This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Wednesday, April 3, 2013

PICHA ZA MATUKIO YA VURUGU HUKO TUNDUMA......DIWANI ( CHADEMA ) NA MCHUNGAJI KKKT WANASAKWA NA POLISI

 

Hii ndiyo hali halisi ya Mji mdogo wa Tunduma leo kuanzia asubuhi

Matairi yanachomwa katikati ya barabara

Mambo hayo 



Mwandishi wetu pamoja na waandishi wenzake walipata shida sana kufika mji wa Tunduma walikutana na vikwazo vingi sana lakini wananchi walikuwa waelewa waliwasaidia kutoa magogo na matairi ili wapite wakapate habari












Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Diwani akiongea na waandishi wa habari
Wanafunzi wakisindikizwa na jeshi la polisi kurudi majumbani mwao
Polisi wakiendelea na kazi yao katika mitaa ya Tunduma
Baadhi ya magari ya IT yaendayo nchini Zambia yakiwa yamepakiwa nnje kidogo ya mji wa Tunduma kuogopa kuharibiwa kwa magari hayo

----------------
Diwani wa kata ya Tunduma Ndugu Frank Mwaijoka (Chadema) pamoja na mchungaji wa kanisa la KKT katika eneo hilo la Tunduma wilayani momba Mkoani mbeya wametakiwa kujisalimisha kituo cha Polisi Tunduma mara baada ya kuhusika na uchochezi wa kidini hali ambayo imepelekea kutokea kwa vurugu  katika eneo hilo.

Vurugu hizo zimeanza majira ya saa 4 asubuhi katika eneo hilo la tunduma mara baada ya kundi la watu wanaodai kuwa wao ni wafuasi wa dini ya kikristo wakidai waruhusiwe kuchinja mifugo na kuuza katika mabucha yao hali iliyo pelekea kuibuka kwa vurugu hizo.

Akizungumza kuhusiana na tukio hilko Kamanda wa Polisi Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani amesema kuwa kufuatia kuwepo kwa tukio hilo jumla ya watu zaidi ya 40 tayari wamekwisha kamatwa .

Amesema mpaka sasa taarifa walizo zipata kufuatia vurugu hizo zinaeleza kuwa miongoni mwa watu walichochea vurugu hizo ni diwani wa kata hiyo ya Tunduma Ndugu John Mwaijoka pamoja na Mchungaji wa kanisa la kkt ndugu Neema Mwaipusa ambao kwa pamoja wametakiwa kujisalimisha kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.

Amesema suala hilo limegubikwa  na siasa kwani tayari viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa mkoa huo Ndugu Abbas Kandoro amekwisha litolea ufafanuzi Apri 02 mwaka huu wakiwepo pia viongozi wa dini .
Amesema kwa asilimia kubwa mgogoro huo juu ya nani achinje umeingiliwa na mambo ya kisiasa kwani hata baadhi ya wananchi wa maeneo hayo wamekuwa wakilalamika juu ya kutokea kwa vurugu hizo.

Amesema shughuli za kibiashara katika eneo hilo zimeshindwa kufanyika katika eneo hilo hivyo kufanya wananchi kupata adha hasa kwa nchi jirani ya Zambia ambao kwa asilimia kubwa wanategema kupata mahitaji kutoka mpakani mwa Tanzania.

Hata hivyo Diwani amesema kuwa katika vurugu hizo askari mmoja  pamoja na mwananchi wamejeruhiwa kwa kupigwa mawe ambapo tayari wamekwisha fikishwa kituo cha polisi.

Kufuatia hali hiyo Kamanda huyo wa Polisi amesema kwa sasa hali imelejea katika hali yake ya kawaida hivyo amewataka wananchi wa maeneo hayo kuwa watulivu wakati jeshi hilo la Polisi likiendela na msako wa kuwatafuta wahalifu wengine.

HII NDO KAULI YA UCHUNGU ALIYOTOA ABSALOM KIBANDA BAADA YA KUTEKWA NA KUTOBOLEWA JICHO



 

 Kauli  hii  ameitoa  kupitia  ukurasa  wake  wa  facebook:

Si jambo rahisi kibinadamu ingawa kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Japo miye ndiye mwenye maumivu makali na machungu mwilini yanayotokana na majeraha na ulemavu niliotiwa, mke wangu kipenzi al maarufu Mama Joshua alikuwa pembeni mwangu wakati wote nikiwa kitandani hospitalini Dar es Salaam hadi Milipark Afrika Kusini. Pole sana Angela. 

Matendo yanasema zaidi kuliko maneno...umepita nyakati nyingi sana ngumu juu yangu tangu mwaka 2000 tulipokutana na kuwa marafiki na hatimaye mwili mmoja. 

Ni Mungu tu atakayekulipa kile kinachostahili na si mwanadam

KAJALA MASANJA AJICHORA TATTOO YA WEMA SEPETU MGONGONI KAMA ISHARA YA KUMSHUKURU KWA ZILE MILIONI 13



Kajala ameamua kuchora Tattoo yenye jina la WEMA mgongoni mwake  baada ya kutolewa faini ya Shilingi Milioni 13 na msanii mwenzake Wema Sepetu,
 
hii ikiwa kama ishara ya shukrani kwa rafiki yake kipenzi Wema Sepetu.

Kupitia ukurusa wake wa instagram Wema nae ameandika hivi:

BEN POL NA LADY JAYDEE WAZINGUANA....JIDE ANADAI WAMEMTAPELI


So much is happening on Twitter these days. Wengi mnafahamu anachokiandika Lady Jaydee siku za hivi karibuni na sasa kibao kimemuendea Linah na Ben Pol.
 


Lady Jaydee anadai wasanii wa THT wamemsaliti kwa kile anachodai walikatazwa kwenda kuperform Nyumbani Lounge licha ya kuwalipa advance.

“Linah na Ben Pol mnabisha hamkukatazwa? Nisalitini ila hamtapata faida mtatoka kapa pia,” ametweet Jide.

Shutuma hizo zimepolekewa kwa hasira na Ben Pol aliyemjibu Jaydee:

“Hiyo show kulikuwa na wengine pia wakuperform je wali perform? kama nililipwa nanikashindwa ku show up, mbona sidaiwi?? Tafakari.”

Aliongeza, “Ben Pol hana muda wa maneno na majungu. Ombi langu ni mmoja kwako. Put me out of your business. PERIOD.”

“Don’t talk about things you don’t know about. DON’T.”

“Ukiwaza kutumia akili kamwe huwezi kukosea, ila utakapotumia hisia lazima ujikanyage somewhere. Nimekua vya kutosha #Trustme,” alimalizia Ben.

Unazungumziaje hiki kinachooendelea sasa na athari yake kwenye muziki wa Tanzania. Maoni yako tafadhari.

PICHA 5 ZA LAANA YA "KANGA MOJA" KATIKA SHOW YA MSANII DIAMOND- BUKOBA

Mambo yanayofanywa na kundi la kanga moja ni ya aibu sana  kwa  sababu  ni  uchafu  unaotendeka  mbele  ya  watoto......

Mwanamke  hujifunga  kanga  moja  tu  bila  chupi  wala  chochote  ndani.Baada  ya  hapo  humwagiwa  maji  kitu ambacho  huanika  kila  kitu  hadharani......

Kama haitoshi, akimwagiwa  maji, wenzie  huanza  kumtia  chupa  matakoni  hali  inayoashiria  VITENDO  VYA  ULAWITI......

Tunawafundisha  nini  watoto???..Tunaifundisha  nini  jamii  na  kizazi  cha  kesho????



PICHA: WEMA SEPETU AAMUA KUMUENZI MCHINA WAKE KWA KUJITANDIKA TATTOO ZA KICHINA SHINGONI NA MGONGONI


3b7e57489bae11e2807c22000a9e06c7_7 
Baada  ya  Kajala  masanja  kujichora  tattoo  zenye  jina  la  Wema  kama  ishara  ya  kumshukuru  kwa  msaada  wake, Wema  naye  ameamua  kujitandika  tattoo  ya  kichina  yenye  maana  ya  "Potential"  kama  ishara  ya  kumuenzi  mchina  wake

Tuesday, April 2, 2013

VODACOM FOUNDATION YASAIDIA UJENZI WA KITUO CHA AFYA PEMBA

Mkuu wa Mfuko wa Vodacom wa Kusaidia Jamii - (Vodacom Foundation), Yessaya Mwakifulefule, akikabdhi kwa mmoja wa wazee wa Shehia ya Michenzani Mkoa wa Kusini Pemba mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. milioni 30. Fedha hizo zimetolewa kumalizia ujenzi wa jengo la kituo cha afya cha Michenzani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya katika eneo hilo. Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa (wa pili kulia) na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim wakishuhudia.…
Mkuu wa Mfuko wa Vodacom wa Kusaidia Jamii - (Vodacom Foundation), Yessaya Mwakifulefule, akikabdhi kwa mmoja wa wazee wa Shehia ya Michenzani Mkoa wa Kusini Pemba mfano wa hundi yenye thamani ya Sh. milioni 30. Fedha hizo zimetolewa kumalizia ujenzi wa jengo la kituo cha afya cha Michenzani ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya katika eneo hilo. Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa (wa pili kulia) na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim wakishuhudia.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa akielezea kwa  Mkuu wa Vodacom Foundation, Yessaya Mwakifulefule na Meneja Uhusiano wa Nje wa Kampuni ya Vodacom, Salum Mwalim (mwenye fulana nyekundu) ujenzi wa jengo jipya la kituo cha Afya cha Michenzani Mkoa wa Kusini Pemba muda mfupi kabla ya Vodacom Foundation kukabidhi hundi yenye thamani ya Sh. milioni  30 kumalizia ujenzi wa jengo hilo.
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa, akiongoza kikundi cha ngoma ya kibati kutoka Chokochoko Mkoa wa Kusini Pemba kucheza ngoma hiyo wakati wa hafla ya kupokea hundi yenye thamani ya Sh. milioni  30 kumalizia ujenzi wa kituo cha Afya cha Michenzani Kisiwani humo zilizotolewa na Mfuko wa Vodacom wa kusaidia Jamii - (Vodacom Foundation). Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mfuko huo, Yessaya Mwakifulefule akifurahia burudani hiyo.
---
WAKAZI wa Shehia ya Michenzani, Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba na maneo ya jirani sasa wana kila sababu ya kuwa na uhakika wa huduma za afya kwa ukaribu zaidi kufuatia msaada wa Sh 30 Milioni uliotolewa na kampuni ya Vodacom kupitia mfuko wake wa kusaidia Jamii – Vodacom Foundation kwa ajili ya kuamlizia ujenzi wa jengo jipya la kituo hicho.
Jengo hilo ambalo kwa sasa lipo katika hatua ya linta linajengwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Tenknolojia Profesa Makame Mbarawa akishirikiana na nguvu za wananchi.
Kutolewa kwa fedha hizo ambazo zitanunulia vifaa vya ujenzi vinavyohitajika kwa ajili ya kazi ya kuezeka pamoja na vifaa vingine vya kumalizia ujenzi ni matokeo ya juhudi za makusudi za mfuko huo za kusaidia miradi ya kijamii yenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa wananchi hapa nchini.
Akikabidhi mfano wa hundi kwa wakazi wa Mkanyageni katika hafla iliyoongozwa na Waziri Profesa Mbarawa, Mkuu wa Mfuko huo Yessaya Mwakifulefule amesema Vodacom Foundation imekuwa na dhamira ya dhati ya kusaidia maisha ya watanzania mijini na vijijini ili kuboresha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya na uwezeshaji wanawake  kiuchumi.
“Tunajisikia furaha sana leo kuona Vodacom Foundation ipo hapa Michenzani kuendeleza azma yake ya kuunga mkono juhudi za maendeleo, tutachangia fedha ambazo zitatumika kununulia vifaa vya ujenzi kumalizia ujenzi wa kituo cha afya katika eno hilli.”Alisema Mwakifulefule.
Hata hivyo Mwakifulefule aliwapongeza wakazi wa Shehia ya Michenzani na jimbo zima la Mkanyageni hususan vijana kwa namna wanavyojitolea kushiriki katika miradi ya maendeleo jambo ambalo amesema huenda limechangia kwa kiasi kikubwa kumpa nguvu Waziri Prof;Mbarawa ambae ni mweneyeji  wa eneo hilo kusaidia maendeleo.
“Nimezunguka sehemu mbalimbali hapa nchini hamasa na ari niliyoiona hapa ni ya kipekee jinsi ambavyo wananchi mnavyojitolea katika miradi ya maendeleo hili ni jambo zuri na linawapa moyo wahisani wa maendeleo.”Alisema Mwakifulefuke na kuongeza. “Na sisi katika fedha tutakazozitoa kumalizia ujenzi zinahusisha fedha za kulipia gharama za mafundi na vibarua mbao ni miongoni mwenu. Kwa namna hiyo tunaamini kuwa tutakuwa pia tunaimarisha hali ya uchumi wa vijana wa eneo hili.”
Kwa upande wake Waziri Profesa Mbarawa ameishukuru Vodacom Foundation kwa kukubali kusaidia kumalizia ujenzi wa kituo hicho,
“Nawashukuru Vodacom Foundation kwa kuja hapa na kusaidia maendeleo yetu ila nataka niwaambie wananchi kwamba haya yote hayaji tu hivihivi bali hutafutwa.”   Alisema Profesa Mbarawa
Waziri huyo wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  aliwashukuru vijana na wakazi wa Mkanyageni kwa jinsi wanavyojitoa na kuwaeleza kuwa hiyo ni silaha muhimu ya maendeleo hivyo waupeke kudanganywa na badala yake waangalie namna gani ya kuleta maendeleo na kiwanga mkono wale wanaowaletea maendeleo badala ya kukubalia hila za kuwabeza.
Vodacom Foundation imekuwa ikichangia miradi mbalimbali ya maendeleo Zanzibar ambapo pia hivi karibuni imeahidi kutoa boti mbili za uvuvi kwa vikundi vya vijana Pemba na Unguja kusaidia juhudi za serikali ya Zanzibar za kutengeza ajira kwa vijana.
Mbali na mchango huo, Mwishoni mwa mwaka jana, Vodacom Foundation ilisaidia wanawake wajasiriamali zaidi ya 300 kwa kuwaptia mikopo nafuu isiyo na riba wala dhamana yenye thamani ya zaidi ya Sh. 27 Milioni katika kisiwa cha Unguja pamoja na kuahidi kuchangia Sh 15 Milioni kwenye mfuko wa maendeleo ya watu wenye ulemavu Zanzibar.