This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Wednesday, April 17, 2013

"WAISLAMU PEKEE NDO WARUHUSIWE KUCHINJA NYAMA YA BIASHARA"....HII NI KAILI YA LEO YA RAIS MWINYI




Hii  ni  video  ikionesha  kauli  ya  Rais  Mwinyi  kuhusu  suala  la  kuchinja.Kauli  hii  amaitoa  leo  alipoongea  na  waandishi  wa 

MUNGU AILAZE PAHALI PEMA PEPONI


Mwanamuziki mkongwe katika Taarab Fatuma Bint Mbaraka maarufu kwa jina la Bi Kidude amefariki dunia leo mchana  huko Bububu Zanzibar, sehemu alikokuwa anaugulia kwa kipindi sasa. Mwili wake utahamishiwa kwake Rahaleo na mazishi yatakuwa kesho. 

Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo..Alikuwa binti... wa mchuuzi wa nazi na hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe ngapi, kuna hata mawazo kuwa alikwishafikisha miaka 102. 

Katika mwaka 1920 tayari alikuwa amekwisha anza kuimba katika vikundi vya sanaa kule kwao...mwaka 1930 alijiunga na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam na kuzunguka miji mingi ya Tanganyika wakati ule .....


Mwaka 1940 alirudi Zanzibar ambako awali alikuwa amekimbia kwa kuwa aliozwa kwa nguvu na mtu aliyemzidi sana umri.

Bi Kidude pia aliwahi kuimba na Sitti Binti Sadi wakati wa ujana wake, na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni


Mungu Amlaze Pema Peponi Bibi yetu. Amen

"COME- ON.....FU*KY YOU"......HILI NI TUSI LA NGUONI TOKA KWA SERUKAMBA BUNGENI LEO....USHAHIDI UPO


Baada ya kuona kusitisha bunge kurushwa live kumepigwa vita, sasa wabunge wamekuja kwa staili ya matusi ili wananchi wasiwe na hamu kabisa ya kuliangalia bunge....

LEO kwa mara nyingine tena, Mh.Peter Serukamba amesikika waziwazi kabisa akitoa tusi mbele ya bunge na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yake.

Bila woga wala aibu ya kuwa huenda anasikilizwa na wakwe zake ,Serukamba amesikika akisema "Come-on F.U.C.K Y.O.U."

 

TUKIO  LENYEWE  LILIKUWA  HIVI: 
 
Hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliitaka serikali iwachukulie hatua kali wahusika wote wanaohusika na matukio ya utekwaji na uteswaji wa baadhi ya watu,kwa kutolea mifano ya Dr.Ulimboka na Kibanda.katika hotuba hiyo,kambi imeonesha kutoridhika na mwendendo wa utendaji wa idara ya usalama wa taifa.
Aidha hotuba hiyo kuna mahali imemtaja Rwakatare na mwenendo wake kabla ya kukamatwa.

Shida imeanza pale ambapo Mh.Serukamaba aliomba mwongozo wa spika,na kusema kuwa,kuna baadhi ya maswala yaliyomo ktk hotuba hiyo( hasa kuanzia ukurasa wa 1-4) yanazungumzia kesi ya Rwakatare ambayo tayari ipo mahakamani.
Na kwamba kuendelea kusomwa kwa hotuba hiyo ingekuwa ni kuingilia mwenendo wa kesi na kwamba hapo ingekuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Katika kutetea hoja zao,wabunge watatu wa kambi ya upinzani(H.Mdee,J.Mnyika na T.Lisu) walisimama na kujaribu kuonesha uhalali wa hoja zao.Wote watatu walijieleza kwa kadiri walivyoona inafaa.
Baada ya hapo ndipo aliposimama Mh.Serukamba na kusisitiza uhalali wa hoja yake.
Sasa kile kitendo cha yeye kusimama tena,inaonekana kulikuwa na minong'ono upande wa pili(lakini hiyo haikusikika) ndipo kwa kujisahau alipojikuta ametupia hewani TUSI HILO  la  "Come-on F.U.C.K Y.O.U."!

Kwa jinsi alivyotukana,aliunganisha haraka na maelezo yake kiasi kwamba Mh.J.Ndugai(aliyekuwa akiongoza) hakumkatisha, akamwacha aendelee.
Baada ya maelezo ya Mh.Serukamba,naibu spika(mwenyekiti) alitoa kauli yake rasmi.
Ndugai amesema kuwa mgogoro huu una mtazamo wa kikanuni,kwa hiyo ameagiza kamati ya kanuni ya bunge ikutane mara moja kujadili swala hilo kisha itoe ushauri kwa kiti cha spika jinsi gani ya kshughulikia mambo hayo yanayoonekana yana utata.
Aidha amesema hotuba hiyo ya kambi rasmi ya upinzani itaendelea kusomwa kipindi cha jioni.

Tuesday, April 16, 2013

SPIKA WA BUNGE AWAVAA WABUNGE "WANAOTUMIA MATUSI" BUNGENI


Akiongea kwa uchungu , Spika wa Bunge bi Anne Makinda amewashambulia wabunge  leo asubuhi na kuwaambia suti zao walizovaa haziendani na matusi  yanatoka  katika vinywa vyao  ambayo yeye ameshindwa kuyataja kutokana kwa  madai  kuwa mdomo  wake hauwezi kutamka matusi hayo.....
Makinda amesema matusi ndiyo yamekuwa yakitawala katika midomo ya wawakilishi hao na kuacha hoja inayojadiliwa hewani....
 
Spika wa bunge amekwenda mbali zaidi na kuwaambia wabunge hao kwamba hataangalia chama endapo mbunge atavunja kanuni za bunge kwa kuwa kanuni za bunge zinampa nafasi ya kuita polisi na kuja kumchukua mbunge huyo kwa hatua za kisheria.

Makinda  amesema ametumiwa sms ambayo mtumaji amedai hatokaa tena na familia yake kuangalia bunge labda ajifungie chumbani.

"NIMEMSAMEHE DIAMOND INGAWA ALINISALITI KWA UWOYA....KWA SASA TUMEYAMALIZA".....HII NI KAULI YA PENNY


Katika muda ambao kila mmoja alikuwa amejaribu kuamini kuwa Diamond Platnumz ameamua kutulia na mpenzi mmoja, mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa, hivi karibuni  staa huyo ameanzisha uhusiano wa kimapenzi na muigizaji wa filamu Irene Uwoya.....
 



Magazeti ya udaku nchini yaliandika habari hiyo ikiwa na picha inazowaoenesha mastaa hao wakichukua chumba kwenye hoteli ambako  walienda kufanya yao.
DIAMOND3
Kufuatia tetesi hizo, mwandishi wetu amezungumza na mpenzi wa sasa wa Diamond, Penny ambaye amesema kwa ufupi kuwa wameshayazungumza na Diamond na wako vizuri kwa sasa lakini akasisitiza kuwa asingependa kuliongelea zaidi suala hilo.

Katia hatua nyingine, Jokate Mwegelo aliyewahi kuwa na uhusiano na Diamond amekanusha  taarifa iliyoandikwa na gazeti moja la udaku kuwa amemcheka Irene kwa kunaswa kwenye himaya ya Diamond.
JOKATE
“Mimi hivyo vitu havinihusu na wanapenda kupata quotes zangu pasipo hitajika. I don’t know why? I don’t why wanatafuta story. That’s their life kiukweli with whatever they choose to do, more power to them,” amesema Jokate.

BOB JUNIOR AINGIZWA MKENGE....LAWAMA ZATUPWA TIGO


Imebainika kuwa kuna mtu aliyetengeneza line mpya kwa kutumia namba ya Bob Junior aliye barani Ulaya kwa sasa na kutaka kuwatapeli watu wake wa karibu kuwa yupo hoi na anahitaji msaada haraka.



Taarifa hiyo imetolewa na baba yake mdogo, Guru Ramadhan ambaye ni mmiliki wa G Records. Kupitia Facebook, Guru aka G Lover ameandika:

“Hii sijaipenda kabisa ni too much sasa..eti mtu yupo Europe na simu yake inaita bongo ukipiga duh kumbe mtu katengeneza line mpya na kutumia namba ya Bob Junior na pia jamaa anayetumia hiyo line ya simu eti anaomba msaada kwa watu kuwa Bob Junior anaumwa sana Ulaya anahitaji msaada wako ili arudi Bongo.

Hivi nini maana ya kusajili namba?…makampuni ya simu ya Bongo mjipange sanaaa…hili limemkuta msanii Bob Junior siku chache hizi, mpaka imeripotiwa polisi eti ndio wamejidai kui block number…t.g. mmeniboaje?..so guyz mnaosafiri muwe makini sana mkisafiri maana mnaweza kukuta madeni kibao mkafa na presha bure…wizi mtupu…I hate dat.”