mzee Majuto, wakati tukiwa kwenye uhusiano, ulipofika Mwezi wa Ramadhani akaona bora tufunge ndoa ili tusiendelee kutenda dhambi, akaniambia dhamira yake hiyo nami sikukataa,” alisema Rahma.
Rahma Abdallah (20).
TOFAUTI MIAKA 40
Mke huyo ambaye ni kibinti cha umri wa miaka 20 aliyepishana na Mzee Majuto kwa umri wa miaka 40 alisema kuwa, mwigizaji huyo alifuata taratibu zote za kufunga ndoa kwa kupeleka barua ya posa nyumbani kwao.
“Alitoa mahari ndipo ilipopangwa siku ya ndoa iliyofungwa nyumbani kwa mama yangu, Mbagala-Zakhem, Dar,” alifafanua Rahma.
ULINZI MKALI, BARAFU MPAMBE
Katika ndoa hiyo iliyofungwa katika Mtaa wa Kibonde-Maji Julai 28, mwaka huu na Shehe Abdurahman Kisoma na kufuatiwa na sherehe nyumbani kwa bibi harusi, ulinzi mkali uliwekwa ili siri ya Mzee Majuto kuoa isivuje.
Mashahidi wa ndoa hiyo walikuwa ni Suleiman Said ‘Barafu’ ambaye ni mwigizaji aliyekuwa mpambe wa bwana harusi pamoja na Mohammed Malila.
...Siku ya ndoa yao.
MAHARI 20,000
Cheti cha ndoa hiyo, kinaonesha kwamba Mzee Majuto alimuoa mwanamke huyo kwa mahari ya shilingi 20,000 aliyolipa yote.
“Baada ya ndoa, Mzee Majuto aliwaomba wazazi wangu nikae nyumbani hadi Mwezi wa Ramadhani utakapoisha ndipo atakapokuja kunichukua, akaniachia shilingi elfu sitini tu, mpaka leo hii sijamuona,” alisikitika mke huyo ambaye alikuwa akijua kama Mzee Majuto alikuwa na mke mwingine.
KAZI KWA PROFESSA J
Mke huyo wa Mzee Majuto alisema kuwa kabla ya kufunga ndoa na gwiji huyo wa uchekeshaji alikuwa akifanya kazi katika saluni ya mwanamuziki Joseph Haule ‘Profesa Jay’ iliyopo Msasani, Dar.
“Nilikuwa nafanya kazi na kupata kipato huku nikiwa nimepanga chumba lakini Majuto aliniambia niache kazi na nirudishe chumba, nami nikafanya hivyo nikijua naenda kuishi kwa mume wangu, kumbe!...” alijuta Rahma.
MESEJI CHAFU ZA MKE MKUBWA
Baada ya Majuto kuondoka mke huyo alikuwa akimpigia simu kutaka fedha za matumizi lakini alikuwa akiambiwa awasiliane na Bi. Rehema, mwanamke ambaye Mzee Majuto huwa anaigiza naye katika filamu zake.
Rahma alilalamika kutumiwa ujumbe wa matusi kwenye simu yake na mke mkubwa wa Mzee Majuto.
“Kitendo hicho kinaniuma sana kwani wakati mwingine huwa ananitukana na kunitishia maisha, akidai eti atanifanyia kitu kibaya, nikimpigia Majuto na kumweleza naye ananijibu mbovu,” aliongeza.
Mke huyo mdogo wa Mzee Majuto alisema kuwa anaumia kutokana na kuharibiwa maisha kwa kuolewa na kuachishwa kazi huku akiendelea kutukanwa na mke mkubwa.
MASHITAKA BAKWATA
Rahma ambaye aliliachia Amani nakala ya cheti cha ndoa alisema msanii huyo amemdhalilisha kwani kila akidai talaka yake anamwambia ameshaituma kwa Bi. Rehema na kumtaka aende akaichukue kitu ambacho ni kinyume na makubaliano yao.
Rahma alisema kuwa amejipanga kwenda kumshitaki Mzee Majuto katika Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) ili amlipe fidia na kumtafutia kazi.
“Yeye ndiye aliyenioa lakini nikimdai talaka ananimbia alimpa Bi.Rehema, wakati mwanamke huyo siye aliyenioa, sasa nampeleka Bakwata ili anikabidhi talaka na kunilipa fidia,” alisema kwa hasira mke huyo.
MSIKIE MZEE MAJUTO
Akijibu tuhuma hizo akiwa jijini Tanga, Mzee Majuto alikiri kufunga ndoa na Rahma na kusema kuwa alishamuacha kwa sababu aligundua hajatulia.
“Huyo mwanamke nimeshaachana naye ila kwa sasa anataka kunichafua, kama anahisi ana haki kwa nini asiende mahakamani? Nimemtuma mshenga ampe talaka hataki kuipokea, anataka nije Dar. Kama huo siyo uhuni ni nini? huyo mwanamke hajatulia,” alisema.
TALAKA KULETWA GLOBAL
Mzee Majuto alidai kwamba, Rahma amekuwa akimpa usumbufu na kufikia kumpa masharti ya ajabu na kuahidi kumtuma mtu ailete nakala ya talaka hiyo katika ofisi

HONGERA KWA KUJIUNGA NA TAIFA STAR

Adam Nditi.

WATANZANIA wawili wenye uraia wa Uingereza, wamekubali kurejea nchini kuichezea timu ya taifa, Taifa Stars.
Adam Nditi anayekipiga timu ya vijana ya Chelsea, mwenye uraia wa England, amesema yupo tayari kuitumikia Stars kama ilivyo kwa Ismail Feruz raia wa Scotland. Kocha Mkuu wa Stars, Kim Poulsen amesema wachezaji hao wawili makinda wamekubali kuichezea Stars.
 “Wote nimezungumza nao na wameonyesha wanataka kuja kuitumikia Taifa Stars badala ya Uingereza. Wako tayari kuja kuitumikia Tanzania ambayo ni nchi ya asili yao.
“Nditi amenifafanulia kwa nini alichukua pasi ya kusafiria ya England, lakini ana mapenzi makubwa na Tanzania.
“Hili si suala la TFF sasa, linakwenda zaidi katika siasa kama Tanzania itakubali kubadili mfumo na kuruhusu pasi mbili za kusafiria. Hii itatusaidia sisi.”

Wednesday, September 11, 2013

SIRI NJE

USIRI ulikuwa umetawala kuhusu mmiliki wa meli ya Kitanzania iliyonaswa juzi nchini Italia, ikiwa na tani 30 za madawa ya kulevya aina ya bangi lakini sasa kila kitu kinaweza kuwekwa nje bin hadharani kutokana na taarifa mpya ambazo gazeti hili limezipata.

Mv Gold Star ikiungua.
Uwazi linazo ‘data’ kuwa mmoja wa wamiliki wa meli hiyo ni mfanyabiashara wa Kitanzania mwenye asili ya Bara la Asia ambaye alipata kuwa memba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu…
Stori: Mwandishi Wetu
USIRI ulikuwa umetawala kuhusu mmiliki wa meli ya Kitanzania iliyonaswa juzi nchini Italia, ikiwa na tani 30 za madawa ya kulevya aina ya bangi lakini sasa kila kitu kinaweza kuwekwa nje bin hadharani kutokana na taarifa mpya ambazo gazeti hili limezipata.
Mv Gold Star ikiungua.
Uwazi linazo ‘data’ kuwa mmoja wa wamiliki wa meli hiyo ni mfanyabiashara wa Kitanzania mwenye asili ya Bara la Asia ambaye alipata kuwa memba wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu zilizopita.
Jina la mfanyabiashara huyo linabaki kwenye kapu letu mpaka baadaye tutakapokuwa kwenye mazingira sahihi ya kumtaja, kwani kufanya hivyo kwa sasa ni kuingilia mamlaka za kisheria ambazo zipo kwenye uchunguzi makini.
Habari zinafafanua kuwa mbunge huyo, hamiliki meli hiyo peke yake, bali kuna watu wengine ambao ni raia wa Visiwa vya Marshall, barani Australia.
Magunia ya bangi japo siyo yaliyokuwa katika MV Gold Star.
Inaelezwa zaidi kwamba watu hao kutoka Marshall ni mabilionea wakubwa ambao wanamiliki visiwa vitatu kwenye Bahari ya Pacific ambavyo ni Ujae Atoll, Ujelang Atoll na Lib.
Mabilionea hao ndiyo wenye Kampuni ya Gold Star Shipping ambayo inajihusisha na utoaji wa huduma za usafiri wa majini hususan kwa njia ya meli.
Gold Star Shipping ni kampuni iliyosajiliwa Visiwa vya Marshall lakini kwa ushirikiano na mbunge huyo wa zamani, waliileta nchini meli yao ya mizigo ya MV Gold Star, ikasajiliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

MAGUMASHI YALIPOANZA
MV Gold Star ilisajiliwa Zanzibar ili tu ipate kibali cha kutumia Bendera ya Taifa la Tanzania, kwani baada ya hapo, imekuwa ikipuyanga kwenye mataifa mengine, ikitoa huduma za usafiri pasipo kurudi kwenye nchi iliyosajiliwa.
Taarifa za hivi karibuni, zinaonesha kuwa imeshakwenda na kurudi Misri mara mbili, Algeria mara mbili na Uturuki, huku Bandari ya Zanzibar ambayo inaitambulisha kama ndiyo nyumbani kwao, haijapata kutia nanga hata mara moja.
Julai 29, 2013, saa 2:04 asubuhi, ilitia nanga Bandari ya Said, Misri. Juni 18, 2013, saa 1:05 jioni, iliwasili Bandari ya Mostaganem, Algeria. Mei 31, 2013, saa 9:04 usiku, ilifika Bandari ya Iskenderun, Uturuki. Mei 24, 2013, saa 1:04 asubuhi, iliingia Bandari ya Said, Misri na Aprili 14, 2013, saa 2:02 asubuhi, ilipiga king’ora Bandari ya Mostaganem, Algeria.

WASIFU WA MELI
Bandari ya nyumbani ni Zanzibar, imetengenezwa mwaka 1975, watengenezaji ni Kampuni ya Astilleros De Mallorca, iliyopo Palma De Mallorca, Hispania, mmiliki ni Gold Star Shipping kutoka Visiwa vya Marshall, meneja ni Gold Star Shipping, ipo katika jamii ya Hellenic Shipping Register.

WAMILIKI WA ZAMANI
Ilimilikiwa na Ibrahim Junior mpaka Februari 2011, Breogan I (aliiuza Novemba 2006), Breogan (Machi 2002), Estela De Mar (Desemba 1996), Inezgane (1996), Puerto Suances (1988) na Suecia (1985).

NI MADAWA YENYE THAMANI KUBWA
Kwa mujibu wa ripoti za mitandao ya Waitaliano na Waingereza, MV Gold Star, ilipakia mzigo wa madawa ya kulevya nchini Uturuki na walikuwa wanafanya jaribio la kuingiza mzigo huo wenye tani 30 nchini Italia.
Walinzi wa ufukweni kwenye Bahari ya Mediterranean, waliishtukia meli hiyo na kuizingira, watu waliokuwemo baada ya kuona hali ni mbaya, waliwasha moto kuiteketeza MV Gold Star kisha kufanya jaribio la kutaka kutoroka kupitia boti ndogo.
Askari hao wa ufukweni, walishirikiana na maofisa uhamiaji wa Italia kuwakamata watu tisa ambao walikuwemo kwenye meli hiyo na baada ya kuwahoji, ilibainika wote wanatokea nchi za Misri na Syria.
Taarifa kutoka kwa maofisa uhamiaji wa Italia zinasema kwamba baada ya kuwahoji watuhumiwa, ilibainika waliamua kuiteketeza meli hiyo kwa moto ili kuondoa ushahidi wa tani 30 za madawa ya kulevya zilizokuwemo.
Ilibainishwa pia kuwa thamani ya madawa hayo ya kulevya yaliyokamatwa ni pauni milioni 50 ambazo kwa chenji ya Tanzania ni shilingi bilioni 126.5.

FEDHA HIZO ZINAWEZA KUENDESHA WIZARA TATU
Kama mzigo huo ungevuka salama na kuuzwa, fedha hizo zinatosha kuendesha wizara tatu katika Serikali ya JK, hii ni kwa mujibu wa makadirio na mapato ya matumizi (bajeti), mwaka wa fedha 2013-2014.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto bajeti yake ni shilingi bilioni 23, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo shilingi bilioni 30 na Wizara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mifugo shilingi bilioni 67, jumla shilingi bilioni 120.
Hii inamaanisha kuwa fedha hizo za wauza unga, zinaweza kuendesha wizara hizo na chenji itabaki shilingi bilioni 6.5 ambazo zinaweza kujenga shule na mabweni mengi tu. Uchambuzi huo ni kuonesha namna ambavyo wauza unga walivyo watu hatari, kwani wana pesa nyingi.

ITALIA KAZI WANAYO
Baada ya kuwakamata watuhumiwa hao, vikosi vya uokoaji nchini humo, kuanzia vya majini, anga na nchi kavu, viliizingira meli hiyo kuzima moto uliokuwa unaiteketeza.
Mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni, taarifa zilieleza kwamba bado shughuli ya kuzima moto ilikuwa inaendelea.

TANZANIA HAKUNA ANAYEJUA
Uwazi lilifanya jitihada za kuwatafuta watu mbalimbali wanaohusika na udhibiti wa madawa ya kulevya nchini lakini hakuna hata mmoja aliyekuwa na taarifa.
Hata Kamanda wa Kikosi cha Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa, aliliambia Uwazi akiwa nchini Ethiopia kuwa hajui chochote kuhusu meli hiyo kukamatwa lakini aliahidi kufuatilia.

NI SKENDO NZITO KWA NCHI
Kukamatwa kwa meli hiyo kunazidi kuipaka matope Tanzania, kwani hivi karibuni raia wake wamekuwa wakikamatwa katika mataifa mengine, wakiwa wanasafirisha madawa ya kulevya. Vilevile, kuna ile skendo ya meli ya Wairan yenye Bendera ya Tanzania ambayo iliibua gumzo mwaka huu lakini suluhisho halijapatikana.