Wednesday, September 11, 2013

Rais Kikwete azindua miradi ya maji na umeme Sengerema

0L7C0442Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi katika mradi wa maji Katika kijiji cha Katunguru/Nyamtelela wilayani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Kulia ni Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe. 0L7C0638Mwakilishi wa Serikali ya watu wa Marekani Bwana Karl Fickenscher akitoa hati ya kukabidhi mradi wa MCC I kwa waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo wakati wa  hafla ya ufunguzi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambaza umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa wilayani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Katikati akishuhudia ni Afisa mtendaji Mkuu wa Millenium Challenge Account-(MCC)Tanzania Bwana Bernard Mchomvu. 0L7C0665Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya utekelezaji wa mradi wa umeme wa MCC unaotekelezwa katika mikoa ya Mwanza na Geita wakati wa  hafla ya ufunguzi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambaza umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa wilyani Sengerema,Mkoani Mwanza leo.Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo. 0L7C0717Mwakilishi wa Millenium Challenge Account nchini Tanzania Bwana Karl Fickenscher akipanda mti wa kumbukumbu muda mfupi baada ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua mradi wa njia mpya za umeme kwenye mifumo ya kusambazia umeme mikoa ya Mwanza na Geita uliofanyika katika kijiji cha Bukokwa,Wilayani Sengerema leo. Kushoto ni Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na kulia ni Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo(picha na Freddy Maro)

RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AZURU WILAYA YA SEGEREMA

IMG_1853Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akivishwa skafu kutoka kwa chipukizi mara tu baada ya kuingia wilayani Sengerema kwa ziara ya siku moja tarehe 10.9.2013. IMG_1893Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Katunguru kilichoko wilayani Sengerema alipokwenda kijijini hapo kwa kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Katunguru/ Nyamtelela tarehe 10.9.2013. IMG_1930Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Katungulu/Nyamtelela utakaogharimu shs milioni 734 na utawanufaisha zaidi ya watu elfu kumi. IMG_1981Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Luchili akiwa njiani kwenda katika kijiji cha Bukokwa kuzindua rasmi mradi wa umeme tarehe 10.9.2013. IMG_2008Wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini sherehe za uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini uliofanywa na Rais Kikwete huko Bukokwa wilayani Sengerema tarehe 10.9.2013. IMG_2032 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akipokea hati ya makabidhiano ya mradi wa umeme wa Bukokwa uliofadhiliwa na Millenium Challenge Co-operation ya Marekani. IMG_2082Rais Jakaya Kikwete akiangalia michoro inayoonyesha usambazaji wa umeme katika mkoa wa Mwanza. IMG_2090Rais Dkt. Jakaya Kikwete akizindua rasmi mradi wa umeme wa Bukokwa tarehe 10.9.2013
PICHA NA JOHN LUKUWI

DIWANI WA TLP :SIASA SI UADUI, AMFAGILIA KINANA KWA BUSARA ZAKE

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa pamoja na diwani wa TLP Ntabo Majabi kata ya MwendaKulima wakati wa uzinduzi wa jengo la kituo cha afya kilichodhaminiwa na mgodi wa Buzwagi kulia ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
……………….
Na Adam Mzee
DIWANI wa Kata Mwendakulima Ntabo Majabi kupitiaTanzania Labour Party (TLP), amesema Katibu Mkuu wa CCM Abdulrhaman Kinana ni kiongozi mwenye busara na hekima kubwa na ndio maana Rais Jakaya Kikwete amemua kumpa nafasi hiyo kwa kuwa atakuwa anamjua vizuri.
Akizungumza katika uzinduzi wa kituo cha afya katika eneo hilo, alisema amefurahishwa na aina ya siasa ambazo zinafanywa na Kinana na yeye binafsi ametambua kuwa Katibu Mkuu huyo wa CCM anaouwezo mkubwa wa kufanya kazi zake.
“Kinana wewe ni jembe, wakati unazungumza nilikuwa nimekaa mbali na kusikiliza lakini maelezo yako yamenifurahisha na ndio maana nimeamua kuja kukupa mkono.Kama nchi hii ingekuwa na makatibu wakuu wengi wa aina yako, tungepiga hatua hasa katika siasa za nchi hii.
“Pia niwaambie wananchi siasa si ugomvi, Kinana ameeleza vizuri, tunatakiwa kushirikiana ili kufanikisha malengo ya kuwatumikia wananchi.Nakupongeza mzee Kinana kwa maelezo yako yamenipa faraja licha ya kwamba mimi ni diwani kupitia TLP,”alisema.
Ndugu Kinana alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wananchi kuwa CCM ndio yenye Serikali na diwani huyo licha ya kuwa TLP bado anatekeleza ilani ya CCM , hivyo wananchi nao wanatakiwa kutambua hakuna sababu ya kulumbana kwasababu tu ya mambo ya siasa.

0 comments: